Mgomo wa madaktari unaendelea; Watanzania tuungeni mkono

Kwakweli leo madakatari wote wamerejea kazini. Muhimbili leo asubuhi wakipishana kila mmoja kuwahi kutia sign daftari la mahudhurio.
Ni wazi wito wa Waziri Mkuu umeitikiwa kwa kasi ya ajabu.

Tatizo la viongozi wetu wengi bado wanafikiri wananchi kwenye zama za RTD! Sasa hivi huhitaji radio wala tv kujua nini kinaendelea duniani let alone hapa bongo! Hawa mabwana wameharibu kabisa TBC sasa hivi imegeuka kuwa national embarrassment. Tangu mgomo umeanza TBC imekuwa na mkakati wa ku-downplay hali halisi. Je, ni kweli watu hawana taarifa? Ukitaka kutatua tatizo sharti ukubali kwanza kuna tatizo.
 
Tupo pamoja na nyie tunayajua madai yenu serikali hi legelege ya CCM imezidi kuwanyanyasa watanzania kila kukicha,madaktari endeleeni na mgomo,tunawaunga mkono na tupo pamoja na nyie.
 
agizo la waziri mkuu limefuatwa?

Tunawaomba wananchi waendelee kutuunga mkono pia sekta zingine sasa nazo zituunge mkono
wazi wazi hivi ni vita amkeni hii ni saa ya ukombozi hawa wanasiasa inabidi waache kufanya mambo ambao yanahitaji utaalam ambao wao hawana

ninachoweza kusema mbeya, dodoma,mwanza-bmc,na dsm confirmed mgomo unaendelea
tutaendelea kuwajuza maendeleo kwenye territories zetu zingine stay tuned

Dr. Klinton, katika taarifa yake ya habari ya saa 4:00 asubuhi hii, TBC imeonyesha ripoti kutoka Mbeya kuwa madaktari wamerejea kazini na huduma zimerejea kama kawaida!. Pia Songea, Lindi na Morogoro, japo kwa Morogoro madaktari wamerea huduma hazijarejea!
 
God bless doctor's strike!
Pamoja sana kama vipi pinda akasomee udaktari na magamba wenzake ili ajue ugumu wake!
 
suala la mgomo kwenye sekta ya afya hata usipotangaza linasambaa kama moto wa petrol achana na tbc watu wenyewe wataisoma Mungu atuepushe na maradhi kipindi hiki kigumu
 
We dr wa private nn sijui kama wenzako watakunga mkono leo walivyopigwe mkwara jana mhh
 
Mimi ni mwananchi wa kawaida sana, na ninajua naweza kuugua saa yeyote ile lakini siko tayari kutibiwa na daktari alesukumwa, ambaye hana maslahi safi.

Endeleeni ndugu zangu Madaktari, kazeni buti
 
Hakuna huduma zinazoendelea... baadhi ya madaktari wamerudi ila wamekaa tu wanawaangalia wagonjwa hakuna kinachofanyika, wanaowaudumia wangonjwa ni ma-medical assistance, manurse hata hao machief doctors hawatoe huduma za kawaida wanatoa huduma za dharura, madaktari wameapa kuwa wako tayari kufukuzwa kazi na sio kudharauliwa.
mgomo bado unaendelea....
 
Dr. Klinton, katika taarifa yake ya habari ya saa 4:00 asubuhi hii, TBC imeonyesha ripoti kutoka Mbeya kuwa madaktari wamerejea kazini na huduma zimerejea kama kawaida!. Pia Songea, Lindi na Morogoro, japo kwa Morogoro madaktari wamerea huduma hazijarejea!

Pasco unategemea nini kwa mfa maji? waulize dodoma hata madaktari wanaotibu wabunge kwa posho ndefu hawapo leo..

Bunge liagize mar kutoka India
 
Wanabodi,

TBC imetangaza taarifa ya baadhi ya madaktari kuitikia wito wa Waziri Mkuu Pinda, na kurejea kazini hii leo asubuhi. Taarifa hiyo imesema huduma katika baadhi ya hospitali za mikoani huduma zimerejea kama kawaida!.

Hata hivyo taarifa hiyo imesema pia kuna baadhi ya hospitali, madaktari wamereja ila huduma bado hazijarea kama kawaida.

Taarifa hiyo ya TBC, imemalizia kwa kumuonyesha Waziri Mkuu Pinda akiahidi kuwa pamoja na amri ya kurejea kazini, serikali serikali haijapuuza madai ya madaktari, bali bado itayafanyia kazi yale madai yao ambayo ni genuine!

My Take:
Taarifa hii ya TBC imeonyesha ripoti za mikoani tuu na sio za hapa jijini!. Kwa vile hapa jijini ni karibu kuliko mikoani, nilitegemea taarifa ionyeshe matukio ya karibu zaidi hapa jijini kwa hospitali kama Muhimbili, Mwananyamala, Ilala na Temeke, hivyo kitendo cha kuonyesha taarifa za mikoani tuu, kinanishawishi niamini TBC inazo taarifa za karibu, ila ila imeamua kuzichagua zile ambazo imeona zinafaa kwa taifa kutangaziwa!.

TBC lazima watangaze habari zenye kuwafaa watawala. Tumeshazoea kutumia uongo kama ndio silaha yetu ya maangamizi. Ila sasa tunaumbuka. Mabavu hayatatoa suluhu kwenye haya matatizo yetu
 
Umati wa watu kutoka tanganyika wanakimbilia hospitali ya taifa ya mnazimmoja kwa matiababu. Muungano oyeeee


Mkuu lakini si unafahamu kuwa nusu ya wapemba wanaishi Tanganyika? pengine ndio hao wamefuata huduma mnazimmoja!
 
Back
Top Bottom