Mgomo wa madaktari unachochewa na chama Pinzani-Gazeti RAIA MWEMA

Jisemee mwenyewe na nafsi yako mkuu.
Sema " mimi sipendi kuletewa yanayotokana na magazeti ya CCMAFISI", nitakuelewa!
Mtu mwerevu atatambua kuwa wewe una ujinga wa kujitakia.

tuyaache magazeti yaandike yaandikavyo. hoja za madaktari ni za kizalendo kuliko hasira za 'wakusanya kodi' wetu. madaktari wamechoka kubeba uovu wa serikali.
 
huu upuuzi wenu wa magamba wa siasa taka



uhuru-tbc1-ze original commed vyote vitakufa 2015
Ungejitahidi, kama thinker mkuu, kujibu hoja.
Empty rhetorics aint making it.
You guys have been caught in bed with your pants down!
 
BigMan,
Ibara ya 13 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inasema Watu wote ni sawa mbele ya sheria,na wanayo haki ,bila ya ubaguzi wowote,kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria' .
Maelezo marefu lakin umeshindwa kutazama picha upande wa pili, hivi Dr. Ulimboka halindwi na katiba ibara hii hii au?
 
Last edited by a moderator:
chadema=nyani mzee... Mpaka 2015 wakati amekwepa mishale mingi.!! Tumwombe Mungu isimkute.!!
 
Mbali na taarifa hii sisi wengine wa Mujini tayari tulisha zisikia habari hizi mapema na ndio maana kuna watu wametunga safari ghafla kutokuwepo bungeni kinyume kabisa cha kanuni na taratibu za bunge..

Yawezekana Chadema hawajui wanachokishabikia lakini ukweli utabakia kwamba JK anapigwa vita toka ndani ya chama chake mwenyewe na watu wake wa karibu toka kuvunjika kwa baraza la kwanza la mawaziri..Sidhani kama Chadema wanaelewa kinachotendeka aidha kwa fikra za viongozi wake vitab hii ni kuindoa CCM madarakani lakini wasichjokifahamu ni kwamba ndani ya CCM kuna vita kubwa ya kumgombea urais mwaka 2015 na chaguo la JK halikubaliwi na wengi..Viongozi wengi wamejiandaa kugombea na wote kwa ujumla wao wanajua jinsi gani JK mwenyewe aliweza kuingia madarakani kwa kupitia maandalizi makubwa ya mtandao dhidi ya chaguo la Mkapa.. What goes around comes around!..

Chadema kama chama sidhani kama wana ushawishi wa kutosha ktk mgomo huu kwa sababu hata wao hawawezi kutoa mishahara mikubwa kwa madaktari pasipo kuathiri sehemu nyinginezo ama kujikuta wana matatizo na watalaam wa sekta nyinginezo. Njama hizi hazikutokana na MAT isipokuwa kundi la watu fulani waliochombezwa kuanzisha vagi hili ndio habari ya Mujini..Kama mwalimu alivyosema nchi yetu maskini, bajeti yetu haifiki hata bajeti ya county au mji mmoja wa nchi zilizoendelea kama hapa nilipo lakini tunataka kulipana mishahara kuliko hata Ulaya, huu wendawazimu halafu tunalalamika kwa nini hatuendelei.

Mkuu umeiweka vizuri japo ina habari ya Madaktari ina mapana yake. Kwa kweli wanasiasa sometimes wajitahidi kuangalia mazingira na madhara ya mambo yanayogusa watu wengi. Kwa hili kuwasukumia Chadema ni kuwaonea, wao wametumia nafasi yao ya kisiasa kuibana serikali na hili ni jambo jema kwa baadae ili serikali isibweteke. Kukiwa hakuna mtu wa kusema mambo yataharibika kabisa. Leo serikali ikitaka kufanya jambo inaangalia mara mbilimbili, "chadema na waandishi watatusumbua tukikosea" na hiyo ndio faida ya demokrasia.
 
Mkuu umeiweka vizuri japo ina habari ya Madaktari ina mapana yake. Kwa kweli wanasiasa sometimes wajitahidi kuangalia mazingira na madhara ya mambo yanayogusa watu wengi. Kwa hili kuwasukumia Chadema ni kuwaonea, wao wametumia nafasi yao ya kisiasa kuibana serikali na hili ni jambo jema kwa baadae ili serikali isibweteke. Kukiwa hakuna mtu wa kusema mambo yataharibika kabisa. Leo serikali ikitaka kufanya jambo inaangalia mara mbilimbili, "chadema na waandishi watatusumbua tukikosea" na hiyo ndio faida ya demokrasia.
Nakuelewa sana mkuu wangu mimi huwa sisemi ya ndani moyoni mwangu hadi pale napolamzimika.. Hakuna mtu anayepinga madai ya madaktari kila mtu anastahili malipo mazuri kwa kazi yake..lakini hata tukirudi nyuma utakuta kwamba madai haya hayakuandaliwa vizuri isipokuwa kwa msukumo wa kisiasa. They madaktari chose who to go, who they wonna meet and where! Wewe uliona wapi mwajiriwa akitaka waziri na naibu wake afukuzwe kazi kwanza ndipo mazungumzo yaendelee wakati wamegoma?

Ulisikia wapi waziri aliyeweza kupinga ujenzi wa gati za bandarini kwa gharama kubwa ndiye awe bangusilo wa kuondolewa ktk madaraka pasipo msukumo wa kisiasa. Hata bandarini wanaweza kusema kuna mapana yake, lakini amini maneno yangu siasa ndani ya CCM ndizo zimepelekea kufikia hapa tulipo. Watu wanakufa wakati wengine wakishangilia wakinywa mvinyo huko waliko... Mbona hatukuwa na matatizo kama haya enzi za Kina Profesa Makene, Profesa Sarungi, Kimati, Kahamba na walikuwa wataalam wakubwa tu na wala hatukuwa na wengi kiasi hiki leo (soko lao lilikuwa kuibwa zaidi).

Tumesomesha vijana wetu bure ili kupambana na adui maradhi, that comes first.. na kama fedha ndio msingi wa maendeleo yao basi tuwadai hizo Usd 200,000 or more toka kila mshahara wao on market rate - tuone itachukua miaka mingapi kwa vijana hawa kuweza kurudisha kodi za wananchi. Guess wote wataikimbia nchi kwenda huko Rwanda, hivyo tuwe makini sana na swala hili japokuwa kweli serikali ima makosa yake na imeshindwa kuwalinda wananchi wake toka enzi za Kolimba sasa wamegusa mahala ambapo tutaiona chachu ya udikteta. Nasikitika tu kwamba chama changu kimeingia mkenge huu pasipo kujua kwamba swala hili lina undani zaidi toka posho za wabunge na mengineyo mengi ya kumdhalilisha JK na chaguo lake.
 
Huo ni ukweli mtupu Chadema wako nyuma ya mgomo huo. Wanataka nchi isitawalike na wananchi waichukie serikali ya CCM na Chadema ipande chati. Lakini sasa watanzania wamejua kwamba chadema ni hatari kuliko sumu.

magamba mna shida, hata mafuta yakipanda bei mtasema ni upinzani
 
'''Mwisho ni malizie kwa kuwataka wanaharakati na wale vyama vya siasa akiwemo Kada ya Chadema, Godbles Lema ambao wametoa matamko ya kulaani kitendo alichofanyiwa Ulimboka na Lema akasema akifa Ulimboka atalala barabarani, nawataka wageuze upande wa pili wa shilingi na waone kuwa kuna mamia ya wagonjwa wanakosa huduma na kupoteza maisha yao kwaajili ya mgomo huo haramu,mbona makundi hayo hatusikii yakitoa tamko ya kuwasema wananchi hao na kulaani mgomo huo haramu wa kisheria ambao mahakama ilisema mgomo huo ni batili?.


Wewe Lema unayesema utalala barabarani Ulimboka akifa, tumuulize huyu Lema ni kwanini alishindwa kulala barabarani siku ile Jaji Gabriel Rwakibalila wa Mahakama Kuu Kanda ua Arusha alipotoa hukumu dhidi yake ambapo alimvua ubunge na kumfungia kugombea ubunge baada ya kumtia hatiani kwa makosa ya kutoa lugha chafu?


Maana hukumu hiyo ndiyo imemfanya Lema hivi sasa awe kaka sisi tusiowabunge kwani analifuatilia bunge kupitia redio na televisheni, hapati tena posho na mshahara na hapewi heshima na stahili za kibunge tena,sasa tumuulize sasa alishindwa kulala barabarani kwa hukumu hiyo iliyokuwa ikumuhusu na imemwathiri yeye binafsi ndiyo leo hii atakuwa na ujasiri wa kufanya hivyo kwa Ulimboka ambaye hawana hata undugu?'''-Happiness Katabanzi.

Huyu dada ndio kanisikitisha kabisa.Hapa Lema kaingiaje?Hata kama mwandishi ameamua kumuhusisha kamnda wetu katika uchambuzi wake uliojaa jazba na kebehi dhidi ya madaktari ,bado haewezi kuwa na mamlaka na uwezo wa kuwachagulia wananchi wenzake,nikiwemo mimi ama Lema ama Molemo masuala ya kusimamamia na kujadili.Ajue hivyo na aache mara moja.Inafaa afahamu kuwa Lema si mbinafsi ,anapigania maslahi mapana ya jamii na amekwisha tamka muda mrefu kuwa kutokuwa mbunge hakumzuii kuwapigania wananchi wenzake.....Eti analeta hoja dhaifu kuwa Lema hana undugu na Ulimboka!!!Nimuulize dada mwandishi swali:hivi madaktari waliopambana hadi Ulimboka anapelekwa South Africa wote ni ndugu zake Ulimboka ?Naomba nitajiwe mwanaharakati anayeyatazama masuala kwa misingi ya undugu,ukabila na bado akabaki kuwa mwanaharakati?Eti anadai Lema sasa hana tena 'heshima ya kibunge' na 'mishahara ya ubunge'!!Hoja dhaifu!!
Yeye,dada mwandishi, anayejifanya anayewatetea wananchi ina maana wananchi wote wa Tanzania ni ndugu zake?
Huyu dada anaandika kihisia zaidi...anatumia lugha ya kuudhi na isiyo ya kindugu kabisa dhidi ya ndugu na rafiki zetu madaktari.Ameuanika udhaifu wa fikra zake.Sidhani kama kuna haja ya kusoma maandiko yake tena.


Kuhusu RAIA MWEMA:Mimi si mwanahabari ingawa,ili kuweza kuzifuatilia vema siasa za Tanzania nalazimika kuwategemea wanahabari ..Habari husika ilinishtua sana hasa baada ya kuona mwandishi ameihusisha CHADEMA.Baada ya kutafakari niliamua kuichukulia kama mawazo na maoni ya mwandishi na si maoni ama msimamo wa gazeti zima. WAKATI WA KAMPENI ZA ARUMERU WALIDAI KUWA NASSARI ANASAFIRIA NYOTA YA DKT.SLAA NA MBOWE NA KUWA VIJANA WENGI HAWAKUWA WAMEJIANDIKISHA KUPIGA KURA NA KUWA WALITAKA TUAMINI KUWA CDM ingeshindwa.Yaliyotokea sote tunajua.
Ujumbe wangu kwa Raia Mwema ni kuwa mjitathmini mjihadhari na uwezekano ama tishio la kuwa co-opted na serikali ama CCM.Pamoja na kosa hili la kiufundi walilotenda ,bado ninawamini kama chanzo cha uchambuzi maridhawa.




 
lakini hiyo habari sijaiona kwenye gazeti la raia mwema
Utakuwa umesoma RAI labda. Raia Mwema ina hiyo habari. Halafu sijui kwanini watu mnashangaa hivyo wakati hawa hjamaa walishaanza kuchemka kwenye mgogoro wa Arusha muda mrefu uliopita? Acha ubahili kanunue hilo gazeti bado liko miataani maana siku hizi wateja wamepungua
 
Happiness Katabazi alikuwa Mwandishi mzuri sana wa Makala zamani na nilikuwa sikosi kusoma na mara nyingi nilikuwa nampa feedback tunachat na kubadilishana mawazo ya hapa na pale. Tatizo lilianza pale aliponunuliwa na Makongoro Mahanga... Duh akawa gamba gamba kuliko magamba wenyewe. Sasa naona anatumika kama mpira wa... ukishatumika unatupwa huko na hauna manufaa tena licha ya uwezo wake wa kuzuia Ukimwi na mimba... Huyo ndio Happiness Katabazi
 
Ni wajinga tu ndiyo wataamini mgomo huu una sura ya kisiasa. Heb tuangalie maeneo mengine ya nchi yetu: Walimu nao wanachochewa na wanasiasa? Ugumu wa maisha unachochewa na wanasiasa? Kuanguka kwa uchumi kunachochewa na wanasiaisa? Wizi wa mamilioni ya dola unachochewa na wanasiasa? Ujinga wa Mwigulu na wenzake Bungeni ni wanasiasa wa upinzani?Ni mpumbavu pekee atakayeamini ujinga huu!
 
Matusi mmeshaanza ya nini tena mtu asitoe mawazo yake mnamnanga. Mm silioni kosa Raia Mwema, Dada Happy au huyo Dr Deo Maiko aliyekuwa na Dr Ulli
Ushabiki mbaya ninyi mmeshaambiwa kachukuliwa na wababe karibu na Victoria kafunikwa kitambaa hakuona k2 kipigo hajakizungumzia, kuvulia suruali, (akaachwa na bukta sina uhakika) kung'olewa kucha na meno KWA AKILI YENU BADO Dr Ulli ALIKUWA HAJATOA SIRI YA MGOMO NA NANI YUPO nyuma yao?
Hao jamaa hawajuachii pumzi mpaka uwashibishe na wanauachia uggai wako
Jiulize je kuna mgomo tena? Quishney Huduma zote zimerudi sisi tusigombane na MITUSI kaa mjue ndio maana kuna watu na viherehere
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom