Katika hali ya kushangaza gazeti la Raia Mwema toleo la leo limeripoti kuwa mgomo wa madaktari nchini unachochewa na chama kimoja cha upinzani kikishirikiana na kundi moja ndani ya CCM linalotaka kudhoofisha serikali na kuijengea chuki kwa wananchi.Gazeti hilo limeendelea kuripoti kuwa baada ya njama hiyo kugundulika ndiyo maana wale madaktari wote wenye nia njema wamerejea kazini.
Pia gazeti hilo limesema limepata uthibitisho kwamba kamanda Ahmed Msangi hakuhusika katika tukio la utekaji na mateso kwa Dr Ulimboka Stephen.
Pia katika gazeti hilo kumetolewa Tangazo maalum la serikali la kurasa 2 lenye hotuba yote ya Rais aliyoitoa mwisho wa mwezi kuhusu onyo lake kwa madaktari
Source:Raia Mwema uk 3
------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Soma habari yenyewe hapa chini:
TAKRIBAN wiki moja baada ya kutekwa, kuteswa na kuumizwa vibaya kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Steven Ulimboka, mmoja wa marafiki zake, Dk. Deogratius Michael (36), aliyeshuhudia tukio la kutekwa amezungumza na Raia Mwema akisema taarifa za baadhi ya vyombo vya habari kwamba ametoweka si za kweli.
"Nasikia kuna redio moja wamesema kwamba mimi sionekani na kwamba nimetoweka. Ukweli ni kwamba nipo. Napatikana na nimekuwa nikiwasiliana na watu mbalimbali. Ushahidi wa hilo ni kama hivi sasa ninavyozungumza nanyi," alisema Dk. Deo jana Jumatano katika mazungumzo na Raia Mwema.
Lakini wakati hayo yakiendelea, taarifa ambazo gazeti hili limezipata zinaeleza kuwa mgomo wa madaktari nchini pamoja na tukio hilo la Dk. Steven Ulimboka, sasa umeingia katika sura mpya baada ya kikundi cha mtandao unaodaiwa kufanikisha ‘kumuingiza' Rais Jakaya Kikwete madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 2005, kudaiwa kuhusika kufadhili baadhi ya madaktari kuchochea mgomo huo.
Pamoja na baadhi ya wanasiasa ndani ya CCM kuhusishwa, lakini pia wamo wanasiasa kutoka chama kimoja cha upinzani kinachotajwa kuwa nyuma ya shinikizo la kuendeleza mgomo huo wa madaktari.
Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari, lengo la ufadhili huo, ni kile kinachodaiwa kuwa ni hatua ya kulipa kisasi kwa kuzingatia mwenendo wa siasa ndani ya CCM na ‘panga-pangua' ya viongozi serikalini, pamoja na mikakati ya vyama pinzani kujenga chuki kwa wananchi dhidi ya Serikali.
Taarifa hizo zilizopatikana zinabainisha kuwa pamoja na madaktari kushinikiza uboreshaji wa maslahi yao, sambamba na utoaji wa huduma bora za afya, siasa za visasi ndani na nje ya CCM, zimeendelea kudandia mgomo huo na kuanza kuwafanya baadhi ya madaktari kufikiri upya ushiriki wao katika mgomo huku kukianza kujitokeza wito wa kutaka kurejea katika meza ya majadiliano.
Kujitenga kwa baadhi ya madaktari dhidi ya mgomo huo wa sasa kunathibitishwa na taarifa rasmi iliyotolewa na Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminiel Aligaesha.
Pia gazeti hilo limesema limepata uthibitisho kwamba kamanda Ahmed Msangi hakuhusika katika tukio la utekaji na mateso kwa Dr Ulimboka Stephen.
Pia katika gazeti hilo kumetolewa Tangazo maalum la serikali la kurasa 2 lenye hotuba yote ya Rais aliyoitoa mwisho wa mwezi kuhusu onyo lake kwa madaktari
Source:Raia Mwema uk 3
------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Soma habari yenyewe hapa chini:
TAKRIBAN wiki moja baada ya kutekwa, kuteswa na kuumizwa vibaya kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Steven Ulimboka, mmoja wa marafiki zake, Dk. Deogratius Michael (36), aliyeshuhudia tukio la kutekwa amezungumza na Raia Mwema akisema taarifa za baadhi ya vyombo vya habari kwamba ametoweka si za kweli.
"Nasikia kuna redio moja wamesema kwamba mimi sionekani na kwamba nimetoweka. Ukweli ni kwamba nipo. Napatikana na nimekuwa nikiwasiliana na watu mbalimbali. Ushahidi wa hilo ni kama hivi sasa ninavyozungumza nanyi," alisema Dk. Deo jana Jumatano katika mazungumzo na Raia Mwema.
Lakini wakati hayo yakiendelea, taarifa ambazo gazeti hili limezipata zinaeleza kuwa mgomo wa madaktari nchini pamoja na tukio hilo la Dk. Steven Ulimboka, sasa umeingia katika sura mpya baada ya kikundi cha mtandao unaodaiwa kufanikisha ‘kumuingiza' Rais Jakaya Kikwete madarakani kwa mara ya kwanza mwaka 2005, kudaiwa kuhusika kufadhili baadhi ya madaktari kuchochea mgomo huo.
Pamoja na baadhi ya wanasiasa ndani ya CCM kuhusishwa, lakini pia wamo wanasiasa kutoka chama kimoja cha upinzani kinachotajwa kuwa nyuma ya shinikizo la kuendeleza mgomo huo wa madaktari.
Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari, lengo la ufadhili huo, ni kile kinachodaiwa kuwa ni hatua ya kulipa kisasi kwa kuzingatia mwenendo wa siasa ndani ya CCM na ‘panga-pangua' ya viongozi serikalini, pamoja na mikakati ya vyama pinzani kujenga chuki kwa wananchi dhidi ya Serikali.
Taarifa hizo zilizopatikana zinabainisha kuwa pamoja na madaktari kushinikiza uboreshaji wa maslahi yao, sambamba na utoaji wa huduma bora za afya, siasa za visasi ndani na nje ya CCM, zimeendelea kudandia mgomo huo na kuanza kuwafanya baadhi ya madaktari kufikiri upya ushiriki wao katika mgomo huku kukianza kujitokeza wito wa kutaka kurejea katika meza ya majadiliano.
Kujitenga kwa baadhi ya madaktari dhidi ya mgomo huo wa sasa kunathibitishwa na taarifa rasmi iliyotolewa na Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminiel Aligaesha.