Mgomo wa madaktari, natamani LOWASA wakati huu angekuwa Rais au Waziri Mkuu

Madaktari wanagoma sasa, wanagoma wakiwa na madai ya msingi mikononi mwao. Lakini wakati mgomo unapamba moto, roho za raia na wananchi ziko mashakani.

Juhudi za serikali kutatua mgogoro huo na kumaliza tatizo zinakwenda taratibu kwa mwendo wa kinyonga mlemavu. Mgomo wa madaktari ni hatari kuliko aina zote za migomo kwa sababu unagusa moja kwa moja uhai wa wananchi.

Suala hili linahitaji kiongozi mwenye maamuzi magumu. Wala siyo watu wenye dharau za kiutendaji kama JK na wasaidizi wake. Natamani sana kipindi hiki LOWASA Ndiyo angekuwa Rais au Waziri Mkuu. Bila ya shaka angechukua maamuzi magumu na tatizo hili lingekuwa mfano wa chai ya baridi kwake. Nani mwingine?

Nani mwingine mwenye uthubutu na roho ngumu ya maamuzi kati ya waliopo CCM sasa zaidi ya mchapakazi LOWASA anayetetea maslahi ya wanyonge? Huu ndiyo ukweli japo wenye akili zilizopiga sarakasi watapinga na kudai nimevuta bahasha kama kawaida yao.

Hapa tu ndo mnaniboaga mkianza kampeni zenu za kuwapigia debe wanasiasa. Bila shaka umepewa ka-mkate kufanya hiyo kazi. Haya bhana endeleeni kumsafisha tunasubiri kuona
 
Narudia tena kwamba licha ya yote yanayosemwa juu ya Lowassa lakini kiutendaji ni bora kulinganisha na wenzake ktk CCM. Mifano ya utendaji wake ipo wazi,anayebisha huyo ana matatizo yake ama ni chuki binafsi!
........................hebu tupe CV ya utandaji wako na wewe !! maana umekalia kusifia wanaume wenzio tuu ! au "Huntha" wewe ? :A S embarassed:
 
Tired na hizi crap za Lowassa!
Mods kama vipi unganisha hii hread na zingine zinazohusu mada husika
sema umechoka wewe siyo yumechoka,usitusemee sisis nani kwambia sisi tumechoka? kwa taarifa yako sakata hili angekkuwa lowasa mambo haya yangekuwa historia.
 
Kwa nini watu wanashikilia msimamo na kuamini maneno ya wazushi? Hii ni kutokana na ushabiki wa kufuata mkumbo. Huu ni ushabiki ulio na msimamo wa makusudi usio na tija hata kidogo. Baada ya hoja chache hapa chini. Nategemea wale wanaomshutumu Lowasa kuwa ni fisadi nao walete ushahidi wenye vielelezo vya ufisadi huo. Na si kuishia kupiga kelele tu kuwa, Lowasa hafai, mara hasafishiki nk. Huo utakuwa unafiki. Watu wenye upeo mdogo wamepandikiziwa uongo katika bongo zao na kuuamini.
BIBLIA inasema, "Mjinga huamini kila neno; bali mwenye busara huangalia sana aendavyo." (Mithali 14:15).
Haya ni maneno ya Lowasa ambayo mpaka sasa hakuna aliyejitokeza kukanusha, kuyapinga wala kuyatolea ufafanuzi wa kina. zaidi ya watu wachahche waliokaririshwa ubaya vichwani mwao kuendelea kupiga kelele bila kujua nini kilichokuwa kinaendelea tangu mwanzo.
"MWENYEKITI utakumbuka kwamba mimi nilishaamua kuvunja mkataba wa Richmond mapema, lakini baada ya kukupigia simu ukiwa katika safari nje ya nchi ulisema tusubiri kwani ulikuwa umepata ushauri wa makatibu wakuu wa wizara, sasa leo hii ninahukumiwa na kuitwa fisadi kwanini?".swali hili linahitaji majibu.
Hiyo ni sehemu mojawapo ya kauli aliyoitoa waziri mkuu wa kwanza na mstaafu katika serikali hii ya awamu ya nne, Edward Lowassa wakati akichangia mada ya kujivua gamba ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa White House uliopo Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mjini Dodoma mnamo Novemba 24, mwaka huu.
Lowassa alikuwa akijibu tuhuma zilizoelekezwa kwake ya kwamba yeye ni fisadi ambapo alielezea mzizi wa neno ‘fisadi' huku akikumbushia suala la City Water, pamoja na mitazamo ya ufisadi dhidi yake kupitia ndani ya CCM na upande wa vyama vya upinzani.
Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli alielezea historia ya neno ‘ufisadi' akisema lililetwa na CHADEMA kupitia mkutano wa Mwembeyanga na kuwataja viongozi 11 wa CCM akiwamo yeye kwa ufisadi.
Mwanasiasa huyo anasema, katika tamko hilo la CHADEMA, alijumuishwa katika orodha ya mafisadi akihusishwa na uamuzi wake wa kuuvunja mkataba wa City Water ambao hata hivyo baadaye serikali ilishinda kesi katika Mahakama ya Kimataifa ya usuluhishi wa mizozo ya uwekezaji. Hapa napo kuna swali; kwa nini tunang'ang'ana na RICHMOND haya mengine hatuyaoni? Kwa nini serikali ilishinda kesi hiyo? Mkataba huo wa city water ulivunjwa na Lowasa.
Anasema ni jambo la ajabu kwamba viongozi wa CCM walilidaka neno hilo na kuanza kulitumia kuwashambulia wenzao akiwamo yeye katika mambo ambayo hayakuwa na ukweli.
Hapa tunahitaji ushahidi wa ukweli kutoka kwa wale wanaomtuhumu kwa ufisadi. Siku zinasonga mbele huku ukimya ukeindelea kutawala
Lowassa alizidi kukana tuhuma za ufisadi dhidi yake na kudai kuwa kujiuzulu kwake ni suala la kawaida kwenye ulingo wa kisiasa kama njia mojawapo ya kuonyesha dhana nzima ya uwajibikaji.
"Nilijiuzulu kuwajibika kwa ajili ya kuilinda serikali yangu na kwa heshima ya chama changu, sasa kwanini leo nahukumiwa kwa jambo hilo, tena natukanwa na wana CCM wenzangu na si wapinzani nchi nzima kwamba mimi eti fisadi?," ananukuliwa akihoji Lowassa.
Hapa jibu la kujiuzulu kwake analiweka wazi na kuonyesha busara zake katika kulinda heshima ya chama chake. Wale wanaomtukana na kumwita fisadi si ndio wale waliompaka matope katika kashfa hiyo ya ufisadi?
Lowassa pia alilimulika zoezi zima la kujivua gamba na uhalisia wake ulivyokuwa hadi ulivyotumiwa. Lowassa aliipongeza NEC kuridhia ombi la Kamati Kuu ya chama hicho (CC) kwamba suala la mageuzi ndani ya CCM maarufu kama kujivua gamba lirejeshwe katika kamati hiyo ili lifanyiwe kazi kwa taratibu za kawaida za kinidhamu baada ya wahusika kukataa kuachia nafasi zao.
"Mwenyekiti kwanza napongeza uamuzi huu wa kurejesha jambo hili katika taratibu za kawaida, lakini napenda kufahamu kwa miezi saba nimetukanwa nikiitwa fisadi, watu wamezunguka nchi nzima kwa fedha za chama wakinitukana, hivi hatukujua kwamba kuna kamati hizo za maadili?" Lowassa ananukuliwa akihoji.
Lowassa alinukuliwa akiwataja Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Tanzania Bara, John Chiligati, kwamba wamekuwa wakitukana watu ovyo kwa fedha wanazopewa na CCM.
"CCM ninayoifahamu ni ile inayotenda haki na hakiwezi kumtuhumu mtu hadharani bila ushahidi kama walivyofanya Chiligati na Nape na kwa mujibu wa kanuni ni vibaya kumtuhumu bila vikao vya maadili ya chama," alisema.
Hao waliotajwa hapo mpaka sasa hawajaleta ushahidi wa kile walichokuwa wakikihubiri kwa mbwembwe nyingi.
Na kuhoji, Nape anapata wapi ‘moral authority' (uhalali wa kimaadili) wa kumtuhumu yeye kwa ufisadi hata kudai kwamba amekipotezea heshima chama hicho wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka jana.
Anafafanua, matokeo ya kura alizopata rais na yeye mwenyewe katika Jimbo la Monduli unazidi asilimia 89 na kwamba wakati yeye (Lowassa) na wengine wakipambana kukijenga na kukipigania chama chao kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu, Nape na wanasiasa wengine wanaomshambulia walikuwa katika harakati za kusajili Chama Cha Jamii (CCJ).
Kwa nini wananchi wake wanamkubali na kumpa ushindi huo wa kishindo?
Kwa nini kundi linalomchafua halijakanusha tuhuma za kusajili chama ndani ya uanachama wa chama kingine? Huu ni uthibitisho kuwa kundi hilo linacheza rafu za kisiasa.
Hayo ni maneno mazito sana kuwahi kutolewa na Lowassa ambapo mimi na wewe tungetamani kuyasikia ‘live' isipokuwa tumeishia kuyaona kupitia vyombo vya habari kama ambavyo mimi nilivyoyanukuu kupitia baadhi ya vyombo vya habari vilivyoandika Novemba 25. Imenilazimu kunukuu taarifa hiyo kwa ufupi sana kutokana na kuwa ndio msingi mkuu wa makala hii.
Lowassa alitumia takribani dakika 10 kutoa madukuduku ya watu ambao walikuwa na mitazamo hasi dhidi yake kwa kuelezea ukweli mtupu wa mambo ulivyo ambao umezua gumzo na kumjengea heshima kubwa ndani ya jamii.
Watu walio wengi walikuwa na mtazamo duni wa kuamini kuwa eti Lowassa ndiye aliyeileta na ndiye mmiliki wa kampuni ya Richmond nchini. Hapa kundi la aina hii ya watu bado wengi na mtizamo wao usio makini.
Watu hawa wamekosa uweledi wa ufahamu kuwa kampuni ya Richmond iliingizwa nchini kwa mara ya kwanza kabisa na huyu huyu Waziri wa Afrika Mashariki, Samueli Sitta kipindi hicho akiwa Mkurugenzi mkuu wa kituo cha uwekezaji nchini (TIC). Kama namsingizia ajitokeze kukanusha hili.
Kama huyu ndiye aliyeileta kampuni ya RICHMOND, kwa nini tuhuma hizi anabeba Lowasa? Kwa nini hakujitokeza kukanusha?
Iweje leo hii umiliki wa kampuni ya Richmond ihusishwe na Lowassa? Huu ni upotoshaji mkubwa usio na tija kwa taifa.
Wapo watu wengine wanasema kuwa Lowassa alishiriki kwa asilimia 100 katika kuipa zabuni kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond.
Ukiachilia tawala za kifalme, binafsi sijapata kuona serikali yeyote ile duniani ambayo Waziri mkuu wake anafanya kazi pasipo kuwashirikisha watendaji wake wa chini ama mabosi zake ambao ni Rais ama Makamu wa Rais.
Hata huyo waziri mwandamizi tu ni lazima kila jambo analolifanya awashirikishe watendaji wake wa chini ama ngazi za juu, iweje kwa waziri mkuu lishindikane kufanyika hilo? Kwa mujibu wa kauli ya Lowassa anadai aliishtukia na mapema yake hili lidudu Richmond na akataka kulitupilia mbali, lakini bosi wake akamkataza kufanya hivyo, ulitegemea yeye (Lowassa) angefanyaje kama si kumsikiliza bosi wake? Watu wenye vichwa vigumu kuelewa bado wanahoji kuhusu hili.
Tunaambiwa kuwa kuna kundi la makatibu wakuu (ambao kicheo ni watendaji wa chini ya waziri mkuu) lilisharidhia mchakato wa kuipa zabuni Kampuni ya Richmond, kwa mantiki hiyo, iweje leo hii zigo zima la sakata hili aangushiwe Lowassa na hata kufikia hatua ya kumuita fisadi? Hii si sawa kabisa!
Halikadhalika kuna kundi lingine la watu ambao wanaamua kujipa mamlaka ya kumuita Lowassa ni fisadi kutokana na kitendo chake cha kuamua kujiuzulu wadhifa wa uwaziri mkuu.
Watu hawa wanajidhihirisha kuwa ni wepesi sana kisiasa kutokana na kushindwa kutambua ya kuwa Lowassa alijiuzulu wadhifa wake kutokana na kupisha dhana nzima ya kuwajibika kisiasa "political responsibility" ichukue mkondo wake kutokana na makosa yaliyofanywa na watendaji wa chini – kama sehemu mojawapo ya aina ya kuwajibika kisiasa. Jambo hili si geni, linatokea kwa kiongozi mwadilifu. Hata Mwinyi aliwahi kujiuzulu lakini baadaye akawa rais.
Hali hiyo ya makosa hayo kufanywa na wataalamu wa Tanesco na wizara yalisababisha wakubwa wao kimadaraka ambao ni Edward Lowassa aliyekuwa Waziri Mkuu na mawaziri wengine wawili ambao ni Ibrahimu Msabaha na Nazir Karamagi kuamua kujiuzulu kutokana na uzembe uliofanywa na maofisa wao wa chini.
Lowassa hakujiuzulu kwa sababu yeye ndiye aliyehusika katika hili au eti alikuwa na maslahi yake binafsi bali Lowaassa aliamua kubeba msalaba kwa kuchukua dhamana ya kuwajibika kisiasa "political responsibility" kwa kuiokoa serikali isiendelee kusurubiwa na Wabunge kwa masilahi ya Serikali ya Awamu ya Nne na chama chake CCM.
Baadhi ya watu wanajaribu kuupindisha ukweli kwa kufananisha tukio la kujiuzulu kwa Lowassa ni kashfa la ufisadi wa Richmond, lakini wanasahau ya kwamba Lowassa aliamua kujivua gamba si tu kwa kujua nini maana ya kuwa kiongozi bali hata pia kwa kuifahamu vyema dhana nzima ya utashi wa kuwajibika kisiasa ulivyo.
Kitendo cha Lowassa kuamua kujiuzulu hakimvui heshima yake aliyokuwa nayo hapo awali. Na haijawahi kutokea duniani kokote kule kwa kiongozi kuamua kuchukua dhamana ya kisiasa kwa kuwajibika kisiasa eti maana yake amepoteza sifa za kuwa kiongozi tena, sijapata kuona.
Suala zima la kuamua kuwajibika kisiasa si geni hapa nchini kutokea. Mathalani, Mwaka 1977 kulianzishwa operesheni kali ya kuwasaka wanaosadikiwa walikuwa ni wauaji na wachawi ambapo watu kadhaa walikamatwa, wakawekwa ndani na kupewa mateso makali, yaliyosababisha vifo vya baadhi ya watu. Operesheni hiyo iliyoendeshwa katika mikoa ya Mwanza na Shinyanga ilisadikiwa kufanywa na maofisa wa kiserikali.
Makosa hayo yaliyofanywa na baadhi ya maofisa wa kiserikali yalisababisha mabosi wao ama wakubwa wao kimadaraka ambao ni Mzee Alhaji Ali Hassan Mwinyi aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Peter Said Sioverwa (kwa sasa ni Marehemu) aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Usalama wa Taifa; bila ya kuwasahau waliokuwa wakuu wa mikoa wa Mwanza na Shinyanga, Peter Kisumo na Marco Mabawa (marehemu) walijiuzulu kutokana na vitendo vya kikatili vilivyofanywa na maofisa wa serikali waliokuwa chini yao.
Hapa mzee Mwinyi aliamua kuwajibika kwa niaba ya makosa yaliyofanywa na maofisa wa ngazi ya chini yake. Yaani makosa wafanye watu wengine ama maofisa wa ngazi ya chini lakini mkubwa wao (mzee Mwinyi) anaamua kubeba msalaba wao, kwa niaba yao. Kitendo hicho kinajulikana kama kuchukua wajibu wa kisiasa yaani "political responsibility" kwa lugha ya kitaalamu na kisomi zaidi.
Makosa walifanya wengine na mzee Mwinyi akaamue kuwajibika kwa niaba ya wengi, kitendo hicho kilimjengea heshima kubwa hadi Mwalimu Nyerere kwa mwaka ule ule kuamua kumteua kuwa Balozi wa Tanzania nchini Misri; baada ya miaka mitano tu alirudi kwenye Baraza la Mawaziri lile lile, chini ya rais yule yule akiwa Waziri wa Maliasili na Utalii (1982), Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (1983); hatimaye alikuja kuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (1984) na baadaye Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania (1985 – 1995).
Kama iliwezekana kwa mzee Mwinyi iweje ishindikane tena kwa Lowassa kuendelea kuwa kiongozi tena?
Pia kuna mzee John Malecela ambaye alilazimishwa kujiuzulu nafasi yake ya uwaziri mkuu baada ya mzee Mwinyi kuvunja Baraza lake la Mawaziri kutokana na waziri mkuu wake kutokumshauri vyema rais wake katika kashfa ya OIC na ile ya kuanzishwa kwa Serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano.
Lakini ni Mzee Malecela huyo huyo alikuja kuwa makamu mwenyekiti wa CCM katika kipindi chote ambacho mzee Mkapa alikuwa mwenyekiti wake.
Si hao tu, pia kuna Abdallaah Natepe ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani aliamua kuwajibika kisiasa kutokana na sakata la mahabusu waliokuwa wakituhumiwa kwa uhaini katika kundi la kina Uncle Tom au Thomas Rugangira kutoroka wakiwa chini ya ulinzi wa maofisa wa magereza.
Haikuwahi kutokea si kwa mzee Mwinyi, Mzee Malecela wala Natepe kuwahi kusikia vikao vya CCM ama viongozi wa CCM wakimwambia waondoke ndani ya chama kutokana na kashfa zilizowakumba na hatimaye kuamua kuwajibika kisiasa kama ambavyo inavyotokea kwa Lowassa leo hii.
Historia inajibainisha yenyewe kwamba watu makini wanaojitambua wa sampuli kama ya Lowassa hawachelei kurejea nafasi zao za hapo awali na ujio wao huwa ni wa kishindo kikubwa na hicho kishindo ndicho haswa kinachowatia viwewe wale mahasimu wake kisiasa kutokana na kuona wazi wazi kushindwa kuhimili historia ya utendaji kazi wa Lowassa unaotambulika na kukubalika ndani ya jamii.
Sote tumeshuhudia utendaji wa Lowassa kwa nyakati zote tangu mwaka 1975 kuanzia ubunge wa taifa hadi hili leo Mbunge wa Monduli kwa kipindi chote hicho anaweza kufanya mambo yanayoonekana kwa macho ambapo kwa namna moja ama nyingine yataendelea kutunufaisha sisi tuliopo na vizazi vijavyo.
Miaka ya nyuma elimu ilitolewa kwa watu wachache mno, hali iliyopelekea taifa kuwa na wasomi wachache (hafifu) mno. Hii inasababishwa na uchache na uhaba wa shule za mzingi na sekondari.
Lakini kwa ujemedari, ushupavu na nia ya dhati ya Lowassa alipigana vilivyo na suala hili hali iliyopelekea ongezeko la shule nchini Lowassa hakuwapa nafasi ya kupumua wakuu wa mikoa na wilaya katika ujenzi huu wa shule za kata.
Hali hii ilipelekea ongezeko kutoka 14,257 mwaka 2005 hadi 15,816 mwaka 2010 ambalo ni sawa na ongezeko la wastani wa shule 1559 hadi iliyopelekea wanafunzi kuongezeka kutoka 7,541,208 hadi 8,419,305. Jamani, haya yote tusisahau ni matunda ya kazi yake Edward Lowassa.
Kwa upande wa shule za sekondari mwaka 2005 kulikuwa na shule 1,202 zilizojengwa tangu uhuru ambapo leo hii kuna jumla ya shule 2,171. Lile lengo la kuwa na sekondari moja kwa kila kata limetimia ambapo pia kuna baadhi ya kata zina shule zaidi ya moja.
Ongezeko hilo la shule limewezesha idadi ya wanafunzi wanaosoma sekondari kuongezeka kutoka 524,325 mwaka 2005 hadi 1,638,669. Kazi hii nzuri ilifanyika ndani ya kipindi kifupi tu, nani kama Lowassa?
Watanzania hawataki wamsahau Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere si tu kwa kutupatia uhuru bali hata kwa kuhakikisha ujenzi wa Muungano, umoja, upendo huku akipinga vikali ukabila na udini baina yetu.
Ama Edward Sokoine hata kaa asahaulike na Watanzania si tu kupinga na kupambana na wahujumu uchumi bali pia ni kwa kuhakikisha uwepo wa haki na usawa ndani ya jamii.
Mathalani pale alipohakikisha usimamiaji wa ugawaji wa chakula kwa kila kaya ambapo kila kiongozi husika alipewa daftari la kuandika jinsi, wanavyogawa chakula. Hali hii iliondoa ubaguzi upendeleo ambapo kila mtu alinufaika na kufurahia zoezi na utaratibu huu uliowekwa na Sokoine.
Vinyo hivyo Watanzania haswa wale wa kanda ya ziwa hawatakaa wamsahau Lowassa katika maisha yao. Hali hii ilitokana na uthubutu wa kuhoji uhalali wa maji ya ziwa Victoria kwenda Misri kupitia Suez Canal wakati wa Kanda ya Ziwa hawana moja.
Lowassa alikuwa kiongozi wa kwanza katika nchi za maziwa makuu kuvunja mkataba huu kongwe wa wakoloni uliotoa mamlaka ya kuamua matumizi ya maji hayo kwa nchi ya Misri wakati maji hayo chanzo chake ni nchi za maziwa makuu Tanzania ikiwamo.
Ni kutokana na ujasiri huo wa Lowassa wa kuamua kuvunja mkataba huo wa kikoloni, sasa wananchi wa Mwanza, Shinyanga na Kahama wanafaidika na maji ya ziwa Victoria kwa matumizi mbalimbali mradi uliogharimu zaidi ya sh bilioni 200 lakini una manufaa kwa vizazi na vizazi.
Achilia hilo, pia tusisahau Lowassa alipokuwa Waziri wa Ardhi alisimama kidete pale alipogundua halmashauri ya jiji wamempa mfanyabiashara eneo la Mnazi Mmoja.
Lowassa hakukubaliana na uamuzi huo na kuamuru wananchi wauvunje uzio wake na mabati alioweka na hivyo eneo la uwanja kurudi kwa serikali na wananchi.
Faida yake ni leo hii eneo hilo limeendelea kubaki wazi kwa huduma wanachi na taifa kwa ujumla. Eneo hilo linatumika kwa shughuli na dhifa mbalimbali kama vile mikutano, semina, makongamano.
Tunakumbuka ya kwamba huyu huyu Lowasa aliweza kuvunja mkataba mbovu wa City Water kwa manufaa ya wananchi na taifa kwa ujumla. Hatua hiyo ilipelekea kampuni kurudishwa kwa wazawa wenyewe mpaka hii leo.
Yapo mambo mengi sana ambayo jamii karibu kila kona ya nchi itaendelea kunufaika na ujemedari wake Lowassa hapo ni achilia mbali na suala zima la Lowassa kutokuwa mangimeza kwa kuamua kuzunguka kote nchini kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya serikali kwa vitendo.
Hali hii ilisababisha Baraza la Mawaziri wakuu wa mikoa, wakuu wa Wilaya na viongozi wa Halmashauri za Wilaya na jiji kuwa makini na uchapaji kazi hali iliyoleta mwamko mkubwa na imani ndani ya serikali kwa wananchi wanaowaongoza.
Ndugu zangu, hakuna binadamu aliyemkamilifu kwa asilimia zote isipokuwa Mwenyezi Mungu pekee Lowassa kama binadamu kuna uwezekano mkubwa alikuwa na upungufu wake lakini si mtu wa kufanya hayo anayofanyiwa sasa.
..............daaaah ! naona umemwaga makala, nimeishia njiani lakini naamini unamtetea Lowasa ! Mna moyo wa kiwenda wazimu wazimu hivi ! :A S embarassed:
:brushteeth::brushteeth:
 
Kwanini upoteze nguvu nyingi kutetea jizi badala ya kutetea mtendaji mwadilifu aliyeibiwa kura? Tunamuhitaji Silaa kwa Tanzania endelevu na sio vibaka wa maamuzi magumu kwa 10%. kumbuka kauli ya Mh. Samuel Sita bungeni, usijifanye maamuzi ni magumu wakati unayo 10% ndani.
 
Kwa nini watu wanashikilia msimamo na kuamini maneno ya wazushi? Hii ni kutokana na ushabiki wa kufuata mkumbo. Huu ni ushabiki ulio na msimamo wa makusudi usio na tija hata kidogo. Baada ya hoja chache hapa chini. Nategemea wale wanaomshutumu Lowasa kuwa ni fisadi nao walete ushahidi wenye vielelezo vya ufisadi huo. Na si kuishia kupiga kelele tu kuwa, Lowasa hafai, mara hasafishiki nk. Huo utakuwa unafiki. Watu wenye upeo mdogo wamepandikiziwa uongo katika bongo zao na kuuamini.
BIBLIA inasema, "Mjinga huamini kila neno; bali mwenye busara huangalia sana aendavyo." (Mithali 14:15).
Haya ni maneno ya Lowasa ambayo mpaka sasa hakuna aliyejitokeza kukanusha, kuyapinga wala kuyatolea ufafanuzi wa kina. zaidi ya watu wachahche waliokaririshwa ubaya vichwani mwao kuendelea kupiga kelele bila kujua nini kilichokuwa kinaendelea tangu mwanzo.
“MWENYEKITI utakumbuka kwamba mimi nilishaamua kuvunja mkataba wa Richmond mapema, lakini baada ya kukupigia simu ukiwa katika safari nje ya nchi ulisema tusubiri kwani ulikuwa umepata ushauri wa makatibu wakuu wa wizara, sasa leo hii ninahukumiwa na kuitwa fisadi kwanini?”.swali hili linahitaji majibu.
Hiyo ni sehemu mojawapo ya kauli aliyoitoa waziri mkuu wa kwanza na mstaafu katika serikali hii ya awamu ya nne, Edward Lowassa wakati akichangia mada ya kujivua gamba ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa White House uliopo Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mjini Dodoma mnamo Novemba 24, mwaka huu.
Lowassa alikuwa akijibu tuhuma zilizoelekezwa kwake ya kwamba yeye ni fisadi ambapo alielezea mzizi wa neno ‘fisadi’ huku akikumbushia suala la City Water, pamoja na mitazamo ya ufisadi dhidi yake kupitia ndani ya CCM na upande wa vyama vya upinzani.
Lowassa ambaye ni Mbunge wa Monduli alielezea historia ya neno ‘ufisadi’ akisema lililetwa na CHADEMA kupitia mkutano wa Mwembeyanga na kuwataja viongozi 11 wa CCM akiwamo yeye kwa ufisadi.
Mwanasiasa huyo anasema, katika tamko hilo la CHADEMA, alijumuishwa katika orodha ya mafisadi akihusishwa na uamuzi wake wa kuuvunja mkataba wa City Water ambao hata hivyo baadaye serikali ilishinda kesi katika Mahakama ya Kimataifa ya usuluhishi wa mizozo ya uwekezaji. Hapa napo kuna swali; kwa nini tunang’ang’ana na RICHMOND haya mengine hatuyaoni? Kwa nini serikali ilishinda kesi hiyo? Mkataba huo wa city water ulivunjwa na Lowasa.
Anasema ni jambo la ajabu kwamba viongozi wa CCM walilidaka neno hilo na kuanza kulitumia kuwashambulia wenzao akiwamo yeye katika mambo ambayo hayakuwa na ukweli.
Hapa tunahitaji ushahidi wa ukweli kutoka kwa wale wanaomtuhumu kwa ufisadi. Siku zinasonga mbele huku ukimya ukeindelea kutawala
Lowassa alizidi kukana tuhuma za ufisadi dhidi yake na kudai kuwa kujiuzulu kwake ni suala la kawaida kwenye ulingo wa kisiasa kama njia mojawapo ya kuonyesha dhana nzima ya uwajibikaji.
“Nilijiuzulu kuwajibika kwa ajili ya kuilinda serikali yangu na kwa heshima ya chama changu, sasa kwanini leo nahukumiwa kwa jambo hilo, tena natukanwa na wana CCM wenzangu na si wapinzani nchi nzima kwamba mimi eti fisadi?,” ananukuliwa akihoji Lowassa.
Hapa jibu la kujiuzulu kwake analiweka wazi na kuonyesha busara zake katika kulinda heshima ya chama chake. Wale wanaomtukana na kumwita fisadi si ndio wale waliompaka matope katika kashfa hiyo ya ufisadi?
Lowassa pia alilimulika zoezi zima la kujivua gamba na uhalisia wake ulivyokuwa hadi ulivyotumiwa. Lowassa aliipongeza NEC kuridhia ombi la Kamati Kuu ya chama hicho (CC) kwamba suala la mageuzi ndani ya CCM maarufu kama kujivua gamba lirejeshwe katika kamati hiyo ili lifanyiwe kazi kwa taratibu za kawaida za kinidhamu baada ya wahusika kukataa kuachia nafasi zao.
“Mwenyekiti kwanza napongeza uamuzi huu wa kurejesha jambo hili katika taratibu za kawaida, lakini napenda kufahamu kwa miezi saba nimetukanwa nikiitwa fisadi, watu wamezunguka nchi nzima kwa fedha za chama wakinitukana, hivi hatukujua kwamba kuna kamati hizo za maadili?” Lowassa ananukuliwa akihoji.
Lowassa alinukuliwa akiwataja Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Tanzania Bara, John Chiligati, kwamba wamekuwa wakitukana watu ovyo kwa fedha wanazopewa na CCM.
“CCM ninayoifahamu ni ile inayotenda haki na hakiwezi kumtuhumu mtu hadharani bila ushahidi kama walivyofanya Chiligati na Nape na kwa mujibu wa kanuni ni vibaya kumtuhumu bila vikao vya maadili ya chama,” alisema.
Hao waliotajwa hapo mpaka sasa hawajaleta ushahidi wa kile walichokuwa wakikihubiri kwa mbwembwe nyingi.
Na kuhoji, Nape anapata wapi ‘moral authority’ (uhalali wa kimaadili) wa kumtuhumu yeye kwa ufisadi hata kudai kwamba amekipotezea heshima chama hicho wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka jana.
Anafafanua, matokeo ya kura alizopata rais na yeye mwenyewe katika Jimbo la Monduli unazidi asilimia 89 na kwamba wakati yeye (Lowassa) na wengine wakipambana kukijenga na kukipigania chama chao kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu, Nape na wanasiasa wengine wanaomshambulia walikuwa katika harakati za kusajili Chama Cha Jamii (CCJ).
Kwa nini wananchi wake wanamkubali na kumpa ushindi huo wa kishindo?
Kwa nini kundi linalomchafua halijakanusha tuhuma za kusajili chama ndani ya uanachama wa chama kingine? Huu ni uthibitisho kuwa kundi hilo linacheza rafu za kisiasa.
Hayo ni maneno mazito sana kuwahi kutolewa na Lowassa ambapo mimi na wewe tungetamani kuyasikia ‘live’ isipokuwa tumeishia kuyaona kupitia vyombo vya habari kama ambavyo mimi nilivyoyanukuu kupitia baadhi ya vyombo vya habari vilivyoandika Novemba 25. Imenilazimu kunukuu taarifa hiyo kwa ufupi sana kutokana na kuwa ndio msingi mkuu wa makala hii.
Lowassa alitumia takribani dakika 10 kutoa madukuduku ya watu ambao walikuwa na mitazamo hasi dhidi yake kwa kuelezea ukweli mtupu wa mambo ulivyo ambao umezua gumzo na kumjengea heshima kubwa ndani ya jamii.
Watu walio wengi walikuwa na mtazamo duni wa kuamini kuwa eti Lowassa ndiye aliyeileta na ndiye mmiliki wa kampuni ya Richmond nchini. Hapa kundi la aina hii ya watu bado wengi na mtizamo wao usio makini.
Watu hawa wamekosa uweledi wa ufahamu kuwa kampuni ya Richmond iliingizwa nchini kwa mara ya kwanza kabisa na huyu huyu Waziri wa Afrika Mashariki, Samueli Sitta kipindi hicho akiwa Mkurugenzi mkuu wa kituo cha uwekezaji nchini (TIC). Kama namsingizia ajitokeze kukanusha hili.
Kama huyu ndiye aliyeileta kampuni ya RICHMOND, kwa nini tuhuma hizi anabeba Lowasa? Kwa nini hakujitokeza kukanusha?
Iweje leo hii umiliki wa kampuni ya Richmond ihusishwe na Lowassa? Huu ni upotoshaji mkubwa usio na tija kwa taifa.
Wapo watu wengine wanasema kuwa Lowassa alishiriki kwa asilimia 100 katika kuipa zabuni kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond.
Ukiachilia tawala za kifalme, binafsi sijapata kuona serikali yeyote ile duniani ambayo Waziri mkuu wake anafanya kazi pasipo kuwashirikisha watendaji wake wa chini ama mabosi zake ambao ni Rais ama Makamu wa Rais.
Hata huyo waziri mwandamizi tu ni lazima kila jambo analolifanya awashirikishe watendaji wake wa chini ama ngazi za juu, iweje kwa waziri mkuu lishindikane kufanyika hilo? Kwa mujibu wa kauli ya Lowassa anadai aliishtukia na mapema yake hili lidudu Richmond na akataka kulitupilia mbali, lakini bosi wake akamkataza kufanya hivyo, ulitegemea yeye (Lowassa) angefanyaje kama si kumsikiliza bosi wake? Watu wenye vichwa vigumu kuelewa bado wanahoji kuhusu hili.
Tunaambiwa kuwa kuna kundi la makatibu wakuu (ambao kicheo ni watendaji wa chini ya waziri mkuu) lilisharidhia mchakato wa kuipa zabuni Kampuni ya Richmond, kwa mantiki hiyo, iweje leo hii zigo zima la sakata hili aangushiwe Lowassa na hata kufikia hatua ya kumuita fisadi? Hii si sawa kabisa!
Halikadhalika kuna kundi lingine la watu ambao wanaamua kujipa mamlaka ya kumuita Lowassa ni fisadi kutokana na kitendo chake cha kuamua kujiuzulu wadhifa wa uwaziri mkuu.
Watu hawa wanajidhihirisha kuwa ni wepesi sana kisiasa kutokana na kushindwa kutambua ya kuwa Lowassa alijiuzulu wadhifa wake kutokana na kupisha dhana nzima ya kuwajibika kisiasa “political responsibility” ichukue mkondo wake kutokana na makosa yaliyofanywa na watendaji wa chini – kama sehemu mojawapo ya aina ya kuwajibika kisiasa. Jambo hili si geni, linatokea kwa kiongozi mwadilifu. Hata Mwinyi aliwahi kujiuzulu lakini baadaye akawa rais.
Hali hiyo ya makosa hayo kufanywa na wataalamu wa Tanesco na wizara yalisababisha wakubwa wao kimadaraka ambao ni Edward Lowassa aliyekuwa Waziri Mkuu na mawaziri wengine wawili ambao ni Ibrahimu Msabaha na Nazir Karamagi kuamua kujiuzulu kutokana na uzembe uliofanywa na maofisa wao wa chini.
Lowassa hakujiuzulu kwa sababu yeye ndiye aliyehusika katika hili au eti alikuwa na maslahi yake binafsi bali Lowaassa aliamua kubeba msalaba kwa kuchukua dhamana ya kuwajibika kisiasa “political responsibility” kwa kuiokoa serikali isiendelee kusurubiwa na Wabunge kwa masilahi ya Serikali ya Awamu ya Nne na chama chake CCM.
Baadhi ya watu wanajaribu kuupindisha ukweli kwa kufananisha tukio la kujiuzulu kwa Lowassa ni kashfa la ufisadi wa Richmond, lakini wanasahau ya kwamba Lowassa aliamua kujivua gamba si tu kwa kujua nini maana ya kuwa kiongozi bali hata pia kwa kuifahamu vyema dhana nzima ya utashi wa kuwajibika kisiasa ulivyo.
Kitendo cha Lowassa kuamua kujiuzulu hakimvui heshima yake aliyokuwa nayo hapo awali. Na haijawahi kutokea duniani kokote kule kwa kiongozi kuamua kuchukua dhamana ya kisiasa kwa kuwajibika kisiasa eti maana yake amepoteza sifa za kuwa kiongozi tena, sijapata kuona.
Suala zima la kuamua kuwajibika kisiasa si geni hapa nchini kutokea. Mathalani, Mwaka 1977 kulianzishwa operesheni kali ya kuwasaka wanaosadikiwa walikuwa ni wauaji na wachawi ambapo watu kadhaa walikamatwa, wakawekwa ndani na kupewa mateso makali, yaliyosababisha vifo vya baadhi ya watu. Operesheni hiyo iliyoendeshwa katika mikoa ya Mwanza na Shinyanga ilisadikiwa kufanywa na maofisa wa kiserikali.
Makosa hayo yaliyofanywa na baadhi ya maofisa wa kiserikali yalisababisha mabosi wao ama wakubwa wao kimadaraka ambao ni Mzee Alhaji Ali Hassan Mwinyi aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Peter Said Sioverwa (kwa sasa ni Marehemu) aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Usalama wa Taifa; bila ya kuwasahau waliokuwa wakuu wa mikoa wa Mwanza na Shinyanga, Peter Kisumo na Marco Mabawa (marehemu) walijiuzulu kutokana na vitendo vya kikatili vilivyofanywa na maofisa wa serikali waliokuwa chini yao.
Hapa mzee Mwinyi aliamua kuwajibika kwa niaba ya makosa yaliyofanywa na maofisa wa ngazi ya chini yake. Yaani makosa wafanye watu wengine ama maofisa wa ngazi ya chini lakini mkubwa wao (mzee Mwinyi) anaamua kubeba msalaba wao, kwa niaba yao. Kitendo hicho kinajulikana kama kuchukua wajibu wa kisiasa yaani “political responsibility” kwa lugha ya kitaalamu na kisomi zaidi.
Makosa walifanya wengine na mzee Mwinyi akaamue kuwajibika kwa niaba ya wengi, kitendo hicho kilimjengea heshima kubwa hadi Mwalimu Nyerere kwa mwaka ule ule kuamua kumteua kuwa Balozi wa Tanzania nchini Misri; baada ya miaka mitano tu alirudi kwenye Baraza la Mawaziri lile lile, chini ya rais yule yule akiwa Waziri wa Maliasili na Utalii (1982), Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (1983); hatimaye alikuja kuwa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (1984) na baadaye Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania (1985 – 1995).
Kama iliwezekana kwa mzee Mwinyi iweje ishindikane tena kwa Lowassa kuendelea kuwa kiongozi tena?
Pia kuna mzee John Malecela ambaye alilazimishwa kujiuzulu nafasi yake ya uwaziri mkuu baada ya mzee Mwinyi kuvunja Baraza lake la Mawaziri kutokana na waziri mkuu wake kutokumshauri vyema rais wake katika kashfa ya OIC na ile ya kuanzishwa kwa Serikali ya Tanganyika ndani ya Muungano.
Lakini ni Mzee Malecela huyo huyo alikuja kuwa makamu mwenyekiti wa CCM katika kipindi chote ambacho mzee Mkapa alikuwa mwenyekiti wake.
Si hao tu, pia kuna Abdallaah Natepe ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani aliamua kuwajibika kisiasa kutokana na sakata la mahabusu waliokuwa wakituhumiwa kwa uhaini katika kundi la kina Uncle Tom au Thomas Rugangira kutoroka wakiwa chini ya ulinzi wa maofisa wa magereza.
Haikuwahi kutokea si kwa mzee Mwinyi, Mzee Malecela wala Natepe kuwahi kusikia vikao vya CCM ama viongozi wa CCM wakimwambia waondoke ndani ya chama kutokana na kashfa zilizowakumba na hatimaye kuamua kuwajibika kisiasa kama ambavyo inavyotokea kwa Lowassa leo hii.
Historia inajibainisha yenyewe kwamba watu makini wanaojitambua wa sampuli kama ya Lowassa hawachelei kurejea nafasi zao za hapo awali na ujio wao huwa ni wa kishindo kikubwa na hicho kishindo ndicho haswa kinachowatia viwewe wale mahasimu wake kisiasa kutokana na kuona wazi wazi kushindwa kuhimili historia ya utendaji kazi wa Lowassa unaotambulika na kukubalika ndani ya jamii.
Sote tumeshuhudia utendaji wa Lowassa kwa nyakati zote tangu mwaka 1975 kuanzia ubunge wa taifa hadi hili leo Mbunge wa Monduli kwa kipindi chote hicho anaweza kufanya mambo yanayoonekana kwa macho ambapo kwa namna moja ama nyingine yataendelea kutunufaisha sisi tuliopo na vizazi vijavyo.
Miaka ya nyuma elimu ilitolewa kwa watu wachache mno, hali iliyopelekea taifa kuwa na wasomi wachache (hafifu) mno. Hii inasababishwa na uchache na uhaba wa shule za mzingi na sekondari.
Lakini kwa ujemedari, ushupavu na nia ya dhati ya Lowassa alipigana vilivyo na suala hili hali iliyopelekea ongezeko la shule nchini Lowassa hakuwapa nafasi ya kupumua wakuu wa mikoa na wilaya katika ujenzi huu wa shule za kata.
Hali hii ilipelekea ongezeko kutoka 14,257 mwaka 2005 hadi 15,816 mwaka 2010 ambalo ni sawa na ongezeko la wastani wa shule 1559 hadi iliyopelekea wanafunzi kuongezeka kutoka 7,541,208 hadi 8,419,305. Jamani, haya yote tusisahau ni matunda ya kazi yake Edward Lowassa.
Kwa upande wa shule za sekondari mwaka 2005 kulikuwa na shule 1,202 zilizojengwa tangu uhuru ambapo leo hii kuna jumla ya shule 2,171. Lile lengo la kuwa na sekondari moja kwa kila kata limetimia ambapo pia kuna baadhi ya kata zina shule zaidi ya moja.
Ongezeko hilo la shule limewezesha idadi ya wanafunzi wanaosoma sekondari kuongezeka kutoka 524,325 mwaka 2005 hadi 1,638,669. Kazi hii nzuri ilifanyika ndani ya kipindi kifupi tu, nani kama Lowassa?
Watanzania hawataki wamsahau Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere si tu kwa kutupatia uhuru bali hata kwa kuhakikisha ujenzi wa Muungano, umoja, upendo huku akipinga vikali ukabila na udini baina yetu.
Ama Edward Sokoine hata kaa asahaulike na Watanzania si tu kupinga na kupambana na wahujumu uchumi bali pia ni kwa kuhakikisha uwepo wa haki na usawa ndani ya jamii.
Mathalani pale alipohakikisha usimamiaji wa ugawaji wa chakula kwa kila kaya ambapo kila kiongozi husika alipewa daftari la kuandika jinsi, wanavyogawa chakula. Hali hii iliondoa ubaguzi upendeleo ambapo kila mtu alinufaika na kufurahia zoezi na utaratibu huu uliowekwa na Sokoine.
Vinyo hivyo Watanzania haswa wale wa kanda ya ziwa hawatakaa wamsahau Lowassa katika maisha yao. Hali hii ilitokana na uthubutu wa kuhoji uhalali wa maji ya ziwa Victoria kwenda Misri kupitia Suez Canal wakati wa Kanda ya Ziwa hawana moja.
Lowassa alikuwa kiongozi wa kwanza katika nchi za maziwa makuu kuvunja mkataba huu kongwe wa wakoloni uliotoa mamlaka ya kuamua matumizi ya maji hayo kwa nchi ya Misri wakati maji hayo chanzo chake ni nchi za maziwa makuu Tanzania ikiwamo.
Ni kutokana na ujasiri huo wa Lowassa wa kuamua kuvunja mkataba huo wa kikoloni, sasa wananchi wa Mwanza, Shinyanga na Kahama wanafaidika na maji ya ziwa Victoria kwa matumizi mbalimbali mradi uliogharimu zaidi ya sh bilioni 200 lakini una manufaa kwa vizazi na vizazi.
Achilia hilo, pia tusisahau Lowassa alipokuwa Waziri wa Ardhi alisimama kidete pale alipogundua halmashauri ya jiji wamempa mfanyabiashara eneo la Mnazi Mmoja.
Lowassa hakukubaliana na uamuzi huo na kuamuru wananchi wauvunje uzio wake na mabati alioweka na hivyo eneo la uwanja kurudi kwa serikali na wananchi.
Faida yake ni leo hii eneo hilo limeendelea kubaki wazi kwa huduma wanachi na taifa kwa ujumla. Eneo hilo linatumika kwa shughuli na dhifa mbalimbali kama vile mikutano, semina, makongamano.
Tunakumbuka ya kwamba huyu huyu Lowasa aliweza kuvunja mkataba mbovu wa City Water kwa manufaa ya wananchi na taifa kwa ujumla. Hatua hiyo ilipelekea kampuni kurudishwa kwa wazawa wenyewe mpaka hii leo.
Yapo mambo mengi sana ambayo jamii karibu kila kona ya nchi itaendelea kunufaika na ujemedari wake Lowassa hapo ni achilia mbali na suala zima la Lowassa kutokuwa mangimeza kwa kuamua kuzunguka kote nchini kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya serikali kwa vitendo.
Hali hii ilisababisha Baraza la Mawaziri wakuu wa mikoa, wakuu wa Wilaya na viongozi wa Halmashauri za Wilaya na jiji kuwa makini na uchapaji kazi hali iliyoleta mwamko mkubwa na imani ndani ya serikali kwa wananchi wanaowaongoza.
Ndugu zangu, hakuna binadamu aliyemkamilifu kwa asilimia zote isipokuwa Mwenyezi Mungu pekee Lowassa kama binadamu kuna uwezekano mkubwa alikuwa na upungufu wake lakini si mtu wa kufanya hayo anayofanyiwa sasa.
..............daaaah ! naona umemwaga makala, nimeishia njiani lakini naamini unamtetea Lowasa ! Mna moyo wa kiwenda wazimu wazimu hivi ! :A S embarassed:
:brushteeth::brushteeth:
 
Na sie watanzania tuwe tunaangalia mbele jamani,kila siku halikosi jina Lowasa humu ndani!
Hata kama ni mzuri au ni mbaya! Akubali na sie tukubali kama waziri mkuu wa Japan, his time is over and over!kesha zeeka! Nchi inataka viongozi wenye nguvu mana matatizo yetu ni mengi mno!
Kwa nini kunga'ng'ania mababu? Cheki US,UK,France,etc then cheki Kenya (75), Uganda(71),Zimbabwe(88),Zambia(72),etc mababu vs hali za nchi!!

Kila enzi na wakati wake mie nampenda ila anapendeza kuwa mzee wa Kanisa
Lowassa anakumbukwa kutokana na ombwe la uongozi lililopo hivi sasa.
 
Kwa hiyo unataka kutuambia LOWASA ni kiongozi REACTIVE na sio PROACTIVE.

  • kawa waziri mkuu kwa miaka mingapi.?
  • Akiwa waziri mkuu migomo mingapi imetokea na nini kilifanyika? Walimu, madaktari,etc
  • Lowasa Akiwa waziri mkuu amesaidia nini au alifanya kufanya ajira na kazi za watendaji zinalipa zaidi na maslahi makubwa kuliko za siasa ?.....
Tanzania inataka kiongozi PROACTIVE wa kuzuia matatizo kabla hayajotea na sio wanasiasa wa kutafuta umaarufu kwenye migomo na misiba.

Sasa ebu tuambie engekuwa Lowasa nini kingefanyika
Kwa kuwa yeye ni mtoa maamuzi magumu angeagiza madaktari kutoka marekani na kuwalipa mara tano ya wanachodai madaktari wa kibongo:behindsofa:
 
........................hebu tupe CV ya utandaji wako na wewe !! maana umekalia kusifia wanaume wenzio tuu ! au "Huntha" wewe ? :A S embarassed:

huu mgomo ni wa kiutendaji zaidi, hatutaki siju mnyika kanya kile au lowasa kameza hiki! Tunataka majibu yaliyo kiutendaji zaidi,hatutaki ahadi! Huwezi ahidi eti utanunua dawa bajeti ikiruhusu.
 
Mgomo wa Madaktari umeanza tangu zamaniiiiiii!!!!! huu ni mgomo moto na mgomo baridi upo muda mrefu roho za watu zimeteketea sana! Tangu Lowassa akiwepo na hakutoa msaada wowote, tuache uzandiki jamani,
 
Mgomo wa Madaktari umeanza tangu zamaniiiiiii!!!!! huu ni mgomo moto na mgomo baridi upo muda mrefu roho za watu zimeteketea sana! Tangu Lowassa akiwepo na hakutoa msaada wowote, tuache uzandiki jamani,

Huo wa enzi ya Lowasa hatukuusikia, tunajadili huu wa sasa.
 
Back
Top Bottom