Mgomo wa Madaktari hautaisha kwa vitisho na Dola; ni kwa Makubaliano tu!

Mwalimu Nyerere wakati akihutubia mkutano wa wafanya kazi siku ya mei mosi kule Mbeya, aliwambia unganeni katika kudai haki zenu kwani hakuna mtakachopoteza bali minyororo yenu, sawasawa na walivyofanya madaktari wetu katika baadhi ya hospitali hapa nchini. Na kawaida migomo duniani kote huwa ni hatua ya mwisho ya mfanya kazi katika kudai haki yake anayodhulumiwa endapo njia nyingine zote zimegonga mwamba. wahenga walisema mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Sasa watanzania tunashuhudia sakata ambalo wasomi wetu waliopewa dhamana ya roho za watu mahospitalini wamesitisha huduma na serikali iliyopewa dhamana ya maisha bora ya watanzania inakosa ufumbuzi wa tatizo hili kwa takribani zaidi ya wiki sasa! hii ni ajabu na aibu ya karne miaka 50 ya uhuru. wagonjwa wanakufa mahospitalini kwa kukosa huduma, hii si haki kabisa kwa serikali iliyokula kiapo cha kuwalinda na kuwatumikia watu wake. Hivi kweli tatizo la msingi liko wapi, nani anastahili asulubiwe katika hili; serikali au madaktari? Kwanini tunafika mahali hapo kama nchi, serikali na madaktari kutunishiana msuri maana mwisho wa siku watanzania wanyonge wasioweza kujighalamia matibabu katika hospitali za binafsi za madaktari hao wenyewe ndio tunaoumia. Kwanini serikali hilo hamlioni! Ni wazi kwamba kazi za madaktari na wauguzi ni ngumu zinazohitaji wito, moyo na kujituma lakini pia siyo kazi ya utawa ile. Hospitali si kanisa wala msikiti. Kama madai yao yanalenga kuboresha huduma wanazozitoa kwanini wasisikilizwe mapema katika hatua za mwanzo kwa ngazi ya uongozi wa chuo ikizidi sana basi wizara husika. Tatizo la nchi yetu ni umangi meza unaotokana zaidi na uteuzi wa viongozi ktk nafasi ambazo si za taaluma zao. Hii nayo ni issue! Lakini kama nchi, tumeutumia wapi msamaha wa madeni ya nchi hisani. Kila siku serikali inalia haina pesa, ni lini basi itakuwa nazo ili watanzania tupumue maana maisha tunayoishi sasa katika uongozi wa awamu ya nne ni kama tupo ICU. Awamu ya tatu pia wimbo ulikuwa uleule, serikali haina pesa! sawa.. lakini Radar ikanunuliwa kwa mabavu, na pia ndege ya rais mtarajiwa ikanunuliwa hata kama haikujulikana kama huyo rais ajaye angekuwa ni kutoka chama gani lakini ilinunuliwa pamoja na kwamba manunuzi hayo yalipingwa vikali sababu kulikuwapo na mahitaji mengine muhimu ya kitaifa likiwamo la huduma ya afya na elimu ambaya kwa kiongozi mwenye uzalendo, ndege ya rais isingekuwa kipaumbele cha taifa! Kumbuka pia katika lile sakata la serikali na chama cha...wafanyakazi nafikiri (serikali vs Mgaya - maarufu kama mbayuwayu), serikali ilipigilia msumari kabisa kwamba haikuwa na uwezo wa kulipa nyongeza ya mishahara hivyo kwamba anayekusudia kugoma ni bora aache kazi kabisa maana isingesaidia sababu pato la taifa halikutosha kufanya hivyo. Sasa ajabu ikawa kwamba wakati wa karibia na uchaguzi pesa zilipatikana nje ya lile pato la taifa na kuingizwa ki-aina katika akaunti za wafanyakazi! zilitoka wapi - fuatilia mwenyewe ni haki yako kujua sababu ni mlipa kodi. Sasa hii inatufundisha nini! Tukija ktk habari ya posho za wabunge, hiyo haina wabunge kugoma ili waipate maana hata mawaziri wote ni wabunge. Ila inapokuja kwa walimu, madaktari na wauguzi hapo ndipo huwa na tatizo miaka nenda rudi. Sasa hii ndio wanaita kula na kipofu kisha ukamgusa mkono. Watanzania tunashuhudia mengi lakini tunafumbia macho ili siku ipite wasiojua magumu tuliyobeba mioyoni waendelee kutuita nchi ya amani na utulivu. amani iko wapi wakati mioyo ya watanzania wengi imegubikwa na hofu ya maisha? mfumuko wa bei utafikiri upo kwenye promotion, bei za vyakula tishio, mafuta na umeme sasa ni anasa. EWURA hii kwa maoni yangu haitusaidii watanzania, kwanza ni mzigo kwetu sababu tunalazimika kumlipa sisi kwa kila manunuzi ya umeme kwa mwezi wakati mwajiri ni serikali. kwa maana nyingine ombi lolote la Tanesco la kutaka kupandisha garama za umeme kwake ewura ni ulaji hivyo akipelekewa atapunguza tu kiwango lakini kukataa ni ngumu. Nchi yetu sasa inahitaji viongozi makini na wabunifu wenye mtazamo wa mbali ili wanusuru kizazi hiki vinginevyo, nahofu tunaweza kuwa kama Rwanda kwanza ili baadae kupata viongozi wenye akili kama Rais Kagame. Huyu sasa ndiye Rais anayefunika marais wote barani Afrika kwa uongozi makini which is a determinant of his I.Q. Kiongozi mwadilifu na mzalendo anatakiwa aione Tanzania ya miaka 35 inayokuja jinsi inavyofanana ikiwa jangwa tupu bila uoto wake wa asili, bila misitu wala maji ya mito, wala wanyama na ndege tunaojivunia sababu mafuta na umeme kila vikipanda bei tunaegemea nishati ya kuni na mkaa maadamu vibali vinatolewa vya kuangamiza misitu, maisha yanaenda! mkaa wa mawe tunao tele ungeweza kuokoa mazingira kwa kuhamasisha biashara ya usambazaji wake katika miji yote nchini kwa msamaha wa kodi lakini kama yupo mwenye wazo hilo basi tayari ni mradi wa fisadi wa kuuza nje ya nchi. Tanzania itajengwa na wenye moyo safi. Madaktari wasikilizwe bila vitisho ili watutumikie sisi tusiotibiwa nje ya nchi. Lakini ombi langu kwa watanzania wote mtakaopata bahati ya kutoa maoni juu ya mswada wa katiba mpya ni muhimu kufuta fursa ya viongozi kutibiwa nje ya nchi. wote tutibiwe hapahapa na watoto wao wasome shule hizihizi ili twende sawa ndio itakuwa suluhisho la migomo. Jambo lingine muhimu, pingeni kwa garama yoyote sheria ya uraia wa nchi mbili. Haina faida yoyote kwa mtanzania wa kawaida bali nahisi inalenga kutoa mwanya wa mafisadi waliokwisha limbikiza nje utajiri wa nchi yetu kwa uficho, sasa waende kuhalalisha na hivyo tushindwe kuwabana kisheria pindi tutakapopata serikali makini. Kumbuka sio jambo rahisi kupatiwa uraia nchi yoyote ughaibuni bila wewe kuwa milionea au kuwa umeishi kule miaka mingi au lah, uwe mkimbizi wa kisiasa. Sasa nambie ni watanzania wangapi wa kawaida wenye uwezo huo kama sio deal la wachache wenye nazo.
 
Ni ukweli usiotiliwa shaka kuwa vifo vya wagonjwa na taabu wanazopata wagonjwa watanzania wenzetu ni matokeo ya ombwe la uongozi ambalo mie binafsi naita kama ni janga la kitaifa. Tatizo la viongozi wetu ni kuwa wanatumia mda mwingi kushughulikia matokeo ya matatzo na wala si vyanzo vya matatzo. Hivi hii ndo Tanzania tuitakayo watanzania wenzangu? Hoja za Mh Pinda hazina mashiko coz hao madaktari wanajeshi kamawapo ,kwanini tunaupungufu wa madaktari wilayani? Huko jeshini tunajua fika kuwa wanamajukumu ya kuwahudumia wagonjwa,je nafasi zao zitajazwa na akina nani? UKITAKA KUTAMBUA DIAGNOSTIC SKILLS KWA WATAWALA NI PALE TU NCHI INAPOKUWA KWENYE SOCIAL UNREST. Wito wangu kwa madokta ni kuwa bora mgomo unaotafuta haki na ustawi wa taaluma kuliko amani na ustaarabu unao dharilisha na kupuuza utu wa binadamu. MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU BARIKI HARAKATI.
 
[QUOTE=dkn;32372.[/QU Ndugu,nakuhakikishia uwezo wa kuwaridhisha madaktari upo,na hiyo pesa ni ya kawaida tu,hii professinal is the most sophisticated! Zingatia taaluma yako,linganisha na hao,acha dharau ndugu,km ungeweza na wewe si ungeweza kufanya,i am sure taaluma ulizotaja hapo ni mismarch kwa mbali,pamoja n kukujuza kwamba hata huyo Pinda anatibiwa nje,na wewe unalalama tu unajua kampuni wako inalipa bima ya afya kiasi gani huko unakotibiwa? Ambayo siyo ya serikali ambako wanagoma! Mkuki kwa nguruwe,kaa ukijua,mapinduzi ya ukweli sharti damu imwagike!
 
IQ yao ishaonekana iko chini. rejea vitisho vya PM,rejea habari za kupikwa juu ya mgomo huo zinazorushwa na baadhi ya vituo vya TV vikiongozwa na tbc
 
Mungu awasimamie wale wote wanaoongoza harakati za ukombozi wa mfanyakazi mzalendo wa taifa hili. Tangu nizaliwe ni malalamiko tu ya wafanyakazi dhidi ya mwajiri wao hawakuwahi kusimama kidete kudai haki zao za msingi kama ninavyoshuhudia leo,huenda hili la madaktari likaleta nuru kwa kila sekta. Hili ni pambazuko jipya lenye fikra mpya zenye kutenda kile zinachonena.
 
Watanzania wenzetu wanakufa bila sababu yoyote, ushabiki wa kisiasa uachwe katika maisha ya watu. .
Acha mawazo ya kuharisha.
Chama gani imewaambia madktari gomeni?
CHADEMA?
CUF?
CCK?
Kitakachofuata hapa ni ku-lebo kuwa chama fulani ni chama cha madaktari baada ya ukabila, ukanda, udini kushindikana.
 
Hii thread ikiunganishwa na nyingine watu watashindwa kupata huu uchambuzi mzuri!!!

Ukweli ni kuwa madaktari wameanza na 3,000, 000 ili wakienda kwenye bagaining walau wanaweza kupata 1.5 m. Sasa serikali inaanza kupoliticise huu mgomo kwa vile wanajuwa ukuiendelea sana unaweza ukabadilika na kuwa wa kisiasa. Kumbuka Tunisia revolution ilianzishwa na machinga moja tu.

Twist nyingine inakuja, serikali inajua kuwa kama itakubali madai yote ya madaktari ............ next watakuwa nurses.................... then Lecturers na baada ya hapo makunguru (Waalimu). Kwa hiyo serikali itakomaa na kujaribu kuwamaliza nguvu taratibu. Nafikiri by the end of next week Rais atakuwa ameshawaita wazee wa CCM kupiga propaganda.

All in all posho ya wabunge imezua mambo!! Pamoja na madai ya madaktari kuwa ya msingi.... Je serikali ina pesa za kumudu hivyo viwango??
mkuu serikali nzima kweli imeshindwa busara za kuweza kuongea na madaktari hadi itoe vitisho? hii ni aibu kubwa kwa watawala wetu.
 
Mwalimu Nyerere wakati akihutubia mkutano wa wafanya kazi siku ya mei mosi kule Mbeya, aliwambia unganeni katika kudai haki zenu kwani hakuna mtakachopoteza bali minyororo yenu, sawasawa na walivyofanya madaktari wetu katika baadhi ya hospitali hapa nchini. Na kawaida migomo duniani kote huwa ni hatua ya mwisho ya mfanya kazi katika kudai haki yake anayodhulumiwa endapo njia nyingine zote zimegonga mwamba. wahenga walisema mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.

Sasa watanzania tunashuhudia sakata ambalo wasomi wetu waliopewa dhamana ya roho za watu mahospitalini wamesitisha huduma na serikali iliyopewa dhamana ya maisha bora ya watanzania inakosa ufumbuzi wa tatizo hili kwa takribani zaidi ya wiki sasa! hii ni ajabu na aibu ya karne miaka 50 ya uhuru. wagonjwa wanakufa mahospitalini kwa kukosa huduma, hii si haki kabisa kwa serikali iliyokula kiapo cha kuwalinda na kuwatumikia watu wake. Hivi kweli tatizo la msingi liko wapi, nani anastahili asulubiwe katika hili; serikali au madaktari? Kwanini tunafika mahali hapo kama nchi, serikali na madaktari kutunishiana msuri maana mwisho wa siku watanzania wanyonge wasioweza kujighalamia matibabu katika hospitali za binafsi za madaktari hao wenyewe ndio tunaoumia. Kwanini serikali hilo hamlioni!

Ni wazi kwamba kazi za madaktari na wauguzi ni ngumu zinazohitaji wito, moyo na kujituma lakini pia siyo kazi ya utawa ile. Hospitali si kanisa wala msikiti. Kama madai yao yanalenga kuboresha huduma wanazozitoa kwanini wasisikilizwe mapema katika hatua za mwanzo kwa ngazi ya uongozi wa chuo ikizidi sana basi wizara husika. Tatizo la nchi yetu ni umangi meza unaotokana zaidi na uteuzi wa viongozi ktk nafasi ambazo si za taaluma zao. Hii nayo ni issue! Lakini kama nchi, tumeutumia wapi msamaha wa madeni ya nchi hisani. Kila siku serikali inalia haina pesa, ni lini basi itakuwa nazo ili watanzania tupumue maana maisha tunayoishi sasa katika uongozi wa awamu ya nne ni kama tupo ICU.

Awamu ya tatu pia wimbo ulikuwa uleule, serikali haina pesa! sawa.. lakini Radar ikanunuliwa kwa mabavu, na pia ndege ya rais mtarajiwa ikanunuliwa hata kama haikujulikana kama huyo rais ajaye angekuwa ni kutoka chama gani lakini ilinunuliwa pamoja na kwamba manunuzi hayo yalipingwa vikali sababu kulikuwapo na mahitaji mengine muhimu ya kitaifa likiwamo la huduma ya afya na elimu ambaya kwa kiongozi mwenye uzalendo, ndege ya rais isingekuwa kipaumbele cha taifa!

Kumbuka pia katika lile sakata la serikali na chama cha...wafanyakazi nafikiri (serikali vs Mgaya - maarufu kama mbayuwayu), serikali ilipigilia msumari kabisa kwamba haikuwa na uwezo wa kulipa nyongeza ya mishahara hivyo kwamba anayekusudia kugoma ni bora aache kazi kabisa maana isingesaidia sababu pato la taifa halikutosha kufanya hivyo. Sasa ajabu ikawa kwamba wakati wa karibia na uchaguzi pesa zilipatikana nje ya lile pato la taifa na kuingizwa ki-aina katika akaunti za wafanyakazi! zilitoka wapi - fuatilia mwenyewe ni haki yako kujua sababu ni mlipa kodi. Sasa hii inatufundisha nini!

Tukija ktk habari ya posho za wabunge, hiyo haina wabunge kugoma ili waipate maana hata mawaziri wote ni wabunge. Ila inapokuja kwa walimu, madaktari na wauguzi hapo ndipo huwa na tatizo miaka nenda rudi. Sasa hii ndio wanaita kula na kipofu kisha ukamgusa mkono. Watanzania tunashuhudia mengi lakini tunafumbia macho ili siku ipite wasiojua magumu tuliyobeba mioyoni waendelee kutuita nchi ya amani na utulivu. amani iko wapi wakati mioyo ya watanzania wengi imegubikwa na hofu ya maisha? mfumuko wa bei utafikiri upo kwenye promotion, bei za vyakula tishio, mafuta na umeme sasa ni anasa. EWURA hii kwa maoni yangu haitusaidii watanzania, kwanza ni mzigo kwetu sababu tunalazimika kumlipa sisi kwa kila manunuzi ya umeme kwa mwezi wakati mwajiri ni serikali. kwa maana nyingine ombi lolote la Tanesco la kutaka kupandisha garama za umeme kwake ewura ni ulaji hivyo akipelekewa atapunguza tu kiwango lakini kukataa ni ngumu.

Nchi yetu sasa inahitaji viongozi makini na wabunifu wenye mtazamo wa mbali ili wanusuru kizazi hiki vinginevyo, nahofu tunaweza kuwa kama Rwanda kwanza ili baadae kupata viongozi wenye akili kama Rais Kagame. Huyu sasa ndiye Rais anayefunika marais wote barani Afrika kwa uongozi makini which is a determinant of his I.Q. Kiongozi mwadilifu na mzalendo anatakiwa aione Tanzania ya miaka 35 inayokuja jinsi inavyofanana ikiwa jangwa tupu bila uoto wake wa asili, bila misitu wala maji ya mito, wala wanyama na ndege tunaojivunia sababu mafuta na umeme kila vikipanda bei tunaegemea nishati ya kuni na mkaa maadamu vibali vinatolewa vya kuangamiza misitu, maisha yanaenda! mkaa wa mawe tunao tele ungeweza kuokoa mazingira kwa kuhamasisha biashara ya usambazaji wake katika miji yote nchini kwa msamaha wa kodi lakini kama yupo mwenye wazo hilo basi tayari ni mradi wa fisadi wa kuuza nje ya nchi. Tanzania itajengwa na wenye moyo safi.

Madaktari wasikilizwe bila vitisho ili watutumikie sisi tusiotibiwa nje ya nchi. Lakini ombi langu kwa watanzania wote mtakaopata bahati ya kutoa maoni juu ya mswada wa katiba mpya ni muhimu kufuta fursa ya viongozi kutibiwa nje ya nchi. wote tutibiwe hapahapa na watoto wao wasome shule hizihizi ili twende sawa ndio itakuwa suluhisho la migomo. Jambo lingine muhimu, pingeni kwa garama yoyote sheria ya uraia wa nchi mbili. Haina faida yoyote kwa mtanzania wa kawaida bali nahisi inalenga kutoa mwanya wa mafisadi waliokwisha limbikiza nje utajiri wa nchi yetu kwa uficho, sasa waende kuhalalisha na hivyo tushindwe kuwabana kisheria pindi tutakapopata serikali makini. Kumbuka sio jambo rahisi kupatiwa uraia nchi yoyote ughaibuni bila wewe kuwa milionea au kwanza uzamie upate sifa ya kuishi kule miaka mingi au lah, uwe ni mkimbizi wa kisiasa.

Well said but nani wa kumvisha paka kengele,watanzania wako kimya kuwasaidia madaktari,wengine ndio kwanza wana furahia kusikia wanavyotaabika.
 
Watanzania wenzetu wanakufa bila sababu yoyote, ushabiki wa kisiasa uachwe katika maisha ya watu. Kama nilivyosema kwenye reply moja hapa JF, madai ya madaktari hayawezi kufanyiwa kazi kwa siku moja au hata mwezi mmoja, serikali inahitaji kukaa chini kuangalia uwezekano wa kupatikana hela au tumesikia kuna mahali kuna hela zisizo kuwa na budget? Tunawasihi madaktari warudi kazini wakati serikali ikijadiliana na uongozi wa madaktari, jinsi siku zinavyoenda ndiyo wagonjwa wanapoteza maisha yao.


Acha ubwege ww, kwani fedha za sherehe ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika zilikuwa kwenye bajeti ipi? au alizitoa baba yako...Crap..
 
yaani PM hataki kujua kitu inaitwa freedom of assembly,ambapo kwa kufanya hivyo anapingana kabisa na human rights

shangaa mkuu, eti mtu kama waziri mkuu aliyesomea sheria na kluijua katiba kwa undani anawapiga watu mkwara kuwa wasikutane popote, hivi huo ubabe na mamlaka ya vitisho hivyo kaitoa kwenye katiba ipi? mbona hata hii katiba tuliyonayo haina kipengele kama hicho? aisee tuna ombwe la uongozi tanzania.
 
na baada ya vitisho hivyo hali imezidi kuwa mbaya bzaidi baada ya huduma za dharura kusitishwa muhimbili na kwingineko japo wanaeneza propaganda za huduma kurejea awali.
 
Hawa madaktari wagome tu hadi kieleweke kwani viongozi wa nchi wanawadhrau sana na ndo maana hata wakiugua hata mafua wanakimblia india kupata tiba af watanzania wanataabika, basi acha madokta wagome ili kama ni kutaabika watz wataabike ili ieleweke kabisa serikali haina msaada kwao na kwamba iko tayari kuona raia wake wakifa.
 
na baada ya vitisho hivyo hali imezidi kuwa mbaya bzaidi baada ya huduma za dharura kusitishwa muhimbili na kwingineko japo wanaeneza propaganda za huduma kurejea awali.
sasa mkwara wa PM kwa madaktari ndo safari ya kifo chake kisiasa, mafukara wanaokufa kwakukosa huduma muhimu za afya kutoka kwa madaktari ndo laana yake.

mkuu sign.. yako imetulia ''.Rather Kill a FRIEND than Risk Missing an ENEMY''
 
Pamoja na kwamba mgomo wa madaktari unaitikisa nchi, wapiga kura ambao kwa 100% ndo wanaotaseka, bado His Exellence anapanga ziara...sometimes back nchi ilikuwa gizani bado His Exellence alienda ziara...Je, huyu jamaa hana priorirty???
 
Hii thread ikiunganishwa na nyingine watu watashindwa kupata huu uchambuzi mzuri!!!

Ukweli ni kuwa madaktari wameanza na 3,000, 000 ili wakienda kwenye bagaining walau wanaweza kupata 1.5 m. Sasa serikali inaanza kupoliticise huu mgomo kwa vile wanajuwa ukuiendelea sana unaweza ukabadilika na kuwa wa kisiasa. Kumbuka Tunisia revolution ilianzishwa na machinga moja tu.

Twist nyingine inakuja, serikali inajua kuwa kama itakubali madai yote ya madaktari ............ next watakuwa nurses.................... then Lecturers na baada ya hapo makunguru (Waalimu). Kwa hiyo serikali itakomaa na kujaribu kuwamaliza nguvu taratibu. Nafikiri by the end of next week Rais atakuwa ameshawaita wazee wa CCM kupiga propaganda.

All in all posho ya wabunge imezua mambo!! Pamoja na madai ya madaktari kuwa ya msingi.... Je serikali ina pesa za kumudu hivyo viwango??

hapo kwenye red ndo msingi mkuu wa kada nyingine za wafanyakazi kudai na wao haki zao.
 
Ni nchi gani inaongozwa na chama ambacho wameshindwa kuvuana Magamba? jaza hapa..................:biggrin:
 
Mods,
Najua mada nyingi zinazowekwa humu zinatolewa ghafla. Sina nia mbaya, Napenda tu kuuliza ni kwa nini Rais wetu asifupishe ziara yake akaja nyumbani kusaidia kutafuta ufumbuzi wa matatizo lukuki yanayoikabili nchi. Watu wanakufa Muhimbili na sidhani kutokuwepo kwake Ethiopia kutahathiri chochote. Mh. Rais, najua unasoma haya maandiko na hata wasaidizi wako wanakuletea hizi taarifa, mbona usirudi nyumbani. Kumbuka hawa wanokufa ndio waliokuchagua na chama chako. Waliwapeni dhamana ya URAIS ili uwalinde. Ungewapa kipaumbele zaidi ya kongamano lolote lile
 
Back
Top Bottom