Mgomo wa Madaktari hautaisha kwa vitisho na Dola; ni kwa Makubaliano tu!

Ccm on the way to damascus
nimeisikiliza hotuba ya waziri mkuu kuhusu mgomo wa madaktari kama mtiririko wa matukio ni ule aliyoeleza waziri mkuu, waziri mkuu ame’missimage mgogoro huo.

kasoro ya 1: yalikuwa ni makosa makubwa kukubali kuongea na madaktari zaidi ya mia nne (400) kwa sababu sio rahisi kupata suluhu ya mvutano katika mkusanyiko wa watu mia nne, yeye angekubali kuongea na wawakilishi.

kasoro ya 2: ni kutoa majibu ya mkato tuu kuwa madai ya nyongeza ya tshs3,000,000/= hayawezekani. Nakubaliana na madai ya nyongeza ya mshahara toka tshs.900,000/= hadi tshs.3,000,000/= ni unrealistic lakini angewauliza hao madaktari wametumia vigezo vipi kufikia ongezeko la madai ya zaidi ya 300%, inawezekana madaktari walijiropokea tu, angewauliza vigezo wangejiona hawana hoja. Pia angewaeleza financial implications za madai yao kitaifa , madaktari ni watu wenye vipaji vya akili ya juu na ni waelewa wangemwelewa. Majibu yaliyotelewa ya mkato hayakuwa ya kutafuta mwanzo wa mazungumzo ya kutafuta mwafaka. Hapa pia ni upungufu wa kutafuta mwafaka.

kasoro ya 3: madaktari pia walitaka walipwe risk allowance, hili lingeweza kutolewa ufumbuzi, wangeambiwa wa classify hizo risks kwa sababu siyo wote wana risk zinazofanana, kukubali hili lingewapa muda wa kutafakari na pia lingeweza kuwagawa na kupunguza makali, hapa sielewi ilipataje kigugumizi . Madaktari pia walitaka walipwe hardship allowance hili pia halina utata, mbona wafanyakazi wengine wanaopelekwa mfano kasulu, kibondo n.k wanalipwa kwanini isiwe madaktari? Hapo waziri mkuu amewapotosha wananchi.

kasoro 4: madaktari walitaka wapewe au wakopeshwe magari, hapa sioni utata. Serikali ingewakopesha kwa awamu na wengine wangelipwa transport allowance, kuna mashirika ya umma karibu yote hapa nchini yanatoa transport allowance kwa wafanyakazi wao kufuatana na vigezo mbali mbali.

kasoro ya 5: waziri mkuu ameshindwa kutoa majibu ya madai ya nyumba kwa madaktari. Naamini madaktari sio vichaa, siamini wangetegemea wapewe nyumba siku ya pili yake. Wangepewa housing allowance ambazo mashirika mengi ya umma hapa nchini wanatoa kwa wafanyakazi wao. Sidhani km ingekuwa mgogoro.

kasoro ya 6. Kwamba madaktari walitaka madai yao yatekelezwe mara moja. Hii tafsiri kwa waziri mkuu ni kama amri au dharau, madaktari walitaka makubaliano sio utekelezaji ufanyike siku hiyohiyo moja, au wajenge nyumba siku hiyo hiyo, hili lingeweza kuongelewa bila viongozi kujiona wamedhalilishwa.

kasoro ya 7: waziri mkuu kugusia maslahi binafsi ya madktari kama yalivyoainishwa kwenye madai yao bila hata kugusa mazingira ya kazi na vitendea kazi kama walivyoainisha kwenye madai yao, hapo waziri mkuu alikuwa na lengo la kuwagombanisha madaktari na wananchi.

mwisho kabisa ni kuwapiga marufuku wasikutane popote. Serikali imewafukuza kazi hii inatosha, wasikutane popote hii inatoka wapi na kwenye katiba ipi, huu ni ufashist.
 
Watanzania wenzetu wanakufa bila sababu yoyote, ushabiki wa kisiasa uachwe katika maisha ya watu. Kama nilivyosema kwenye reply moja hapa JF, madai ya madaktari hayawezi kufanyiwa kazi kwa siku moja au hata mwezi mmoja, serikali inahitaji kukaa chini kuangalia uwezekano wa kupatikana hela au tumesikia kuna mahali kuna hela zisizo kuwa na budget? Tunawasihi madaktari warudi kazini wakati serikali ikijadiliana na uongozi wa madaktari, jinsi siku zinavyoenda ndiyo wagonjwa wanapoteza maisha yao.
 
hapa mnaigiziwa governance maana huko kwenye serikali zao waziri mwenye dhamana na naibu wake wangeshawajibika kisiasa maana kilichotokea ni kinyume na sera ya afya waliyoaminishwa kuisimamia.katibu mkuu na mkurugenzi mkuu wa muhimbili wangejiuzulu au rais awapige bao,lakini waona mauzauza haya?pinda hoi,billali the physicist bubu na dr jmk kakimbilia uswisi kwenye baridi katuachia joto mifukoni,nyumbani na hata hospitalini,twafa
 
Watanzania wenzetu wanakufa bila sababu yoyote, ushabiki wa kisiasa uachwe katika maisha ya watu. Kama nilivyosema kwenye reply moja hapa JF, madai ya madaktari hayawezi kufanyiwa kazi kwa siku moja au hata mwezi mmoja, serikali inahitaji kukaa chini kuangalia uwezekano wa kupatikana hela au tumesikia kuna mahali kuna hela zisizo kuwa na budget? Tunawasihi madaktari warudi kazini wakati serikali ikijadiliana na uongozi wa madaktari, jinsi siku zinavyoenda ndiyo wagonjwa wanapoteza maisha yao.
Hapo kwenye red, Hiyo serikali ilikuwa wapi siku zote?
 
Watanzania wenzetu wanakufa bila sababu yoyote, ushabiki wa kisiasa uachwe katika maisha ya watu. Kama nilivyosema kwenye reply moja hapa JF, madai ya madaktari hayawezi kufanyiwa kazi kwa siku moja au hata mwezi mmoja, serikali inahitaji kukaa chini kuangalia uwezekano wa kupatikana hela au tumesikia kuna mahali kuna hela zisizo kuwa na budget? Tunawasihi madaktari warudi kazini wakati serikali ikijadiliana na uongozi wa madaktari, jinsi siku zinavyoenda ndiyo wagonjwa wanapoteza maisha yao.
idai seli dr.hapigiwi kura.
 
Watanzania wenzetu wanakufa bila sababu yoyote, ushabiki wa kisiasa uachwe katika maisha ya watu. Kama nilivyosema kwenye reply moja hapa JF, madai ya madaktari hayawezi kufanyiwa kazi kwa siku moja au hata mwezi mmoja, serikali inahitaji kukaa chini kuangalia uwezekano wa kupatikana hela au tumesikia kuna mahali kuna hela zisizo kuwa na budget? Tunawasihi madaktari warudi kazini wakati serikali ikijadiliana na uongozi wa madaktari, jinsi siku zinavyoenda ndiyo wagonjwa wanapoteza maisha yao.

Labda utuambie kuwa wewe ndio msemaji wa wizara na serikali...sijui kama tatizo la madaktari ni kupata hizo hela kesho au leo,jifunze masuala ya negotiation,unamdai mtu unaweza ukasema mara moja nataka uniletee pesa yangu,lakini kama mdaiwa akija na lugha nzuri na ya kueleweka manaweza mkaongea na hata wakati mwingine deni kufutwa...suala hapa linaloweza kuwa linawatia hasira madaktari ni kauli za Pinda za kejeli na ubabe...
 
Mr pm atakuwa amekosea,mbona wabunge walipodai nyongeza ya posho hakutoa vitisho,kati ya daktari na mbunge nani anaefanya kazi kubwa .kama ndo hivyo basi kuwe na level moja ya mshahara bila kujal ni mbunge au nani ila kwa kuzingatia ngazi ya elimu aliyonayo mtu husika,kwa mfano km ni std 7 walipwe lak 2 wote ht km ni mbunge,diploma labda iwe ni laki 3 kwa.wote had kwa wabunge walio na dipl then kwa degree labda iwe lak 4.Na kama ikipanda ipande kwa wote hapo hakutakuwa na migomo.
 
Nisaidien jaman vp mgomo umeyeyuka au bado upo?? au ndo kiranja mkuu kachimba mkwala wamelegea hawa jmaa zetu doctz..
 
Serikali haiwezi kupanga mishahara kama unavyofikiria, kwani walimu, polisi etc hawahitaji nyongeza...mishahara inaendana na uchumi wa nchi, hatuwezi kushindana na Rwanda kiuchumi ndiyo maana wanalipa zaidi hapa kuna nini cha zaidi walipwe zaidi? Ndiyo maana mtizamo wangu hii issue siyo ya leo au kesho, wakipewa jibu la YES leo ujue kabisa serikali imeamua kufanya hivyo kupata ufumbuzi lakini haitakuwa kitu sustainable? hela watapata wapi? budget ndiyo hiyo ilishapita, makusanyo ya serikali yamepungua na matatizo kama umeme, hatuuzi bidhaa zetu nje kwa wingi, sasa hela watoe wapi? hapa lazima wakae chini wachumi na wadau wengine kama Wizara ya Fedha, Afya, Utumishi waone kama itawezekana na hii siyo kitu ya kujadili siku 1 hata mwezi. MADAKTARI TUNAWAOMBA MRUDI KAZINI KUOKOA MAISHA YA WATANZANIA WASIO NA HATIA.
 
Angalia post reply zangu, nilisema kama kwenye Pinda ametoa vitisho then negotiation skill yake si nzuri.
 
Inabidi JK aingilie kati mgomo huu kuliko kukaa kimya maana nchi ikikaa hivi ni kama hakuna rais.

Urais siyo kusafiri tu na kutembea na ving'ola bali ni kuwajibika.
 
Pinda angetumia mabavu kupambana na ufisadi ama Jairo ningemwelewa. Mbona ni kwa madaktari tu na Chadema.

Yule ana matatizo sana. Alitaka kulia pale alipojikuta yuko na timu ya wapambe wake tu, wakati Wanaume wametoa nje.
 
Ni nchi gani duniani,wahudumu wa afya hawana matumaini.Jaza............
Wahudumu wa afya hawajapata mishahara kwa miezi kadhaa sasa.Jaza...............
Nchi hiyo inatumia mabavu na kujitangaza ktk luninga kwamba warudi kazini badala ya maongezi ya faragha?Jaza..............
Nchi gani mkuu wake anaponda raha nje huku wananchi hawana huduma za tiba kwa nchi nzima? Jibu............
Nchi gani madaktari wamelazimishwa kurudi kazini lakini wanatoa huduma duni?Jaza............
ONGEZA NA UNAYOYAFAHAMU
 
Mzee Mwanakijiji,Niseme mathlan unakubaliana na madai ya madaktari..mimi siyajui vizuri zaidi ya yale yaliyowekwa hapa JF..nakuomba wewe kama serikali au waziri mkuu ni yapi utakubaliana nayo na yapi hutakubaliana nayo na kwa kufanya nini?. Ili madaktari warudi kazini ni mazingira gani ya kazi utayabadilisha kulingana na madai yao.

Mkandara, nimependakweli swali lako.

Kuna mambo ambayo ni lazima yakubaliwe kwanza mara moja ilimadaktari warudi kazini mara moja na kuelekea kuponya hili jeraha la mgomo. Kwahiyo, kama mimi ningekuwea serikali na kuona mgomo umefika hapa kuna mamboambayo ningeyafanya kumaliza mgomo na kati ya hayo hakuna ambalo lingehusishavitisho, ubabe au nguvu za dola za ‘kamata kamata'.

a. Ningewafuta kazi viongozi watatu wa Wizara yaAfya, Waziri, Katibu Mkuu na Mganga Mkuu. Mgomo huu usingefika hapa kama hawawatatu wangekuwa na hekima na nidhamu ya kuzungumza kwa ukweli na madaktari. Badala ya kuona madaktari niwasumbufu walitakiwa wawe wa kwanza kupigania maslahi yao madaktari. Uamuzi wakuwafukuza ma-interns kwa kukataa kuwaongezea posho wakati siku chache nyumaWaziri Mkuu alihalalisha posho nono kwa wabunge usingeweza kumshawishimwananchi yeyote yule kuwa serikali haina fedha. Walivyoshughulikia mgomo huutoka mwanzo ni aibu kwa mtu yeyote aitwaye kiongozi. Hawa watatu wamepotezaheshima ya madaktari. Hawawezi kuaminika tena. They must go. Hii itawafanyamadaktari waamini serikali inachukulia madai yao kwa umakini mkubwa.

b. Nitaunda negotiation team kati ya madaktari,wauguzi, na serikali ambayo itapewa siku saba kuja na mapendekezo ya kuboreshaposho mara moja wakati timu hiyo pia itakuwa na jukumu la kuandaa policy reviewya sekta ya afya ili mapendekezo yake yaingizwe kwenye bajeti ijayo. Kutangazakuundwa kwa timu ya mazungumzo (ambayo haina viongozi wale watatu waliofukuzwa)kutafanya madaktari warudi kazini mara moja wakati timu yao inafanya mazungumzona serikali na baada ya siku saba, madaktari wataitishwa kupitisha mapendekezoya madaktari na serikali. Wakikubali kwa kura serikali itatakiwa ifanyie kazimambo hayo mara moja.

c. Serikali kufuta tishio lake la kuwafukuza kazimadaktari walioshiriki mgomo na kutochukua hatua yoyote dhidi ya uongozi wawalioitisha mgomo. Hili ni jambo muhimu kwa sababu kuna hisia ya kuabudiwa nakuogopwa na serikali kiasi kwamba serikali kwa vile inaona "imedhalilishwa"inaweza kuja na kisasi – ni tabia ya serikali zote zisizo maarufu duniani.Ukitangazwa mgomo kwisha na wote wamesamehewa kusiwe na kumtaka mtu afutiweleseni au asimamishwe kazi kwa kushiriki mgomo. Endapo serikali itaanzakuchukua hatua dhidi ya madaktari walioshiriki mgomo, basi madaktari wanareserve the right to strike again in protest!

d. Serikali kuonesha kuwa inajali hali inayoonekanaya kujipendelea wenyewe isitishe ongezeko la posho za wabunge na kupunguzaposho zote za serikali kwa kati ya asilimia 50 na 80 na badala yake kuboreshamishahara yote. Siyo tu kupunguza kiasi cha posho bali pia kupunguza aina zaposho zinazotolewa. Serikali ikisitishaposho zilizoongozwa za wabunge ambazo tayari wameanza kuzikomba leo hiiitaonesha iko sensitive na sauti za wananchi.

Haya yakifanyika madaktariwatarudi kwani wataona kweli serikali "inafanyia kazi" madai yao. Lakinikuwaambia ati "warudi wakati tunafanyia kazi madai yao" wakati hakuna hatuahata moja ya serikali kuonesha inafanyia kazi ni kejeli kwa akili za madaktarina za wale wanaowaunga mkono.
 
Kama kawaida ya serikali yetu 'sikivu', wanaburuza punda hadi kwenye mto, wakitumaini kuwa akiona kiboko atakunywa maji kwa lazima!
 
ni nchi gani ambayo ina manufacture walimu instead of training them..na kiongozi wake akijisifu kwa mbwe mbwe na kukenua kama hayawani huko ughaibuni..
 
Back
Top Bottom