Mgomo wa Madaktari hautaisha kwa vitisho na Dola; ni kwa Makubaliano tu!

Hizo Hospital zingekuwa zinatibu viongozi wangesikilizwa lakini ni za walalahoi, they don't care.
 
Serikali inachezea shilingi Chooni - itajuta muda si mrefu.
Ubora wa Kiongozi hupimwa nyakati kama hizi -Pinda ameonesha kuwa yeye ni failure.


Pinda na Kikwete ni sawa na Kiziwi na Kipofu, sijui nani atamuongoza mwezake, two hopeless people
 
Mwanakijiji,

Tuko pamoja hapa. Tatizo serikali yetu inafikiria kufanya ubabe tu badala ya kutumia busara. Kama ulivyosema, mwaka jana pale Kenya madakatari waliamua kuweka manyanga chini kwa siku kadhaa. Serikali iliwaomba wapeleke ujumbe wao kukutana na serikali na kuangalia ni njinsi gani matatizo yao yanaweza kutatuliwa. At the end of the day, muafaka ulifikiwa na madaktari walikubaliana na serikali na hivyo kurudi kazini. Vitisho havikutumika hata kidogo. Inakuwaje huyo anayejiita mtoto wa mkulima atumie ubabe kuwarudisha madakatari kazini?

Anajidanganya!!!!!

Tiba
 
Baada ya kusikiliza maneno ya Pinda jana,niliwaza na kukosa usingizi usiku kucha.Nimekubaliana na wengi wanaosema hivi sasa upeo wa viongozi wetu umeshuka kwa kiwango cha kasi sana.

MM nakubaliana na yote uliyosema,bado natamani Watanzania walio wengi walitambue hili ili tuweze kuungana nao.

Vitisho na Dola haviwezi kuendelea kutawala katikati yetu bila kutafuta suluhisho.

Ni wakati muafaka sasa kujua ni nini cha kufanya.

Pinda ameonyesha ni jinsi gani serikali yake imefika mwisho wa kufikiri.kwani matatizo hupimwa kwa kiwango cha kuyatatua.kwa maanaa hiyo Nchi yetu itaendelea kuwa na matatizo makubwa zaidi ya hayo.
 
Mwanakijiji M.M naomba ushauri huu au mawazo yako yaandikwe gazetini,maana nimesikiliza tamko la PM nimesoma bandiko lako nimeona mawazo yako ndio yalitakiwa ayatoe PM wakati akijadiliana na M-dr,na Tamko la PM ni kama tamko la mtu ambaye alikuwa anapiga porojo wala hakuwa amejiandaa ku-address issue kubwa kama hii,sijui tatizo liko wapi kwa viongozi wetu,sijui ni kweli kwamba wao wanaamini kila migomo inayotokea hapa nchi inakuwa backed up na Chadema?
Please mwanakijiji naomba mawazo haya yawe published soon kwenye moja ya print media.

subiri baada ya siku mbili tu utayana magazetini
 
Makubaliano ni muhimu sana. Lakini mbona madaktari hawakutaka kukutana na PM? Hayo makubaliano bila mazungumzo yatapatikanaje kwa njia ya kuandikiana barua?

Utawezaje kuka meza moja na watu ambao ndio channzao cha mgomo huo, kama kweli serikali ingekuwa makini inewaondoa kwanza waziri, katibu mkuu na mganga mkuu (huyu alikuwa mganga wa Manispaa, Jiji ndipo kwa uswahiba akwa Chief Medical Doctor) ndipo mazungumzo yafanyike
 
Sikuamini kama ilikuwa speech ya PM jana. Ni kitu kimenikosesha usingizi. Hao madaktari wa Jeshi na wengineo alowataja hawataweza acha pengo huko watokako?
 
mkuu Pasco nakubaliana na wewe kabisa, Pinda kama Pinda hawezi kabisa kusema vile, mkuu kamchoka na anamtafutia sababu ya kumuondoa na jamaa haoni mbali , sema ndiyo hivyo still atakuwa anapata 75% ya mshahara wake na miradi miradi yake na madeal ya ardhi maisha yatakuwa yanaendelea kama kawaida, watu wanaumwa na wanaotegemewa kuwatibu ni hao wanaogoma, kiongozi makini alipaswa anyenyekee haswa,lakini sasa anafawafanya wagome zaidi, kweli tuna viongozi

Mkuu Mzee Mwanakijiji, kama unafikiri aliyoyasema Pinda ni ya kwake, you are wrong!. Unless things get off hand na Pinda nae aendoke kumnusuru mtutu yule yule ambaye Lowassa aliondoka kumnusuru kwenye Richmond!.
 
Tamko la Pinda kwa Madaktari ni la enzi zile za mwalimu ambapo chama kilikuwa kimeshika hatamu. Katika wakati huu wa dot.com inahitajika busara zaidi.
Lazima kwanza Waziri Mkuu akiri kuwa watendaji wa Wizara hawakutumia hekima katika hatua za mwanzo za mzozo huu kwa kutumia maneno ya kejeli na dharau bila kusikiliza hoja za madaktari, kwa hiyo inatakiwa hawa wawajibike kwanza ama kwa kuomba radhi kwa madaktari na watanzania ama kwa kuachia ngazi ili watanzania wengine wanaoweza kuzitatua changamoto za wizara ya afya wapewe nafasi hiyo, kuwaamrisha madaktari warudi kazini bila kwanza ya kuwawajibisha waliosababisha mgomo huu ni kuendeleza "impunity" ambazo wanasiasa na wateule wa wanasiasa wamekuwa wakizionyesha (mfano mtakula majani lakini ndege ya rais itanunuliwa, rada ni yetu kwa hiyo tutanunua hata waseme namna gani, na mengine mengi)
 
Kama imeuzwa na sisi watupatie mgao wetu!
avatar41784_2.gif
 
Uzoefu unaonyesha kila madaktari walipotishwa wakatishika basi mazoea hayo yaligeuka kuwa tabia.Endapo madaktari hawa kwa mara ya kwanza watakuwa wameenda kinyume na matakwa ya mazoea na utamaduni wa kutishika basi ni kweli Taifa litakuwa limesonga mbele kwa namna yake.Kwa kuwa kwa mara ya kwanza Wananchi wa Tanzania kupitia taaluma ya udaktari watakuwa wameipa fundisho Serikali kujifunza na kuangalia njia sahihi za kuondoa kero zinazotokana na kutofautina na kada za kitaaluma Tanzania.

Kwa hakika madaktairi wakiafiki na kuludi kukubaliana na matakwa yaliyotamkwa na Pinda, basi tukili kuwa bado tuna safari ndefu sana ya ukombozi wa kifikra kwa Watanzania hasa kada ya wasomi kitaaluma.Na cha ubaya sana ni hatari kwa kada ya kitaaluma kushindwa kusimamia haki zake za msingi ambazo wao kwa udhahiri wanaona zinapokwa pasipo sababu.

Kama kada ya wanataluuma watashindwa kusimamia haki zao, watu wasio na upeo wa kuchambua hoja na matukio kwa upeo wa juu watakwamuka vipi na kwa msaada wa nani kama si wasomi.

Natumaini madakati walio wengi ni vijana wa miaka ya sabini,themanini na tisini basi watende kwa kufuata mioyo yao wasiige mioyo ya kizazi cha miaka ya sitini,na hamsini, ambayo utii ulipotiliza kwa wakuu umelifikisha Taifa hapo tulipo kwa mfumo wa OBEY YOUR SUPERIOR, hata kama hao Superior wako chaka kiupeo, wewe obey tu kwa kuwa wanamamlaka.Noooooooooo way HAIWEZEKANI AMKENI JAPO WATANZANIA WATAUMIA LAKINI DAMU YA KUJIBU YA WATAKAO ATHIRIKA NA MAAMUZI YENU WAKATI WA HATUA ZA KUPIGANIA MASLAHI YENU ZITAENDA KWA WATAWALA WA TAIFA HILI.

HAKI UINUA TAIFA.
 
nani kakwambia walikataa kukutana nae...embu soma hapo juu..si walienda jaman..na wakaishia kutukanwa...jumapili wakakubaliana kabisa jumatatu..
 
MaDaktari, WanaSheria( Mwakili, Mahakimu) wanaponiambia wanagoma kwa ajili ya maslahi duni moyo unanikataza kuamini kabisa. Wanafanya madudu mengi mno kwa kutumia fani zao hizi kwa migongo ya uelewa wetu mdogo na kutokuwa na pa kwenda.
Ninawaelewa MaDaktari wakilalamikia vifaa na mzingira duni ya kazi. Hili lisingesababisha WAGONJWA duni kukosa huduma hata ile ya msingi kabisa.
 
Makubaliano ni muhimu sana. Lakini mbona madaktari hawakutaka kukutana na PM? Hayo makubaliano bila mazungumzo yatapatikanaje kwa njia ya kuandikiana barua?
Mi nawaunga mkono kwa kuto taka kukutana na PM, Mi naamini PM ni bendera fuata upepo, ni mangapi ameshindwa kuyatatua mpaka amngoje JK? Kumbuka ya Jairo na lile la kuongeza posho, ameshindwa kabisa kuact km PM na kuacha watu wamburuze km toroli, mi ningeshauri waseme kuwa wao wanataka kumuona JK mwenyewe sio PM cha uoga.Jana kaongea lakini ukimcheck tu utaona confidence hana sema tu kaamua kusema.Kingine mi madaktari bila kukamalia yule katibu mkuu wa wizara ua afya kuondolewa pale na kuletewa mtu makini basi hakuna kitakacho endelea. Mi nawaunga mkono madaktari waendelee na mgomo wao ili sekta ya afya ipate ukombozi, kila kwenye kutafuta mabadiliko lazima vifo vitokee, kwa hio kwa hili sioni tatizo.
 
Pinda ana damu ya kutetewa kila wakati , ati maneno yake atakuwa kaelekezwa na Mkuu wa nchi....Huu ni uongo kabisa, Pinda mwenyewe is a problem. Consider maamuzi yake toka ameingia Uwaziri Mkuu wa JMT :
1.Alipobanwa kuhusu kero ya mauaji ya Albino aliishia kulia lia tu, mpaka leo hatuoni kama hilo swala amelimaliza kivipi. Maana wanunuzi wa viungo vya ndugu zetu Albino hakuna hata mmoja aliyekamatwa au kutangazwa kakamatwa . Unataka kusema wale vijana waliokamatwa kwa kosa la mauaji hawajawataja hao wanunuzi wa vioungo vya Albino? Mbona Pinda hili kalifumbia macho, na bado watu wanamung'unya maneno kumweleza ukweli Pinda kwamba yeye si Mtoto wa Mkulima kama anavyojiita: Ni mtu anayekuchekea huku akikumaliza na watu wanamwamini
2. Puinda alitoka wizara ya TAMISEMI kabla hajawa Waziri Mkuu. Yeye mwenyewe amewahi kuongea kwamba fedha nyingi zinafujwa kule kwenye Halmashauri. Wizara ya TAMISEMI iko chini ya ofisi ya Waziri Mkuu. Amefanya nini kuondo tatizo la ufujaji wa fedha hizo huko TAMISEMI wakati anajua kila linaloendelea huko? Au umesikia wapi Pinda amemwondo Mkurugenzi kwa utendaji mbovu pamoja na CAG kuanika madudu mengi ya halmashauri zetu? Sana sana alimwondoa Mkurugenzi wa wilaya ya HAI kwa sababu za kisiasa tu ambazo watu wote walizishitukia wakati ule wa uchaguzi 2010i. Pinda hawezi kutetewa kwamba ni mzuri, eti anashindwa kwa ajili ya JK, NO ! Tuliona akina Sokoine wakifanya kazi hata kumzidi Mwalimu Nyerere, haiwezekani waziri Mkuu ashindwe kufanya kazi eti kwa ajili ya kumwogopa Boss wake, kama kweli ni mwadilifu si angejiuzuru kuliko kuonekana kituko? Ni wazi kwamba yeye ndio failure ns si JK kama watu wanavyotaka kutuaminisha.
3.Swala la posho za wabunge CHADEMA walivyozigomea , wote tulimsikia huyu huyu mnaemwita mtoto wa Mkulima akiwakejeli wapinzani kwa kusema " WANAMEZEA" mate posho zile. Hii ni wazi kwamba haguswi ghata kidogo na matatizo ya wananchi, bali yeye anaangalia faida yake , chama chake na mtandao wake basi..
4. Pinda huyu huyu anatetea uporaji wa ardhi tena nyumbani kwao kwa be ya $0.25 /HA per year huku wanakijiji wakihamishwa kupisha wawekezaji. Kama kweli nia yake ni kusaidia hao wakulima, ameshindwa nini kuwalazimisha wawekeza hao waingie ubia na wenyeji , badala ya kuwafukuzi sehemu zuisizo na rutuba? Pinda ni mnyonyaji tu kama wote aliozungukwa nao....asitetewe kabisa ati ni mwadilifu...No!
5.Pinda ndiye aliyeshindwa kutimiza mapendekezo ya Richmond. Haiwezekani aaminiwe huyu, kama angekuwa na uchungu na nchi hii, basi baada ya kushindwa hili asingekubali kuwa PM tena , maana ni aibu sana kwake na watoto wake.
6. Huyu Pinda anayewatishia madaktari, ndo huyo huyo aliyegwaya kuwashitaki watuhumiwa wa ufisadi. Tena bila aibu alitamka kwamba kushitaki hao watu ni kama kujitia kitanzai, na mpaka kesho hataiki mijadala ya Meremeta nk. Whata do you expect from this failed man? Anawatetea wezi, anapandisha gharama za umeme kwa haop Watnzania ambao Mishahara yao ipo chini. Maisha yanapaa kwa ugumu, bado huyu mtu tunamwona anaweza kuitoa TZ hapa ilipo? Huyu ni katili tu, na anapenda madaraka. Haiwezekani useme unaleta madaktari wa jeshi hospitali zote za TZ, hivi hao wanajeshi wapo wangapi? Na je wao ndo wanastahili kulipwa posho kidogo kwa sababu tu ya utii wao? Ana uhakika gani kwamba hao madaktari wa jeshi wana furaha ni mapato au na miundo mbinu ya hospitali watokako?
Pinda aache kulewa madaraka, ni wakati sasa wa kumweleza ukweli na si kumfichaficha....
 
Utawezaje kuka meza moja na watu ambao ndio channzao cha mgomo huo, kama kweli serikali ingekuwa makini inewaondoa kwanza waziri, katibu mkuu na mganga mkuu (huyu alikuwa mganga wa Manispaa, Jiji ndipo kwa uswahiba akwa Chief Medical Doctor) ndipo mazungumzo yafanyike

Mkuu serikali inayoweza kufanya hivyo labda ni serikali ya kijiji cha ujamaa. Waondolewe kwa kosa gani? Wao ndio wanatoa posho? Kwa jinsi PM alivyosema inaonekana mambo haya yalikuwa yakiongelewa na serikali kwa ujumla. Pia PM hajatoa tamko lake ametoa tamko la Serikali.
 
Hebu tujiuleze, je serikali ilkuwa tayari kuongea na kuwasikiliza madaktari?

Kinacho nishangaza ni speech ya saa moja iliyosomwa na PM mara baada ya kuingia na kuelezwa position na waziri wa afya, moja kwa moja akaanza kusoma kwenye statement iliyotayarishwa ambayo ilikuwa na hitimisho kama tulivyosikia jana.

Walijuaje kama madaktari hawatatokea?

walijuaje kama madaktari watakataa upuuzi wa serikali?

Hebu tujadili hili ili tuone kama kulikuwa na utayari wa kumaliza mgogoro huu kwa upande wa serikali.
 
RichardBrunwick
26 January 2012 2:33PM
Tanzania's Kikwete is one of the most pathetic African leaders of our times. He is a peacetime leader for a country known to be one of the richest in the world in terms of natural resources, yet he leades the world with begging. Foreign companies have known Tanzania to be a free land in which you can go in and take all you can without being asked a question. I really don't get the mind set of its leaders especially their prsident Mr. Kikwete, a Muzungu worshiper. Having worked with the UNDP in that country for 8 years, I realized how inneficient and corrupt the country's leadership is. His ministers that requested bribes from BAE have never been tried despite the damning evidence against them. British TAX payers must stop funding this man's corruptin and foreign trips. His human rights record is horrible. Mr. Kikwete had no business of going to Davos to ask for foreign aid. Already his country is the world third leading foreign Aid dependant nation. He should be embarassed to say to the world that people are poor. His people living "hand to mouth " is his own is own ignorance and stupidity.That is hiw own problem, Brits are having their own problems he must realize that. We cant bankroll his foreign trips. He should make good use of his country's wealth. Instead of letting his corrupt officials and foreigners loot his country, he needs to think before letting himself be a global loughing stock. I read in one of the regional (kenyan) publication the mockery nature related to his frequent foreign trips. Palestinian, Haiti, Lebanon, Somalia and even Rwanda economies are more robust that of Tanzania. We must question the nations that welcomes this "Joker's" request for AID. He needs to be on a "no-fly" list so he can be serious. Hopefully the billionaires questions what he has done with the Money he has received for decades. The Arab spring should turn into the African summer and get rid of the Kikwete likes
(http://www.guardian.co.uk/discussion/comment-permalink/14344505)
 
Back
Top Bottom