Mgomo wa Daladala Kigamboni

Watendaji na wapangaji wa haya mambo sijui huwa wanafikiria vitu gani au kwa sababu wao hawatumii huu usafiri wa uma ndio maana hawazingatii athari kwa walaji.

Pale kivukoni ndio center kubwa ambayo watu kutoka viunga vyote vya kigamboni huletwa na mabasi kisha baada ya hapo wavuke kwenda mjini au wapande hizo machinga kupitia darajani, sasa leo unapohamisha basi za machinga na kuzipeleka ndani ya mji wakati bado kituo kikuu cha hizi basi nyingine kinabaki kuwa kivukoni hapo unakua unawalazimisha abiria wanaotaka kuvuka kupitia darajani wapande bajaj (Tsh 500) ili kuzifata hizo machinga huko Tungi na baadae alipe tena kiasi hicho hicho anapokua anarudi.

Kwa mtu wa kipato cha chini nyongeza hii ktk gharama ya usafiri ni kubwa, mamlaka husika inabidi walitazame vizuri ili maboresho wanayofanya yasiumize watumiaji wa huduma husika.
Hilo ndo tatizo la wanyonge wanavurugwa vurugwa kama maandazi kikangoni,
 
Nchi inarudi kwenye migomo? Iringa wamegoma mwezi uliopita, Mbeya wamegoma juzi, leo hii tena jijin huko duuu.
Wacha watu waonyeshe matatizo yao mbalimbali kwa uwazi ili wahusika watafute ufumbuzi wa kudumu utakao nufaisha pande zote.Tabia ya uko nyuma serikali yakutotaka matatizo yasemwe kwa uwazi na kuyaficha kwa ubabe haikuyafanya matatizo hayo yaondoke badala yakuyafunika kwa muda.
 
Leo Tar 20 May 2021 kuanzia Majira ya Asbuhi Magari ya Abiria maarufu kama Daladala Yaendayo Kigamboni Kupitia Daraja kuu la Kigamboni (Mwl.Nyerere) Yamegoma kufanya Safari zake kutoka Kigamboni hadi Karume Ilala kupitia Kilwa Road.

Sababu ni Kupinga kuhamishwa kwa Kituo kikuu cha Mabasi hayo kutoka Ferry Kivukoni hadi Kata ya Tungi. Abiria /Wananchi wengi wanapata Tabu sana muda huu.

Pia njia ya Mji Mwema kuelekea PembaMnazi wamegoma.

HII PICHA SI YA KIGAMBONI
 
Ww unatoka cheka gari linafika mnadani upande bajaji jero harafu tena ulipe mia mbili uvuke ukijumilsha na nauli ya kutoka cheka ni 900 ....900+500+200=1600 .Tukisema wapanga mipango ni machizi au wakitumbuliwa wanaanza kuona Mama anawaonea kumbe nyie ndo hamna huruma na wananchi wa hali ya chini
 
HII PICHA SI YA KIGAMBONI

IMG_20210520_115725_486.jpg
 
Leo Tar 20 May 2021 kuanzia Majira ya Asbuhi Magari ya Abiria maarufu kama Daladala Yaendayo Kigamboni Kupitia Daraja kuu la Kigamboni (Mwl.Nyerere) Yamegoma kufanya Safari zake kutoka Kigamboni hadi Karume Ilala kupitia Kilwa Road.

Sababu ni Kupinga kuhamishwa kwa Kituo kikuu cha Mabasi hayo kutoka Ferry Kivukoni hadi Kata ya Tungi. Abiria /Wananchi wengi wanapata Tabu sana muda huu.

Pia njia ya Mji Mwema kuelekea PembaMnazi wamegoma.

Miaka mitano na ushee ya JPM haya yalikuwa historia.
 
Leo Tar 20 May 2021 kuanzia Majira ya Asbuhi Magari ya Abiria maarufu kama Daladala Yaendayo Kigamboni Kupitia Daraja kuu la Kigamboni (Mwl.Nyerere) Yamegoma kufanya Safari zake kutoka Kigamboni hadi Karume Ilala kupitia Kilwa Road.

Sababu ni Kupinga kuhamishwa kwa Kituo kikuu cha Mabasi hayo kutoka Ferry Kivukoni hadi Kata ya Tungi. Abiria /Wananchi wengi wanapata Tabu sana muda huu.

Pia njia ya Mji Mwema kuelekea PembaMnazi wamegoma.

SAmia : "Sijaribiwi"

Abiria wa Mbagala Zakhem kupitia Vikunai, Mgeni nani -chekechea nao wagome, wanalipishwa nauli 500 sehemu waliyopaswa kulipa 300.
 
SAmia : "Sijaribiwi"

Abiria wa Mbagala Zakhem kupitia Vikunai, Mgeni nani -chekechea nao wagome, wanalipishwa nauli 500 sehemu waliyopaswa kulipa 300.
Sukari ilitoka 1400 hadi 2400 na ikasemwa bei imeshuka!! Bado mazwazwa yakashangilia na kuona "wanyonge wametetewa!!" Akili za kidanganyika tunazijua wenyewe...
 
Sukari ilitoka 1400 hadi 2400 na ikasemwa bei imeshuka!! Bado mazwazwa yakashangilia na kuona "wanyonge wametetewa!!" Akili za kidanganyika tunazijua wenyewe...
Ndio maana wameanzisha shue za kata na wakasema kiswahili ni lugha ya kimataifa huku wanyonge wakishangilia kwa vifijo , wakati watoto wetu wanasoma international school kuja kuwatawala mazwazwa milele.
 
Back
Top Bottom