Mgomo Umemalizika Rasmi!. Jee Bado Kuna Umuhimu Rais Kukutana na Wazee wa Darisalama?!.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,442
113,452
Wanabodi,

JK ilikuwa akutane na Wazee wa Darisalama siku ya Ijumaa ili kutoa msimamo wake juu ya mgomo wa Madaktari!.
Ijumaa hiyo akaamua kabla hajatoa msimamo, akatumia busara kuwasikiliza hao madaktari, yeye mwenyewe kwa masikioo yake, licha ya taarifa zote alizoletewa na wasaidizi wake na vyombo vyake!. Hivyo akaahirisha kukutana na wazee mpaka Jumatatu, ili kutoa fursa ya mawasiliano zaidi.

Badda ya kuahirishwa ule mkutano wa jana, nilisema hivi
Wanabodi,

Kwa mliosoma baadhi ya sifa nzuri za JK ni "a good sense of humour", hivyo JK akaamua kuwatafuta madaktari, aka wa 'charm' with a good sense of humour, kina Ulimboka wakalainika, kesho mtashuhudia wakitoa tamko la kuumaliza rasmi mgomo huo bila masharti yoyote!. JK atakapokutana na Wazee hiyo Jumatatu itakuwa ni kuwapatia tuu mrejesho!.

Pasco.

Leo Chama cha Madaktari MAT, kimekutana na kutoa tamko la kuumaliza mgomo wao unconditional!.

Sasa baada ya mgomo huu kumalizika rasmi, jee bado kuna haja ya JK kukutana na Wazee wa Darisalama?.

Mkumbuke taarifa ya madaktari, haukusema, waliongea na rais Ikulu, na hakuna taarifa ya Ikulu kueleza wamekubaliana nini na madaktari, bali ni MAT, ndio wametoa taarifa ya kuumaliza rasmi mgomo huo!. Kwa vile sasa mgomo umeisha, bado kuna haja ya kuendelea kuuzungumzia mgomo huu?.

Ningekuwa mshauri wa JK, ningemshauri hata hiyo Jumatatu, asizungumze na Wazee wa Darisalama, unless alikuwa na mengine ya kuongea nao na sio lazima lihusu huo mgomo wa madaktari!.

Maadam ameonana na madaktari, walichozungumza wanakijua wenyewe, na baadae madaktari wametoa taarifa kusitisha mgomo unconditional, nadhani sasa ni busara, tusiendelee kuuzungumzia mgomo huu ili kuepusha kumtafuta mshindi na mshindwa!.

Uamuzi wa madaktari kusitisha mgomo ni uamuzi wa busara unaopaswa kuungwa mkono na wote wenye mapenzi mema na nchi yetu!. Pia tuchukue fursa hii kuleta umoja na mshikamano, yale makundi yote tuliohasimiana kutokana na mgomo huu kwa baadhi ya wenzetu kuwaunga mkono madaktari na wengine tukipinga, sasa mgomo umeisha, tuwe wamoja tusonge mbele kwa maslahi ya taifa!.

Wasalaam

Pasco.
 
unconditional kivipi mkuu? Unaweza ukatufafanulia labda...!
Sweke, walipolianzisha tena, walitoa masharti lazima kibarua cha waziri na naibu wake kiote ndipo warejee kazini. Leo wamekubali kuumaliza rasmi mgomo wao bila masharti yoyote!
 
Afadhali madokta wamemaliza huo mgomo wao. Nilijua tu yaani JK ashiriki kumaliza migogoro ya Kenya na Zanzibar pamoja na ule ww Mauritania wakati akiwa Mwenyekiti wa AU halafu leo ashindwe kumaliza mgogoro wa madaktari. Ilikuwa haiingii akilini.

Mgomo umeisha, madokta fanyeni kazi kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.

Ni muhimu Rais akutane na wazee aongelee sakata zima la mgomo hadi alipoingilia jana na kuumaliza kidiplomasia.
 
Wanabodi,

JK ilikuwa akutane na Wazee wa Darisalama siku ya Ijumaa ili kutoa msimamo wake juu ya mgomo wa Madaktari!.
Ijumaa hiyo akaamua kabla hajatoa msimamo, akatumia busara kuwasikiliza hao madaktari, yeye mwenyewe kwa masikioo yake, licha ya taarifa zote alizoletewa na wasaidizi wake na vyombo vyake!. Hivyo akaahirisha kukutana na wazee mpaka Jumatatu, ili kutoa fursa ya mawasiliano zaidi.

Badda ya kuahirishwa ule mkutano wa jana, nilisema hivi


Leo Chama cha Madaktari MAT, kimekutana na kutoa tamko la kuumaliza mgomo wao unconditional!.

Sasa baada ya mgomo huu kumalizika rasmi, jee bado kuna haja ya JK kukutana na Wazee wa Darisalama?.

Mkumbuke taarifa ya madaktari, haukusema, waliongea na rais Ikulu, na hakuna taarifa ya Ikulu kueleza wamekubaliana nini na madaktari, bali ni MAT, ndio wametoa taarifa ya kuumaliza rasmi mgomo huo!. Kwa vile sasa mgomo umeisha, bado kuna haja ya kuendelea kuuzungumzia mgomo huu?.

Ningekuwa mshauri wa JK, ningemshauri hata hiyo Jumatatu, asizungumze na Wazee wa Darisalama, unless alikuwa na mengine ya kuongea nao na sio lazima lihusu huo mgomo wa madaktari!.

Maadam ameonana na madaktari, walichozungumza wanakijua wenyewe, na baadae madaktari wametoa taarifa kusitisha mgomo unconditional, nadhani sasa ni busara, tusiendelee kuuzungumzia mgomo huu ili kuepusha kumtafuta mshindi na mshindwa!.

Uamuzi wa madaktari kusitisha mgomo ni uamuzi wa busara unaopaswa kuungwa mkono na wote wenye mapenzi mema na nchi yetu!. Pia tuchukue fursa hii kuleta umoja na mshikamano, yale makundi yote tuliohasimiana kutokana na mgomo huu kwa baadhi ya wenzetu kuwaunga mkono madaktari na wengine tukipinga, sasa mgomo umeisha, tuwe wamoja tusonge mbele kwa maslahi ya taifa!.

Wasalaam

Pasco.

Watanzania bwana mbwembwe nyingi ohooo, Jk atakiona na mengine kibao, sasa mnaenedelea na hayo hayo ili iweje. Jk ni rais wa watu bwana mnatapa tapa tu.
 
Wanabodi,

Leo Chama cha Madaktari MAT, kimekutana na kutoa tamko la kuumaliza mgomo wao unconditional!.

Pasco.

TAMKO LETU:

JANA TAREHE 9/3/2012, TULIKUTANA NA MH. RAIS WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MH. DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE. TULIMWELEZA HOJA ZETU, AMBAZO ALIZIELEWA NA ALIAHIDI KUZISHUGHULIKIA KIKAMILIFU. TUNA IMANI SANA NA MH. RAIS KWAMBA HATATUANGUSHA.

KUTOKANA NA HILO, TUNAPENDA KUUTANGAZIA UMMA WA WATANZANIA KUWA TUNARUDI KAZINI RASMI KUANZIA LEO TAREHE 10/3/2012, WAKATI MHESHIMIWA RAIS AKISHUGHULIKIA MADAI YETU.

PIA WAKATI MADAI YETU YAKISHUGHUKLIKIWA TUNAPENDA KUSEMA KUWA HATUNA IMANI NA WAZIRI WA AFYA MH. DR. HAJI MPONDA NA MH. DR. LUCY NKYA, NA KUWA TUNAMSIMAMISHA RASMI UANACHAMA WA MAT MH. DR. LUCY NKYA.

MADAKTARI TUNATAMKA WAZI KUWA WAZIRI WA AFYA DR. HAJI MPONDA NA NAIBU WAKE DR. LUCY NKYA NI MAADUI WA MADAKTARI NA SEKTA YA AFYA KWA UJUMLA HAPA NCHINI NA TUNAAHIDI KUTOKUWAPA USHIRIKIANAO WA AINA YOYOTE WA KIBINAFSI AU WA KIUTENDAJI.

SOLIDARITY FOREVER.
RAIS(MAT)
Blue siyo conditions? Tafadhali sana uwe na kiwango cha kusema ukweli
 
Mkuu Pasco,
Rais JK kama umemsoma ni mtu asiependa migogoro ebu angalia kundi lolote linalokwenda Ikulu kwa ajili ya mazungumzo uwa linarudi na majibu ya kukubaliana na JK.

Watu wengi walikuwa wanategemea na kutaka waone JK kawafukuza kazi Madaktari wetu, ili mgogoro uwe mkubwa na usambae.

Bahati mbaya au nzuri JK ni msikivu na mvumilivu ana akili za kesho, hujui kwa nini kabadilisha ratiba yake kabla ya kuongea na Taifa kupitia Wazee wa Dar es Salaam, kaongea kwanza na Madaktari na kutatua mgogoro kwa amani.

Kuongea na Wazee Jumatatu JK hatakuja kivingine kabisa na hotuba ya huruma kwa Watanzania.

Pamoja kuwa JK baadhi ya vitu kashindwa kufanya kama rais lakini kwenye mazungumzo ya kutatua migogoro JK siku zote anafanikiwa kuwashawishi wapinzani wake wakubaliane nae.
 
..Huwa najiuliza hivi pale Ikulu kuna nini, "nna mashaka pale Getini kuna kitu kimewekwa ukiingia tu kutaka kuonana na Baba Riz unalainika". Walianza Chadema na issue ya Katiba wakalainika, leo hii na Madaktari wamelainika.
Kuna nini Ikulu.
 
Sweke, walipolianzisha tena, walitoa masharti lazima kibarua cha waziri na naibu wake kiote ndipo warejee kazini. Leo wamekubali kuumaliza rasmi mgomo wao bila masharti yoyote!
hapo kwenye masharti yeyote nadhani ndiyo upatazame vizuri. Conditions zile bado zipo ila wamerudi kazini baada ya kuahidiwa hizo conditions zitashughulikiwa...!
 
..Huwa najiuliza hivi pale Ikulu kuna nini, "nna mashaka pale Getini kuna kitu kimewekwa ukiingia tu kutaka kuonana na Baba Riz unalainika". Walianza Chadema na issue ya Katiba wakalainika, leo hii na Madaktari wamelainika.
Kuna nini Ikulu.

Ukishakubali kuingia pale........na wewe in a way unageuka (kisaikolojia) kuwa kama mmoja wao.........

Nilishawaambia hawa madakta wetu............maneno yao ya kipuuzi eti wanataka Mawaziri wajiuzulu they were UTTERLY NONSENSE.........kama kuna mtu mpumbavu aliwashauri kusema hayo basi na wao siju tuwaweke kwenye kundi gani...........
 
Mkuu Pasco,
Pamoja kuwa JK baadhi ya vitu kashindwa kufanya kama rais lakini kwenye mazungumzo ya kutatua migogoro JK siku zote anafanikiwa kuwashawishi wapinzani wake wakubaliane nae.
Hapa umenena vyema ila si kila mara anafanikiwa kuwashawishi wapinzani wake...kuna wakati huwa hata hawasilikilizi.
Ni kweli mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni...!
 
Afadhali madokta wamemaliza huo mgomo wao. Nilijua tu yaani JK ashiriki kumaliza migogoro ya Kenya na Zanzibar pamoja na ule ww Mauritania wakati akiwa Mwenyekiti wa AU halafu leo ashindwe kumaliza mgogoro wa madaktari. Ilikuwa haiingii akilini.

Mgomo umeisha, madokta fanyeni kazi kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.

Ni muhimu Rais akutane na wazee aongelee sakata zima la mgomo hadi alipoingilia jana na kuumaliza kidiplomasia.

There are times when children want to hear the voice of their father....
 
hapo kwenye masharti yeyote nadhani ndiyo upatazame vizuri. Conditions zile bado zipo ila wamerudi kazini baada ya kuahidiwa hizo conditions zitashughulikiwa...!

It has been long overdue kubadilisha/kuli-amend baraza la mawaziri..........however the changes to baraza la mawaziri tuwaachie JK na Waziri wake Mkuu at their own pace that suits them...........na sio kutokana na ultimatum ya kipuuzi kutoka kwa madaktari........
 
unconditional kivipi mkuu? Unaweza ukatufafanulia labda...!

Wamerudi bila madai yao mapya ya Mponda na Nkya kuwachishwa kazi, walisema hawarudi kazini mpaka hao waachishwe kazi. Kwa hiyo wamerudi "unconditional".
 
It has been long overdue kubadilisha/kuli-amend baraza la mawaziri..........however the changes to baraza la mawaziri tuwaachie JK na Waziri wake Mkuu at their own pace that suits them...........na sio kutokana na ultimatum ya kipuuzi kutoka kwa madaktari........
Upuuzi ni huu ulioandika wewe na huu wanaofanya kikwete na pinda. Ni nini kiliwanyima kufanya hiki alichofanya jana kabla hata ule mgomo wa kwanza haujatokea. naamini ni kweli IQ ya mwafrika haitilafiani sana na ya nyani. Mtu unaacha kidonda kigeuke kidonda ndugu kwa kukataa matibabu halafu baadae unapokubali mguu ukwatwe unapongezwa? Elimu inatusaidiaje waafrika? Mtu kama wewe ogah bila shaka umesoma angalau f 4 lakini mbona unatenda kufikiri kama kima? angalia unasema madiliko ya baraza waachiwe wafanya kipindi wanachotaka na kwa muda unaowafaa wao.... sio wananchi wote..... comments za aina hii zinatolewa na na wajinga wasiojua n nini maana ya kutawala.....
 
Blue siyo conditions? Tafadhali sana uwe na kiwango cha kusema ukweli
Mkuu Mimibaba, niendeshe na darasa la conditions?. Hiyo kwako ndio condition?. Walipogoma si waliweka masharti, kuwa hawarudi kazini mpaka Dr. Mponda na Dr. Nkya wang'olewe?. Jee tangazo lao la kumaliza mgomo lina masharti?., jee wameweka sharti lolote lazima litekelezwe ndipo warejee kazini?. Baada tuu ya kuongea na JK wamekubali kumaliza mgomo na kurejea kazini!. Hakuna sharti lolote lililowekwa, wanarejea kazini unconditional!.
 
Ukishakubali kuingia pale........na wewe in a way unageuka (kisaikolojia) kuwa kama mmoja wao.........

Nilishawaambia hawa madakta wetu............maneno yao ya kipuuzi eti wanataka Mawaziri wajiuzulu they were UTTERLY NONSENSE.........kama kuna mtu mpumbavu aliwashauri kusema hayo basi na wao siju tuwaweke kwenye kundi gani...........
hivi ubongo wako unajaza kizibo cha bia kweli? sidhani
 
Back
Top Bottom