falcon mombasa
JF-Expert Member
- Mar 5, 2015
- 9,158
- 9,239
Wakuu habari
Habari za kuaminika za kutoka chanzo changu ninachokiamini kabisa zinanitaarifu niwaambie wale wanaotaka kusafiri siku hizi za karibuni wajiandae haswa
Madereva wote wa mabus wa Tanzania nzima kwa umoja wao wameadhimia kugoma kutoa huduma hiyo muda wowote kuanzia sasa (hapa sitasema siku)
Lengo kubwa la mgomo huu ni kutokana na kauli tata zinazopishana zinazotolewa na vyombo vinavyosimamia usalama wa barabarani,ambapo baadhi ya kauli ya viongozi wa usalama zimekuwa zikipishana kila kukicha
siku chache zilizopita alisikika afisa mmoja mkubwa wa jeshi la polis kitengk cha usalama barabarani akitumia vyombo vya habari akiweka katazo kuwa gari halitakiwi kusimama kwenye zebra endapo hakuna mtu bali lipunguze mwendo tu na ukisimama bila kuwepo mtu kwenye kivuko utakuwa umetenda kosa na utawajibishwa
Afisa wa pili mwingine wa juu kabisa alitumia vyombo vya habari kuwaonya madereva wasiosimama kwenye zebra hata kama hakuna mtu.Jambo lilozua utata mkubwa kwani madereva hawajui wafuate kauli ipi
kauli iliyoleta hasira zaidi ni hivi juzi ambapo kiongozi mwingine alinukuliwa akisema "madereva wanapaswa kuogopa kama shetani au kama simba"
Hayo ni baadhi yatakayopelekea kuanza mgomo huu mkubwa kabisa licha ya kuwa yapo mengi pamoja na yale ya kukosekana alama za barabarani na ubovu wa barabara huku lawama zote zikielekezwa kwa madereva pindi ajali zinapotokea
Narudia tena wasafiri wajiandae kisaikolojia
Habari za kuaminika za kutoka chanzo changu ninachokiamini kabisa zinanitaarifu niwaambie wale wanaotaka kusafiri siku hizi za karibuni wajiandae haswa
Madereva wote wa mabus wa Tanzania nzima kwa umoja wao wameadhimia kugoma kutoa huduma hiyo muda wowote kuanzia sasa (hapa sitasema siku)
Lengo kubwa la mgomo huu ni kutokana na kauli tata zinazopishana zinazotolewa na vyombo vinavyosimamia usalama wa barabarani,ambapo baadhi ya kauli ya viongozi wa usalama zimekuwa zikipishana kila kukicha
siku chache zilizopita alisikika afisa mmoja mkubwa wa jeshi la polis kitengk cha usalama barabarani akitumia vyombo vya habari akiweka katazo kuwa gari halitakiwi kusimama kwenye zebra endapo hakuna mtu bali lipunguze mwendo tu na ukisimama bila kuwepo mtu kwenye kivuko utakuwa umetenda kosa na utawajibishwa
Afisa wa pili mwingine wa juu kabisa alitumia vyombo vya habari kuwaonya madereva wasiosimama kwenye zebra hata kama hakuna mtu.Jambo lilozua utata mkubwa kwani madereva hawajui wafuate kauli ipi
kauli iliyoleta hasira zaidi ni hivi juzi ambapo kiongozi mwingine alinukuliwa akisema "madereva wanapaswa kuogopa kama shetani au kama simba"
Hayo ni baadhi yatakayopelekea kuanza mgomo huu mkubwa kabisa licha ya kuwa yapo mengi pamoja na yale ya kukosekana alama za barabarani na ubovu wa barabara huku lawama zote zikielekezwa kwa madereva pindi ajali zinapotokea
Narudia tena wasafiri wajiandae kisaikolojia