Elections 2015 Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,428
113,431
Wanabodi,

Leo nimekutana na rafiki yangu wa siku nyingi tuliyepotezana naye kipindi kirefu nyuma, ambaye ni mtu wa sehemu na wa kuaminika sana ambaye yuko attached CCM kama kada tuu wa kawaida wa Chama cha Mapinduzi-CCM, akanieleza seriously habari za kushtusha kidogo ambazo mimi zimenitisha, zimenisikitisha, kunihuzunisha, kuniogopesha, kunisononesha na kuninyongonyeza!, kuwa eti imeishaamuliwa (sitaji imeamuliwa na nani), kuwa mgombea wa urais wa mwaka 2015 kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi-CCM ni Mhe. John Pombe Magufuli!.

Kilichonistua, kunitisha, kunihuzunisha, kunisikitisha, kunisononesha, kunigopesha na kuninyongoneza ni the reasons behind, sababu alizonitajia kada huyu za why mgombea wa CCM mwakani ni Magufuli, ambazo ndizo zimepelekea the inner core ya CCM kuamua mgombea wake wa urais wa 2015 ni lazima awe John Pombe Magufuli tuu, and no one else!.

Kwa vile sababu hizo alizonitajia, baadhi kweli ni sababu za msingi na ziko justifiable kwa any reasonable man, sababu nyingine alizonitajia sio tuu ni unreasonable, bali pia ni unjustifiable! na hazikubaliki kabisa katika Tanzania ya leo!.

Naomba kwa sasa nisizitaje kwanza hizo sababu nilizotajiwa za kwa nini ni Magufuli, kwa sababu habari zenyewe nimezisikia juu juu tuu tena from just a single source, hivyo nahitaji kwanza kujiridhisha kwa kufanya verification kwa ku double check, na ku cross check ikiwemo kupata a collaborative verification na attribution ya third parties ili nijiridhishe kuwa hii ni habari za kweli na kuthibitisha kuwa kumbe hivyo ndivyo the inner core ya CCM inavyoweza kufikia maamuzi ya mgombea wake wa urais based on sababu nilizo tajiwa!, then nitaziweka hadharani hizo sababu za kwa nini CCM imeamua mgombea wake wa urais kwa uchaguzi wa 2015 lazima awe ni John Pombe Magufuli tuu na sio mtu mwingine yoyote!, na kiukweli mkizisikia hizo sababu nilizotajiwa, naamini hata nyinyi sio tuu mtashangaa, bali mtakubaliana na mimi kwanini mtu huyu asiwe!.

Kwa kawaida sisi waandishi wa habari, ukipata taarifa kama hii, huwa inaitwa "a news tip", haukimbilii kuiandika mbio mbio mpaka kwanza uifanyie verification kwa kui double check na kui cross check ili kujiridhisha kwa kuthibitisha ukweli wa taarifa yenyewe, baada ya kuthibitisha na kujiridhisha kuwa ni kweli, ndipo unaiandika.

Lakini kwa vile sasa tunaishi kwenye dunia ya taarifa moto moto, "the world of information age", ukipokea tuu taarifa, unashare na wenzio, ndio maana na mimi nimeamua kuileta humu jf hii "news tip" hivi hivi ilivyo ikiwa kwenye hatua ya "tip" kabla hata ya verification, ili wewe kama mwana JF, uipate ile "JF advantage" ya "be the first to know!", yaani ukiwa mwana jf, unakuwa wa kwanza kujua, hivyo nawaombeni tuu sasa wana jf mkae mkijua kuwa "Mgombea wa urais wa CCM kwa mwaka 2015 ni John Pombe Magufuli!".

Hili la kuamua ni Magufuli, limenistua kidogo kwa sababu kwa sisi tuliomfuatilia utendaji kazi wa Magufuli kwa kauli na matendo tangu akiwa waziri, japo kiukweli ni mchapa kazi, yaani ni jembe kazi la ukweli, lakini mtu huyu ameonyesha wazi sio mzuri sana in terms of stability in decision making!, amefanya baadhi ya maamuzi mengi tuu kwa jazba, pupa, papara na kukurupuka kwa mtindo wa nimeamua mimi na liwalo liwe!, mwisho wa siku baadhi ya maamuzi yake ambayo mengine ni very rational yanakuja kutu cost sisi kama taifa, mifano ipo, ikiwemo kuvunjwa ile Petro Station Mwanza, Uuzaji wa nyumba za serikali, Samaki wa Magufuli, just to mention but few, hivyo akipita na kuwa rais wa nchi hii, kama huu ndio mfumo wake wa kufikia maamizi, then you can just imagine, akiwa rais, atafanya maamuzi mangapi ambayo yatatucost kama taifa, ila pia kwa hulka yake, ana chance ya kuja kuwa the worst dictator this nation has ever had!. Tuombe Mungu asaidie, hili likitimia, huyu mtu abadilike, na kuwa a benevolent one, labda karma ije kuingilia kati, vinginevyo...!.

Nikiisha "confirm" neno "tetesi" litaondolewa na kuwa replaced na neno "confirmed!", na nitaziweka hizo sababu nilizotajiwa ili sasa ndio zijadiliwe!, na nawahakikishia wale wote wenye mapenzi mema na taifa hili, mkizisikia hizo sababu za huyo kada wa CCM alizonipa kwa nini ni Magufuli!, na nyinyi pia zitawashitua, zitawatisha, zitawaogopesha, kuwahuzunisha, kuwasikitisha, kuwasononesha na kuwanyongonyeza!.

Naomba nisiwatajie jina la huyo source wangu chini ya kinga ya kihabari kwa ma source inayoitwa "The Confidentiality of the source", na hapa wakati naileta taarifa hii humu jf, kwa vile zoezi la kumteua mgombea wa CCM bado liko mbali hadi mwaka ujao, unaweza kukuta hata Magufuli mwenyewe bado hajui kuwa ni yeye ndie atakuwa mgombea wa CCM, kwa sababu walio amua kuwa ni Magufuli sio kikao chochote rasmi na halali cha Chama Cha Mapinduzi, CCM bali ni "The Inner Circle" hivyo hii ni tip from the deep inside ya "the inner circle", na bahati mbaya sana, Magufuli mwenyewe hayuko kwenye hiyo "the inner circle!".

NB. Sio kila thread ni lazima ichangiwe, saa nyingine itoshe kujisomea tuu na kujipitia bila kuchangia chochote!. Hii ni just a news tip, kwa vile nimewaahidi naifanyia verification kuithibitisha, nawaombeni msiniulize swali lolote at this stage, kwa sababu sitajibu chochote!, and if possible nawashauri na nyingi msome FYE only na sio lazime mchangie kwa sasa na badala yake mvute subira kusubiria verification.

Sababu ya kuiwahisha humu JF kabla ya verification ni ili tuu wewe kama mwana JF to be the first to know!. Information is power!, if you are the first to know, then you'll have the powers to make good things happen or not to happen if they are bad things!.


Asante.
Paskali


Update: 12/07/2015

Leo hili limetimia ni kweli aliyepita ni Magufuli, nimezitafakari sababu nilizotajiwa ile siku napewa tetesi hii, na kuzipima na hiki kilichotokea, nimejikuta nimelazimika kutoziamini kuwa zile nilizosikia ndizo sababu zenyewe halisi.

Kwa sisi waandishi tuna kanuni ya kuandika only the truth, yaani kuandika nothing but the truth, sasa ili uweze kuandika jambo lolote, ni lazima jambo hili uwe ama umelishuhudia mwenyewe likitokea na ama umeelezwa na trusted sources na kujiridhisha kuwa ni la kweli, ndipo unaliandika.

Ikitokea ukilisikia jambo la mashaka mashaka, unapaswa ulipime kwanza, ujiridhishe na ukweli wake, ukiisha ridhika ndipo uliamini na ndio uliandike.

Kama ikitokea wewe kama mwandishi wa habari, ukasikia jambo lolote ambalo ni la mashaka huliamini, then hupaswi kuliandika, tena hata ikibidi usiliseme wala kuliandika ili lisijulikane.

Hivyo hizo sababu nilizotajiwa siku hiyo napewa tetesi hii kuwa mgombea urais wa CCM atakuwa ni John Magufuli, and why he has to John Pombe Magufuli only and nobody else, kwa sasa mimi siziamini, na kwa vile siziamini, naomba nisizitaje wala nisiziseme kabisa humu.

Hivyo naomba sasa tuchukulie bandiko hili kuwa ni mwana JF mmoja kwa jina la Paskali, nilijiandikia tuu kuwa mgombea urais wa CCM kwa mwaka 2015 atakuwa ni Dr. John Pombe Magufuli, na ikatokea tuu kuwa ni kweli, mgombea urais wa CCM kwa 2015 akawa ni John Pombe Magufuli, yaani it just happened!.

Nawaombeni sana tuchukulie kupitishwa kwa jina la Dr. John Pombe Magufuli, kuwa mgombea urais wa CCM, has just happened tuu na has nothing to do bandiko hili wala na sababu nilizotajiwa, bali kuhesabike tuu kuwa kumetokea tuu naturally, by chance, bila any pre meditated moves, na hili bandiko lichukuliwe tuu kama just a coincidence, kuwa mwana jf mmoja nilisema mgombea wa CCM kwa mwaka 2015 atakuwa ni John Pombe Magufuli na kweli ikatokea tuu coincidentally, mgombea urais wa CCM kwa mwaka 2015 kweli akawa ni Dr. John Pombe Magufuli.

Kwa mtakaonielewa asanteni kwa kunielewa, na kwa wale ambao ni wazito kuelewa mambo ya kufikirika tuu au ambao msio nielewa poleni na samahanini sana!.

Hongera sana Dr. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuteuliwa kuwa mgombea urais wa Chama cha Mapinduzi, CCM.

Paskali
 
Tunahitaji rais kama magufuli,nchi hii imechoshwa na siasa na sasa inataka utendaji na vitu vionekane kwa mipango,watu wanafanya nchi kama idara ya zimamoto, nchi imekuwa na slogani nyingi,mara ari mpya,maisha bora,kilimo kwanza, big result now,mabilioni ya kikwete...magufuli hana upuuzi huo,yeye anafanya kazi japo ana mapungufu, mapungufu hayo yanafunikwa na utendaji,usimamiaji.KAMA HAMTAMPA WA MUUNGANO,NI BORA TANGANYIKA IRUDI TUTAMPA URAIS WA HUKU
 
[h=1]Magufuli hakustahili baraza jipya[/h]

Na Nyaronyo Kicheere - Imechapwa 09 May 2012

MIONGONI mwa mawaziri machachari walioteka hata nyoyo za wananchi ni Waziri wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli.
Waziri Magufuli ni mtu anayejifunza kwa haraka kazi na mazingira ya kila wizara anayopangiwa. Hii ndiyo sababu amekuwa bingwa wa kukariri vituo vya daladala, treni, viwanja vya ndege, na hata mifugo na samaki katika wizara alizowahi kusimamia.

Kukariri barabara za lami na za changarawe, zilijengwa lini na nani na kwa gharama gani ndipo kumempa sifa na umashuhuri, lakini yanayofanyika katika wizara yake yanatisha.

Hata hivyo, rais makini, anayefuatilia utendaji kazi wa mawaziri katika kila wizara, angemwajibisha siku nyingi Dk. Magufuli kwa kushindwa kuzuia wizi, ubadhirifu au kutoa maagizo yaliyolisababishia taifa hasara kubwa.

Katika baraza hilo jipya ambalo aliyeteua anatuaminisha kwamba ni zuri kuliko lile la akina William Ngeleja, Omar Nundu, Mustapha Mkullo, Haji Mponda, Cyril Chami, Ezekiel Maige itabidi tujiulize kwa kigezo gani?

Kama ni ubadhirifu, wizi na udanganyifu Wizara ya Ujenzi ni nambari moja. Hii ndiyo wizara iliyonunua ile meli au boti maarufu pale Magogoni iitwayo MV Magendo ingawaje ubavuni imeandikwa RESCUE, yaani UOKOZI.

Boti hii ilinunuliwa enzi zile Magufuli akiwa Waziri wa Ujenzi chini serikali ya awamu ya tatu iliyoongozwa na Rais Benjamin Mkapa. Hadi leo boti ile iliyonunuliwa kwa fedha za kigeni haijafanya kazi.

Ilipofika kwenye fukwe za Tanganyika boti hiyo ikawa inatumika kuchota na kufyonza mafuta kwenye meli na boti zingine bandarini na kuyauza kwa wavuvi, ndiyo maana ikaitwa MV Magendo.

Baada ya muda kidogo boti hiyo ikapwelezwa kwenye mchanga ambako hadi leo haifanyi kazi ya kuokoa kama tulivyotangaziwa siku ya uzinduzi kwenye kivuko cha kuelekea Kigamboni.
Bahati mbaya si wafanyakazi wa wakala wa vivuko au serikali wanaohoji aliyehusika kuagiza boti mbovu isiyofanya kazi wala kudai wahusika waitengeneze boti hiyo ili iweze kuwadumia wananchi.
Si hivyo tu, hakuna hata mfanyakazi mmoja kuanzia watendaji serikalini hadi wakala wa vivuko aliyepewa adhabu. Hata Waziri Magufuli hakuwajibishwa kwa hilo na sasa yumo kwenye baraza jipya.
Ubadhirifu mwingine uliofumbiwa macho katika wizara hiyo ni juu ya uagizaji, ununuzi na ufungaji mitambo ya kukatia tiketi kwenye kivuko cha kigamboni ambayo haikuwahi kufanya kazi tangu inunuliwe miaka yapata sita au saba iliyopita.
Sisi tunaokaa Kigamboni tunakumbuka vizuri sana jinsi serikali ilivyotutangazia kuwa wafanyakazi Kivukoni ni wezi sana na kwamba wanaiba mapato hivyo ikasema imekuja na mbinu mpya ya kukomesha wizi huo wa mapato â€" ikanunua wa mitambo ya kukatia tiketi.
Mitambo iliagizwa kwa pesa za kigeni, ikafungwa pale Kivukoni upande wa Magogoni na kusababisha milango miwili ya wapita kwa miguu kufungwa kwa miaka yote sita sasa.
Mitambo haitumiki, haitengenezwi na wala haiondolewi licha ya kusababisha kero ya msongamano kwa wasafiri kulazimika kupita mlango mmoja uliobaki.
Japokuwa hakuna ushahidi wa Magufuli kuhusika moja kwa maoja katika ununuzi wa boti mbovu na mitambo chakavu ya kukatia tiketi, alipaswa kuwashtaki wahusika au yeye mwenyewe kuwajibishwa kutokana na makosa ya waliochini yake. Magufuli hakuwajibishwa.
Lakini hakuna atakayebisha Magufuli alivyohusika kupigia debe uuzwaji wa nyumba za serikali bila kujali gharama ya maeneo nyumba hizo zilipokuwa zimejengwa.
Mbaya zaidi baadhi ya watu waliouziwa nyumba hizo hawakustahili kwani hawakuwa watumishi wa serikali. Kwa nini Magufuli hakuwajibishwa?
Wauzaji nyumba walitoa kigezo kwamba anayestahili kuuziwa nyumba hizo lazima awe mfanyakazi tu wa serikali ya muungano. Kigezo hicho hakikuzingatiwa.
Hii si mara ya kwanza habari hizi kuandikwa. Wakati zilipoandikwa magazetini yapata miaka minne iliyopita si Magufuli aliyejali wala mamlaka iliyomteua. Mpaka leo hajawajibishwa.
Dk. Magufuli pia aliagiza kuvunjwa kituo cha mafuta jijini Mwanza na kuliingiza taifa katika mgogoro mkubwa ambao uliishia mahakamani na serikali ikatakiwa kulipa mamilioni ya shilingi. Magaufuli hakuwajibishwa.
Kituo cha mafuta kimejengwa ndani ya mipaka ya jiji la Mwanza kwa vibali vya uongozi wa jiji. Lakini badala ya Magufuli kufuata taratibu za kisheria za kuchukua eneo la mtu binafsi alitumia mabavu na jazba huku akidai anatekeleza sheria.
Dk. Magufuli pia alilazimisha kuvunjwa nyumba katika barabara ya Morogoro pale Ubungo na Kimara mwaka 1997 na kuliingiza taifa katika mgogoro na raia wake na kuisababishia serikali hasara ya Sh. 65 milioni. Magufuli hakuwajibishwa.
Kwa bahati nzuri kwa upande wa serikali wakazi wa Ubungo - Kimara walikuwa mbumbumbu hawakwenda mahakamani kudai fidia ya mamilioni ya shilingi baada ya kuelewa vibaya hukumu ya maombi yaliyowasilishwa na wakili wao Profesa Mgongo Fimbo ndiyo maana hawakwenda mahakamani kudai.
Mmoja wa raia hao ambaye alilielewa vizuri shauri hilo Bw. Ebeneza Massawe, alikwenda mahakamani na kushinda kesi. Alilipwa na serikali Sh. 65 milioni.
Je, wote waliovunjiwa nyumba zao Ubungo na Kimara wapatao zaidi ya 350 wangefika mahakamani kudai fidia, serikali ingelipa kiasi gani?
Ikiwa mawaziri sita waliotemwa, Rais Jakaya Kikwete amesema ni uwajibikaji wa kisiasa, kwa rekodi hii ya usimamizi wa Dk. Magufuli alipaswa kuwajibishwa kwa kuondolewa kwenye baraza la mawaziri mara moja kwa sababu hatufai.
nkicheere@gmail.com; 0787788727/0718582755
 
Kitabu cha siri ndani ya CCM kinasema " ni haramu kafiri (mkristo) kuwa mgombea uraisi kwa tiketi ya CCM. Mi sishangahi kuona Magufuli ndo mgombea uraisi kwa tiketi ya CCM ila watambue kuwa nchi hii haina dini, kabila, wala kanda.Nchi ni yawote...
Jiulize je! Katika historia ya Tanzania kashatokea mgombea uraisi mkristo kwa tiketi ya CCM?
Waache ujinga tuijenge nchi.
 
Tunahitaji rais kama magufuli,nchi hii imechoshwa na siasa na sasa inataka utendaji na vitu vionekane kwa mipango,watu wanafanya nchi kama idara ya zimamoto, nchi imekuwa na slogani nyingi,mara ari mpya,maisha bora,kilimo kwanza, big result now,mabilioni ya kikwete...magufuli hana upuuzi huo,yeye anafanya kazi japo ana mapungufu, mapungufu hayo yanafunikwa na utendaji,usimamiaji.KAMA HAMTAMPA WA MUUNGANO,NI BORA TANGANYIKA IRUDI TUTAMPA URAIS WA HUKU
Pasco naona ulikuwa na nia ya kuwasiliana na mke wa magufuli naona kaingia hapa na id nyingine baada ya ile ya iparamasa kupigwa ban
 
Mimi naweza nikataja baadhi ya sababu ulizoambiwa.
Mosi, anatoka kanda ya ziwa ambako inadaiwa kuwa ni kanda iliyoikimbia ccm 2010. Hata majimbo waliyonayo mengi waliyachakachua.
Ile hoja ya kitoto ya kidini inaweza kuwa imejificha humo
Umachachari wake inaweza kuwa sababu mojawapo
Inaweza kuwa ni mtu muhimu kuwasaidia akina nani hili kumdhibiti mtu kwa kuwa kanda ya ziwa ina watu wengi. Nawaza tu shemeji yangu pasco
 
Kumbe kampeni zishaanza,EL vipi au umesusa???
Tunahitaji rais kama magufuli,nchi hii imechoshwa na siasa na sasa inataka utendaji na vitu vionekane kwa mipango,watu wanafanya nchi kama idara ya zimamoto, nchi imekuwa na slogani nyingi,mara ari mpya,maisha bora,kilimo kwanza, big result now,mabilioni ya kikwete...magufuli hana upuuzi huo,yeye anafanya kazi japo ana mapungufu, mapungufu hayo yanafunikwa na utendaji,usimamiaji.KAMA HAMTAMPA WA MUUNGANO,NI BORA TANGANYIKA IRUDI TUTAMPA URAIS WA HUKU
 
Kitabu cha siri ndani ya CCM kinasema " ni haramu kafiri (mkristo) kuwa mgombea uraisi kwa tiketi ya CCM. Mi sishangahi kuona Magufuli ndo mgombea uraisi kwa tiketi ya CCM ila watambue kuwa nchi hii haina dini, kabila, wala kanda.Nchi ni yawote...
Jiulize je! Katika historia ya Tanzania kashatokea mgombea uraisi mkristo kwa tiketi ya CCM?
Waache ujinga tuijenge nchi.
Are you ok....?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom