Elections 2015 Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John Pombe Magufuli

Tunachosahau tu ni kwamba utake usitake unaposhika ile nafasi kuna tabia baadhi za mtu hubadilika sababu lile ni jukumu zito sana. Mara nyingi huwa kuna mazuri na mabaya ambayo mtu huweza kuwa nayo pindi tu anapopata ile nafasi.
 
Basi wewe pia ni mhanga wa mwalimu nyerere alikamata wahujumu uchumi,lkn na wale waliopata mali kwa jasho lao nao walifilisiwa,Pia wewe ni mhanga wa mh. Mwinyi kwani yalikamatwa mapesa mengi uwanja wa ndege na Mrema ikulu ikamnyamazisha na kipindi hicho ndo skandari za kusafirisha wanyama zilianzia, wewe pia ni mhanga wa mh, mkapa kwani uwekezaji na mikataba inayoitesa nchi hadi sasa ilianzia hapo,ya sasa unayajua sina haja ya kueleza ninachotaka kusema ni kwamba hakuna mtu perfect,tunalinganisha mapungufu yake na mema ya mtu mema yakizidi mabaya tunasema ni mwema hata kama kuna baadhi ya mabaya aliyoyatenda

Pia nikukumbushe tunachotafsiri kuwa ni kibaya ni nia ya mtendaji,alikuwa na nia gani alipotenda jambo hilo.Kuna wengine nia yao inakuwa nzuri lkn utekelezaji unazaa matokeo hasi hadi yule mtu anajutia,lkn wapo wengine tokea mwanzoni nia yao inakuwa ovu ili wapate maslahi.

Magufuri wakati anauza nyumba za serikali alikuwa anakomesha tabia ya watu kupitisha fedha nyingi kwa kisingizio cha ukarabati na hivyo kutumia hela nyingi kuliko thamani ya nyumba zenyewe,matokeo yake akajikuta ameuza na ardhi ya maeneo nyeti kama vile masaki.lAITI ANGEZIBOMOA NYUMBA ARDHI IKABAKI,INGETUMIWA KWA FAIDA.

Natamani watanzania tuwapime watu kwa uwezo wao binafsi bila kuwahusisha na vyama vyao,ukimhusisha magufuri na chama chake kweli utasema hafai,lkn akiwa mkuu wa nchi atakuwa msemaji mkuu na hivyo kutakuwepo mabadiliko.
swali langu ni je hicho chama kitamchagua awe mgombea urais? maana wengi ni wahanga wa magufuri.
ONGERA MAGUFURI KWA KAZI NZURI KAMA WATZ HAWAONI MUNGU ANAONA.

..hivi kwa exposure ya Magufuli unataka kuniambia alikuwa hajui thamani halisi ya nyumba na viwanja kwa maeneo zilipokuwa nyumba za serikali?

..nakuhakikishia kwamba hawa waliamua kwa makusudi kabisa KUIBA nyumba zile na hakuna haja ya sisi wananchi kumung'unya maneno kuhusu nini kilitokea.

..Magufuli alikwenda mbali zaidi kwa kuwabeza waliokuwa wakipinga wizi ule na kutamka bungeni kwamba serikali itapata mapesa mengi na kuweza kujenga nyumba nyingi zaidi ya zile ilizouza.

..wa-Tz tunapaswa kubadilika na kukataa kuwa ABUSED na hawa tunaowaita viongozi. why put up with these ppl? kila mara wakiboronga basi tunatengeneza visababu[walikuwa na nia nzuri, tuangalie mema yao] vya kuendelea kuwahifadhi madarakani.

..binafsi sioni faida yoyote ile ya kuendelea kuwa na kiongozi ambaye tunajua kabisa ameisababishia nchi hasara inayoweza kufikia trillion of shillings.

NB:

..hivi Magufuli aliyeiba akiwa waziri wa ujenzi unategemea ataacha wizi tukimpa madaraka makubwa zaidi ya Uraisi?

..Magufuli huyu mwenye kiburi, dharau, na kauli za hovyo-hovyo akiwa waziri, unategemea atakuwa na staha na unyenyekevu akiwa Raisi?

cc Pasco
 
Last edited by a moderator:
Tunachosahau tu ni kwamba utake usitake unaposhika ile nafasi kuna tabia baadhi za mtu hubadilika sababu lile ni jukumu zito sana. Mara nyingi huwa kuna mazuri na mabaya ambayo mtu huweza kuwa nayo pindi tu anapopata ile nafasi.

..lakini ukiangalia kwa umakini utakuta wanabadilika kwa kupungukiwa kimaadili.

..Raisi wa Tanzania ana madaraka makubwa sana. yuko sawa na "mungu mtu."

..sasa ukimpa nafasi hiyo mtu asiye na maadili basi uwezekano mkubwa ni ku-abuse the office.

cc Pasco, tz2015, Kigogo
 
..lakini ukiangalia kwa umakini utakuta wanabadilika kwa kupungukiwa kimaadili.

..Raisi wa Tanzania ana madaraka makubwa sana. yuko sawa na "mungu mtu."

..sasa ukimpa nafasi hiyo mtu asiye na maadili basi uwezekano mkubwa ni ku-abuse the office.

cc Pasco, tz2015, Kigogo

mkuu,wewe binafsi unadhani nani angeweza kuwa Rais bora kwa Tanzania baada ya Kikwete kumaliza muda wake kati ya hawa wagombea wanaotajwa au hata wasiotajwa?
 
..lakini ukiangalia kwa umakini utakuta wanabadilika kwa kupungukiwa kimaadili.

..Raisi wa Tanzania ana madaraka makubwa sana. yuko sawa na "mungu mtu."

..sasa ukimpa nafasi hiyo mtu asiye na maadili basi uwezekano mkubwa ni ku-abuse the office.

cc Pasco, tz2015, Kigogo
Iwapo vetting ya viongozi ingefanywa na JF asingepita mtu labda aje malaika!
 
Iwapo vetting ya viongozi ingefanywa na JF asingepita mtu labda aje malaika!

..hatujasema tunataka Malaika.

..lakini pamoja na hayo hatuhitaji mtu ambaye tunajua ameshatutia hasara ya matrilioni kutokana na maamuzi yake.

..baya zaidi Dr.Magufuli haonekani kujutia uamuzi wake, na kufanya juhudi zozote zile kurekebisha makosa yake.

cc tz2015
 
Last edited by a moderator:
mkuu,wewe binafsi unadhani nani angeweza kuwa Rais bora kwa Tanzania baada ya Kikwete kumaliza muda wake kati ya hawa wagombea wanaotajwa au hata wasiotajwa?

..kwanza tunatakiwa tubainishe tunahitaji kiongozi wa aina gani.

..nini malengo yetu na vipaumbele vyetu ktk miaka 5, 10, 20, ijayo.
 
..kwanza tunatakiwa tubainishe tunahitaji kiongozi wa aina gani.

..nini malengo yetu na vipaumbele vyetu ktk miaka 5, 10, 20, ijayo.

mkuu mahitaji yetu ni mengi na yanajulikana,na hata wewe unayajua.Kwa kifupi sana,binafsi ningetamani tupate mtu wa kututoa hapa tulipo na kutupeleka pazuri zaidi kimaendeleo ya kijamii,kiuchumi na kisiasa kwa miaka mitano kwa kuanzia ie 2015-2020..kati ya hao wanaotajwa na wengine wasiotajwa,unadhani nani anafaa mkuu?naomba unitajie jina lake
 
..hatujasema tunataka Malaika.

..lakini pamoja na hayo hatuhitaji mtu ambaye tunajua ameshatutia hasara ya matrilioni kutokana na maamuzi yake.

..baya zaidi Dr.Magufuli haonekani kujutia uamuzi wake, na kufanya juhudi zozote zile kurekebisha makosa yake.

cc tz2015
Labda mkuu wewe tupe pendekezo lako la rais mtarajiwa 2015,unaweza ukawa unatumia sheria ya dawa ya moto ni moto,ikiwa na maana ya mahali palipoharibika weka aliyeharibika. Kama unatumia sheria hii basi Dr Magufuri hafai.
ieleweke kwamba naongelea chama tawala najua nje ya ccm wapo watu wenye uwezo mkubwa wa kuleta mabadiliko nchi hii.
 
Tumeisha waona wapole na wasikivu...wanavyoendesha nchi...tumejua faida zao na hasara zao...sasa tunataka tuwaone ambao ni wakali na si wasikivu linapokuja suala la kufuata sheria....kama hizo sheria wanazijua wao tu watafsri sheria (judiciary) na raia wengine zinawatatiza basi mfumo wa judiciary una matatizo makubwa...unahitaji kufumuliwa ili uweze kutuletea sheria upitia miswada ya sheria inyoeleweka kwa watu wote...maana sheria ni kwa ajili ya watu wote siyo wanasheria tu.

Apite Maghufuli.
 
mkuu mahitaji yetu ni mengi na yanajulikana,na hata wewe unayajua.Kwa kifupi sana,binafsi ningetamani tupate mtu wa kututoa hapa tulipo na kutupeleka pazuri zaidi kimaendeleo ya kijamii,kiuchumi na kisiasa kwa miaka mitano kwa kuanzia ie 2015-2020..kati ya hao wanaotajwa na wengine wasiotajwa,unadhani nani anafaa mkuu?naomba unitajie jina lake
NgumiJiwe, tz2015,

..mgombea ninayemtaka mimi sidhani kama atapatikana CCM.

..nasema hivyo kwasababu CCM wameshauhalalisha ufisadi.

..tunahitaji mtu ambaye atakuja kusimika namna mpya ya kuendesha nchi ambapo tutaongozwa kwa haki, maadili, na sheria.
 
Last edited by a moderator:
Wanabodi,

Leo nimekutana na rafiki yangu wa siku nyingi, ambaye ni mtu wa kuaminika na ni kada wa Chama cha Mapinduzi-CCM, akanieleza seriously habari za kushtusha kidogo ambazo mimi pia zimenihuzunisha, kunisikitisha na kunisononesha!, kuwa eti imeishaamuliwa mgombea wa urais wa mwaka 2015 kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi-CCM ni Mhe. John Pombe Magufuli!.

Kilichonistua, kunihuzunisha, kunisikitisha na kunisononesha, ni the reasons behind alizonitajia ambazo ndizo zimepelekea CCM kuamua why ni lazima awe Magufuli tuu, and no one else!.

Kwa vile sababu hizo alizonitajia, baadhi ni justifiable na nyingine sio tuu ni unjustifiable!, bali hazikubaliki kabisa katika Tanzania ya leo!. Naomba kwa sasa nisizitaje kwanza, kwa sababu habari zenyewe nimezisikia from a single source, nahitaji kwanza kufanya collaborative verification na kupata attribution ili nijiridhishe kuwa ni za kweli na kuthibitisha kuwa hivyo ndivyo CCM inavyoweza kufikia maamuzi based on hayo niliyoyasikia!, then nitaziweka hadharani hizo sababu za CCM on Why ni Magufuli!.

Kwa kawaida sisi waandishi, ukipata taarifa kama hii, huwa inaitwa "news tip", haukimbilii kuiandika mbio mbio mpaka kwanza uifanyie verification kuthibitisha ukweli wa taarifa yenyewe, lakini kwa vile sasa tunaishi kwenye "the world of information age", nimeamua kuileta hii "news tip" humu jf, hivi hivi ikiwa kwenye hatua ya "tip" kabla hata ya verification, ili wewe kama mwana jf, uipate ile advantage ya jf, "be the first to know!", hivyo nawaombeni tuu sasa mkae mkijua, "Mgombea wa CCM 2015 ni John Pombe Magufuli!"

Nikiisha "confirm" neno "tetesi" litaondolewa na kuwa replaced na neno "confirmed!", na nitaziweka hizo sababu ila sasa ndio zijadiliwe!, na nawahakikishia wale wote wenye mapenzi mema na taifa hili, mkizisikia hizo sababu za CCM!, na nyinyi pia zitawashtua, kuwahuzunisha, kuwasikitisha na kuwasononesha!. Naomba nisiwatajie jina la huyo source wangu chini ya kinga ya kihabari inayoitwa "The Confidentiality of the source".

NB. Sio kila thread ni lazima ichangiwe, saa nyingine itoshe kujisomea tuu na kujipitia bila kuchangia chochote!. Hii ni just a news tip, kwa vile nimewaahidi naifanyia verification kuithibitisha, nawaombeni msiniulize swali lolote at this stage, kwa sababu sitajibu chochote!, and if possible nawashauri na nyingi msome FYE only na sio lazime mchangie kwa sasa na badala yake mvute subira kusubiria verification.
Sababu ya kuiwahisha humu jf kabla ya verification ni ili tuu wewe kama mwana jf to be the first to know!. Information is power!, if you are the first to know, then you'll have the powers to make good things happen or not to happen if they are bad things!.


Asante.
Pasco.
Nafanya tuu rejea!.

Pasco
 
Nafanya tuu rejea!.

Pasco

Huu uzi wako wako ni sawa na uzi mmoja wa Weston Songoro uliandikwa wiki moja iliyopita kuhusu mipango ya Nchimbi, Sophia Simba na Jerry Silaha kuleta MTITI endapo EL asipopitishwa alafu usiku wa kuamkia jana kina Kimbisa, Sophia Simba na Nchimbi wakaibuka kwa waandishi wa habari kupeleka kilio chao
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom