Mgombea wa nafasi ya uwakilishi kwa tiketi ya chadema katika jimbo la Uzini Zanzibar anatarajiwa kurudisha fomu yake leo Tume ya Uchaguzi Zanzibar ili ateuliwe kukiwakilisha Chama hicho katika uchaguzi huo.
Zoezi hilo linatarajiwa kuanza majira ya saa 4 asubuhi ambapo Fuso la matangazo, magari, pikipiki na baiskeli zitamsindikiza mgombea huyo. Habari kutoka Zanzibar zinasema Makamanda maalum wa Chadema waliokuwa wametangulia Zanzibar wamefanikiwa kufungua matawi 20 katika Shehiya zote 13 yenye jumla ya wanachama 1236.
Mgombea huyo wa Chadema alishika nafasi ya pili katika uchaguzi wa mwaka 2010 akifuatiwa na mgombea wa CUF.
Zoezi hilo linatarajiwa kuanza majira ya saa 4 asubuhi ambapo Fuso la matangazo, magari, pikipiki na baiskeli zitamsindikiza mgombea huyo. Habari kutoka Zanzibar zinasema Makamanda maalum wa Chadema waliokuwa wametangulia Zanzibar wamefanikiwa kufungua matawi 20 katika Shehiya zote 13 yenye jumla ya wanachama 1236.
Mgombea huyo wa Chadema alishika nafasi ya pili katika uchaguzi wa mwaka 2010 akifuatiwa na mgombea wa CUF.