Uchaguzi 2020 Mgombea wa kumshinda Magufuli 2020 awe na sifa zifuatazo

ndege JOHN

JF-Expert Member
Aug 5, 2015
19,551
44,704
Vigezo anavyotakiwa Kuwa navyo Ni pamoja na

1.Atuambie ni hatua gani mpya atakazochukua za kumaliza kabisa suala la ufisadi ambalo bado linaonekana kutajwa lipo.Atuambie atavitumiaje vyombo husika ku deal na corruption kikamilifu.

2.Atuambie atashughulikiaje ishu ya Kuwa na KATIBA MPYA dakika za mwisho katiba mpya inahitajiwa na wengi unfortunately mliokuwa wajumbe wa bunge la katiba mkatuangusha.Lakini tunataka vipaumbele vya katiba viwe vitakavoweza kubadilisha Hali hii ya matumizi makubwa serikalini na sio kujadili namna ya kugawana POWER za kisiasa.

3.Kuna ishu hii ya watu kuongezeka sambamba na miundominu.magufuli anajenga reli huyo anayetaka kumshinda Magufuli kwenye uchaguzi aje na ahadi ya kuunganisha mikoa yote nchini na reli na kununua treni nyingi Zaidi

4.Aje na ahadi ya kubadilisha SHERIA ya vyombo vya ulinzi na usalama ili katika majukumu yake viingiliane kikamilifu.Kwa mfano haiwezekani mpaka sasa Kuna maeneo yana uhalifu kwa sababu tu hakuna Askari wa polisi,wakati tuna wanajeshi wengi sana katika makambi kwanini wasigawanyishwe nusu wasimamie mipaka ya nchi na nusu wengine waungane na polisi wetu ili kudhibiti kabisa uhalifu mitaani kwani na uhakika wanajeshi wanaogopwa sana na watu so hata wakipangiwa tu patrol kuwa wanapita mitaani,mijini na uhakika matukio ya uhalifu na utapeli yataisha.

Ebu imagine kila siku wanajeshi wawe wanaingia mtaani kulinda raia wamevaa kijeshi wanazunguka zunguka yale maeneo yanayoonekana Kuwa korofi na wahuni wengi mitaa ya Dar es salaam kusingesikika makundi ya vibaka.
 
Bashite hiyo kazi akipewa anaimaliza saa nne asubuhi.
ndio mwanadamu pekee anayeweza kumshinda JPM wakishindana 2020.

Ni kijana mwenye uwezo mwingi na mkubwa sana
 
Kumbe ni kuahidi tu.. Khaa sasa ata mimi si nina weza kukuahidi hayo yote ulio orodhesha
 
Back
Top Bottom