Mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Miraji Mtaturu amepita bila ya kupingwa katika uchaguzi mdogo kwenye Jimbo la Singida Mashariki, baada ya wagombea 12 wa vyama vya upinzani kutorejesha fomu. Uchaguzi mdogo utafanyika Julai 31 kufuatia Wakili Tundu Lissu kuvuliwa ubunge.