barafu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2013
- 6,726
- 32,818
Akiwa Wilayani Chemba-Dodoma, akielekea makao makuu ya nchi Dodoma, mgombea Urais wa CCM amesimama na kuhutubia hadhira ya wana-Chemba. Lakini katika jambo la kushangaza ambalo pengine NEC wanapaswa kuliona kama sehemu ya kinyume na utaratibu, Mgombea Urais wa CCM anasema wagombea wengine wanaoonekana kwenye karatasi ya kupigia kura siyo halali na hawapaswi kupigiwa kura. Jina halali na linalopaswa kupigiwa kura ni jina namba moja ndio maana hata NEC wameliweka juu.
Mgombea huyo amenukuliwa akisema
"Unapopiga kura Jumatano, angalia jina la kwanza kabisa, ndio Chama Cha Mapinduzi na jina langu lipo, weka tiki hapo. Usiangalie majina mengine ya chini, hayo yote siyo majina halali ya wagombea. Usipoteze muda kuyaangalia, angalia jina la kwanza na ukimaliza kupiga nenda ukalale. Mkawape fundisho wale wanaohubiri kuwa muandamane baada ya kupiga kura"--
Je kutangazia umma kuwa majina na wagombea wengine siyo halali ni sehemu ya kampeni? Mgombea ambaye ana nafasi ya Urais anaposema wagombea wengine siyo halali na majina yao si halali, Je haiathiri uchaguzi katika uvunjaji wa kanuni? Nini nafasi ya NEC katika kauli kama hizi?
Mgombea huyo amenukuliwa akisema
"Unapopiga kura Jumatano, angalia jina la kwanza kabisa, ndio Chama Cha Mapinduzi na jina langu lipo, weka tiki hapo. Usiangalie majina mengine ya chini, hayo yote siyo majina halali ya wagombea. Usipoteze muda kuyaangalia, angalia jina la kwanza na ukimaliza kupiga nenda ukalale. Mkawape fundisho wale wanaohubiri kuwa muandamane baada ya kupiga kura"--
Je kutangazia umma kuwa majina na wagombea wengine siyo halali ni sehemu ya kampeni? Mgombea ambaye ana nafasi ya Urais anaposema wagombea wengine siyo halali na majina yao si halali, Je haiathiri uchaguzi katika uvunjaji wa kanuni? Nini nafasi ya NEC katika kauli kama hizi?