Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,463
- 113,531
Asante uchambuzi mzuri.Hii aya ndiyo iliwapukutisha watajwa sifa za kuwa halali kupewa kijiti cha kuwakilisha vyama vyao.
Mfano: 1. Kitendo cha mleta mada kudai kuwa "....bado wana kazi kubwa ya kuaminisha watanzania kwamba atakayepita atakuwa Rais Bora na sio Bora Rais;....", ilikuwa wazi kabisa Mchambuzi alikuwa anajua fika hawa kwawakati huo walikuwa na sifa ya " bora rais". Hivyo wafuatilia mambo waling'amua mapema.
Mfano: 2. Pia Mchambuzi aling'amua mapema kuwa hata vyama vya ukawa vilijikita kwenye personalities badala ya issues. Hata mtanjwa alijikita zaidi kwenye personalities kumbuka "... orodha ya aibu ya Mwembeyanga...", wàandaji wa orodha wote hawakuwa na issues bali personalities matters kama ngao zao za kuaminiwa nawatanzania.
CCM ilitumia ushauri wa Mchambuzi kufanya maamuzi sahihi. Na baada ya CCM kushughulikia issues na kuua kabisa mambo ya personalities kwenye uendeshaji waserikali wale watumia hoja za personalities hawana lao kisiasa.
Watu kama hawa Mchambuzi, ndio ma GT wa ukweli!, sijui amepotelea wapi?!.
P