Mgombea udiwani Kata ya Elerai Manispaa ya Arusha kwa tiketi ya Chama cha Tanzania Labour(TLP), Boysafi Peter Shirima jana alitangaza kujiondoa katika kinyanganyiro hicho na kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Akitangaza uamuzi huo mbele ya umati wa watu, waliohudhuria mkutano wa hadhara wa kampeni zinazoendelea katika kata hiyo, alidai kuwa amejitoa katika chama hicho kutokana na chama kushindwa kuzindua kampeni za kumnadi licha ya kuwa mgombea kwa mkoa mzima wa Arusha.
Akitangaza uamuzi huo mbele ya umati wa watu, waliohudhuria mkutano wa hadhara wa kampeni zinazoendelea katika kata hiyo, alidai kuwa amejitoa katika chama hicho kutokana na chama kushindwa kuzindua kampeni za kumnadi licha ya kuwa mgombea kwa mkoa mzima wa Arusha.