Nyange
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 3,516
- 1,865
Ama kweli watanzania sijui itakuwaje! Napiga picha wajukuu zetu watatuelewaje jinsi tulivyo changia kuharibu nchi tuliyo jaliwa yenye maziwa na asali.
Juma pili nikiwa nyumbani, baada ya kutoka kazini, nilikuta ujumbe kuwa natafutwa sana kuna kikao cha wanachama wa thithiem, japo mi ni mwanachama lakini sijawahi kumpigia kura mwanachama wangu kwa sababu mi nachagua uwezo wa mtu na si chama. Ukweli ni kwamba nimeshiriki kupiga kura mara nne tangu kuzaliwa, japo huwa nachagua uwezo wa mtu na si chama hivo sijawahi kumchagua mgombea wa thithiem kwakuwa wanaoteuliwa kugombea binafsi naona hawafai.
Nikiwa naangalia taarifa ya Aljazira jioni, nikapigiwa simu na mzee maarufu kuwa nasubiliwa. Ikabidi niende mbio kuona kulikoni. Kufika kwenye kusanyiko hilo, mara VX ikawasili ikiwa na mgombea mtarajiwa wa udiwani akiongozana na mamaa. Mara akaanza kuelezea kwa nini ametuita, pia kuelezea jinsi alivyo tenda kipindi kinacho malizika cha miaka mitano iliyopita. (alikuwa diwani wa Kimara Baruti). Na baada ya hapo akaomba watu watoe maoni na ushauri.
Nilikuwa wa kwanza kushauri, nikasema ' nakushukuru sana mtarajiwa make we si wa design ninazo ziona za wagombea, kwani kugombea ni kwenda kutatua matatizo ya watu hivyo kutoa pesa, haiingii akilini kwa kuwa uongozi ni shida tupu kwa nini ununue shida? Sana sana tunatarajia wanachama wa ku-support ili uweze kuweka mafuta kwenye gari ili uwazungukie wapiga kura wako na kuwaelezea malengo yako. Nikasisitiza kuwa, ukiona mgombea anatoa fedha, ujue kuwa hajui anafanya nini na akiwa kiongozi atafanya nini'
Wakati akijibu ushauri huo, alijibu kuwa ' mgonjwa mwenye kansa ya damu, akienda Hospitali dakitari hawezi kumwacha hivihivi, atampa panado ili impunguzie maumivu tu japo kuwa ina tazamiwa atakufa tu'
Kauri hii imethibitisha kuwa kweli chama kilichopo madarakani hakijui kina fanya nini, na viongozi wa thithiem wamezoea rushwa na hivyo hawawezi kusaidia nchi.
Mara baada ya yeye kuondoka kumbe kaacha mtu agawe sh. 5,000 kwa waliofika! Mi nilikimbia nikaona ni uchuro!
WADAU KWELI NCHI HII THITHIEM INAIPELEKA WAPI?
Juma pili nikiwa nyumbani, baada ya kutoka kazini, nilikuta ujumbe kuwa natafutwa sana kuna kikao cha wanachama wa thithiem, japo mi ni mwanachama lakini sijawahi kumpigia kura mwanachama wangu kwa sababu mi nachagua uwezo wa mtu na si chama. Ukweli ni kwamba nimeshiriki kupiga kura mara nne tangu kuzaliwa, japo huwa nachagua uwezo wa mtu na si chama hivo sijawahi kumchagua mgombea wa thithiem kwakuwa wanaoteuliwa kugombea binafsi naona hawafai.
Nikiwa naangalia taarifa ya Aljazira jioni, nikapigiwa simu na mzee maarufu kuwa nasubiliwa. Ikabidi niende mbio kuona kulikoni. Kufika kwenye kusanyiko hilo, mara VX ikawasili ikiwa na mgombea mtarajiwa wa udiwani akiongozana na mamaa. Mara akaanza kuelezea kwa nini ametuita, pia kuelezea jinsi alivyo tenda kipindi kinacho malizika cha miaka mitano iliyopita. (alikuwa diwani wa Kimara Baruti). Na baada ya hapo akaomba watu watoe maoni na ushauri.
Nilikuwa wa kwanza kushauri, nikasema ' nakushukuru sana mtarajiwa make we si wa design ninazo ziona za wagombea, kwani kugombea ni kwenda kutatua matatizo ya watu hivyo kutoa pesa, haiingii akilini kwa kuwa uongozi ni shida tupu kwa nini ununue shida? Sana sana tunatarajia wanachama wa ku-support ili uweze kuweka mafuta kwenye gari ili uwazungukie wapiga kura wako na kuwaelezea malengo yako. Nikasisitiza kuwa, ukiona mgombea anatoa fedha, ujue kuwa hajui anafanya nini na akiwa kiongozi atafanya nini'
Wakati akijibu ushauri huo, alijibu kuwa ' mgonjwa mwenye kansa ya damu, akienda Hospitali dakitari hawezi kumwacha hivihivi, atampa panado ili impunguzie maumivu tu japo kuwa ina tazamiwa atakufa tu'
Kauri hii imethibitisha kuwa kweli chama kilichopo madarakani hakijui kina fanya nini, na viongozi wa thithiem wamezoea rushwa na hivyo hawawezi kusaidia nchi.
Mara baada ya yeye kuondoka kumbe kaacha mtu agawe sh. 5,000 kwa waliofika! Mi nilikimbia nikaona ni uchuro!
WADAU KWELI NCHI HII THITHIEM INAIPELEKA WAPI?