Mgombea ubunge Jimbo la Kilolo kwa tiketi ya CHADEMA, Brian Kikoti atimkia CCM. Alimchachafya Mwamoto mwaka 2015

Daimler

JF-Expert Member
Sep 11, 2018
556
973
IMG_9811.JPG

Brian Kikoti.

Aliyekuwa Mgombea ubunge katika Jimbo la Kilolo, mkoani Iringa kwa tiketi ya CHADEMA, Brian Kikoti amejiunga na CCM. Kikoti alitoa ushindani mkubwa kwa Mgombea wa CCM, Venance Mwamoto mwaka 2015. Katika matokeo hayo, Kikoti alipata kura 32,926, sawa na asilimia 41.6%.
IMG_9813.jpg

IMG_9809.JPG

Kikoti alipokuwa Mgombea Ubunge wa Kilolo mwaka 2015 kwa tiketi ya CHADEMA.
 
IIe kesi yake ya kumtapeli Mke wa Marehemu Fundikira iliishia wapi. Hivi hili suala Masauni alilipuuzia au ilikuwaje!?
 
View attachment 914533
Brian Kikoti.

Aliyekuwa Mgombea ubunge katika Jimbo la Kilolo, mkoani Iringa kwa tiketi ya CHADEMA, Brian Kikoti amejiunga na CCM. Kikoti alitoa ushindani mkubwa kwa Mgombea wa CCM, Venance Mwamoto mwaka 2015. Katika matokeo hayo, Kikoti alipata kura 32,926, sawa na asilimia 41.6%.
View attachment 914534

View attachment 914535
Venance Mwamoto aliyeshinda Uchaguzi Mkuu mwaka 2015. Mwamoto alikuwa pia Mbunge wa Kilolo mwaka 2000 - 2005.
Huyu mmepa dau lake shingapi maana na mimi niligombea ubunge kupitia TADEA lakini nilishindwa kwenye kura za maoni ndani ya Chama nataka ntumie fursa dau langu laweza kuwa kiasi gani?
 
fukueni tu makaburi
Jamaa kwa kutumia Benki moja nchini alituhumiwa kuchukua Hati ya nyumba ya Marehemu Fundikira na kwenda kukopea bila ya uelewa wa Mjane wa mke wa Fundikira. Hili jambo inasemwa lilifikishwa mpaka kwa Masauni ili alishughulikie. sasa kwa kuwa karudi "kulikonoga" inawezekana kesi ikafa na Mjane wa Fundikira kudhulumiwa!
 
Bryn bwana!! Huyu jamaa atajutia kujitoa CHADEMA. Kwa kweli watu wengi sana walimuunga mkono si kwa ubora wake bali kutokana na uchadema wake!!
Yes, walimuunga mikono kwa uchadema wake but still usisahau kuwa anajiweza kifedha. Na kwa taarifa yako, Kikoti aliwazidi wagombea wengine 4 wa CHADEMA tena kwa mbali akipata kura 215 huku aliyemfuatia Ahaz Challi akipata kura 12 pekee. Ajabu ni kwamba hata huyo Challi alipinga matokeo hayo na kutimkia CCM.
IMG_9818.jpg
 
Nilisikia huko Arumeru wanachama wa ccm kama mia moja hivi wamekikimbia chama chao sasa hii imekaaje
 
Aisee akili ulizokabidhi kwa mbowe kazichukue mkuu,

Mtu mliempitisha awe mgombea wenu mnamuita duni?

No wonder mnakili kwenye chama chenu kuna malaya wa kisiasa.
Duni kwa kuwa hana wadhifa hivi akili yako ipo sawa na ww unashindwa kuelewa mantiki ya jamaa?
 
Ni kawaida kwa mgonjwa mahututi kuomba kurudi kijijini kwao akafie huko ili awe jirani na makaburi ili asiwasumbue ndugu zake kusafirisha mwili.....ndugu huwa hawataki kumsikiliza mgonjwa.
 
Back
Top Bottom