Elections 2010 Mgombea ubunge Busega afa kifo cha utata

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
  • Yadaiwa ni mkono wa mtu
  • Aliugua gonjwa la ajabu
  • Alikataa kubadili nia hiyo
  • Jiji la Mwanza lazizima

Mwanamke aliyekuwa ametangaza nia ya kuomba uteuzi wa kugombea ubunge katika jimbo la Busega kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Magu, Mkoa wa Mwanza katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu, Nsega Aloyce Ntobi, amefariki dunia katika mazingira ya kutatanisha.

Kifo cha Nsega kimezua mjadala katika Jiji la Mwanza huku baadhi ya wakazi wakikihusisha na nia yake ya kutaka kugombea wadhifa huo wa kisiasa.

Habari zinasema kuwa Nsega alifariki usiku wa kuamkia juzi jijini Mwanza, wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando baada ya kuugua ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu.

Kifo hicho kimeghubikwa na utata huku baadhi ya wananchi wakidai kuwa kuna mkono wa wanasiasa kadhaa.

“Taarifa mpya inasema kuwa mgombea ubunge wa Busega, Nsega amepata ugonjwa huo siku mbili tu baada ya kukutana na (mwanasiasa ambaye jina tunalihifadhi) akiombwa ajitoe kwenye mchakato na yeye kukataa,” kilidai chanzo kimoja cha habari.

Habari zinadai kuwa saa chache kabla ya kuugua, Nsega alikutana na mwanasiasa mmoja aliyekuwa na nia ya kugombea ubunge katika jimbo hilo kwa ajili ya mazungumzo yaliyohusu mchakato wa kugombea ubunge katika Jimbo la Busega.

Inadaiwa kuwa Nsega ambaye ni mkazi wa Pasiansi jijini Mwanza, alikimbizwa Bugando kwa ajili ya matibabu Aprili 28, mwaka huu.

“Kabla ya kukukutana na mwanasiasa huyo, aliwahi kumtumia ‘message’(ujumbe mfupi wa maneno) akimsihi ajiondoe kwenye kinyang’anyiro cha kugombea ubunge katika jimbo la Busega. Hata hivyo, Nsega alikataa,” kilidai chanzo kingine cha habari kwa njia ya simu jana.

Chanzo hicho kilifafanua kada huyo wa CCM aliendelea kufanya mawasiliano na marehemu na kwamba baadaye walikutana kwa ajili ya mazungumzo zaidi.

Kwa mujibu wa habari hizo, Nsega alivyorudi nyumbani alijifungia chumbani kwake na hakuwa na uwezo wa kuzungumza. Hata hivyo, haijafahamika Nsega alikutana wapi na mwanasiasa huyo.

Hata hivyo, mmoja wa ndugu wa marehemu huyo (jina tunalo), jana alithibitisha kwamba Nsega amefariki dunia na kuongeza kuwa marehemu ameacha watoto kadhaa.

Alisema kuwa mwili wa marehemu bado umehifadhiwa Bugando ukisubiri kusafirishwa kwenda katika kijiji cha Nsora wilayani Magu kwa mazishi, ambayo yamepangwa kufanyika Jumamosi.

“Mwili utaondolewa Bugando keshokutwa (kesho) hadi nyumbani kwa marehemu, Pasiansi kwa ajili ya kuagwa na baadaye kusafirishwa kwenda Nsora-Magu kwa ajili ya mazishi siku ya Jumamosi,” alisema ndugu huyo.

Mwenyekiti wa CCM mkoani Mwanza, Clement Mabina, alithibitisha kwa njia ya simu kutokea kwa kifo hicho.

Mabina ambaye ni Diwani wa Kata ya Kisesa wilayani Magu, alizungumza jana na Nipashe baada ya Katibu wa CCM mkoani Mwanza, Rajabu Kundya, kutopatikana ofisini na simu yake ya kiganjani kuita bila kupokelewa. “Ndiyo, hata mimi nimesikia hivyo. Nilipigiwa simu na ndugu yake mmoja jana (juzi) kwamba Nsega amefariki na kwamba aliugua ugonjwa wa kuvua nguo na kubaki uchi,” alisema Mabina.

Mabina pia alithibitisha kuwa kabla ya mauti, Nsega alikuwa amejitambulisha kwake kuwa alikuwa na nia ya kugombea ubunge katika Jimbo la Busega katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.

“Alishafika hata kwangu kunieleza kuwa atagombea, kwa hiyo ninaamini hata ofisi ya Katibu wa CCM mkoa ina taarifa kama hizo,” alisema Mabina.

Mwandishi wa habari hizi alifika nyumbani kwa marehemu Iloganzala ambako alikuta umati wa waombolezaji wakiwemo wana-CCM.

“Kwa kweli tumeupokea msiba huu kwa masikitiko makubwa. Hadi mauti, Nsega alikuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Ilemela.

“Aidha, alikuwa katibu wa tawi la CCM Pasiansi Magharibi,” alisema Katibu Mwenezi wa CCM tawi la Iloganzala Magharibi, Emmanuel Magoti, na kuongeza kwamba:

“Ni kweli alikuwa ametangaza nia ya kugombea ubunge katika jimbo la Busega. Ni juzi tu walikuja wazee ambao ni wana-CCM wakihitaji picha yake kwa ajili ya kutengeneza vipeperushi.” Magoti alisema kuwa jina la Nsega ni chimbuko la jina na Jimbo la Busega.

Magoti alithibitisha kuwa mazishi yatafanyika Jumamosi katika kijiji cha Nsora wilayani Magu, baada ya shughuli za maombi kufanyika nyumbani kwa marehemu.


CHANZO:
NIPASHE
 
Vituko hivi...
Anyway, hata natural death kipindi hiki itaenda likizo kidogo, akifa mgombea itaonekana mkono wa mtu!
 
headline_bullet.jpg
Yadaiwa ni mkono wa mtu
headline_bullet.jpg
Akaugua gonjwa la ajabu
headline_bullet.jpg
Alikataa kubadili nia hiyo
headline_bullet.jpg
Jiji la Mwanza lazizima



CCM%2827%29.jpg

Chama Cha Mapinduzi (CCM)



Mwanamke aliyekuwa ametangaza nia ya kuomba uteuzi wa kugombea ubunge katika jimbo la Busega kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Magu, Mkoa wa Mwanza katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu, Nsega Aloyce Ntobi, amefariki dunia katika mazingira ya kutatanisha.
Kifo cha Nsega kimezua mjadala katika Jiji la Mwanza huku baadhi ya wakazi wakikihusisha na nia yake ya kutaka kugombea wadhifa huo wa kisiasa.
Habari zinasema kuwa Nsega alifariki usiku wa kuamkia juzi jijini Mwanza, wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando baada ya kuugua ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu.
Kifo hicho kimeghubikwa na utata huku baadhi ya wananchi wakidai kuwa kuna mkono wa wanasiasa kadhaa.
“Taarifa mpya inasema kuwa mgombea ubunge wa Busega, Nsega amepata ugonjwa huo siku mbili tu baada ya kukutana na (mwanasiasa ambaye jina tunalihifadhi) akiombwa ajitoe kwenye mchakato na yeye kukataa,” kilidai chanzo kimoja cha habari.
Habari zinadai kuwa saa chache kabla ya kuugua, Nsega alikutana na mwanasiasa mmoja aliyekuwa na nia ya kugombea ubunge katika jimbo hilo kwa ajili ya mazungumzo yaliyohusu mchakato wa kugombea ubunge katika Jimbo la Busega.
Inadaiwa kuwa Nsega ambaye ni mkazi wa Pasiansi jijini Mwanza, alikimbizwa Bugando kwa ajili ya matibabu Aprili 28, mwaka huu.
“Kabla ya kukukutana na mwanasiasa huyo, aliwahi kumtumia ‘message’(ujumbe mfupi wa maneno) akimsihi ajiondoe kwenye kinyang’anyiro cha kugombea ubunge katika jimbo la Busega. Hata hivyo, Nsega alikataa,” kilidai chanzo kingine cha habari kwa njia ya simu jana.
Chanzo hicho kilifafanua kada huyo wa CCM aliendelea kufanya mawasiliano na marehemu na kwamba baadaye walikutana kwa ajili ya mazungumzo zaidi.
Kwa mujibu wa habari hizo, Nsega alivyorudi nyumbani alijifungia chumbani kwake na hakuwa na uwezo wa kuzungumza. Hata hivyo, haijafahamika Nsega alikutana wapi na mwanasiasa huyo.
Hata hivyo, mmoja wa ndugu wa marehemu huyo (jina tunalo), jana alithibitisha kwamba Nsega amefariki dunia na kuongeza kuwa marehemu ameacha watoto kadhaa.
Alisema kuwa mwili wa marehemu bado umehifadhiwa Bugando ukisubiri kusafirishwa kwenda katika kijiji cha Nsora wilayani Magu kwa mazishi, ambayo yamepangwa kufanyika Jumamosi.
“Mwili utaondolewa Bugando keshokutwa (kesho) hadi nyumbani kwa marehemu, Pasiansi kwa ajili ya kuagwa na baadaye kusafirishwa kwenda Nsora-Magu kwa ajili ya mazishi siku ya Jumamosi,” alisema ndugu huyo.
Mwenyekiti wa CCM mkoani Mwanza, Clement Mabina, alithibitisha kwa njia ya simu kutokea kwa kifo hicho.
Mabina ambaye ni Diwani wa Kata ya Kisesa wilayani Magu, alizungumza jana na Nipashe baada ya Katibu wa CCM mkoani Mwanza, Rajabu Kundya, kutopatikana ofisini na simu yake ya kiganjani kuita bila kupokelewa. “Ndiyo, hata mimi nimesikia hivyo. Nilipigiwa simu na ndugu yake mmoja jana (juzi) kwamba Nsega amefariki na kwamba aliugua ugonjwa wa kuvua nguo na kubaki uchi,” alisema Mabina.
Mabina pia alithibitisha kuwa kabla ya mauti, Nsega alikuwa amejitambulisha kwake kuwa alikuwa na nia ya kugombea ubunge katika Jimbo la Busega katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.
“Alishafika hata kwangu kunieleza kuwa atagombea, kwa hiyo ninaamini hata ofisi ya Katibu wa CCM mkoa ina taarifa kama hizo,” alisema Mabina.
Mwandishi wa habari hizi alifika nyumbani kwa marehemu Iloganzala ambako alikuta umati wa waombolezaji wakiwemo wana-CCM.
“Kwa kweli tumeupokea msiba huu kwa masikitiko makubwa. Hadi mauti, Nsega alikuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Ilemela.
“Aidha, alikuwa katibu wa tawi la CCM Pasiansi Magharibi,” alisema Katibu Mwenezi wa CCM tawi la Iloganzala Magharibi, Emmanuel Magoti, na kuongeza kwamba:
“Ni kweli alikuwa ametangaza nia ya kugombea ubunge katika jimbo la Busega. Ni juzi tu walikuja wazee ambao ni wana-CCM wakihitaji picha yake kwa ajili ya kutengeneza vipeperushi.” Magoti alisema kuwa jina la Nsega ni chimbuko la jina na Jimbo la Busega.
Magoti alithibitisha kuwa mazishi yatafanyika Jumamosi katika kijiji cha Nsora wilayani Magu, baada ya shughuli za maombi kufanyika nyumbani kwa marehemu.




CHANZO: NIPASHE
 
Kwani Busega pia ilitabiriwa na Sheikh Yahya???????????????

Haya tena imani za kishirikina in the making. Anywayz ni lini watanzania tutabadilika? Jmani this is 2010. Ok if the death of this lady is in any how of criminal in nature why not bringing the suspects forward to face justice? C'moon! Tutaendelea na hizi imani za kipumbavu mpaka lini????? What the fcuk is this mkono wa mtu?????
 
Kwani Busega pia ilitabiriwa na Sheikh Yahya???????????????

Haya tena imani za kishirikina in the making. Anywayz ni lini watanzania tutabadilika? Jmani this is 2010. Ok if the death of this lady is in any how of criminal in nature why not bringing the suspects forward to face justice? C'moon! Tutaendelea na hizi imani za kipumbavu mpaka lini????? What the fcuk is this mkono wa mtu?????

sio ya kuamini sana na sio ya kupuuza kabisa kwa sababu haya mambo yapo mkuu, sasa inategemea na imani tu, kama una imani ya dini (ya kumuamini Mungu ), basi lazima ujue kuna mpinzani wa Mungu na anafanya kazi
 
sio ya kuamini sana na sio ya kupuuza kabisa kwa sababu haya mambo yapo mkuu, sasa inategemea na imani tu, kama una imani ya dini (ya kumuamini Mungu ), basi lazima ujue kuna mpinzani wa Mungu na anafanya kazi

Mkuu whilst simaanishi kudhoofisha hoja yako lakini kuna mambo ya kujiuliza. Kwa nini uwepo wa mambo haya uwepo hapo kwetu tu ina maana mtu kuugua ghafla na kufariki imeanza leo??? Na kama tuna wataalamu wa namna hiyo kwa nini basi wasituondolee mafisadi, majambazi, wauwaji etc.?????? Sijawahi kusikia katika nchi zilizoendelea hii masuala ya mkono wa mtu.
 
Haya mambo hayapo kwetu tu ni dunia nzima, isipokuwa nitakukubalia kitu kimoja tu ukiniambia wewe hujasikia, Hivi mtu wa MArekani anaeamini kuwa Michael Jackson Ghost ilionekana na mpaka CNN wakaweka Hewani na Video clip wewe hiyo imani unaiona ndogo?
 
Haya mambo hayapo kwetu tu ni dunia nzima, isipokuwa nitakukubalia kitu kimoja tu ukiniambia wewe hujasikia, Hivi mtu wa MArekani anaeamini kuwa Michael Jackson Ghost ilionekana na mpaka CNN wakaweka Hewani na Video clip wewe hiyo imani unaiona ndogo?

Ok but was there anyone portraying, indicating or suspecting kifo cha Michael kina mkono wa mtu????? Na kumbuka hii ya Michael ni juzi tu lakini hizi habari bongo ni toka enzi na enzi. Cha ajabu the so thought or imagined to have all those powers na wenyewe wanakufa, wanafiwa, wanaugua.

Pia naomba msaada ndugu nini tofauti ya kifo cha kawaida na hiki chenye mkono wa mtu, maybe hapa ndiyo napomiss the point.
 
Mungu muweza wa yote na ailaze roho ya marehemu
Mama yetu mpendwa Nsega mahali pema peponi
lakini kama ni mkono wa mtu,kwa maana ya kwamba
alihusika mtu ktk kifo hicho basi na yeye pia ipo siku
atafariki na yeye pia kamwe hataishi milele
.
 
Msemaji wa Familia ambaye ni kaka wa Marehemu Leornad Bugomola amekanusha kifo cha ndugu yake kuhusishwa na Imani za kishirikina. Amesema kuwa ndugu yao alikuwa na matatizo ya kiafya, alikuwa ni Mgonjwa wa Kichaa na hili familia nzima wanalijua.
Alisema wamesikitishwa na kifo cha Ndugu yao kuhusishwa na siasa.
 
Msemaji wa Familia ambaye ni kaka wa Marehemu Leornad Bugomola amekanusha kifo cha ndugu yake kuhusishwa na Imani za kishirikina. Amesema kuwa ndugu yao alikuwa na matatizo ya kiafya, alikuwa ni "Mgonjwa wa Kichaa" na hili familia nzima wanalijua.
Alisema wamesikitishwa na kifo cha Ndugu yao kuhusishwa na siasa.

Nadhani unamaanisha alikuwa kichaa au mgonjwa wa akili. Kama hili ni kweli basi ni hatari tupu kwa kichaa kutangaza nia ya kugombea ubunge. Kulingana na CV ya marehemu kama ilivyoelezewa kwenye habari, napata ugumu kuamini huyu mtu alikuwa kichaa. Hata mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza anasema alijua huyu ametangaza nia ya kugombea ubunge. Huyo anayejiita ndugu wa marehemu isijeikawa ndiye kigagula mwenye mzigo.

Ni kweli watu huwa wanakufa lakini ni ukweli pia kuwa si vifo vyote ni vya ukweli. Vingine ni vya kutengenezwa. Unadhani mtu kafa kumbe kachukuliwa msukule. Hili jambo lipo kabisa hata kama tukijidai hatutaki kulikubali. Uchawi upo na wachawi wapo, hili halijalishi tumeendelea kivipi. As long as the devil exist, his servants (socerers/witch doctors) will continue to exist. Wapigweeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Mapepo Shi--shiiindwa ---shiiindwa Kwajina la Yesu, Majini to-tooka tokaa kwa jina la Yesu......Nawaamuru wa chawi wote mteketee kwa Moto wa Mbinguni. Malaika wa Mungu Makerubi na Maserafi wawashughulikie..........

Mungu ailaze roho ya mama huyu Pema Peponi Amina...Amina....Amina
 
Kwa kuwa njia yetu ni moja mi nafikiri tumuombee marehemu mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya maremu mahala pema peponi.AMINA
 
Katibu CCM auawa kwa kisu ofisini


PostDateIcon.png
Saturday, 15 May 2010 09:08

Na Daud Magesa,Mwanza

KATIBU wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Isamilo, Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza, Bi.Bahati Stephano (49) ameuawa kwa kuchomwa kisu baada ya kuvamiwa ofisini kwake jana mchana.

Habari zilizopatikana kutoka katika eneo la tukio na kutihibitishwa na Jeshi la
Polisi mkoani Mwanza, zimesema kuwa marehemu Stepheno alifariki wakati akikimbizwa katika Hospitali Bugando kwa matibabu.

Kwa mujibu wa watu walioshuhudia tukio hilo Bi. Stephano aliuawa na Bw.Jumanne Oscar (30) kwa kuchomwa kisu baada ya kuzozana wakati wakiwa katika ofisi ya marehemu.

“Kijana huyo alitokea ghafla na kuingia ofisini na mara tukaona wakizozana kabla ya kumchoma kisu juu ya titi la kushoto na tumboni,” alisema mmoja watu walioshuhudia tukio hilo ambaye hakutaka kujitambulisha jina lake.

Alisema, baada ya kumchoma, alitimua mbio huku na akimuacha Bi. Stephano akilia na kupiga kelele za kuomba msaada kwa watu waliokuwa jirani na eneo hilo. Alisema kijana huyo alikamatwa kandokando ya Ziwa Victoria kwa ushirikiano wa wananchi na polisi. “Tulimzingira akafanikiwa kukimbilia katika ufukwe wa ziwa jirani na eneo hilo kisha akajitosa majini lakini tukafanikiwa kumkamata kwa kushirikiana na polisi,” alisema.

Kamanda wa polisi mkoani Mwanza, Bw. Simon Sirro amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo alisema kuwa Bi. Stephano alifariki wakati akikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa matibabu na mtuhumiwa anashikiliwa polisi kwa mahojiano.

source: Majira


 

Similar Discussions

Back
Top Bottom