Pre GE2025 DSM Mgombea makamu mwenyekiti ashindwa kutaja falsafa ya Chadema

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
May 16, 2024
2,482
6,977
Wakuu

Mgombea akiwa Kikaangoni

Katika hali ya kushangaza mgombea wa umakamu mwenyeketi Chadema Zanzibar, Suleiman Makame Issa (62) ameshindwa kuitaja falsafa ya chama hicho wakati akijinadi.

Issa alishindwa kuitaja falsafa hiyo baada ya kuulizwa swali na mjumbe Suzan Lyimo akimtaka kutaja, ndipo mgombea huyo alisema kuwa falsafa ya chama hicho ni 'Strong Together' jibu lililosababisha wajumbe waangue kicheko.

Msingi wa swali hilo, ni kile muuliza swali Suzan alichokitaja kuwa mgombea huyo ameshindwa kutamka vyema salamu ya chama hicho.

Falsafa ya chama hicho ambacho kinafanya uchaguzi wake leo Jumanne Januari 21, 2025 katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam ni 'Nguvu ya umma'.

 
Back
Top Bottom