MGOMBEA wa ubunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika jimbo la Mpanda Mjini, Sebastiane Kapufi katika Mkoa mpya wa Katavi, anadaiwa kutishia kumuua kada mwenzake kwa tuhuma za kwamba amekuwa akimchafua kisiasa.
Hayo yalibainishwa jana na kada huyo, John Kikwala (38) wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi ambapo alisema kuwa Kapufi anadaiwa kutoa wiki moja kwa kumtuhumu kuwashawishi wana CCM kumpigia kura mgombea wa Chadema.
Kwa mujibu wa Kikwala, Kapufi anadaiwa kutoa tishio hilo la mauaji juzi saa tatu usiku baada ya kuzungumza naye (Kikwala) kwa simu ya kiganjani ambapo inadaiwa alimtaka kada mwenzake huyo kuacha mpango wake wa kumchafua kisiasa.
Inadaiwa Kikwala amekuwa akiwaambia wanachama wenzake kuwa Kapufi hafai na hana sifa za kuwa mbunge wa jimbo hilo na kuwashawishi wapige kura kumchagua mgombea Chadema, mbunge aliyemaliza muda wake, Said Arfi.
"Nimetoa taarifa Polisi ya kutishiwa kuuawa kwa kuwa eti simuungi tena mkono katika harakati zake kugombea ubunge kwenye jimbo hili, amenituhumu kwamba namuunga mkono na kumpigia debe mgombea wa Chadema.
Lakini ukweli ni kwamba tangu mchakato wa kura za maoni tulikuwa tukishirikiana mpaka akashinda kwa kishindo.... mie namshangaa kwa tuhuma anazodai," alisema.
Kikwala alisema amefunguliwa RB yenye namba 3412/2010 dhidi ya Kapufi na kuelezea tuhuma nzito za kutishiwa kuuawa na mgombea huyo wa nafasi ya ubunge jimbo hilo kwa tiketi ya CCM.
Kapufi alipohojiwa kuhusu tuhuma hizo, alikana kumtishia maisha Kikwala lakini alikiri kufanya mawasiliano na kada huyo wa CCM kwa njia ya simu usiku huo wa juzi na kueleza kuwa kwa muda mrefu amekuwa hana uhusiano mzuri na Kikwala.
Mgombea ubunge huyo aliendelea kusema kuwa Kikwala anamsononesha kwa kuendelea na jitihada zake za kumchafua kisiasa na kumuunga mkono mgombea wa Chadema .
" Huyu Kikwala ni mtu wa ajabu sana, kama ndugu yangu amekuwa akinifuata mara kadhaa na kuniomba msaada wa mafuta na pesa lakini cha kushangaza amekuwa akitumia msaada huo kunichafua kisiasa na kumpigia debe mgombea wa chama kimoja cha upinzani.
Hayo yalibainishwa jana na kada huyo, John Kikwala (38) wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi ambapo alisema kuwa Kapufi anadaiwa kutoa wiki moja kwa kumtuhumu kuwashawishi wana CCM kumpigia kura mgombea wa Chadema.
Kwa mujibu wa Kikwala, Kapufi anadaiwa kutoa tishio hilo la mauaji juzi saa tatu usiku baada ya kuzungumza naye (Kikwala) kwa simu ya kiganjani ambapo inadaiwa alimtaka kada mwenzake huyo kuacha mpango wake wa kumchafua kisiasa.
Inadaiwa Kikwala amekuwa akiwaambia wanachama wenzake kuwa Kapufi hafai na hana sifa za kuwa mbunge wa jimbo hilo na kuwashawishi wapige kura kumchagua mgombea Chadema, mbunge aliyemaliza muda wake, Said Arfi.
"Nimetoa taarifa Polisi ya kutishiwa kuuawa kwa kuwa eti simuungi tena mkono katika harakati zake kugombea ubunge kwenye jimbo hili, amenituhumu kwamba namuunga mkono na kumpigia debe mgombea wa Chadema.
Lakini ukweli ni kwamba tangu mchakato wa kura za maoni tulikuwa tukishirikiana mpaka akashinda kwa kishindo.... mie namshangaa kwa tuhuma anazodai," alisema.
Kikwala alisema amefunguliwa RB yenye namba 3412/2010 dhidi ya Kapufi na kuelezea tuhuma nzito za kutishiwa kuuawa na mgombea huyo wa nafasi ya ubunge jimbo hilo kwa tiketi ya CCM.
Kapufi alipohojiwa kuhusu tuhuma hizo, alikana kumtishia maisha Kikwala lakini alikiri kufanya mawasiliano na kada huyo wa CCM kwa njia ya simu usiku huo wa juzi na kueleza kuwa kwa muda mrefu amekuwa hana uhusiano mzuri na Kikwala.
Mgombea ubunge huyo aliendelea kusema kuwa Kikwala anamsononesha kwa kuendelea na jitihada zake za kumchafua kisiasa na kumuunga mkono mgombea wa Chadema .
" Huyu Kikwala ni mtu wa ajabu sana, kama ndugu yangu amekuwa akinifuata mara kadhaa na kuniomba msaada wa mafuta na pesa lakini cha kushangaza amekuwa akitumia msaada huo kunichafua kisiasa na kumpigia debe mgombea wa chama kimoja cha upinzani.