Uchaguzi 2020 Mgombea atakayetuahidi kufyekelea mbali mishahara na posho nono za Wabunge na Wanasiasa, tutampa kura

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,952
4,325
Sasa, sasa: kama kweli Mgombea huyu wa Upinzani ni jasiri wa kutosha na mwenye uchungu na sisi wavunja jasho na walipa kodi wa nchi hii, atuahidi hadharani katika kampeni zake kwamba tukimchagua atafyekelea mbali mishahara na maposho manono manono ya wabunge na wanasiasa. Na kwamba atafuta ruzuku ya serikali kwa vyama vya siasa mara atakapochaguliwa.

Akiweza kufanya hivyo anaweza kupata kura nyingi. Hili linawezekana, linahitaji tu utashi wa huyu mgombea. Manufaa yake ni makubwa sana kwa ustawi wa taifa letu. Ila akisema hivyo rungu la wanasiasa wenzake na hasa walio ndani ya chama chake lazima atalipata fresh.

Kwani akifanya hivyo ataweza kuokoa matrillioni ya pesa kila mwaka ambayo yatamuwezesha kutimiza hizo ndoto zake za kuongeza mishahara ya watumishi wa umma mara dufu, kutoa bima ya afya kwa wote, kutoa mikopo kwa wanafunzi wote wa vyuo na kadhalika.

Maana Lema (mbunge wa Arusha) alishawahi kututambia kwamba mishahara na marupurupu yao ni kiboko. Kwamba posho yao ya kikao kimoja cha masaa machache ni sawa na take home salary ya mwezi ya mtumishi wa umma mwenye elimu ya shahada ya kwanza (bachelor degree). Kuna wakati Zitto alipokuwa bado mzalendo aligomea posho hiyo kwa sababu aliiona siyo fair. Lema alishatutambia kuwa gratuity yao kila baada ya miaka mitano nayo ni kiboko. Yaani wanaishi kama malaika.

Ndiyo maana uchaguzi mkuu unapofika tumekuwa tukishuhudia maelfu kwa maelfu ya watu wakigombania kinyang'anyiro cha kuwa wabunge. Tumekuwa tukishuhudia maprofesa, madaktari, ma engineers, maaskofu, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na kadhalika wakiacha kazi zao na kwenda kugombania kinyang'anyiro hicho!

Enzi za Mwalimu wawakilishi wetu hawa (wabunge) hawakuwa na mshahara wo wote kwani walitakiwa kuwa ni watu ambao wana kazi zao. Sifa moja wapo ya kuomba kuwa mbunge ilikuwa ni lazima uwe ni mtu uliye na kazi inayokupatia kipato halali kuendeshea maisha yako. Uwakilishi/ ubunge ilikuwa siyo ajira bali ni ya kujitolea or just an extra community duty. Vikao vya bunge vilikuwa wala havichukui siku nyingi kihivyo. Serikali iligharimia tu transport warrant na perdiem za wabunge hao wakati wa vikao vya bunge. Hakukuwa na sitting allowances wala mfuko wa mbunge.

Sasa, sasa: huyu mgombea asitufanyie sisi danganya toto ya kuambiwa mkinichagua, mabomba yote ya maji yatatoa pia maziwa na asali. Anatuambia eti kwamba tukimchagua:

1. Hatawasumbua wakwepa kodi, mafisadi, wabadhilifu wa pesa za umma, watakasishaji fedha, wanaoshindwa kurejesha mikopo ya mabenki, watuhumiwa wa ugaidi( upasho), ujangiri na ujambazi. Wote hawa anasema atakuwa mpole sana kwao. Anasema ataifumua TRA ili isibughudhi wafanyabiashara. Matokeo yake ni kuwa lazima makusanyo ya kodi yatatelemka kutoka huu wastani wa sasa wa sh 1.5 trillion kwa mwezi hadi kuwa kule tulikotoka kwa wastani wa billion 500 kwa mwezi sawa na payroll ya watumishi wa umma ya sasa kwa mwezi!

2. Atapandisha mishahara ya watumishi wa umma mara dufu. Watu wote watapewa bima ya afya bure. Wanafunzi wa vyuo wote watapewa mikopo ya masomo na hawatabughudhiwa kuirejesha wamalizapo masomo yao. Sasa hizo pesa atazitoa wapi?

3. Vyombo vya habari ataviruhusu kusema cho chote hata kama kinakiuka maadili ya taaluma hiyo. Hata matusi na kudhalilisha wengine itakuwa ni ruhusa. Na haki za faragha zitazingatiwa hata kama ni za jinsia ile ile.

4. Eti atabadili na kutunga sheria mbali mbali zinazompendeza wakati anajua fika kuwa chama chake hakitakuwa na idadi ya kutosha kutunga hizo sheria anazozitaka. Maana yake atatumia udikteta (presidential decrees) kutunga sheria hizo za kuendesha nchi kwa matakwa yake.

Masikini watanzania ambao wengi wao hawana uelewa wa kutosha, wanafurika kwenye hizo kampeni wakiamini kuwa kile wanachoambiwa ni cha kweli. Watanzania tusifanywe danganywa toto. Atamke wazi kwamba atafyekelea mbali mishahara na marupurupu manono ya wabunge na wanasiasa ili nao wateremuke kutoka kuishi kama malaika hadi kuishi kama tunayoishi sisi maisha ya ki.... Atamuke wazi kuwa atafyekelea mbali ruzuku ya serikali kwenye vyama vya siasa. Vyama hivi vinapaswa kujitengemea.

Sasa hivi vina umri wa miaka 30, havipaswi tena kubebwa na serikali. Pesa hiyo iende kuboresha maisha ya watanzania. Vyama vya siasa ambavyo hadi sasa havijaweza kujitegemea viachwe vife kifo cha mende. Yaani chama kinapewa mabilioni ya pesa kila mwaka lakini kinashindwa kujenga hata jengo la ofisi ya makao makuu yake kwa miaka 30, kinaendelea kutembeza bakuli kwa walala hoi -hili halikubaliki hata kidogo. Vyama hivi ambavyo haviko serious viachwe vifwe. Serikali inavipa ruzuku halafu vinaitukana hiyo serikali. Hapana.
 
Unaongea nini sikusikii una sema tusimchague Magufuli tumchague Lissu, ebuh ongeza sauti kidogo kwenye simu yako bro.
 
Tanzania ni moja kati ya nchi masikini zaidi zaidi Duniani, masikini Iliyotopea.

Tunabunge lenye wabunge idadi yao ni kubwa sana ni matumizi mabaya kabisa ya fedha.

Wabunge zaidi ya 300.
Kwa nchi masikini kama hii ni Laana.
 
Anaweza asipatikane kabisa mwenye Sera hzo
Ni kweli. Kwenye sera zao za maandishi zinazoitwa ilaani hazipo. Na kwenye hizo ilani zao za vichwani tumeangalia hazipo isipokuwa kwa mbali zinaonekana kwenye chama cha ccm.
 
Haya mambo ya serikali kutoa ruzuku kwa vyama vya siasa ndiko kumezalisha utitiri wa vi saccos vya vivyama vya siasa. Lengo lake ni kupata hiyo ruzuku kwa manufaa yao binafsi hao wamiliki wa saccos hizo.

Hakuna nchi yo yote nyingine hapa duniani inayotoa ruzuku kwa vyama vya siasa. Ni Tanzania pekee. Serikali za walioendelea hutoa ruzuku kwa wamiliki wa viwanda vya kimkakati na wakulima /wafugaji wa mazao ya kimkakati.

Ipo haja na sisi watanzania ya kufuta ruzuku hizi vya vyama vya siasa na kuzielekeza ruzuku hizi kwa kampuni za wazawa wenye viwanda vya kimkakati hususani zile zinazotengeneza nguo na ngozi na kwa kulima / wafugaji wanaozalisha mazao ya kimkakati hususani pamba, kahawa na korosho.

Harakati nyingi tunazoziona kwenye vyama hivi vya upinzani kwenye kinyang'anyiro cha urais ni kwa ajili siyo ya kushinda urais bali kupata idadi kubwa ya kura za urais kwani formula (kikokotozi) inayotumika kupata kiasi cha pesa ya ruzuku ya chama kinategemea na idadi ya kura za urais chama kilizopata kwenye uchaguzi mkuu. Dr Slaa alishawahi kutuambia alilazimishwa na Mbowe kugombea urais mwaka 2010 badala ya ubunge. Mwaka huo Dr Slaa alikuwa ana uhakika wa kushinda ubunge na hivyo kupata mshahara na marupurupu mazuri ya ubunge. Yeye pamoja na Mbowe walikuwa na uhakika wa kutoshinda kura za kumuwezesha Dr Slaa kuwa rais wa JMT ila walikuwa na hakika ya kupata kura nyingi kiasi za urais zitakazokiwezesha chama kupata ruzuku nono. Wakakubaliana kwa kuwa Dr Slaa atakuwa amepoteza ubunge wake baada ya uchaguzi mkuu, chama chake kitamlipa mshahara na marupurupu yote anayopata mbunge. Mengine alilipwa lakini mengine hakulipwa hususani yale ya kinua mgongo baada ya miaka 5. Ikabidi akimbilie Canada kwa usalama wake.

Haya mwaka huu tunayashuhudia hayo hayo kwa Tundu Lissu. Mwenyekiti ana uhakika kwamba chama chake hakitashinda kura za kutosha kumwezesha TL kuwa rais wa JMT. Angekuwa ana uhakika huo yeye mwenyewe hangalijitoa kugombea nafasi hiyo. Ndiyo maana yeye kagombea tu ubunge huko kwao ambako ana uhakika wa kuendelea kuwa mbunge na KUB - ingawa mwaka huu inaweza ikawa suprize kwake.

Tunayashuhudia hayo kwa chama cha ACT-wazalendo. Zitto ana uhakika kuwa chama chake hakiwezi kutoa rais wa JMT kwenye uchaguzi huu. Angekuwa na uhakika yeye mwenyewe lazima angaligombea nafasi hiyo ya urais. Kaamua kugombea ubunge kwao Kigoma ambako ana uhakika wa kurudi bungeni kama KUB - ingawa naye zamu hii anaweza pata suprize!

Hivyo harakati hizi za akina Lissu na Membe ni kwa ajili ya kuongeza kiwango cha ruzuku kwenye vyama vyao. Nothing more, nothing less. Watakapomaliza kazi hiyo watafanywa kama alivyofanywa Dr Slaa. Kwa nini watanzania hawajifunzi kutokana na historia?
 
Sasa, sasa: kama kweli Mgombea huyu wa Upinzani ni jasiri wa kutosha na mwenye uchungu na sisi wavunja jasho na walipa kodi wa nchi hii, atuahidi hadharani katika kampeni zake kwamba tukimchagua atafyekelea mbali mishahara na maposho manono manono ya wabunge na wanasiasa. Na kwamba atafuta ruzuku ya serikali kwa vyama vya siasa mara atakapochaguliwa.

Akiweza kufanya hivyo anaweza kupata kura nyingi. Hili linawezekana, linahitaji tu utashi wa huyu mgombea. Manufaa yake ni makubwa sana kwa ustawi wa taifa letu. Ila akisema hivyo rungu la wanasiasa wenzake na hasa walio ndani ya chama chake lazima atalipata fresh.

Kwani akifanya hivyo ataweza kuokoa matrillioni ya pesa kila mwaka ambayo yatamuwezesha kutimiza hizo ndoto zake za kuongeza mishahara ya watumishi wa umma mara dufu, kutoa bima ya afya kwa wote, kutoa mikopo kwa wanafunzi wote wa vyuo na kadhalika.

Maana Lema (mbunge wa Arusha) alishawahi kututambia kwamba mishahara na marupurupu yao ni kiboko. Kwamba posho yao ya kikao kimoja cha masaa machache ni sawa na take home salary ya mwezi ya mtumishi wa umma mwenye elimu ya shahada ya kwanza (bachelor degree). Kuna wakati Zitto alipokuwa bado mzalendo aligomea posho hiyo kwa sababu aliiona siyo fair. Lema alishatutambia kuwa gratuity yao kila baada ya miaka mitano nayo ni kiboko. Yaani wanaishi kama malaika.

Ndiyo maana uchaguzi mkuu unapofika tumekuwa tukishuhudia maelfu kwa maelfu ya watu wakigombania kinyang'anyiro cha kuwa wabunge. Tumekuwa tukishuhudia maprofesa, madaktari, ma engineers, maaskofu, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na kadhalika wakiacha kazi zao na kwenda kugombania kinyang'anyiro hicho!

Enzi za Mwalimu wawakilishi wetu hawa (wabunge) hawakuwa na mshahara wo wote kwani walitakiwa kuwa ni watu ambao wana kazi zao. Sifa moja wapo ya kuomba kuwa mbunge ilikuwa ni lazima uwe ni mtu uliye na kazi inayokupatia kipato halali kuendeshea maisha yako. Uwakilishi/ ubunge ilikuwa siyo ajira bali ni ya kujitolea or just an extra community duty. Vikao vya bunge vilikuwa wala havichukui siku nyingi kihivyo. Serikali iligharimia tu transport warrant na perdiem za wabunge hao wakati wa vikao vya bunge. Hakukuwa na sitting allowances wala mfuko wa mbunge.

Sasa, sasa: huyu mgombea asitufanyie sisi danganya toto ya kuambiwa mkinichagua, mabomba yote ya maji yatatoa pia maziwa na asali. Anatuambia eti kwamba tukimchagua:

1. Hatawasumbua wakwepa kodi, mafisadi, wabadhilifu wa pesa za umma, watakasishaji fedha, wanaoshindwa kurejesha mikopo ya mabenki, watuhumiwa wa ugaidi( upasho), ujangiri na ujambazi. Wote hawa anasema atakuwa mpole sana kwao. Anasema ataifumua TRA ili isibughudhi wafanyabiashara. Matokeo yake ni kuwa lazima makusanyo ya kodi yatatelemka kutoka huu wastani wa sasa wa sh 1.5 trillion kwa mwezi hadi kuwa kule tulikotoka kwa wastani wa billion 500 kwa mwezi sawa na payroll ya watumishi wa umma ya sasa kwa mwezi!

2. Atapandisha mishahara ya watumishi wa umma mara dufu. Watu wote watapewa bima ya afya bure. Wanafunzi wa vyuo wote watapewa mikopo ya masomo na hawatabughudhiwa kuirejesha wamalizapo masomo yao. Sasa hizo pesa atazitoa wapi?

3. Vyombo vya habari ataviruhusu kusema cho chote hata kama kinakiuka maadili ya taaluma hiyo. Hata matusi na kudhalilisha wengine itakuwa ni ruhusa. Na haki za faragha zitazingatiwa hata kama ni za jinsia ile ile.

4. Eti atabadili na kutunga sheria mbali mbali zinazompendeza wakati anajua fika kuwa chama chake hakitakuwa na idadi ya kutosha kutunga hizo sheria anazozitaka. Maana yake atatumia udikteta (presidential decrees) kutunga sheria hizo za kuendesha nchi kwa matakwa yake.

Masikini watanzania ambao wengi wao hawana uelewa wa kutosha, wanafurika kwenye hizo kampeni wakiamini kuwa kile wanachoambiwa ni cha kweli. Watanzania tusifanywe danganywa toto. Atamke wazi kwamba atafyekelea mbali mishahara na marupurupu manono ya wabunge na wanasiasa ili nao wateremuke kutoka kuishi kama malaika hadi kuishi kama tunayoishi sisi maisha ya ki.... Atamuke wazi kuwa atafyekelea mbali ruzuku ya serikali kwenye vyama vya siasa. Vyama hivi vinapaswa kujitengemea.

Sasa hivi vina umri wa miaka 30, havipaswi tena kubebwa na serikali. Pesa hiyo iende kuboresha maisha ya watanzania. Vyama vya siasa ambavyo hadi sasa havijaweza kujitegemea viachwe vife kifo cha mende. Yaani chama kinapewa mabilioni ya pesa kila mwaka lakini kinashindwa kujenga hata jengo la ofisi ya makao makuu yake kwa miaka 30, kinaendelea kutembeza bakuli kwa walala hoi -hili halikubaliki hata kidogo. Vyama hivi ambavyo haviko serious viachwe vifwe. Serikali inavipa ruzuku halafu vinaitukana hiyo serikali. Hapana.
Hivi kwa nini ukiwa CCM lazima usiwe na akili...Marekani Republican na Democratic wanafanya fund raising ya uchaguzi..nimemsikia hadi Jiwe anashangaa..jifunzeni kuangalia CNN,BBC ,Al Jazeera nk hata kama hamuelewi lugha hata picha
 
Tatizo hapa ni Katiba.
Nani kakwambia kwamba haya maruzuku, mamishara manono na maposho manono ya wabunge yako kwenye katiba? Kwa taarifa yako huwa wanajitungia wenyewe saa yo yote. Na kwa swala ya aina hiyo huwa hakuna upinzani bungeni: wote wanakuwa wamoja, hakuna wakutoka nje wala wa kusema taarifa!
 
Kwenye hilo wanasiasa wote wamoja


Ova
Jiwe yuko tofauti.
1. Tumeshuhudia katika kipindi chake cha miaka mitano watumishi wa umma waliokuwa wakipata mishahara (net take home) ya hadi TSh 50 million kwa mwezi akiwateremsha hadi sh 15 million.
2. Tumeshuhudia wabunge ambao katika awamu zilizopita walikuwa wakijipandishia mishahara na posho kila baada ya muda mfupi, katika awamu ya Jiwe hakuna mshahara au posho yo yote ya wabunge iliyopanda.
3. Tumeshuhudia katika kipindi chake idadi ya siku za bunge zilipungua kwa zaidi ya 50%. Bunge la bajeti kwa mfano huko nyuma lilikuwa linachukua miezi 3 sasa linachukua mwezi mmoja tu. Hivyo kufanya posho za wabunge kupungua kwa asilimia hiyo hiyo ya 50%. Na bado. Sasa hivi mfumo wa kieletronic wa uendeshaji wa bunge umeanzishwa na unaendelea kuboreshwa. Hii pia itapunguza matumizi ya bunge letu.
4. Tumeshuhudia kutokana na kubana matumizi yasiyo ya lazima ya bunge letu, pesa zilizookolewa zimejenga shule za sekondari na zingine zimetolewa kwa serikali kama gawio.

Hivyo tutegemee makubwa katika kipindi kijacho cha miaka mitano. Fikira za Mwalimu zitatekelezwa kwa vitendo likiwamo hili suala la moshahara na sitting allowance za wabunge na lile la ruzuku ya vyama vya siasa.
 
Back
Top Bottom