Mgogoro wa Ziwa Nyasa: Punda afe mzigo wa tajiri ufike?

PakaJimmy

JF-Expert Member
Apr 29, 2009
16,203
8,723
Mara nyingine kuna hatari kubwa kwa migogoro inayotokea katika nchi zetu hizi kuvishwa sura zenye malengo binafsi ya watu au kundi la watu hasa malengo ya kisiasa na umaarufu au kufuta kashfa fulani zinazoikabili nchi husika.

Tanzania kwa sasa tuko katika mgogoro wa mpaka na nchi ya Malawi, unaohusisha Ziwa Nyasa. Mgogoro huu ni wa ukweli kabisa na si wa kutungwa maana upo tangu enzi za Mwalimu. Lakini kitu cha kuwa nacho makini ni upande wa maamuzi sahihi juu ya kukabiliana na mgogoro huu mzito ambapo usipokabiliwa kwa umakini, tutashuhudia nchi ikiingia kwenye vita na kumwaga damu za Watanzania, maana vita haina macho!

Hapa jamvini kwa sasa kuna threads ambazo zinasema wazi kuwa majeshi yetu yameshaanza kufanya mobilisation ya kusogea eneo la Kyela. Kuna mdau mmoja jana alisema kuwa mida ya saa 3.30 za usiku amekutana na Army Deployment ya hatari ambapo msafara mzito wa magari ya jeshi yapatayo 200 yakitokea PANDE ZA Arusha na Moshi yanaelekea kusini mwa nchi, ambapo kama ni kweli, basi hali si shwari.

Naomba kutoa tahadhari kwa wanadiplomasia, Wanasiasa na Jeshi kuwa tusipokuwa makini mgogogoro huu unaweza kuwa mtaji na kinga kisiasa(political camouflage) wa baadhi ya manyang'au wa hapa nchini kwetu, ambapo wanaweza kuamua ku'capitalize on it kwa kuiingiza nchi vitani kwa malengo kama:

I. Kuwafool wananchi wajue kuwa serikali yao inawajali sana na kulinda mipaka yake, wakati ambapo ukweli ni kuwa kila kona ya mpaka wa nchi yetu inapitika kirahisi tu na wazamiaji toka nchi za jirani(mifano ipo mingi).

II. Ku-divert attention ya wananchi ambapo sasa wako katika mijadala mizito juu ya hatima ya nchi yao. Kuna masuala mazito ambayo yametokea of recent ambapo mengine yameibuliwa Bungeni, na mengine yakiwa yanahusisha migomo na maslahi wa Tanatanzania kwa ujumla.

III. Kujisafisha na kutengeneza image inayopendeza usoni pa wananchi, ili kujiwekea malengo ya kufikiriwa kwa uongozi huko mbele ya safari.

IV. Kupata sababu ya kutotimiza ahadi nyingi zilizoahidiwa kwa wananchi nyakati za uchaguzi.

Isije kuwa tunalazimisha Punda afe lakini mzigo wa tajiri lazima ufike sokoni.

Nawasilisha.
 
All these are simulations results, tusubiri practical/experimental results mgogoro ulivyo kwa sasa ni vigumu mtu kukaa tu yapite, lazima tuonyeshe kuwa nasi tupo tayari kuilinda mipaka yetu. Isipokuwa, kuna watu wanatumia hii kama njia ya kujitafutia ushujaa kwa wananchi. Tulishaona watu wenye makundi yao ndani ya chama tawala ndiyo wamekuwa wasemaji na wahamasishaji wa kutangaza hali ya hewa ilivyo. Nadhani tusubiri
 
Mkuu! Hawa mafisadi ni kawaida yao kufanya hivyo ila hakika tunawaambia ya kwmb hapa tulipo si karne yaijuayo wao,tumeshasanuka Kitambo kama wanatarajia kufanya hili la ziwa nyasa kama mradi wao hakika itakula kwao!

Ngoja kwanza tuweke mambo ya siasa pembeni halafu bila shaka hili likipita tutajua yaliyojiri hapa ktk matumizi!

Hakuna mjinga ktk Tanzania yetu ya leo zaidi ya mafisadi wakubwa wa chama tawala tu!

Kudadekii itakula kwao mafisadi safari hii!
 
Mimi tangu waanze kauli zao za kishetani nimekataa kabisa kuingizwa mkenge katika hili, Kikwete amekwenda Uganda kwenye mkutano wa Amani ya maziwa makuu, huku nyumbani vibaraka wake wanahubiri vita!! my self am out of this na niko tayari kuishi uhamishoni kuliko kuifia nchi inayotuuwa huku tukiwa hai.

Anayetaka kuninyooshea kidole mimi siyo Mzalendo na anaipe kwanza tafsiri isiyo na shaka ni nini maana ya neno uzalendo.
 
Hii vita tutakapo anza kucharazwa lazima watasema kuna mkono wa Chadema
Ni muhimu sana kutunza kumbukumbu ya kila kauli inayotolewa kwa sasa na kiongozi yeyote wa siasa kuhusiana na mgogoro huu, ili tupate nafasi ya kuzichambua kwa wakati muafaka...
Hii ishu ina sura ya pili hii!...Bilieve me or not!
 
Mkuu PakaJimmy labda kidogo mimi sijakuelewa.

Unavyosema kuwa vita huenda ikawa ni political camouflage unamaana kuwa tumekuwa wepesi sana kupeleka vikosi vya jeshi badala ya kuumaliza mgogoro kidiplomasia au una maana gani? Kwa kauli tata wanazotoa wamalawi mimi nadhani kumobilize jeshi ni sahihi kabisa na sioni tatizo ya hilo ilimradi hakuna shughuli yeyote ya kijeshi iliyofanyika mpaka sasa lakini ni lazima tuwe alerted.

Kama ni political camouflage basi ni heri yao hao viongozi wachafu hapa naona ni circumstance ndiyo imewaokoa maana hali hii haiepukiki.
 
Last edited by a moderator:
Hiyo ipo wazi sana, kwa namna upepo unavyovuma katika matukio ya siasa zetu ni wazi sana watawala wamebanwa na "viongozi" wameparaganyika hadi kufikia kupitisha sheria kinyemela na hujuma, hii ni zaidi ya aibu sana!

Katika hali ambapo, hata bunge letu limepoteza utukufu wake kwa wabunge wenyewe kukata tamaa na kujidumbukiza katika rushwa ya wazi sana na kupitisha bajeti za wizara kwa hongo na maelekezo toka juu, ni lazima tukubali kuwa tumekwama...

Na sitaki kusikia kelele za kuhamasishana uzalendo kwenye sakata hili la "Ziwa Nyasa", sababu kama ni uzalendo watu haujawahi kutupungukia toka kwenye malezi tuliyolelewa tulipokuwa watoto wachanga tumekuwa wazelendo tuliotukuka kwenye Taifa hili linaloongozwa na watu wasio na fadhira kwa wazelendo wake...!

Ukweli ni kuwa, pamoja na mgogoro huu wa kimataifa, haitaleta maana kama eti wananchi wote tukalilishwe mgogoro huu tu mithiri ya kwamba nchi sasa imesimama na inashughulika na Malawi.......hapana, huu utakuwa ni ujuha ambao tumeendelea kuwa nao kuwa sisi ni taifa la matukio, kwamba tukio moja linazima mengine na maisha yanendelea kama kawaida....!

Kwenye hili ni lazima tusimame imara na tuendelee kupaza sauti za wasiochoka kuwa "Tunaitakia heri nchi yetu imalize salama mgogoro huu ikipendeza zaidi bila umwagaji wa damu, ila hiyo isiwe kisingizio cha masuala yetu kama taifa kutelekezwa"

Hivyo, ni wito kwetu sisi wana-JF na wanajumuia hii ya kitanzania kada zote hasa waandishi wa habari.... Tusikubali kutumika kwa jina la "Mgogoro na Malawi"
 
Wamalawi bado wanakaribisha mazungumzo kulingana na Taarifa zilizotoka jana usiku. Mwenzetu Lowasa anataka vita ( M/K wa kamati ya Ulinzi na Usalama) cha kushingaza si mtendaji wa serikali ni mshauri wa mambo ya ulinzi. Anashauri vita. Tumemgundua wanataka kututoa kafara ssi watz tunaoishi kando ya ziwa nyasa upande wa Tz ili waonewe huruma ya uraisi. Hapana ingieni katika mazungumzo. Na kimsingi Wamalawi wanawauliza mbona kauli za vitisho zinatoka kipindi hiki na si kipindi kingine? Kumbe mna yenu ingawa wana kubali kuwa kiini cha hasa hili tatizo la leo ni Selikali ya Malawi kuto vibali vya utafutaji na uchimbaji wa Mafuta kwenye ziwa letu zuri Nyasa, Mbassaa mweh:
 
Mkuu! Hawa mafisadi ni kawaida yao kufanya hivyo ila hakika tunawaambia ya kwmb hapa tulipo si karne yaijuayo wao,tumeshasanuka Kitambo kama wanatarajia kufanya hili la ziwa nyasa kama mradi wao hakika itakula kwao!

Ngoja kwanza tuweke mambo ya siasa pembeni halafu bila shaka hili likipita tutajua yaliyojiri hapa ktk matumizi!

Hakuna mjinga ktk Tanzania yetu ya leo zaidi ya mafisadi wakubwa wa chama tawala tu!

Kudadekii itakula kwao mafisadi safari hii!

Wanadai kuwa wako tayari na majesh yetu yako tayari.... ukitaka wafikirie mara mbili kuhusu kumwaga damu za watanzania.. waambie tu ni lazima kila kiongozi atoe wanae kuonyesha mfano, hawa watoto wao nao waende vitani, uone kama hawata amua kutumia njia za kidplomasia...
 
hata yale mabomu ya mbagala na gmboto ilikuwa changa la macho kuzima baadhi ya issues.
nisingependa vita na nchi jirani ila napenda iibuke vita ya wenyewe kwe wenyewe ili tuanze kuheshimiana.
 
Suala ambalo lipo ni kuwa Wamalawi wametangaza ziwa lote ni lao na wameanza kufanya utafiti wa mafuta ndani ya ziwa bila kujali mpaka katikati ya ziwa! sasa je waachiwe tu waendelee? nani anajua kesho congo watasema tanganyika lote ni lao uganda wakasema victoria lote lao? mimi naona hatua za kijeshi dhidi ya malawi zinacheleweshwa bila sababu jeshi li strike haraka sana na kuwaondoa ndani ya mipaka yetu!tuacheni woga!
 
Mpaka sasa kauli nzito za kutishia vita zimeshatamkwa na wafuatao:
1. Samwel Sitta
2. BERNARD Membe
3. Edward Lowassa.
Ukiangali nyuma ya pazia utajua kuwa hawa wote wana Political Motive, na ni prospectives wa 2015!
ABIRIA CHUNGA MZIGO WAKO!
 
Suala ambalo lipo ni kuwa Wamalawi wametangaza ziwa lote ni lao na wameanza kufanya utafiti wa mafuta ndani ya ziwa bila kujali mpaka katikati ya ziwa! sasa je waachiwe tu waendelee? nani anajua kesho congo watasema tanganyika lote ni lao uganda wakasema victoria lote lao? mimi naona hatua za kijeshi dhidi ya malawi zinacheleweshwa bila sababu jeshi li strike haraka sana na kuwaondoa ndani ya mipaka yetu!tuacheni woga!

Mkulu

Unaweza kusababisha nipate ban...
 
Mara nyingine kuna hatari kubwa kwa migogoro inayotokea katika nchi zetu hizi kuvishwa sura zenye malengo binafsi ya watu au kundi la watu hasa malengo ya kisiasa na umaarufu au kufuta kashfa fulani zinazoikabili nchi husika.

Tanzania kwa sasa tuko katika mgogoro wa mpaka na nchi ya Malawi, unaohusisha Ziwa Nyasa. Mgogoro huu ni wa ukweli kabisa na si wa kutungwa maana upo tangu enzi za Mwalimu. Lakini kitu cha kuwa nacho makini ni upande wa maamuzi sahihi juu ya kukabiliana na mgogoro huu mzito ambapo usipokabiliwa kwa umakini, tutashuhudia nchi ikiingia kwenye vita na kumwaga damu za Watanzania, maana vita haina macho!

Hapa jamvini kwa sasa kuna threads ambazo zinasema wazi kuwa majeshi yetu yameshaanza kufanya mobilisation ya kusogea eneo la Kyela. Kuna mdau mmoja jana alisema kuwa mida ya saa 3.30 za usiku amekutana na Army Deployment ya hatari ambapo msafara mzito wa magari ya jeshi yapatayo 200 yakitokea PANDE ZA Arusha na Moshi yanaelekea kusini mwa nchi, ambapo kama ni kweli, basi hali si shwari.

Naomba kutoa tahadhari kwa wanadiplomasia, Wanasiasa na Jeshi kuwa tusipokuwa makini mgogogoro huu unaweza kuwa mtaji na kinga kisiasa(political camouflage) wa baadhi ya manyang'au wa hapa nchini kwetu, ambapo wanaweza kuamua ku'capitalize on it kwa kuiingiza nchi vitani kwa malengo kama:

I. Kuwafool wananchi wajue kuwa serikali yao inawajali sana na kulinda mipaka yake, wakati ambapo ukweli ni kuwa kila kona ya mpaka wa nchi yetu inapitika kirahisi tu na wazamiaji toka nchi za jirani(mifano ipo mingi).

II. Ku-divert attention ya wananchi ambapo sasa wako katika mijadala mizito juu ya hatima ya nchi yao. Kuna masuala mazito ambayo yametokea of recent ambapo mengine yameibuliwa Bungeni, na mengine yakiwa yanahusisha migomo na maslahi wa Tanatanzania kwa ujumla.

III. Kujisafisha na kutengeneza image inayopendeza usoni pa wananchi, ili kujiwekea malengo ya kufikiriwa kwa uongozi huko mbele ya safari.

IV. Kupata sababu ya kutotimiza ahadi nyingi zilizoahidiwa kwa wananchi nyakati za uchaguzi.

Isije kuwa tunalazimisha Punda afe lakini mzigo wa tajiri lazima ufike sokoni.

Nawasilisha.

Kwenye hiyo niliyo highlight RED nakubaliana nawewe kuwa hii ndiyo sababu mimi nionayo SIRIKALI inatafuta kujirudishia umaarufu kwa wananchi:-(
 
Suala ambalo lipo ni kuwa Wamalawi wametangaza ziwa lote ni lao na wameanza kufanya utafiti wa mafuta ndani ya ziwa bila kujali mpaka katikati ya ziwa! sasa je waachiwe tu waendelee? nani anajua kesho congo watasema tanganyika lote ni lao uganda wakasema victoria lote lao? mimi naona hatua za kijeshi dhidi ya malawi zinacheleweshwa bila sababu jeshi li strike haraka sana na kuwaondoa ndani ya mipaka yetu!tuacheni woga!
Wewe unasema hayo maneno coz uko Mbali na eneo la tukio!
Mtu anayeishi Mbeya au pale pale Kyela hawezi kuthubutu kuongea kitu hicho.
Ukitaka kujua zaidi waulize watu wa Uganda wa miaka ya 1978/79 wakueleze shughuli ya vita inamaanisha nini kwa raia wanaoishi hapo.
Just as we are talking here, nothing is the same in Kyela. Kuna jamaa yangu hapa kila baada ya masaa mawili anapokea simu za kuombwa hifadhi huku kutoka kwa watu wa kwao huko Kyela!
Think about it from the obtuse angle.
 
Mpaka sasa kauli nzito za kutishia vita zimeshatamkwa na wafuatao:
1. Samwel Sitta
2. BERNARD Membe
3. Edward Lowassa.
Ukiangali nyuma ya pazia utajua kuwa hawa wote wana Political Motive, na ni prospectives wa 2015!
ABIRIA CHUNGA MZIGO WAKO!

Asha Rose wewe kaa kimya tu,waache hawa wanaume wachumia tumboni wapayuke kwani hawajui uchungu wa kuzaa na ndio maana wanashabikia vita!!
 
Mara nyingine kuna hatari kubwa kwa migogoro inayotokea katika nchi zetu hizi kuvishwa sura zenye malengo binafsi ya watu au kundi la watu hasa malengo ya kisiasa na umaarufu au kufuta kashfa fulani zinazoikabili nchi husika.

Tanzania kwa sasa tuko katika mgogoro wa mpaka na nchi ya Malawi, unaohusisha Ziwa Nyasa. Mgogoro huu ni wa ukweli kabisa na si wa kutungwa maana upo tangu enzi za Mwalimu. Lakini kitu cha kuwa nacho makini ni upande wa maamuzi sahihi juu ya kukabiliana na mgogoro huu mzito ambapo usipokabiliwa kwa umakini, tutashuhudia nchi ikiingia kwenye vita na kumwaga damu za Watanzania, maana vita haina macho!

Hapa jamvini kwa sasa kuna threads ambazo zinasema wazi kuwa majeshi yetu yameshaanza kufanya mobilisation ya kusogea eneo la Kyela. Kuna mdau mmoja jana alisema kuwa mida ya saa 3.30 za usiku amekutana na Army Deployment ya hatari ambapo msafara mzito wa magari ya jeshi yapatayo 200 yakitokea PANDE ZA Arusha na Moshi yanaelekea kusini mwa nchi, ambapo kama ni kweli, basi hali si shwari.

Naomba kutoa tahadhari kwa wanadiplomasia, Wanasiasa na Jeshi kuwa tusipokuwa makini mgogogoro huu unaweza kuwa mtaji na kinga kisiasa(political camouflage) wa baadhi ya manyang'au wa hapa nchini kwetu, ambapo wanaweza kuamua ku'capitalize on it kwa kuiingiza nchi vitani kwa malengo kama:

I. Kuwafool wananchi wajue kuwa serikali yao inawajali sana na kulinda mipaka yake, wakati ambapo ukweli ni kuwa kila kona ya mpaka wa nchi yetu inapitika kirahisi tu na wazamiaji toka nchi za jirani(mifano ipo mingi).

II. Ku-divert attention ya wananchi ambapo sasa wako katika mijadala mizito juu ya hatima ya nchi yao. Kuna masuala mazito ambayo yametokea of recent ambapo mengine yameibuliwa Bungeni, na mengine yakiwa yanahusisha migomo na maslahi wa Tanatanzania kwa ujumla.

III. Kujisafisha na kutengeneza image inayopendeza usoni pa wananchi, ili kujiwekea malengo ya kufikiriwa kwa uongozi huko mbele ya safari.

IV. Kupata sababu ya kutotimiza ahadi nyingi zilizoahidiwa kwa wananchi nyakati za uchaguzi.

Isije kuwa tunalazimisha Punda afe lakini mzigo wa tajiri lazima ufike sokoni.

Nawasilisha.

Chezea wana siasa wewe...sioni logic ya kwenda kupigana vita na Malawi. Migogoro yote ya mipaka inatatuliwa na kundi maalumu la wasuluhishi na sio vitisho na kuletea vita zisizokuwa na mpango. Tutapa aibu sana kama tukikimbilia kuanzisha vita bila kufanya kwanza taratibu za kidiplomasia....we will be losers na tutachekwa na ulimwengu mzima....teh teh teh...ila marathon ya kukimbilia na wanajeshi wanaoikamata hiyo nchi mbona itakuwa supa.
 
Tumezoea ubabe ubabe...siku hizi hatuna tena diplomasia kwenye handling ya mambo yetu iwe kwenye migomo au mambo mengine yoyote yale. Jamani ina maana hatuna watu wenye hekima na kufikiria tena? Tutachekwa kweli kweli tukikimbilia kuanzisha vita.
 
Back
Top Bottom