Mgogoro wa MAREKANI na CHINA I stand with Chinese nitatoa sababu A to Z

kimsboy

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
8,991
17,888
Asallam alyekum/shalom wapendwa

Kwanza nianze kumshukuru mungu kila siku anatubariki njia na mawazo mapya ya maisha na teknolojia mbalimbali.
.
.
Kumekua na mgogoro wa kibiashara kati ya marekani na China muda mrefu..mgogoro huu umestafidi sana toka rais Trump alipoingia madarakani
.
.
Wote ni mashahidi mnakumbuka jinsi marekani wakati wa kampeni alivyoahidi kuibana China endapo angeshinda
.
.
Jee sababu zote hizo ninini?
Sababu kubwa naweza kusema ni chuki,kiburi,na wivu wa marekani dhidi ya kasi ya maendeleo na kukua kwa china...
.
.
Wote tunashuhudia maendeleo makubwa ya kiuchumi,kijamii na kisiasa inayopiga china hatua zinazoifanya Washington ijitafakari sana
.
.
Hofu ya Washington ninini?
Hofu ya marekani ni kuwa wanaiogopa china itawapiku kwa kila kitu hatimaye kuwa super power mpya duniani
.
.
Lakini naweza kukiri kitu kimoja kwamba Beijing imeiacha mbali Washington kwa ushawishi kwa sasa kiuchumi hususan katika nchi za dunia ya tatu mfano Africa na America ya kusini (latini)
.
.

Vita vya kibiashara kati ya marekani na China kampuni kubwa ya Huawei imepata pigo kubwa baada ya marekani kuanza kuishughulikia kampuni hiyo ya kichina kwa tuhuma ambayo ni za kushangaza...wote mnajua kuwa huawei ni kampuni iliyoongoza kwa mauzo ya simu duniani ikizipiku ,apple,lg,google nk
.
.
Ndipo marekani ilipoanza figisu za kutaka kuiangusha kampuni hii huku makampuni ya teknolojia kama google,facebook,instagram wakipiga marufuku huawei kutumia apps na teknolojia yao..Jee huawei itashinda hili jambo?Yetu macho....
.
.
Tuhuma ambazo Washington inaishutumu china ni kuwa anaiba teknolojia.Tuseme ukweli jee ni nchi gani iliyoendelea ambayo haitumii au kucopy au kupambana teknolojia kutoka nchi nyingine?
.
.
Ukifatilia historia ya marekani wakati wa vita vya pili utagundua teknolojia nyingi za kijeshi waliiba,kucopy na kutoa kwa manazi wa ujerumani wakati huo
.
.
Suala la China kucopy teknolojia sio la ajabu wala kushangaza madhali ni jambo zuri la maendeleo basi sioni tatizo...laiti na nchi za africa zingalikua na uwezo hata wa kucopy au kuiba teknolojia kama china basi tungelikua mbali mno
.
.
Kwanini nasimama na China???
Katika hii vita ya biashara kati ya China na marekani nasimama na china dhidi ya marekani kwasababu zifuatazo:--
.
.

1.China ndo ameifanya Africa tuwe walau hapa tulipo leo, mfano bila China sisi africa tusingekua na uwezo wa kumiliki bidhaa nyingi za kiteknolojia ambazo kwa dunia ya magharibi na bei zao ni ghali mno...mfano simu kama sio China tungeweza kumiliki?Tv,redio,magari,s imu,computer,na vinginevyo vingi tusingeweza kuvimudu kama sio china maana china wanajitahidi kuwa na bidhaa na vitu vya bei nafuu...
.
.


2.China amesaidia kuleta ushindani na kuleta ahueni ya bei za bidhaa dunuani:Uwepo wa bidhaa za china unazoshindana na za magharibi umezifanya nchi na makampuni kushusha bei ya bidhaa au bidhaa zao kuwa katika affordable price ambayo inawezesha watu wengi kuwa navyo..
Nawaambia ukweli kama sio China hata hizi simu tunazotumia zingekua zinatoka magharibi tu tungeuziwa bei kubwa na tusingemudu kununua na zingekuja na masharti kibao.
.
.

3.China kama rafiki wa kweli wa wa tanzania:Nikiri kuwa china alikua rafiki wa kweli wa tanzania hususan kipindi cha baba wa taifa reli ya Tazara,kujenga viwanda nchini wakati wa ujamaa,uungaji mkono wa hali na mali katika vita ya kagera...tukumbuke kipindi hicho china alikua rafiki wa dhati kwa wakati ule na pia alikua ni hali duni ya uchumi ya kiuchumi iliyofanana na sisi lakini ajikiongoja hivyo hivyo akatusaidia.Lakini utawala wa ccm ulishindwa kuendeleza viwanda vile au kuvibinafsisha na kuendelea kuvisimamia kwa umakini kwa ubia na private sector leo tungekua mbali.
.
.

4.Mikopo na misaada na ushirika wa kiuchumi toka China:Nikiri tunamuhitaji china sana katika kipindi hichi hususan tukipambana tufikie uchumi wa kati...Tunahitaji support kubwa sana kutoka china..wengi mnajua kidemografia china ni nchi yenye watu zaidi ya milioni 1600...Idadi kubwa ya watu ni fursa kubwa kwetu sisi kuuza bidhaa zetu china na kuleta wawekezaji wa kutosha..
.
.

Kisiasa na kijamii
Kuna maneno mengi yanazungumzwa kuwa China inawalinda madikteta Africa hili ni jambo lina ukweli lakini pia Washington inawalinda madikteta tena nchi zenye rasilimali..au madikteta wa kistatejia wa kulinda maslah yao mfano nchi jirani hapo...na nchi za kidikteta zinazolindwa na marekani ni nyingi mfano Saudi arabia...
.
.
Nikiri jambo moja kuwa tunazihitaji both side west na china....likija suala la democracy na utawala bora tunahitaji sapoti kutoka marekani na nchi za magharibi maana Africa bado tuna safari ndefu sana....
.
.


HITIMISHO LENYE MANENO YA KUTILIA MANANI
-Tunalia mikopo ya China hailipiki jee mikopo ya IMF na WB ndo inalipika??Jibu ni kuwa mikopo yote si mizuri ila wb na imf ni mibaya sana. Halafu pia tunafeli kuifanyia mikopo kinachostahili kwasababu ya watawala wa africa wengi wao hawatumii bongo zao kufikiri wanatumia sifa na ulimbukeni wa kufanya miradi isiyoweza kulipa deni na isiyokua na tija na wengine wanafanya miradi mikubwa tu ili washinde chaguzi
Mfano misaada inayotolewa ingelikua inagusa miradi kwa 100% au kwa wananchi kwa 100% tungekua mbali na sio tegemezi tena..mfano nchi nyingi za Africa pesa ya misaada inaliwa kuanzia kwa mkuu,mawaziri,wabunge,mikoa wilaya mpaka watendaji wa chini mpaka ifike kumgusa mwananchi wa kawaida inabaki 30% huku 70% ya pesa ikiishia kudonolewa huko kote inapita ikidonolewa kidogo kidogo halafu mnataraji misaada au mikopo itatusaidia?
.
.


Tunahitaji pande zote ili kufikia mbali kimaendeleo...suala la kusema tumuache mchina halifai tuende na marekani tu?hapana marekani si yule anayetoa msaada kwa masharti ya ajabu ajabu mfano ushoga na usagaji?...Tukiegemea upande mmoja hatuwezi tukasonga mbele...Tunahitaji yote hayo hususan china kwa sasa ndo maana nasimama na china

Imeandikwa na Ridhiwani Kimaro (kimsboy)
4bsh730f24e5dd1eyxq_800C450.jpeg
 
Marekani baada ya Donald Trump kuingia madarakani, na mpango wake wa "Make America Great Again" inaweza ikakupa picha kwamba To Some Extent, Trump alihisi kuwa huenda Marekani ilianza kupungua nguvu au ushawishi mahala fulani. Na anachojaribu kukifanya DT si cha kushangaza sana kama watu wanavyodhani ila ni matokeo tu ya sera zake za "Marekani Kwanza".

Kwa upande wangu MIMI. Sioni vita yeyote ile ya kiuchumi kwa SASA kati ya Marekani na China au naweza kusema kama ni "Vita" basi bado HAIJAANZA!.....
Ninachokiona mimi hapa ni "Mgogoro" tu wa kimaslahi. Naomba nieleweke hapo... Linapokuja swala la vipaumbele vya taifa hasa katika kukuza Uchumi kila nchi huwa na maslahi yake na huyatanguliza kwanza yake kabla ya mwingine na ndio maana kuamua kujiweka upande fulani katika mgogoro huu ni kama "Ushabiki" tu wa kawaida.

Wakati mgogoro huu ukiendelea, Marekani na China, kumekuwa na majibizano ya hapa na pale na kila upande umekuwa ukimshutumu mwenzake. Ikumbukwe kuwa bado kuna Commercial Activities nyingi mbalimbali zinaendelea kati ya nchi hizi mbili ingawa kilichofanyika ni kuongezeana tu ushuru wa bidhaa zinazoingia kutoka upande wa pili.

Nisiseme mengi. Kuna wanaoona kwamba Marekani ataathirika katika mgogoro huu na wapo wanaosema China ataathirika. Wote wanaweza kuwa "Sahihi" kwa namna fulani ukizingatia ni jinsi gani kila mmoja anaona maslahi yake yako upande gani. Ndio maana kuna michango mbalimbali mitandaoni unakuta mtu anasema, "China wana bidhaa za bei rahisi" ndiyo unamkuta huyu ana-Support China huku mwingine akisema "China ni wezi sana wa kiteknolojia" ndiyo maana anakaa upande wa Marekani. Lakini yote hiyo ni maslahi tu. Kila mmoja anaangalia maslahi yake binafsi na kwa Dunia ya sasa, mwenye nguvu na ushawishi zaidi kuliko mwingine ndiye ambaye ana nafasi kubwa ya kuyalinda maslahi yake kuliko mwingine. Niishie hapa kwa sasa.

Vita ya kiuchumi kati ya hao wawili bado haijaanza. Tuendelee kuisubiri!
 
Huawei haijawai kuongoza kwa mauzo ya simu duniani,acha kureport uongo mkuu.
 
Waliotaka kujenga bandari ya bagamoyo ni china,umeona mkataba ulivyo hadi magufuli kachoka,acha kuongea vitu usivyovijua,china ni hatari Sana aisee,kuna kipindi raisi wao alisepa na pembe za ndovu kwenye plane yake,how come uone anafaa au ww ni kiziwi.
 
Marekani baada ya Donald Trump kuingia madarakani, na mpango wake wa "Make America Great Again" inaweza ikakupa picha kwamba To Some Extent, Trump alihisi kuwa huenda Marekani ilianza kupungua nguvu au ushawishi mahala fulani. Na anachojaribu kukifanya DT si cha kushangaza sana kama watu wanavyodhani ila ni matokeo tu ya sera zake za "Marekani Kwanza".

Kwa upande wangu MIMI. Sioni vita yeyote ile ya kiuchumi kwa SASA kati ya Marekani na China au naweza kusema kama ni "Vita" basi bado HAIJAANZA!.....
Ninachokiona mimi hapa ni "Mgogoro" tu wa kimaslahi. Naomba nieleweke hapo... Linapokuja swala la vipaumbele vya taifa hasa katika kukuza Uchumi kila nchi huwa na maslahi yake na huyatanguliza kwanza yake kabla ya mwingine na ndio maana kuamua kujiweka upande fulani katika mgogoro huu ni kama "Ushabiki" tu wa kawaida.

Wakati mgogoro huu ukiendelea, Marekani na China, kumekuwa na majibizano ya hapa na pale na kila upande umekuwa ukimshutumu mwenzake. Ikumbukwe kuwa bado kuna Commercial Activities nyingi mbalimbali zinaendelea kati ya nchi hizi mbili ingawa kilichofanyika ni kuongezeana tu ushuru wa bidhaa zinazoingia kutoka upande wa pili.

Nisiseme mengi. Kuna wanaoona kwamba Marekani ataathirika katika mgogoro huu na wapo wanaosema China ataathirika. Wote wanaweza kuwa "Sahihi" kwa namna fulani ukizingatia ni jinsi gani kila mmoja anaona maslahi yake yako upande gani. Ndio maana kuna michango mbalimbali mitandaoni unakuta mtu anasema, "China wana bidhaa za bei rahisi" ndiyo unamkuta huyu ana-Support China huku mwingine akisema "China ni wezi sana wa kiteknolojia" ndiyo maana anakaa upande wa Marekani. Lakini yote hiyo ni maslahi tu. Kila mmoja anaangalia maslahi yake binafsi na kwa Dunia ya sasa, mwenye nguvu na ushawishi zaidi kuliko mwingine ndiye ambaye ana nafasi kubwa ya kuyalinda maslahi yake kuliko mwingine. Niishie hapa kwa sasa.

Vita ya kiuchumi kati ya hao wawili bado haijaanza. Tuendelee kuisubiri!
Well said
 
Mkuu Hivi ni Lini uliwahi kusimama upande wa USA? Maana wewe ni pro-communist countries hasa zile zinazojitokeza kukinzana na USA,so nothing new.
Fatilia threads zangu kule jukwaa la siasa...tatizo mnaangaliaga hapa international forum tu
 
Waliotaka kujenga bandari ya bagamoyo ni china,umeona mkataba ulivyo hadi magufuli kachoka,acha kuongea vitu usivyovijua,china ni hatari Sana aisee,kuna kipindi raisi wao alisepa na pembe za ndovu kwenye plane yake,how come uone anafaa au ww ni kiziwi.
Soma vizuri bandiko langu mwanzo mwisho uelewe vizuri...nilichozungumzia kuhusu both sides
 
Huawei haijawai kuongoza kwa mauzo ya simu duniani,acha kureport uongo mkuu.


 
Huawei haijawai kuongoza kwa mauzo ya simu duniani,acha kureport uongo mkuu.
Hajawah kuongoza mauzo unaishi karne gani mkuu??
Angalia hapo baada ya samsung ni yeye apple keshaachwa mbali
IMG_20190609_223336_806.JPG
 
Huawei anatisha sasa katoka na 5G kasi kubwa ya Internet haijawahi kitokea wiki hii wamesaini mkataba na kandarasi wake na wamefikia makubaliano ya kutotumia dola ya marekani hii vita ni tamu kinyama Kwa watazamaji
 
Me nadhani kujadili hiyo migogoro ya wenzetu walioko miaka 1000 mbele yetu kiteknolojia haitusaidii wakuu, bora tujadili reli yetu ya stigler george na daraja letu la aga khan lina manufaa gani kwetu, Hao wachina na wamerakani wote wanafanya mambo kwa maslahi yao binafsi hakuna hata mmoja anaetaka Africa iendelee, Vyema tungejadili maendeleo ya kwetu kwanza.
🚶‍♂️
 
Kinachoniuzi kwa Mchina nikutengeneza vitu feki yaani havina ubora kabisa. Napata ugumu sana ninapotaka kununua flash drive, hard disk, usb cable na memory card. Kiufupi china kaharibu soko la bidhaa japo watu wanaona kama hajaribu kisa kwa sasa kuna simu zinauzwa mpaka 15,000. Bila TCRA kudhibiti kungekuwa na uchafu wa simu. Ukitaka kuona nunua simu ya marekani na ya mchina uone shughuli yake. Nina nokia belle 500 ya korea, ishadondoka mara nyingi sana lakini mpaka sasa sijawahi kuibadilishia hata kioo ni ya 2013. Ingekuwa ya Mchina ingekuwa ishakufa zamani sana.
Mchina kinachomponza na kuonekana wa ovyo ni kucopy na kupaste na kutengeneza vitu visivyo na ubora. Wenzake wanaumiza kichwa kuja na kitu kipya yeye anapita humo humo kwa wenzake. Simu ya Nokia, Blackebery, na iPhone za Kichina utazikuta. Ukishika simu ya Mchina lazima uifananishe na ya marekani tu.
 
Wewe Umeona wamesema Huawei ni first au second one,just surpassed iPhone,and they never lead before till now.au hujasoma ulicho ki quote mkuu.
Huawei kawa wa pili kwa mauzo duniani sijui tatizo lako ninini maana nimekuwekea mpaka na links za kusoma
Soma links ndo urudi
 
Huawei anatisha sasa katoka na 5G kasi kubwa ya Internet haijawahi kitokea wiki hii wamesaini mkataba na kandarasi wake na wamefikia makubaliano ya kutotumia dola ya marekani hii vita ni tamu kinyama Kwa watazamaji
Marekani anawafanya china wajipange vizuri
 
Mkuu migogoro yetu hatuwezi kuiongea hata kidogo maana hatuwezi kufika muafaka mzuri kwakuwa tunaogopa wenye mamlaka
Me nadhani kujadili hiyo migogoro ya wenzetu walioko miaka 1000 mbele yetu kiteknolojia haitusaidii wakuu, bora tujadili reli yetu ya stigler george na daraja letu la aga khan lina manufaa gani kwetu, Hao wachina na wamerakani wote wanafanya mambo kwa maslahi yao binafsi hakuna hata mmoja anaetaka Africa iendelee, Vyema tungejadili maendeleo ya kwetu kwanza.
 
Back
Top Bottom