mzee wa njaa
JF-Expert Member
- Jun 16, 2011
- 1,366
- 223
Kama JK yuko hivi basi hafai. Ila mambo haya yanahitaji uchunguzi wa kina isijekuwa una mchafua Rais wetu mwema.
Wana JF,
Taarifa za kiintelijensia toka kwa wanaTISS wachache waliobakia na uzalendo kwa taifa lao zinsema, Rais wetu JK ndiye aliyetega mirija kila kona kuhakikisha anachota kila kinachoingia Tanesco.
IKO HIVI:
Mtakumbuka vizuri kuwa kampuni ya Richmond ilitengenezwa mikononi mwake huku akimtumia Lowassa kufikisha ujumbe Tanesco. Mambo yalipoharibika alimtoa kafara rafiki yake. Japo Lowassa amejigamba mara nyingi kuwa hawakukutana barabarani, ukweli ni kuwa bado hamjui vizuri swahiba wake.
Mgogoro uliopo Tanesco baina ya Muhando na wakuu wake ni wa kutengenezwa ili kuwaokoa katibu mkuu bwana Maswi na waziri wake Prof. Muhongo. Pamoja na kwamba Muhando ametengeneza tenda aliyompa mkewe hiyo si ishu kubwa kwa kuwa vifaa kweli vitakuwa supplied ila deal alilopiga katibu mkuu la kuingia mkataba Puma Company Ltd (zamani BP) ambayo haina sifa na pia kufanya kinyume na sheria za PPRA simply because JK anahisa hukoa ndiko kulikokuza ishu ya mhando ili atolewe kafara uma usiangalie deal hilo lenye thamani ya bilioni 26.
Ukweli ni kwamba wabunge wakiamua kukomaa JK bye bye. Lakini taarifa zinasema JK amemwagiza Pinda kuhakikisha anawaziba midomo wabunge wote wazalendo. Taarifa zinasema Anne Kilango ameingia laini na katika moja ya vikao vyao vilivyoongozwa na Pinda alisimama kidete kutetea kuwa joja hii ikijadiliwa bungeni serikali na chama chao cha CCM vitaanguka!
Aidha taarifa zinazidi kusambaa kuwa JK ametoa maagizo kwa viongozi wa wizara ya nishati na madini tangu wakati wa Ngeleja kuwa hakuna kutumia gesi kwa ajili ya kuzalisha umeme badala yake majenereta yatumie mafuta mazito ambayo asilimia kubwa yatatoka GAPCO ambako yeye anahisa tangu akiwa waziri.Swali la msingi; Kama gesi imetoka all the way from mtwara to ubungo, mafuta ya nini?
Aidha Tanesco hulazimishwa kutengeneza mgao feki ili bwana mkubwa achote chake. Isitoshe maajabu mengine ni kwamba Tanesco wameingia mkataba na kampuni ya Ridhiwani ya kuleta nguzo za umeme toka Afrika Kusini na si Iringa tena. Yapo mambo mengine mengi tangu Richmond, DOWANS, Symbion na haya ma-IPTL, Agreko n.k ambayo JK anayajua vema lakini ameendelea na roho ngumu ya kuwanyonya watanganyika.
Ombi langu kwa Mungu, Avuruge nchi hii ili tuanze upya.
Wana bodi mnasemaje?
Hivi kwanini kampuni imebadili jina kutoka BP?
kimbunga na mafisadi patamu hapo!!Siku hizi tunaweza kutunga story tamu! Yaani tunafika mahala tunasema Mhando kaonewa? Kiongozi mwadilifu ya nini uchukue familia yako ifanye biashara na kampuni unayoiongoza. Hata kama alipata tenda kihalali lakini sheria ya manunuzi haitaki hasa kama haku declare conflict of interest. Kuhusu Puma kama zerikali iliweza kuokoa Tshs. 400.00 kwa lita ubaya uko wapi hasa ukizingatia Puma inamilikiwa kwa kiasi kikubwa na serikali. Pia ikumbukwe kwamba kabla Serikali haijaamua hivyo ilipata ushauri toka Mamlaka ya Usimamizi wa Manunuzi ya Umma.
Sasa naanza kuamini kwamba mhando ni mwizi na kwa maana hiyo naendelea kuprove kuwa nchi hii kila mtu ni fisadi.
Hivi kwanini kampuni imebadili jina kutoka BP?
walifungiwa kutokana na kuendesha mgomo wa kuuza mafuta! pia wanakwepa kodi!
rais mkapa alifanya biashara na mkewe akiwa ikulu na kuiba pesa nyingi mbona hakuna anayelalamika???siku hizi tunaweza kutunga story tamu! Yaani tunafika mahala tunasema mhando kaonewa? Kiongozi mwadilifu ya nini uchukue familia yako ifanye biashara na kampuni unayoiongoza. Hata kama alipata tenda kihalali lakini sheria ya manunuzi haitaki hasa kama haku declare conflict of interest. Kuhusu puma kama zerikali iliweza kuokoa tshs. 400.00 kwa lita ubaya uko wapi hasa ukizingatia puma inamilikiwa kwa kiasi kikubwa na serikali. Pia ikumbukwe kwamba kabla serikali haijaamua hivyo ilipata ushauri toka mamlaka ya usimamizi wa manunuzi ya umma.
rais mkapa alifanya biashara na mkewe akiwa ikulu na kuiba pesa nyingi mbona hakuna anayelalamika???