Mgogoro wa CUF ni pigo kubwa kwa ukawa uchaguzi wa 2020

Bernard bakari

JF-Expert Member
Mar 30, 2016
407
780
Chama cha Wananchi CUF, kipo kwenye mgogoro mkubwa wa kiutawala uliosababishwa na kurudi kwa prof Lipumba kwenye uenyekiti wa chama hicho.

Prof Lipumba alijihudhuru nafasi ya Uenyekiti kwenye Chama cha wananchi CUF mnapo tarehe 5/8/2015 kwa madai kuwa dhamira yake inamsuta kushirikiana na mheshimawa Edward Lowassa katika uchaguzi wa 2015, Hivyo ameamua kuachia ngazi na yeye angebaki kama mwanachama wa kawaida,uchaguzi wa 2015 hakufanya kampeni hata chembe.

Prof lipumba ametumia mapungufu ya kikatiba yaliyofanywa na Aliyekuwa katibu mkuu wa chama hicho Maalim seif na kamati ya uongozi wa muda chini ya mwenyekiti Julius Mtatiro kutopeleka mabadiliko kwa msajiri mkuu wa vyama vya siasa pamoja na barua yake kutojadiliwa na kamati kuu kijirudishia nafasi yake ya kuwa mwenyekiti tena wa chama hicho.

Kurudi kwa mara nyingine kwa prof Lipumba kumeleta mpasuko mkubwa kwenye chama hicho, ikiwepo kumwondoa Aliyekuwa Katibu mkuu Mheshimwa Maalim Seif na kumteua mbunge Magdelina sakaya kuwa katibu mkuu mpya kitu kinachoongeza mpasuko mkubwa na kuna dalili zote za chama hicho kukosa ushirikiano baina ya wanachama wake wa bara na wa zanzibar.

Mgogoro huu wa Cuf unamadhara mawili juu ya maendeleo ya ukawa. Kwanza kuna kila dalili ya chama cha CUF kuweza kujiondoa ndani ya Ukawa, hii inatokana na prof Lipumba kutoona faida ya ukawa kwa Cuf, pili ukawa kukosa makubaliano ya kusimamisha mgombea mmoja mmoja kwa kila jimbo ili kutoa nafasi kwa wao kuchukua majimbo mengi kama tulivyoshuhudia uchaguzi wa 2015, hivyo kutapelekea Wapinzani kupoteza baadhi ya majimbo.

Mgogoro huu ni pigo kubwa kwa wapinzani unatakiwa utatuliwe, kukimbia mazungumzo au kumsusia Lipumba chama ni kujihatarishia ushindi katika ngazi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi ujao. Wapinzani wajikite kuutafutia ufumbuzi kuliko kurushiana vijembe kwenye vyombo vya habari. Mgogoro na kuvunjika kwa Ukawa furaha kwa CCM
 
Sidhani so long as Maalim Seif yupo na ukawa hata chama kikikatika bado Seif ana kundi kubwa tu.
 
Tanzania hakuna mpinzani kwa serikali ila kuna upinzani ndani ya vyama likitokea hakuna wa kusulihisha mpaka mmoja anyooshe mikono,rejea nyuma cuf,nccr,chadema na tlp
 
Mjifariji hakuna upinzan2015 ilikuwaje kama sio akina Nape wanaolialia Leo ingekuwaje?jitoe ufahamu babu!2020 sio mbali ikija tume huru utaelewa kilichomnyoa kanga manyoya!;;
 
Tanzania HAKUNA upinzani mkuu...karibia ya wote walioko upinzani ni makada wa CCM, wako kule kwa ajili ya kula ruzuku tu.

Bila shaka huelewi matokeo halali ya uchaguzi wa Zanzibar yalikuwaje.
Lipumba hana madhara yoyote maana hajawahi kuwa hata Diwani.
 
Bila shaka huelewi matokeo halali ya uchaguzi wa Zanzibar yalikuwaje.
Lipumba hana madhara yoyote maana hajawahi kuwa hata Diwani.


Unayajuwa anayofanya chini kapeti? Penye moshi siku zote uwa kuna moto, jiulize why CUF hawaishi kugombana na kuvunja nguvu chama? Utaona wanakuja juu kuipiku CCM, mwisho wa siku wanavurugana wenyewe kwa wenyewe, wanachogombania cha msingi hakuna.
 
Chama cha Wananchi CUF, kipo kwenye mgogoro mkubwa wa kiutawala uliosababishwa na kurudi kwa prof Lipumba kwenye uenyekiti wa chama hicho.

Prof Lipumba alijihudhuru nafasi ya Uenyekiti kwenye Chama cha wananchi CUF mnapo tarehe 5/8/2015 kwa madai kuwa dhamira yake inamsuta kushirikiana na mheshimawa Edward Lowassa katika uchaguzi wa 2015, Hivyo ameamua kuachia ngazi na yeye angebaki kama mwanachama wa kawaida,uchaguzi wa 2015 hakufanya kampeni hata chembe.

Prof lipumba ametumia mapungufu ya kikatiba yaliyofanywa na Aliyekuwa katibu mkuu wa chama hicho Maalim seif na kamati ya uongozi wa muda chini ya mwenyekiti Julius Mtatiro kutopeleka mabadiliko kwa msajiri mkuu wa vyama vya siasa pamoja na barua yake kutojadiliwa na kamati kuu kijirudishia nafasi yake ya kuwa mwenyekiti tena wa chama hicho.

Kurudi kwa mara nyingine kwa prof Lipumba kumeleta mpasuko mkubwa kwenye chama hicho, ikiwepo kumwondoa Aliyekuwa Katibu mkuu Mheshimwa Maalim Seif na kumteua mbunge Magdelina sakaya kuwa katibu mkuu mpya kitu kinachoongeza mpasuko mkubwa na kuna dalili zote za chama hicho kukosa ushirikiano baina ya wanachama wake wa bara na wa zanzibar.

Mgogoro huu wa Cuf unamadhara mawili juu ya maendeleo ya ukawa. Kwanza kuna kila dalili ya chama cha CUF kuweza kujiondoa ndani ya Ukawa, hii inatokana na prof Lipumba kutoona faida ya ukawa kwa Cuf, pili ukawa kukosa makubaliano ya kusimamisha mgombea mmoja mmoja kwa kila jimbo ili kutoa nafasi kwa wao kuchukua majimbo mengi kama tulivyoshuhudia uchaguzi wa 2015, hivyo kutapelekea Wapinzani kupoteza baadhi ya majimbo.

Mgogoro huu ni pigo kubwa kwa wapinzani unatakiwa utatuliwe, kukimbia mazungumzo au kumsusia Lipumba chama ni kujihatarishia ushindi katika ngazi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi ujao. Wapinzani wajikite kuutafutia ufumbuzi kuliko kurushiana vijembe kwenye vyombo vya habari. Mgogoro na kuvunjika kwa Ukawa furaha kwa CCM
Itakuwa vizuri sana Wapinzani wakichukua majimbo machache sana na ikiwezekana wakose kabisa maana tumewachoka na ulaghai wao bila vitendo!!! Wananchi tumeielewa, tumeikubali na tunaipenda CCM. Chama pekee chenye nia ya dhati ya kuleta maendeleo katika Nchi hii!!
 
Unayajuwa anayofanya chini kapeti? Penye moshi siku zote uwa kuna moto, jiulize why CUF hawaishi kugombana na kuvunja nguvu chama? Utaona wanakuja juu kuipiku CCM, mwisho wa siku wanavurugana wenyewe kwa wenyewe, wanachogombania cha msingi hakuna.

Mamluki wapo kila chama.Hukumbuki hata CCM imewavua uanachama baadhi ya wenyeviti wa CCM wa Mikoa kwa kuwatuhumu kuhujumu chama.
CUF ina nguvu sana kama hujui muulize Jecha kwa nini alikataa kutangaza matokeo ya tarehe 25.10.2015 na kuamuru uchaguzi urudiwe upya.
 
Mamluki wapo kila chama.Hukumbuki hata CCM imewavua uanachama baadhi ya wenyeviti wa CCM wa Mikoa kwa kuwatuhumu kuhujumu chama.
CUF ina nguvu sana kama hujui muulize Jecha kwa nini alikataa kutangaza matokeo ya tarehe 25.10.2015 na kuamuru uchaguzi urudiwe upya.


Nimepigia simu lakini hapokei. Hii ya mwisho kapokea msaidizi wake na kasema wazanzibar kuongea ni ajira yao, hata kama hawajuwi kitu lazima wataongea tu. Kanisihi niachane nao.
 
Wachambuzi wako wengi siku hizi
haya mtuambie ni lini na wapi Maalim seif aliwahi kufanya mkutano wa siasa na kuinadi cuf upande wa Tanzania bara
Siasa za Maalim seif ni Zanzibar tu na hata prop lipumba aliingia mkenge kwa sera za Maalim seif za kutaka Zanzibar kwanza ,na wakisha ichukua Zanzibar ndio warudi sasa Tanzania bara
Prop lipumba alikubaliana na ili waanze na Zanzibar kisha warudi bara
Kilichomuuzi lipumba ni usultan wa Maalim seif ya kwamba yeye ndio kila kitu ana hata haja ya kuifuhata katiba ya chama achosema sema yeye Seif ndio sheria
Watu wamechoka na usultan ndio wakaenda kumfuata lipumba nyumbani kwake na kuanza kumshawishi ili arudi chamani kwa sababu Seif afuati katiba anaendesha chama kama mali yake binafsi
hiki ndio chanzo kikubwa cha mgogoro wa cuf zingine zote ni mbwembwe tu..
 
Ukiacha mihemko ya kitoto
Kila Taasisi inaendeshwa na KATIBA na hiyo katiba ya Taasisi kuna maamlaka zinazo isimamia endapo itakiukwa upo uwezekano hata hiyo Taasisi 1)kufutwa au kuonywa

Ndio maana hata jana uliona ile barua ya RITA ikikanusha kusajiliwa kwa Bodi ya wadhamini ya Maalim seif
Mbaka waone katiba yao inasemaje na hao waliondolewa kama wadhamini je,sheria imefuhatwa ..
 
Mamluki wapo kila chama.Hukumbuki hata CCM imewavua uanachama baadhi ya wenyeviti wa CCM wa Mikoa kwa kuwatuhumu kuhujumu chama.
CUF ina nguvu sana kama hujui muulize Jecha kwa nini alikataa kutangaza matokeo ya tarehe 25.10.2015 na kuamuru uchaguzi urudiwe upya.
Kulitokea udanganyifu mkubwa kwenye karatasi za matokeo ndio maana J S J aliamua kuhesabu kura, walipokataa akaDELETE
 
Back
Top Bottom