Mgogoro na Kenya: Kwanini Kikwete, Membe & Nyalandu hawataki kutuambia ukweli?

CRITICAL MIND

JF-Expert Member
Sep 1, 2013
415
386
Lazaro-Nyalandu1.jpg



JK na Nyalandu tumewapa mandate sisi wananchi na kazi yao ni kutuwakilisha kama taifa na maslahi ya taifa. Haimaanishi kuwa JK ni Sultan hivyo asitueleze kinachoendelea au asiwajibike kwa sisi wananchi. JK asipowajibika kwetu inamaana atakuwa anakwenda kinyume na katiba aliyoapa kuitetetea na maslahi ya nchi hii.

Hivyo bas, tunaweza kusema kuwa kinachoendelea na mgogoro na Kenya ni aibu kitaifa na mbaya zaidi kuna issues za NATIONAL INTEREST ambazo ziko at stake na moja wapo ni mapato.

Sasa kwa nini hawa masultani wetu hawataki kutuambia kwa nini waligoma kwenda kwenye mkutano na Kenya kutatua hili tatizo? Kwa nini tunafichwa? hii hiki kimya maana sisi kama wananchi tukitafsiri vipi?

Kwa sababu hawa watawala wetu hawataki kuwa honest na sisi basi wengine hatuna namna bali kuweka wazi tunayojua halafu ikifika AlHamis wiki hii Kurugezi ya mawasiliano ikulu itatoa statement kupinga tunayosema humu JF, Wizara ya Utalii nao watatoa statement kupingana na Ikulu, kule mambo ya nje nako wapambe wa Membe watatulea story kupingana na Ikulu na wizara ya Utalii na mwisho kabisa bodi ya utaliii nao watakuja na yao na bila kusahau MAELEZO watakuja na ngojenra tofauti ambazo zitalenga kuishambulia JF.

In short serikali hii ya BIG RESULTS NOW imekuwa incompetent kuliko club ya wendawazimu.

So far FACTS ni hizi:


1. Serikali ya JK ilijulishwa kuhusu mkutano na Kenya kujadili na kusuluhisha hili jambo zaidi ya miezi 3 iliyopita na walikubali watahudhuria na wenzao kule kenya waliwapa list ya agenda za mkutano


2. Serikali ya JK wakakumbushwa tena na wakasema hamana neno. Lakini out of blue KAMA VINYONGA wakaaanza na mambo ya "SUBRA" na mwishowe wakadai kuwa pamoja na facts zote kuwa on the record na wao kuwa na wasomi walio bobea wakadai waongezewe muda, ili wataalam or who ever those wonks are eti watengeneze comprehensive list ya madai ili kupata mbadala wa mkataba wa 1985 baina ya Kenya na Tanzania juu ya utalii.


3. waziri wa utalii wa Tanzania NDUGU Nyalandu amekuwa kama vile anaongoza team ya wapiga ramli ambayo kila mmoja anasema lake. Inaovyoonekana kuwa kulikuwa hakuna coordination kama kawaida ya hii serikali, Maofisa wake walikuwa wanaendelea na mikakati ya kufanya huo mkutano lakini wakapigwa STOP na mabosi wa Wizara ya Mmabo ya Nje bila kupewa sababu zizote zile. Wakati huo huo Ndugu Nyalandu alikuwa anaendelea kuwaambia waziri mwenzake wa kule Kenya kupitia e-mail yake kuwa : "the meeting will take place without any delays considering it might cost Tanzania greatly if nothing has been agreed"


4. Nyalandu alijua kuwa mkutano uliongezwa tena wiki 2 zingine lakini si yeye wala maofisa wa serikali ya JK walifanya juhudi zozote zile huku wakijua wazi kuwa muda wa huo mkutano usingeongezwa tena na walijua fika the price watu wetu wangelipa kama kusingekuwepo na makubaliano hata ya muda mfupi ili faifa lisipate hasara.


5. Ukweli ni kuwa tatizo ni JK na serikali yake kwa sababu watalii wanashindwa kutua Kilimanjaro kwa sababu hakuna connectivity kubwa na hii inatokana na serikali ya nchi hii kutoona umuhimu wa kuongeza investments kwenye KIA na wanajua kama investments kwenye uwanja wa Kia mapato yangezidi na ndege nyingi zingekuwa zinatua hapo na hii kadhia ya kutua JKIA isingekuwepo.


6. Kma serikali iligoma kwenda kwenye huo mkutano wa tarehe 5 kwa nini hawakuwajulisha TATOA mapema? Hivi serikali ita wa refund haya makampuni au itakuwaje? na kwa nini serkali haitaki kuwa wakweli kwa watanzania? na kwa nini kila kitu chenye maslahi kwa wananchi kinafanywa kisiri siri? na je nani ananufaika na huu mgogoro?


Sasa ngoja nitafute CAG report juu ya hii wizara ya utalii na maliasili nione wana madudu gani.
 
Last edited by a moderator:
Sunlight is said to be the best of disinfectants.

Unfortunately for us, the concepts of openness and transparency in government are seemingly foreign.

If they don't even tell us (and most people don't even demand to know) how much we pay them in remunerations what makes you think they will tell us the truth in this ongoing saga, really?
 
Acha tuendelee kuweka "usawa" kwa wagombea ubunge ili kila mwananchi awe na haki ya kuwa mbunge, ili mambo ya faida kwa Taifa yaatamiwe na wachache. . . . . . . . .
 
Kwahiyo unataka kuambiwa ukweli gani hivi huoni kuwa wakenya ni wajinga wanaanzisha mambo ambayo yapo kinyume na utaratibu halafu ukajadilili nini.

kumbuka mtu akianzisha jambo la kijinga na wewe ukakubali kulijadili utakuwa mjinga pia.
 
Ccm imeua KIA na imebaki kulalamika tu. Sijaona sababu ya kuilaumu kenya katika mgogoro huu. Wa kujilaumu ni sisi wenyewe, kwa kuwa na sera na mipango mibovu kwenye miundo mbinu yetu ya uchumi.
Wewe ndiyo hujitambui kabisa unadhani uongo unajenga mantiki?
 
Tunasonga kistim na ndoto kede, Tanzania works for miracle not reality product of BRN
 
Kwahiyo unataka kuambiwa ukweli gani hivi huoni kuwa wakenya ni wajinga wanaanzisha mambo ambayo yapo kinyume na utaratibu halafu ukajadilili nini.

kumbuka mtu akianzisha jambo la kijinga na wewe ukakubali kulijadili utakuwa mjinga pia.


Tunataka serikali aiache kutufanya wajinga na iweke wazi FACTS kuhusu huu mgogoro

btw


 
Last edited by a moderator:
Tunataka serikali aiache kutufanya wajinga na iweke wazi FACTS kuhusu huu mgogoro

btw



Hakuna kitu cha kushangaa hapo. Kama tulidanganywa na kuuziwa ndege mbovu toka senegal . What do you expect? Donkey brain.
 
Last edited by a moderator:
mkuu usitegemee kuambiwa ukweli wowote toka kwa watawala walioshindwa kuongoza nchi na sera zao mbovu! hapa wanataka kuendelea kutumia ujinga wa wananchi ili wasijue kinachoendelea, si unajua tena hii 2015!
 
Halafu Zitto kanakimbilia kwenye mitandao ya kijamii kuongea ongea tu,nakachukia kale kanifiki kwa kugeuka kuwa ngao na kajibwa ka hii serikali dhaifu.
 
Kwahiyo unataka kuambiwa ukweli gani hivi huoni kuwa wakenya ni wajinga wanaanzisha mambo ambayo yapo kinyume na utaratibu halafu ukajadilili nini.

kumbuka mtu akianzisha jambo la kijinga na wewe ukakubali kulijadili utakuwa mjinga pia.

Umeongea vizuri kabisa. Hivi kati ya ccm na waislamu nani aliyeanzisha mambo (kadhi court)kinyume na utaratibu.? Sasa ma sheikh waliendea nini Dodoma? Au na wenyewe ni wajinga? Muswada aliuandaa nani.
 
Tuwekeze kwenye kuimaliza ccm la sivyo tukifanya kosa tena tukairudisha madarakani itatumaliza sisi
 
Hapa shisa ni yetu wote maana ni sisi ndio tuliowapa dhamana hawa tunaowalaumu.

Tusifanye makosa yaleyale tena,huu ndio wakati wetu wa kufanya mabadiliko kwa kutoruhusu kurubuniwa kwa njia yoyote ile.
 
Watu wapo busy kutangaza nia za kugombea Urais na kutuchagulia wagombea hayo mambo mengine hayana umuhimi kwao........Tanzania ya Kikwete.
 
Back
Top Bottom