Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 46,909
- 32,329
Wanabodi..
Mgogoro mkubwa unakinyemelea Chadema wilayani Arumeru baadhi ya wananchama na wagombea waliochukuwa fomu za kuomba nafasi ya kupeperusha bendera ya chama hicho.
Wagombea pamoja na wanachama wa chama hicho wanapinga kitendo cha mgombea mwenzao, Joshua Nassari kuitisha harambee na kuchangisha fedha kwa ajili uchaguzi huo wakati chama bado hakijapitisha jina la mgombea.
Nassari, aliitisha harambee ya kuchangisha fedha Arusha alipata takribani Sh10 milioni katika harambee hiyo iliyohudhuriwa na Lema.
Wafuasi wa Chadema waliochukuwa fomu mbali na Nassari, ni Goodlove Temba, Yohane Kimuto, Rebbeca Mugwisha, Samwel Shami Sanjari na Anna Mgwilla.
Mchakato wa kuchukuwa fomu umefungwa juzi na jina la mgombea kujulikana Machi 3.
Wagombea wote kwa ujumla wamepinga kitendo hicho kuwa kimekiuka taratibu za chama.
Wagombea hao wamekwenda mbali zaidi na kusema hawapewi ushirikiano kama anaopewa mwenzao Nassari.
Mgogoro mkubwa unakinyemelea Chadema wilayani Arumeru baadhi ya wananchama na wagombea waliochukuwa fomu za kuomba nafasi ya kupeperusha bendera ya chama hicho.
Wagombea pamoja na wanachama wa chama hicho wanapinga kitendo cha mgombea mwenzao, Joshua Nassari kuitisha harambee na kuchangisha fedha kwa ajili uchaguzi huo wakati chama bado hakijapitisha jina la mgombea.
Nassari, aliitisha harambee ya kuchangisha fedha Arusha alipata takribani Sh10 milioni katika harambee hiyo iliyohudhuriwa na Lema.
Wafuasi wa Chadema waliochukuwa fomu mbali na Nassari, ni Goodlove Temba, Yohane Kimuto, Rebbeca Mugwisha, Samwel Shami Sanjari na Anna Mgwilla.
Mchakato wa kuchukuwa fomu umefungwa juzi na jina la mgombea kujulikana Machi 3.
Wagombea wote kwa ujumla wamepinga kitendo hicho kuwa kimekiuka taratibu za chama.
Wagombea hao wamekwenda mbali zaidi na kusema hawapewi ushirikiano kama anaopewa mwenzao Nassari.