Mgogoro Arusha - Tatizo ni Pinda

Kamende

JF-Expert Member
Mar 1, 2008
416
45
Wajameni nimelazimika kuingia jukwaani jioni hii na kuleta msimamo wangu kwa mujibu wa mambo yanavyoendelea siku kwa siku ili yatakapotokea makubwa zaidi ifahamike wazi nani kichocheo kikuu cha matatizo yote ya Arusha.

Mheshimiwa WM Pinda December mwaka jana aliiahidi CHADEMA kwamba ifikapo Januari 5 mwaka huu atakuwa amemaliza tatizo la utata wa kuchaguliwa meya wa jiji la Arusha. Akawaomba wasifanye maandamano yoyote wala kuchukua hatua yoyote kwani ana uhakika wa kutatua tatizo hilo.

Mhe. Pinda alinukuliwa akisema bungeni kuwa Mauaji ya Arusha yalisababishwa na CHADEMA na hivyo wao ndo wakubebeshwa lawama. Hata pale Mhe. Lema alipoleta ushahidi bingeni kuonyesha wazi kwamba WM aamelidanganya bunge bado si bunge wala serikali ilishadiriki kuweka ushahidi huo bayana.

mazungumzo ya kinachoitwa MUAFAKA WA ARUSHA yamefanyika kwa maelekezo ya Uongozi wa CHADEMA kwamba "kwa kweli kuna umuhimu wa kumaliza sintofahamu ya Arusha kwa kujadiliana na kuafikiana namna njema ya kufikia MUAFAKA WA HAKI KWA PANDE ZOTE. Katika madai ya muhimu ya CHADEMA kwenye meza ya majadiliano zilikuwepo hoja kuu zifuatazo:
  1. Kwamba uchaguzi wa Meya uliowapa CCM ushindi ulikuwa batili na kwa hiyo lazima kuwepo mgawano mpya wa haki wa madaraka.
  2. Kwamba serikali iwajibike kuwafidia marehemu waliofariki kutokana na vurugu zile za tr. 5/1/2011
  3. Kwamba majeruhi wanaoendelea na matibabu wapatiwe huduma stahiki
  4. Kwamba OCD wa Arusha (W) awajibishwe kwa aliyoyafanya binafsi.
  5. Kwamba kesi iliyoko Mahakamani dhidi ya Viongozi wa CHADEMA walioandamana tr. 5/1/2011 ifutwe.
Alipopelekewa draft ya kwanza tu ya kuanza kwa MAJADILIANO na akijua kuwa madiwani wana kikomo cha MAKUBALIANO Pinda aliwakwepa viongozi wa CHADEMA siku hadi siku kwa lengo la kuhakikisha kuwa MUAFAKA unafikiwa kwa makubaliano kwenye hoja ya kwanza peke yake. Wakati huo shughuli zote za uratibu wa MAJADILIANO zilikuwa zikifanyika chini ya Mhe. Raymondo Mushi - DC wa Arusha.

Ipo nguvu kubwa sana inashinikiza miuafaka huu ubaki ulivyo. lengo ni kumnusuru Pinda na tuhuma za kuongopea bunge na pia kuinusuru CCM na dhambi ya kusababisha umwagaji wa Damu kwa tamaa yao ya kutawala kwa nguvu.

Waungwana hebu angalieni ukweli ninyi wenyewe; iko sababu gani ya kuukubali MUAFAKA wa kugawana madaraka tu na kuachana na hoja zote hizo nyingine? Kwa nini serikali inataka kuamini kuwa inaweza kuwaendesha watu wote kama wajinga?
Kwa hakika kama Pinda anataka amani itamalaki Arusha, aondoe wingu linalofunika MUAFAKA huu feki kwa kuondoa kila visingizio vya kinafiki. Likitokea lolote sasa Arusha hakuna namna litakavyokosa kuunganishwa moja kwa moja na WM Mizengo Pinda.

Umefika wakati muafaka kwa WM kupasuka kichwa akitafuta namna ya kuzima mioto yote ya mgogoro wa Arusha kwani yeye ndiye aliyeuwasha, akauchochea, akauongezea magogo na sasa unafikia kiwango cha kutozimika kirahisi tena.

Wakuu naomba kuwasilisha!!!
 
mazungumzo ya kinachoitwa MUAFAKA WA ARUSHA yamefanyika kwa maelekezo ya Uongozi wa CHADEMA kwamba "kwa kweli kuna umuhimu wa kumaliza sintofahamu ya Arusha kwa kujadiliana na kuafikiana namna njema ya kufikia MUAFAKA WA HAKI KWA PANDE ZOTE. Katika madai ya muhimu ya CHADEMA kwenye meza ya majadiliano zilikuwepo hoja kuu zifuatazo:
  1. Kwamba uchaguzi wa Meya uliowapa CCM ushindi ulikuwa batili na kwa hiyo lazima kuwepo mgawano mpya wa haki wa madaraka.
This sounds stupid to me. Mgawano wa haki wa madaraka ndiyo kitu gani? Leo utawaambiaje hao madiwani kuwa walichofanya siyo kutekeleza hayo maagizo ya makao makuu? Ubebe lawama huo uongozi wa CDM uliotoa hayo maelekezo na siyo Pinda!
 
Hivi hayo majadiliano kuanzia namba moja mpaka namba tano ni viongozi gani walioandaa CDM taifa au CDM mkoa!

Naona Madiwani wameyafanyia kazi haya majadiliano namba moja ya kugawana madaraka wakati watu wauwawa na wengine wana vilema vya maisha
 
kipengele cha kwanza kinasema uchaguzi wa meya urudiwe , mtoa mada huenda amepitiwa au anamaslahi na kipengele hicho
 
Wajameni nimelazimika kuingia jukwaani jioni hii na kuleta msimamo wangu kwa mujibu wa mambo yanavyoendelea siku kwa siku ili yatakapotokea makubwa zaidi ifahamike wazi nani kichocheo kikuu cha matatizo yote ya Arusha.

Mheshimiwa WM Pinda December mwaka jana aliiahidi CHADEMA kwamba ifikapo Januari 5 mwaka huu atakuwa amemaliza tatizo la utata wa kuchaguliwa meya wa jiji la Arusha. Akawaomba wasifanye maandamano yoyote wala kuchukua hatua yoyote kwani ana uhakika wa kutatua tatizo hilo.

Mhe. Pinda alinukuliwa akisema bungeni kuwa Mauaji ya Arusha yalisababishwa na CHADEMA na hivyo wao ndo wakubebeshwa lawama. Hata pale Mhe. Lema alipoleta ushahidi bingeni kuonyesha wazi kwamba WM aamelidanganya bunge bado si bunge wala serikali ilishadiriki kuweka ushahidi huo bayana.

mazungumzo ya kinachoitwa MUAFAKA WA ARUSHA yamefanyika kwa maelekezo ya Uongozi wa CHADEMA kwamba "kwa kweli kuna umuhimu wa kumaliza sintofahamu ya Arusha kwa kujadiliana na kuafikiana namna njema ya kufikia MUAFAKA WA HAKI KWA PANDE ZOTE. Katika madai ya muhimu ya CHADEMA kwenye meza ya majadiliano zilikuwepo hoja kuu zifuatazo:
  1. Kwamba uchaguzi wa Meya uliowapa CCM ushindi ulikuwa batili na kwa hiyo lazima kuwepo mgawano mpya wa haki wa madaraka.
  2. Kwamba serikali iwajibike kuwafidia marehemu waliofariki kutokana na vurugu zile za tr. 5/1/2011
  3. Kwamba majeruhi wanaoendelea na matibabu wapatiwe huduma stahiki
  4. Kwamba OCD wa Arusha (W) awajibishwe kwa aliyoyafanya binafsi.
  5. Kwamba kesi iliyoko Mahakamani dhidi ya Viongozi wa CHADEMA walioandamana tr. 5/1/2011 ifutwe.
Alipopelekewa draft ya kwanza tu ya kuanza kwa MAJADILIANO na akijua kuwa madiwani wana kikomo cha MAKUBALIANO Pinda aliwakwepa viongozi wa CHADEMA siku hadi siku kwa lengo la kuhakikisha kuwa MUAFAKA unafikiwa kwa makubaliano kwenye hoja ya kwanza peke yake. Wakati huo shughuli zote za uratibu wa MAJADILIANO zilikuwa zikifanyika chini ya Mhe. Raymondo Mushi - DC wa Arusha.

Ipo nguvu kubwa sana inashinikiza miuafaka huu ubaki ulivyo. lengo ni kumnusuru Pinda na tuhuma za kuongopea bunge na pia kuinusuru CCM na dhambi ya kusababisha umwagaji wa Damu kwa tamaa yao ya kutawala kwa nguvu.

Waungwana hebu angalieni ukweli ninyi wenyewe; iko sababu gani ya kuukubali MUAFAKA wa kugawana madaraka tu na kuachana na hoja zote hizo nyingine? Kwa nini serikali inataka kuamini kuwa inaweza kuwaendesha watu wote kama wajinga?
Kwa hakika kama Pinda anataka amani itamalaki Arusha, aondoe wingu linalofunika MUAFAKA huu feki kwa kuondoa kila visingizio vya kinafiki. Likitokea lolote sasa Arusha hakuna namna litakavyokosa kuunganishwa moja kwa moja na WM Mizengo Pinda.

Umefika wakati muafaka kwa WM kupasuka kichwa akitafuta namna ya kuzima mioto yote ya mgogoro wa Arusha kwani yeye ndiye aliyeuwasha, akauchochea, akauongezea magogo na sasa unafikia kiwango cha kutozimika kirahisi tena.

Wakuu naomba kuwasilisha!!!

Mkuu Ninawasiwasi na aunthenticity ya hizo dondoo. Ni kweli ndizo zilizokuwa dondoo za CDM??? Kwani hiyo namba moja imekaa vibaya sana. Namba Moja nahisi ni kurudia uchaguzi wa Meya sio kugawana madaraka. Kama ndivyo ilikuwa kama unavyowakilisha ni upuuzi tu.
 
Hili mbona linaeleweka toka siku nyingi na hisi hata kamanda wetu Dr. W.Slaa alishalijua hilo ndiyo maana taratibu za chama zinafuatwa kuwawajibisha wale wote waliohusika na ujinga kama huu.
 
Back
Top Bottom