Mgogoro ardhi LUCHERERI jijini Mwanza, CCM coming elections, ukimya wa TIBAIJUKA, NA MEYA MABULA

bnf

JF-Expert Member
Oct 13, 2012
218
79
Kwa ufupi eneo la Luchereri mwanza lipo kama km 8 kutoka mwanza mjini, km 3 kutoka stendi ya mabasi nyegezi na almost linapakana na chuo kikuu cha SAUT

Luchereri linazungukwa na ziwa victoria upande wa kas na mashariki,ni eneo linalofaa kwa uwekezaji wa hotel, bichi na the likes..kwa walio dar hili ni eneo kigeografia kama mbezi beach kwa dar

hii pia ni sahemu ambapo mh. RAIS alipewa zawadi ya kipande cha ardhi kutoka kwa wakazi wa mwanza

Kisiasa hili eneo lipo katika kata ya MKOLANI NA DIWANI WAKE NI MH. MABULA.huyu pia ndie MEYA WA NYAMAGANA au JIJI LA MWANZA

hili ni eneo lililofanyiwa usaili, upimaji na uthaminishaji wa ardhi kwa kila mmiliki wa ardhi..shida kubwa na mgogorto mkubwa ni kwamba viongozi hawataki KUMILIKISHA HII ARDHI KWA WALEGWA KWA KUTOA HATI..
na tetesi zilizopo ni kwamba eneo hili wanataka kuliuza kinyamela kwa wawekezaji wajenge Apartments, hotels na mengineyo mengi na kutuacha wenye ardhi bila kitu

Sasa wameanza na sheria ndogondogo kwamba kama tukimilikishwa ni kwamba haturuhusiwi kuwa na viwanja vya 15x30m2 zaidi ya viwili na vikizidi itabidi kila kiwanja kinachozidi ununue kwa sh 6000/ kwa m2 moja..sisi huku tulikuwa tunamashama itakuwaje wachukue ardhi yetu inayozidi kirahisi hivyo. kwa maisha yetuu hatuwezi nunua ardhi m2 moja 6000/

sasa kisiasa sahauni kupata kula wawakilishi wetu kwenye uchaguzi serikali za mitaa na uchaguzi mkuu bila kumaliza huu mgogoro

SISI WANAKIJIJI LUCHERERI KATA MKOLANI JIJINI MWANZA
 
Mkuu, niko hapa jijini natamani plot maeneo hayo ila hiyo migogoro ndo ilikuwa inanivunja steem. Kamanda, kama inawezekana naomba unimegee kidogo aisee kabla hao manyang'ao hawajawavamia.
 
karibu luchereri kaka..withought takng s risk, uwezi fanya kitu hapa bongo because every bisness hapa lazima u risk kitu coz things are not straight
 
isotope...sasa kuna unafuu mbona unataka plot uku...nipe tetesi kamanda
 
Vipi Nyamhongolo pakoje kuna jamaa anataka niuzia nyumba na sijawahi fika huko zaidi ya kuishia mwanza mjini
 
kama ana hati ni pazuri, c unajua umiliki wa ardhi au nyumba ni hati.mkuu
 
Kwa kifupi mgogoro huuu ni wa kisiasa kwani Mkurugenzialiyekuwepo aliwafukuza wasukuma kw akigezo cha kumpa mkuu wa kaya eneo lakujenga, so wasukuma kwa uoga wao(ntuhu tabu gete gete…) wakakimbilia sengeremana Kwimba, sasa baadhi wamerudi baada ya mvua kulegalega, sasa wamekuwa vibaruawa kufagia ROYAL RESORT (Hotel ya aliyekuwa mkurugenzi wa jiji la Mwanza)
Haikutosha - Masha naujanja wake wote hatukumpa ng'o! Mkolanitulimheshimu Mabula(CCM) kumbe naye ni mwiba, mwizi, asiye na fadhila kwawapiga kura wake….asiye na huruma kwa wasukuma wenzake. E.g Kabwe amejimegea eneo si chini ya eka 5ziwani(0 distance from Lake) na kujijengea hoteli yake, wengine wameshanzaujenzi pia.

 
Viongozi wa jiji la mwanza ni washenz wakubwa wamekwamisha pia mpango wa kusambazia watu umeme eneo hilo kupitia mpango wa usambazaji umeme vijijin ili watu wakate tamaa ya kuhamia na kujenga huko, wameshindwa kujenga kipande kidogo cha barabara kwa kiwango cha lami chenye kilometa km 2 tokea barabara ya chuo cha SAUT iliyojengwa kwa nguvu ya magufuri baada kuombwa na uongoz wa chuo inapoishia,wanatishia watu wasiendeleze maeneo yao huku watendaji wao wakiendelea kujimilikisha maeneo! Tibaijuka ebu njoo Mwanza kuna madudu kwenye ardhi kuliko hata dar
 
wananchi wa nyamagana wameshamkumbuka masha uchaguzi ujao hata akiweka koti lake litashinda uchaguzi, pia wananchi wa ukerewe wameshamkumbuka getrude mongela yaani ukienda nansio kagunguli buguza hadi ukara makamasi yanawatoka kwa kumlilia mama mongela, wafuasi wa msekwa wanajilaumu kwa kumfitini mama wa watu, wanasema mwakani hatakama akiweka mtandio wake watauchagua. hawana hamu na cdm.
 
wananchi wa nyamagana wameshamkumbuka masha uchaguzi ujao hata akiweka koti lake litashinda uchaguzi, pia wananchi wa ukerewe wameshamkumbuka getrude mongela yaani ukienda nansio kagunguli buguza hadi ukara makamasi yanawatoka kwa kumlilia mama mongela, wafuasi wa msekwa wanajilaumu kwa kumfitini mama wa watu, wanasema mwakani hatakama akiweka mtandio wake watauchagua. hawana hamu na cdm.

Acha uzushi hiyo migogoro yote inayosemwa hapo ilianza kipindi cha huyo mbunge wako Masha na alikuwa haongelei lolote kuhusu hiyo migogoro kwahiyo hakuna anaemkumbuka bora hata ya Wenje alijitahid kufuatilia migogoro lkn akazidiwa nguvu na mkurugenz fisad
 
acha uongo masha ndiye aliyeandaa mastaplan ya luchelele ikabaki ugawaji wa viwanja, matatizo ya luchelele yameanza wakati wa wenje, wenye jukumu la kuidhinisha viwanja ni madiwani ambao ni wa cdm wamekalia kula rushwa tu.
 
acha uongo masha ndiye aliyeandaa mastaplan ya luchelele ikabaki ugawaji wa viwanja, matatizo ya luchelele yameanza wakati wa wenje, wenye jukumu la kuidhinisha viwanja ni madiwani ambao ni wa cdm wamekalia kula rushwa tu.

Kweli we ni mzee wa propaganda mgogoro wa luchelele ulianza 2007 wenje alitoka wapi hapo labda wabunge walikuwa wawili mkuu!
 
wananchi wa nyamagana wameshamkumbuka masha uchaguzi ujao hata akiweka koti lake litashinda uchaguzi, pia wananchi wa ukerewe wameshamkumbuka getrude mongela yaani ukienda nansio kagunguli buguza hadi ukara makamasi yanawatoka kwa kumlilia mama mongela, wafuasi wa msekwa wanajilaumu kwa kumfitini mama wa watu, wanasema mwakani hatakama akiweka mtandio wake watauchagua. hawana hamu na cdm.
Umetumwa na Masha kuja kupima upepo hapa? Kwa taarifa yako hapati kitu hapa!!
 
acha uongo masha ndiye aliyeandaa mastaplan ya luchelele ikabaki ugawaji wa viwanja, matatizo ya luchelele yameanza wakati wa wenje, wenye jukumu la kuidhinisha viwanja ni madiwani ambao ni wa cdm wamekalia kula rushwa tu.

Duuuh, hii kali, master plan inaandaliwa na mbunge. Labda kama ameandaa ya Malimbe "Kwa Masha"
 
Viongozi wa jiji la mwanza ni washenz wakubwa wamekwamisha pia mpango wa kusambazia watu umeme eneo hilo kupitia mpango wa usambazaji umeme vijijin ili watu wakate tamaa ya kuhamia na kujenga huko, wameshindwa kujenga kipande kidogo cha barabara kwa kiwango cha lami chenye kilometa km 2 tokea barabara ya chuo cha SAUT iliyojengwa kwa nguvu ya magufuri baada kuombwa na uongoz wa chuo inapoishia,wanatishia watu wasiendeleze maeneo yao huku watendaji wao wakiendelea kujimilikisha maeneo! Tibaijuka ebu njoo Mwanza kuna madudu kwenye ardhi kuliko hata dar

Tibaijuka aliishafika hapo mapema kabisa baada tu ya kuukwaa uwaziri akaishia kutamani plot na yeye. Aliaga kuwa akifika Dar atatoa majibu lakini ishapita miaka mitatu sasa kimya kabisa maana bosi wake ana plot kadhaa hapo Luchelele....
 
Back
Top Bottom