kanta
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 343
- 65
Mgodi wa Dhahabu wa Geita umejibu tuhuma mbalimbali zilizotolewa na CCM
Mnamo Tarehe 23 Novemba 2012, wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM), akiwemo Naibu Waziri wa Nishati na Madini Bw. Steven Masele walifanya mkutano wa hadhara Geita mjini, katika mkutano huo walilalamikia mgodi wa Geita kwamba unahusika na vifo vya wanajamii wanaofia Mgodini hapa,na pia walizidi kusema kwamba mgodi haulipi kodi ya kutosha na wakazidi kungumza kuwa GGM inasuasua katika kukamilisha mradi wa maji. Kutoakana na kauli hiyo Mkurugenzi wa mgodi huo amelazimika kutolea ufafanuzi madai hayo na kuyaita ya kizushi huku akisisitiza kwamba GGM inafuata misingi ya haki za binadamu ambayo ilikubali kutia sahihi.
Ifuatayo ni taarifa ya mkurugenzi huyo aliyotoa kwa umma na kusambazwa kwa wafanyakazi wote pamoja na wananchi wa Geita.
Kodi na Michango
Mkurugugenzi Mtendaji wa Mgodi Wa Geita (GGM), Bw. Gary Davies alisema kwamba GGM ni kati ya kampuni pekee inayochangia kodi ya mapato kubwa zaidi Tanzania. '‘Tunachangia kulipa kodi ya mapato(Corporate), mirahaba (royalties), utendaji, ada na kodi ya mishahara yetu, michango yetu kwa Serikali ya Tanzania kwa mwaka jana 2011,ilikuwa zaidi ya dola $100M, na huenda mwaka huu 2012 kodi hii ikaongezeka mara mbili na kuwa dola zaidi ya $200M. Mgodi huu unazingatia ulipaji wa kodi kwa mda mwafaka kama inavyotakiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)'', aliongeza.
Malipo ya michango hii ya kodi yanadhibitishwa kwa usahihi kupitia Mpango wa uhamasishaji uwazi katika mapato ya Madini, Gesi na Mafuta (Tanzania Extractive Industry Transparency Initiative (TEITI).
Vifo vinavyohusu wanajamii.
Kampuni ya uchimbaji ya Geita (GGM) inadhibitisha kutokea kwa vifo vya watu 23 wasio wafanyakazi wa mgodi (third party) kwa mwaka huu wa 2012, na kwamba vifo hivi vimesababishwa na wanajamii kujiweka katika hali ya hatari, wanapokuwa wanavamia na hata kuuibia mgodi, wanafanya vitendo hivi bila kuzingatia usalama wa maisha yao na hii hupelekea hata kutokuogopa muingiliano kati ya na Mashine zinazotumika katika uzalishaji (Haul trucks).
'‘Kampuni inahuzunishwa kwa vifo vinavyotokea ndani ya maeneo ya Mgodi, na pindi matukio hayo yanapotokea taratibu zote za kutoa taarifa kwa vyombo husika ikiwemo Polisi na ofisi za Madini hufuatwa'', alisema.
GGM inafanya kazi kwa mujibu wa Kanuni za Umoja wa Mataifa kwa kufuata Usalama na Haki za Binadamu (VPSHR) na inashirikiana kikamilifu na tume ya polisi na serikali katika kufanya uchunguzi panapo hitajika. GGM inadhamini maadili ya uwazi na ukweli kama misingi ya mahusiano ya kuaminiana na kuthaminiana na jamii inayozunguka mgodi.
Urasimishaji wa Wachimbaji wadogo wadogo (ASM).
Bw. Davies alisema kwamba GGM inaunga mkono juhudi za Serikali za kuongeza tija na kuboresha uchimbaji mdogo wa madini, hali itakayo ipatia serikali fursa ya kujiongezea kipato kwa njia ya mrahaba na pia kuboresha hali ya usalama na mazingira, hali hii pia itapunguza uhalifu na uvamizi unaojitokeza kwa sasa.
Aliongeza kwamba ni vyema kujikita katika kuangalia mazingira endelevu kwa kuboresha hali ya wachimbaji wadogo wadogo (ASM),na alisisitiza kwamba kwa wanasiasa kupendekeza kuwa Kampuni iwapatie wachimbaji wadogo wadogo makapi ya mawe( magwangala) halitakuwa suluhisho la mda mrefu kwani kuna changamoto za Usalama na afya na pia nikinyume kwa mujibu wa sheria za nchi.
Mgodi wa Geita una nia na mpango wa kushirikiana na kufanya utafiti na Migodi mingine, Serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia ili kuwawezesha wachimbaji wadogo wadogo nchini.
Kusaidia uramishaji wa wachimbaji wadogo wadogo unao endana na sera ya serikali kuhusu mkukuta ambao unasisitiza kusaidia sekta binafsi kwaajili ya maendeleo na faida kwa watanzania wanaotaka kushiriki katika uchimbaji halali wa madini.
Uwekezaji katika Jamii
BW. Davies vilevile amesema Mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM) inaendelea kwa haraka iwezekanavyo kumaliza sehemu yake ya ujenzi wa mradi wa maji wa Geita. Kazi hiyo inayohusisha ujenzi wa sehemu ya kuhifadhia na kusafishia maji ilianza mwezi wa sita 2012.
Mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM) itakamilisha sehemu yake ya mradi ifikapo mwezi wa pili 2013.Mradi huu unatarajiwa kuwapa maji safi na salama yakunywa zaidi ya wakazi 100,000 wa Geita mjini, na unajengwa kwa ufadhili wa Mgodi na ushiriakiano na serikali ya Tanzania.Mchango wa GGM katika mradi huu inakadiriwa kufikia Dola za kimarekani 4.5M' alisema.
Mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM) inaoanisha uwekezaji wake katika jamii na sera ya umoja wa mataifa (United Nation's Millennium development Goals), unaohusisha matumizi makubwa ya ubia na serikali na jumuia za kijamii za mwaka 2011, kampuni (GGM) imewekeza zaidi ya Dola za Marekani 4M katika miradi ya maendeleo ya jamii. Miradi hiyo inajumuisha shule ya Sekondari ya Wasichana ya Nyankunbu; Chuo cha ufundi cha madini Moshi (the Integrted mining Technical Training course at Veta Moshi); Hospitali ya wilaya ya Geita; upasuaji wa midomo ya sungura(cleft palate), Kituo cha Watoto yatima cha Moyo wa Huruma, na matembezi ya kila Mwaka ya Kupanda Mlima kilimanjaro ikiwa ni kampeni ya kupambana na vita dhidi ya Ukimwi (HIV/AIDS).
Mtazamo wangu:
CCM iache kutapatapa kutokana na ukweli kwamba mikataba yote mibovu ya madini imesimamiwa na Serikali yake, haya yanayotokea sasa ni sehemu tu ya utumbo wa mikataba hiyo mibovu, tangu hapo mwanzo walikuwa wapi mpaka sasa ndio wanajifanya wanashtuka, wasubiri tu kiama chao hapo 2015.
Mnamo Tarehe 23 Novemba 2012, wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM), akiwemo Naibu Waziri wa Nishati na Madini Bw. Steven Masele walifanya mkutano wa hadhara Geita mjini, katika mkutano huo walilalamikia mgodi wa Geita kwamba unahusika na vifo vya wanajamii wanaofia Mgodini hapa,na pia walizidi kusema kwamba mgodi haulipi kodi ya kutosha na wakazidi kungumza kuwa GGM inasuasua katika kukamilisha mradi wa maji. Kutoakana na kauli hiyo Mkurugenzi wa mgodi huo amelazimika kutolea ufafanuzi madai hayo na kuyaita ya kizushi huku akisisitiza kwamba GGM inafuata misingi ya haki za binadamu ambayo ilikubali kutia sahihi.
Ifuatayo ni taarifa ya mkurugenzi huyo aliyotoa kwa umma na kusambazwa kwa wafanyakazi wote pamoja na wananchi wa Geita.
Kodi na Michango
Mkurugugenzi Mtendaji wa Mgodi Wa Geita (GGM), Bw. Gary Davies alisema kwamba GGM ni kati ya kampuni pekee inayochangia kodi ya mapato kubwa zaidi Tanzania. '‘Tunachangia kulipa kodi ya mapato(Corporate), mirahaba (royalties), utendaji, ada na kodi ya mishahara yetu, michango yetu kwa Serikali ya Tanzania kwa mwaka jana 2011,ilikuwa zaidi ya dola $100M, na huenda mwaka huu 2012 kodi hii ikaongezeka mara mbili na kuwa dola zaidi ya $200M. Mgodi huu unazingatia ulipaji wa kodi kwa mda mwafaka kama inavyotakiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)'', aliongeza.
Malipo ya michango hii ya kodi yanadhibitishwa kwa usahihi kupitia Mpango wa uhamasishaji uwazi katika mapato ya Madini, Gesi na Mafuta (Tanzania Extractive Industry Transparency Initiative (TEITI).
Vifo vinavyohusu wanajamii.
Kampuni ya uchimbaji ya Geita (GGM) inadhibitisha kutokea kwa vifo vya watu 23 wasio wafanyakazi wa mgodi (third party) kwa mwaka huu wa 2012, na kwamba vifo hivi vimesababishwa na wanajamii kujiweka katika hali ya hatari, wanapokuwa wanavamia na hata kuuibia mgodi, wanafanya vitendo hivi bila kuzingatia usalama wa maisha yao na hii hupelekea hata kutokuogopa muingiliano kati ya na Mashine zinazotumika katika uzalishaji (Haul trucks).
'‘Kampuni inahuzunishwa kwa vifo vinavyotokea ndani ya maeneo ya Mgodi, na pindi matukio hayo yanapotokea taratibu zote za kutoa taarifa kwa vyombo husika ikiwemo Polisi na ofisi za Madini hufuatwa'', alisema.
GGM inafanya kazi kwa mujibu wa Kanuni za Umoja wa Mataifa kwa kufuata Usalama na Haki za Binadamu (VPSHR) na inashirikiana kikamilifu na tume ya polisi na serikali katika kufanya uchunguzi panapo hitajika. GGM inadhamini maadili ya uwazi na ukweli kama misingi ya mahusiano ya kuaminiana na kuthaminiana na jamii inayozunguka mgodi.
Urasimishaji wa Wachimbaji wadogo wadogo (ASM).
Bw. Davies alisema kwamba GGM inaunga mkono juhudi za Serikali za kuongeza tija na kuboresha uchimbaji mdogo wa madini, hali itakayo ipatia serikali fursa ya kujiongezea kipato kwa njia ya mrahaba na pia kuboresha hali ya usalama na mazingira, hali hii pia itapunguza uhalifu na uvamizi unaojitokeza kwa sasa.
Aliongeza kwamba ni vyema kujikita katika kuangalia mazingira endelevu kwa kuboresha hali ya wachimbaji wadogo wadogo (ASM),na alisisitiza kwamba kwa wanasiasa kupendekeza kuwa Kampuni iwapatie wachimbaji wadogo wadogo makapi ya mawe( magwangala) halitakuwa suluhisho la mda mrefu kwani kuna changamoto za Usalama na afya na pia nikinyume kwa mujibu wa sheria za nchi.
Mgodi wa Geita una nia na mpango wa kushirikiana na kufanya utafiti na Migodi mingine, Serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia ili kuwawezesha wachimbaji wadogo wadogo nchini.
Kusaidia uramishaji wa wachimbaji wadogo wadogo unao endana na sera ya serikali kuhusu mkukuta ambao unasisitiza kusaidia sekta binafsi kwaajili ya maendeleo na faida kwa watanzania wanaotaka kushiriki katika uchimbaji halali wa madini.
Uwekezaji katika Jamii
BW. Davies vilevile amesema Mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM) inaendelea kwa haraka iwezekanavyo kumaliza sehemu yake ya ujenzi wa mradi wa maji wa Geita. Kazi hiyo inayohusisha ujenzi wa sehemu ya kuhifadhia na kusafishia maji ilianza mwezi wa sita 2012.
Mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM) itakamilisha sehemu yake ya mradi ifikapo mwezi wa pili 2013.Mradi huu unatarajiwa kuwapa maji safi na salama yakunywa zaidi ya wakazi 100,000 wa Geita mjini, na unajengwa kwa ufadhili wa Mgodi na ushiriakiano na serikali ya Tanzania.Mchango wa GGM katika mradi huu inakadiriwa kufikia Dola za kimarekani 4.5M' alisema.
Mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM) inaoanisha uwekezaji wake katika jamii na sera ya umoja wa mataifa (United Nation's Millennium development Goals), unaohusisha matumizi makubwa ya ubia na serikali na jumuia za kijamii za mwaka 2011, kampuni (GGM) imewekeza zaidi ya Dola za Marekani 4M katika miradi ya maendeleo ya jamii. Miradi hiyo inajumuisha shule ya Sekondari ya Wasichana ya Nyankunbu; Chuo cha ufundi cha madini Moshi (the Integrted mining Technical Training course at Veta Moshi); Hospitali ya wilaya ya Geita; upasuaji wa midomo ya sungura(cleft palate), Kituo cha Watoto yatima cha Moyo wa Huruma, na matembezi ya kila Mwaka ya Kupanda Mlima kilimanjaro ikiwa ni kampeni ya kupambana na vita dhidi ya Ukimwi (HIV/AIDS).
Mtazamo wangu:
CCM iache kutapatapa kutokana na ukweli kwamba mikataba yote mibovu ya madini imesimamiwa na Serikali yake, haya yanayotokea sasa ni sehemu tu ya utumbo wa mikataba hiyo mibovu, tangu hapo mwanzo walikuwa wapi mpaka sasa ndio wanajifanya wanashtuka, wasubiri tu kiama chao hapo 2015.