Mgodi wa Bulyanhulu wafukuza wafanyakazi 700

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Posted Date::10/27/2007
Mgodi wa Bulyanhulu wafukuza wafanyakazi 700
*Watakiwa kuondoka mgodini kuanzia leo
*Wenye mafao kuyakuta katika akaunti zao

Na Julieth Kulangwa
Mwananchi

WAFANYAKAZI zaidi ya 700 wa mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu Wilayani Kahama wamefukuzwa kazi kuanzia leo kwa kushiriki katika mgomo.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani kutoka mgodini hapo, hadi jana idadi ya wafanyakazi zaidi ya 700 walikuwa tayari katika orodha ya kuachishwa kazi baada ya jopo la ukaguzi kuhusu nani alishiriki katika mgomo kufanya kazi yake.

"Hapa tuna wafanyakazi wengi, wanafikia zaidi ya 2,000 hivyo hatuoni umuhimu wa kukaa na watu wasiofuata taratibu na sheria," kilitueleza chanzo chetu cha habari na kuongeza;

"Tumejitahidi kukaa nao na kuwataka kufuata taratibu. Awali walionyesha kukubali lakini wakabadilika baadaye. Kutokana na wao kutotaka suluhu hatuoni umuhimu wa kuwa nao tena."

Chanzo chetu kilifafanua pia kuwa, wafanyakazi watakaopata barua za kuachishwa kazi watatakiwa kuondoka mgodini na wale wanaotakiwa kulipwa mafao kwa mujibu wa taratibu watapata mafao hayo katika akaunti zao za benki.

"Kilichobakia ni hicho, wataondoka na kama kuna mafao watayachukua benki na sio vinginevyo. Tumejitahidi sana ili tusifikie hapa lakini wafanyakazi wameonyesha kutothamini hata umuhimu wa kazi zao. Kilichobakia ni kuwa tutatangaza kazi hizo ili waombaji wapya wafanye hivyo," chanzo chetu kilifafanua.

Oktoba 17, 2007 wafanyakazi wa mgodi wa Bulyanhulu walianza mgomo majira ya asubuhi kwa lengo la kuushinikiza uongozi wa mgodi huo kutekeleza makubaliano baina ya uongozi na Chama cha Wafanyakazi wa Madini na Ujenzi (Tamico) tawi la Bulyanhulu.

Malalamiko hayo yalikuwa pamoja na utekelezwaji wa makubaliano ya kuondoa askari wa Kikosi cha Kuzuia Ghasia (FFU) ndani ya eneo la mgodi huo, kwa kuwa kwa kuwepo kwa kikosi hicho katika eneo hilo kunawafanya wao na familia zao kuishi kwa hofu.


Kwa mujibu wa maelezo yaliyotolewa na uongozi wa Barrick, mgomo huo ulianza baada ya Tamico kuueleza uongozi wa mgodi huo juu ya adhma ya kuanza rasmi kwa mgomo huo jana, baada ya kutoona utekelezaji wa makubaliano waliyofikia.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa uongozi ulilazimika kujibu barua hiyo na kuwashauri wafanyakazi hao kutogoma, kwa kuwa kufanya hivyo ni kwenda kinyume na sheria na utaratibu na kwa kufanya hivyo uongozi huo utalazimka kuchukua hatua kali kwa maslahi ya kampuni ya Barrick.

Hata hivyo taarifa hiyo ilieleza kuwa uongozi wa Barrick upo tayari kuendelea kutafuta ufumbuzi wa matatizo hayo kwa njia ya mazungumzo hadi kuhakikisha kuwa yanamalaizika.

Lakini hili haliwezi kufanyika iwapo wafanyakazi wanaendelea na mgomo, makubaliano yetu yalikuwa wazi kuwa tutaendelea kufanya mazungumzo hatua kwa hatua hadi tutakapoyapatia ufumbuzi kwa pande zote, ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Hata taarifa hiyo ya Barick ilieleza kuwa uongozi umekuwa ukiendelea kuwaomba wafanyakazi wote kuendelea na kazi kwa mujibu wa utaratibu na kuahidi kuendelea kujali mikataba baina yake na wafanyakazi wote waliogoma.

Mgodi huo wa Bulyanhulu unaomilikiwa na kampuni ya Barrick Gold Tanzania limited ni mgodi mkubwa kuliko yote nchini, una wafanyakazi takribani 1971 wakiwemo raia wa kigeni 178.

Kati ya hao wafanyakazi 90 wako kwenye menejimenti waliobaki wapo kwenye ufundi uendeshaji na utawala.
 
Tusubiri sasa watawaajiri wageni kutoka nje kwa pesa nyingi zaidi ya WTZ huo ndio mwendo. WTZ hawatakiwi kulipwa kitu chochote waendelee kuwafanyia kazi mafisadi bure.
 
Tusubiri sasa watawaajiri wageni kutoka nje kwa pesa nyingi zaidi ya WTZ huo ndio mwendo. WTZ hawatakiwi kulipwa kitu chochote waendelee kuwafanyia kazi mafisadi bure.

..tulizoea migomo ya vibarua darsilamu,sasa hata migodini imeanza!

..kimbunga kikitaka kuanza,utaona upepo halafu vumbi linaanza tartiibu!
 
Mimi hakuna jambo lililonishtua kama uwepo wa FFU mgodini. Umuhimu wa ulinzi unaeleweka...Lakini ndiyo wawekee Fanya Fujo Uone?
 
Mimi hakuna jambo lililonishtua kama uwepo wa FFU mgodini. Umuhimu wa ulinzi unaeleweka...Lakini ndiyo wawekee Fanya Fujo Uone?

Hao ni bei chee ukilinganisha na kuajiri private contractors kama "Blackwater"
 
Kwa nini usiwe ulinzi wa kawaida kama polisi wa kawaida au ultimate security, and the like?

..kwa ufahamu wangu mdogo,ffu hulinda pale polisi watakapoweza kuleta maruweruwe[wanapoweza shindwa!]

..na mara nyingi ni sehemu nyeti tena za umma,sasa,inawezekana buly ishanunuliwa na govt!huwezi jua!
 
I don't like where this is going, especially with FFU ndani ya mgodi. Hawa FFU na security organs zote za bongo siku hizi zinatumika kuwakandamiza wananchi na kuwalinda hawa wazungu. We've gone back to the colonial days ambapo vyombo vya dola vilikua vinatumika kuwalinda watawala (then the British colonialists and now CCM) pamoja na biashara zao(Barrick and everyone like them)
 
Watanzania hawana haki ndani ya nchi yao kudai ujira mzuri toka kwa mwajiri wao. Kufanya hivyo ni kuwapa waajiri haki ya kuwafukuza kazi.
 
Wakati umefika wafanyakazi wa migodi yote nchini waweke nyenzo zao zote chini na kuungana na wenzao wa Bulyanhulu.. wakati umefika kuonesha utawala wa mabavu haukubaliki. Natoa wito kwa wafanyakazi wengine wa sekta mbalimbali "unganeni na onesheni mshikamano"..
 
...and i hate to say this, but class struggles are becoming more apparent now in Tanzania and it won't take long for some smart guys in "UNIFORM" to take matters in their own hands. I think the time is coming fast and our unique national history will be comprised to get us in the same 'league' of nations as Nigeria, Ghana etc. We need to pray hard.
 
Hii ni mikwara tu wanajifanya kufukuza watu wakati kazi hawajui-wanaforum hamuwezi kuamini hao wanaoitwa expats is just bcoz of rangi za ngozi zao subirini updates. Hii imetolewa 28/10/07 - 08:30 (GMT + 3)

Hi ALL

Everything is quite at this time, however TAMICO will be holding a meeting at 1600hrs (4.00pm) this afternoon, I will keep you informed. As I suggested yesterday our best defence is to communicate to all the staff regarding re-employment and the fact that if anyone engages in violence, abuse etc they will not only have no job but will also be arrested for breaking the law, they need to consider their own future as well as their families.

Currently we have a total 68 Police / FFU officers in this location (on site or patrolling around the various villages).

Have a restful day.

Regards

Albie Hunia
Security Manager
Bulyanhulu Gold Mine Limited
TANZANIA
Tel: +255 22260 0508 Ext. 2631
Mob: +255 767206205
 
Watu 200 kule UK walisababisha Tanzania kuuziwa Rada ambayo inaipa hasara na maisha magumu watanzania 36m leo hii . CCM hawashangai hata mara moja kwa watu 700 kufukuzwa na wazungu ili wakaishi kwa shida na kukosa kusomesha na kujiletea maendeleo ila wata side na barrick kudai kwamba taratibu hazikufuatwa . Je Barrick can they do this to their fellow Canadians ?
 
Nyambala said:
Hii ni mikwara tu wanajifanya kufukuza watu wakati kazi hawajui-wanaforum hamuwezi kuamini hao wanaoitwa expats is just bcoz of rangi za ngozi zao subirini updates. Hii imetolewa 28/10/07 - 08:30 (GMT + 3)

Basi ni bora kusiwe na madini kabisa Tanzania kazi ndio imeanza hawa maexpert uchwara tunawafahamu sana hawana wajualo lakini ndio wanaokomba mamillioni bila kulipa kodi kwa kuwapa peremende viongozi wa ngazi za juu wa serikali.

Sasa hao FFU nani anawalipa? Je FFU wanaweza kukodishwa na kampuni binafsi? Je kwa nini FFU wamewekwa tayari tayari kwenye mgodi wakati hakuna fujo? Nani ameidhinisha FFU waende kwenye eneo la mgodi?

Tupo pamoja na wafanyakazi kwenye eneo la mgodi na mkwara mbuzi hauwezi kuwababaisha Watanzania.
 
Kama nilivyosema mwanzo pamoja na hii memo lakini naomba mtulie mtapata updates kila wakati. Mpaka sasa tayari kuna taarifa kwamba serikali imeintarvene na mkuu wa mkoa atakuwepo huko saa 7
mchana. Anyways all in all managemend ndio loosers. Na uhakika kitakachotokea ni kwamba watu watalipwa mafao, watachukua nssf na watarudi kazini. Halafu sasa kutakuwa na ule mgomo maarufu ujulikanao kama "Go slow" ambao ni hatari kuliko hata ule real!

Let us wait and see!
 

Attachments

  • Memorandum - Employees Termination.pdf
    60.6 KB · Views: 62
Kama nilivyosema mwanzo pamoja na hii memo lakini naomba mtulie mtapata updates kila wakati. Mpaka sasa tayari kuna taarifa kwamba serikali imeintarvene na mkuu wa mkoa atakuwepo huko saa 7
mchana. Anyways all in all managemend ndio loosers. Na uhakika kitakachotokea ni kwamba watu watalipwa mafao, watachukua nssf na watarudi kazini. Halafu sasa kutakuwa na ule mgomo maarufu ujulikanao kama "Go slow" ambao ni hatari kuliko hata ule real!

Let us wait and see!

Hapa kwetu bado Sana.
 
Katika huo mgomo Kuna jamaa yangu alikuwepo na ni miongoni mwa waliongoza mgomo huo.

Anasema hao jamaa ni wanyanyasaji sana hajapata kuona alisema na litakalotokea na litokee tu ila lazima mazingira ya kazi yabadilike na Maslahi ya wafanyakazi yaboreshwe na si vinginevyo kwasababu kama ni wizi wa dhahabu hawa jamaa wanafanya wizi mkubwa sana ambayo taarifa haziko Serikalini.
 
Back
Top Bottom