Mghwira aagiza Mkurugenzi Mwanga asilipwe mshahara kwa kushindwa kujibu swali

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,000
9,862
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira ameagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga Zefrin Lubuva asilipwe mshahara wa Februari hadi atakapojirekebisha.

Hatua hiyo imekuja baada ya Mghwira kukasirishwa na kitendo cha mkurugenzi huyo kushindwa kujibu maswali aliyomuuliza kwanini halmashauri hiyo imeshindwa kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya wanawake, vijana na walemavu.

Sakata hilo limetokea leo Ijumaa Februari 14, katika kikao maalumu cha kamati ya ushauri ya mkoa cha makisio ya mpango wa bajeti ya mwaka wa fedha 2020/2021, kilichofanyika leo.

“Mkurugenzi wa Mwanga kila wakati umekuwa ukishindwa kujibu maswali vile inavyopaswa sijajua ni nani anakulipa mshahara, ila mamlaka inayohusika kukulipa isikulipe mshara wa mwezi huu,” amesema.

Chanzo: Mtanzania
 
Huyu Zefrin ambaye ni mtoto wa Jaji Lubuva aliyempa Jiwe ushindi hawawezi kumfanya kitu pamoja na kulalamikiwa sana , hiyo nafasi kapewa kama fadhila kwa kazi kubwa aliyofanya baba yake kwenye matokeo ya uchaguzi 2015 uliompa Jiwe ushindi
 
Back
Top Bottom