Mgao wa umeme: WaTanzania tuamke, tuukatae

Tumekuwa wazuri sana kulalamika na kutoa yetu kwenye mitandao. Baada ya hapo kila mmoja anaenda kwenye net yake na kero zake! Hivi kulalamika hapa pekee inatosha?
 
Watanzania tumenyanyasika sana, tumeonewa sana, tumedhulumiwa sana, tumeumizwa sana na hii serikali yetu kwa hii migao ya umeme isiyokwaisha na inayokuja na visingizio lukuki. Imefika wakati sasa tuamke na kudai haki yetu ya kupata umeme masaa 24 kama wanavyopata wao. Kwani wao wana haki ya nchi hii kuliko sisi? Nani atutetee watanzania katika huu mgao mkali.
Njo na bango lako ubungo mataa tukuunge mkono!!! Kama mkweli
 
daah kama sasa haya tu gizani yaani ni mateso juu ya taabu,kuumiza macho tu hpa
 
Mkuu inategemea wewe unatoka Tanzania ipi. Cahnzo cha mgao au tatizo la umeme kinajulikana, lakini still bado watu wamelala. Tunatatzi la kulalamika tu lakini hatufanyi lolote.

Nakumbuka General Ibrahim Badamasi Babangida aliwahi kusema akiwa ziarani hapa Tanzania kuwa "it is easy to rule Tanzania than to ride a herd of cattle", wakati ule tuliona kejeli, lakini ni ukweli sasa tunauona. Ujinga huu ungetokea Lagos au Abuja sidhani kama "TANESCO" wa kule wangechekewa kama hapa.

Huko Senegal tu mbilinge imeonekana sisi mmh ,hata jirani zetu Kenya wametushinda,kwa hasira nilizonazo juu ya huu mgao wa umeme nachelea nisije katukanna watu hapa nikapigwa ban,inaamana toka richmond ilipoanza hawa wakubwa na tanesco hawakuwa hata na plan B,ghalafu bado wanapata mishahara mikubwa pa diem za kufa mtu na safari za kujifunza kibao,NYUSO ZAO HAZINA HAYA WALA AIBU NI KAMA VILE WANEVAA MASK NA MASIKIONI WAMEWEKA NTA
 
Seriously something has to be done, hakuna wa kututetea sisi wananchi wa kawaida zaidi yetu wenyewe. Huu mgao una siri kubwa ndani yake becoz kusema kuwa kina cha maji hakitoshi mimi sikubaliani nao, mvua zimetoka kunyesha muda mfupi sn ulopita iweje kina kiwe kimeshuka?? Halafu kingine kibaya zaidi ni vile ambavyo wanakata wanavyotaka wao tu, wameshatuona watanzania wajinga ni watu wa 'hewala' tu ndo maana wanatuchezea km kichwa cha mwendawazimu!! Umeme is no longer a service, it is purely business, sasa kwanini wasituheshimu sisi wateja wao tena ambao wengi wetu tumeshawalipa in advance..... Ukiwa na LUKU manake ni kuwa unawalipa in advance then matokeo yake hawakupi huduma uliyoshailipia in advance, huo si ni wizi???
 
naomba kama kuna mwenye taarifa za kuwepo kwa huu mgao pia pande za zanzibar anijulishe-isijekuwa sisi huku ndo tunataabika kwa mgao ukaja kuta wao hawana mgao
 
Hatma ya matatizo lukuki yanayotukumba Wananchi wa Tz tunajitakia wenyewe na waliopo madarakani wanajua udhaifu wetu kwamba hatuwezi kuchukua hatuas yeyote hata wakisema mgao utadumu kwa miaka 20.
 
Duh na kweli inabidi tutoke kwenye usingizi tuliolala miaka mingi. Maana haiwezekani Waziri aseme mgao utaisha karibuni na Injinia wa TANESCO aseme utaenda mpaka Febr. Sababu hasa ya mgao ni nini maana nionavyo mimi ni uzembe tu wa viongozi wetu kwamba kwanini wasubiri mpaka mafuta mazito yaishe ndo waanze kutafuta pesa ya kununua mengine? Kwanini kampuni kampuni zilizoingia mikataba kuzalisha umeme zisizalishe umeme katika kiwango kilichotakiwa au mikataba yao kufutwa na kuwadai fidia ambayo itasaidia kulipia gharama zingine za upatikanaji umeme.
 
Nimeona jana sikumbuke kama ni Guinea wameandamana Guinea
baada ya kukosa mgao kwa masaa 48 ,,na vurugu kutokea ..
Lakini hapa kwetu hata tukikatiwa umeme mwaka tutaishia kulalamika tu
 
basi hawa viongozi wa upposition wako wapi waongoze mapinduzi? vijana tuamke, lets take to the streets.
 
Muda wa kupata umeme na muda wakuwa gizani ukweli ni kwamba muda wa kuwa gizani ni mkubwa kuliko wa kuwa na umeme kwa kweli hali ni ngumu sana tunavumilia ila ukweli safari hii tunashindwa hii ndio kusherehekea mika hamsini ya uhuru fedha za maandalizi bora ziende kwenye vitu vingine tusiadhimishe hali ni mbaya sana
 
Muda wa kupata umeme na muda wakuwa gizani ukweli ni kwamba muda wa kuwa gizani ni mkubwa kuliko wa kuwa na umeme kwa kweli hali ni ngumu sana tunavumilia ila ukweli safari hii tunashindwa hii ndio kusherehekea mika hamsini ya uhuru fedha za maandalizi bora ziende kwenye vitu vingine tusiadhimishe hali ni mbaya sana

Kabisa hakuna haja ya kusherehekea giza.
Fedha hizo ziende kwa umeme tusherehekee kimya kimya na huku tukiwa tumelimaliza hili la giza totolo
 
hongera sana kaka kwa kuibua suala la msingi,imefika wakati jamii kuingia barabarani kwa masuala yanayotuathiri wote, wanachuo,walimu,wafanyabiashara,wakulima na walipa kodi wote kuandamana kutokomeza tatizo hili.kama senegal!!! pamoja tunaweza
 
Jamani wanasiasa mbona mnatupa adhabu,vyakula vinaharibika uchumi utazidi kuporomoka eti sababu mgao wa umeme.Kuna Ma-geologist wa kutosha hapa nchini na wamegundua madini nyie wanasiasa mkaingia mikataba mibovu,leo wamegundua uranium huenda tena mkatupoteza,Huu sio mgao ni adhabu 12hrs.kweli maisha bora kwa kila mtanzania.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom