Mgao wa umeme wa kufa mtu watangazwa, Juni 2011 na kuendelea

Fedha za mafuta mazito ni kiasi gani kwa siku IPTL?
Kuna mwekezaji, anayo tender!
Fikiria!
Huna haki ya kuchukua hatua.
Kimya.
 
haya ndo matunda ya uongozi mbovu siku zote tegemea mfuatano wa matatizo kama haya, ccm imefikia kifo cchake hivyo kila mti kwake unateleza awezi tena kwenda juu ngoja simba afike amtafune kiulaini kabisa! waswahili walishasema sikio la kufa halisikii dawa:A S cry::A S cry::A S cry:
 
Ni kweli ndugu zangu mgao utakuwa kwa sababu ya ukaguzi wa mitambo ya songosongo. Mbaya zaidi ni mitambo ikutwe haifai tena kuwa operational. Tutalizoea giza aisee!
 
Nadhani inatakiwa isomeke Mgawo wa umeme kuendelea......na siyo kuanza....
 
Mwanzoni nlizani tatizo la viongozi ni ufisadi peke yake, sasa nimebaini kwmba tatizo huenda pia haw jamaa ni ma-sadists who enjoy to inflict pain to the masses. Kha!
 
Mgao umeanza upya, gesi imeadimika kutoka Songosongo

Mkuu,

Acha kuposha. Otherwise tutakuwa tunawapa nafasi hao wanaoponda kuwa JF tunaweka habari za uongo. The fact ni kuwa kutawepo na upungufu mkubwa wa umeme katika Gridi ya Taifa kuanzia Mei 19 hadi 26 ili kutoa nafasi ya matengenezo makubwa katika visima vya gesi Songo Songo. Haina maana kuwa gesi imeadimika. Taafifa iliyotolewa na Tanesco ni kwamba mgao unatokana na kusimamishwa kwa uzalishaji wa gesi asili iliyopo katika Kisiwa cha Songo Songo mkoani Lindi na wamiliki wa visima hivyo Pan African Energy Tanzania Limited, wakiwa na lengo la kuvifanyia ukaguzi na ukarabati ili kuboresha uzalishaji wa gesi kwa ajili ya kufulia umeme.

Lengo la kuzimwa visima na mitambo hiyo ya gesi ni kuboresha viwango vya gesi inayozalishwa na kusafirishwa kutoka kisiwa cha Songo Songo hadi Dar es Salaam kwa kufua umeme na kutumiwa viwandani. Kati ya Mei 19 hadi 23, utakuwepo upungufu wa megawati 200 zinazofuliwa kwa kutumia gesi kutokana na visima vya Songo Songo kuzimwa kimoja baada ya kingine kwa ukaguzi wa kiufundi.

Kutokana na kuzimwa kwa visima hivyo vituo vya Songas, Ubungo Gas Plant na Tegeta Gas Plant vinavyotumia gesi asilia kufua umeme vitasitisha shughuli zake kwa siku hizo nne na hivyo kusababisha upungufu wa umeme katika Gridi ya Taifa kwa sababu umeme wa gesi huchangia karibu nusu ya umeme unaofuliwa katika vituo vyote nchini.

kuanzia Mei 23 hadi 26, mchana mgao wa umeme utakuwa megawati 300 kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 5 usiku na megawati 50 kuanzia saa 5 usiku hadi saa 2 asubuhi, hivyo kuwaomba wenye viwanda vikubwa kutumia kipindi hicho cha mgao kufanya usafi na matengenezo ya mitambo yao, hususan viwanda visivyokuwa na jenereta za dharura.

HabariLeo | Tanesco yatangaza mgao nchi nzima
 
Serikali haiwezi kucontrol inflation rate, harafu Tax Collection ndo hivyo tena, Idara nyingi za serikali zimejaa walafi huwezi kupata huduma hadi ute cha juu, utegemee kutakuwa na jambo la kufikiria maendeleo hapo? Never nasema never kwani matokeo ya mambo tajwa hapo juu ni kuona watu bar asubuhi asubuhi ikimaanisha watu hawaendi kazini hata wakienda wanababaisha tu na kuishia kutongozana, ulevi au kufanya mission town (corruption games, frauds etc).
Fikiria kwa ufupi sana wala usiende mbali, Hivi Tanzania tuna nini cha kujivunia kama watanzaniaa tulichofanya sisi? Kwa hiyo viongozi wetu bado wanaroho za umimi, kubebana, kutaka aonekane mtu safi kwa watu wakati anaua watu wengine kwamaksudi/bila yeye kujijua.
 
Wapi watoto wa magamba mnaolipwa kwa kuandika pumba za kutetea magamba makubwa?Teteeni na hilo la mgao usiokwisha.Waliweka PAUSE ss hivi wamebonyeza PLAY mziki unaendelea vile vile,kinachotakiwa Kudance tu.
 
Hivi ule mchakato wa JK wa kununua mitambo ya IPTL uliishia wapi? Je wakati huo wa mgao mkuu IPTL watakuwa wanazalisha umeme?
 
hii serikali yetu bana,walisema kina cha maji kimepungua.sasa ivi mvua zinanyesha wanasema gesi ni hadimu.nachojiuliza wakati wanaanza uwo mradi wa gesi,awakufanya tafiti kujua ni kiasi gani cha gesi kinachopatikana?
 
Mkuu,

Acha kuposha. Otherwise tutakuwa tunawapa nafasi hao wanaoponda kuwa JF tunaweka habari za uongo. The fact ni kuwa kutawepo na upungufu mkubwa wa umeme katika Gridi ya Taifa kuanzia Mei 19 hadi 26 ili kutoa nafasi ya matengenezo makubwa katika visima vya gesi Songo Songo. Haina maana kuwa gesi imeadimika. Taafifa iliyotolewa na Tanesco ni kwamba mgao unatokana na kusimamishwa kwa uzalishaji wa gesi asili iliyopo katika Kisiwa cha Songo Songo mkoani Lindi na wamiliki wa visima hivyo Pan African Energy Tanzania Limited, wakiwa na lengo la kuvifanyia ukaguzi na ukarabati ili kuboresha uzalishaji wa gesi kwa ajili ya kufulia umeme.

Lengo la kuzimwa visima na mitambo hiyo ya gesi ni kuboresha viwango vya gesi inayozalishwa na kusafirishwa kutoka kisiwa cha Songo Songo hadi Dar es Salaam kwa kufua umeme na kutumiwa viwandani. Kati ya Mei 19 hadi 23, utakuwepo upungufu wa megawati 200 zinazofuliwa kwa kutumia gesi kutokana na visima vya Songo Songo kuzimwa kimoja baada ya kingine kwa ukaguzi wa kiufundi.

Kutokana na kuzimwa kwa visima hivyo vituo vya Songas, Ubungo Gas Plant na Tegeta Gas Plant vinavyotumia gesi asilia kufua umeme vitasitisha shughuli zake kwa siku hizo nne na hivyo kusababisha upungufu wa umeme katika Gridi ya Taifa kwa sababu umeme wa gesi huchangia karibu nusu ya umeme unaofuliwa katika vituo vyote nchini.

kuanzia Mei 23 hadi 26, mchana mgao wa umeme utakuwa megawati 300 kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 5 usiku na megawati 50 kuanzia saa 5 usiku hadi saa 2 asubuhi, hivyo kuwaomba wenye viwanda vikubwa kutumia kipindi hicho cha mgao kufanya usafi na matengenezo ya mitambo yao, hususan viwanda visivyokuwa na jenereta za dharura.

HabariLeo | Tanesco yatangaza mgao nchi nzima

Mkuu,
Uko sawa, ila kuna tatizo ambalo sina hakika linafanywa na media au wale wanaotoa habari kwani ninavyojua Panafrican energy haimiliki kitu chochote Kule Songosongo wao ni waendeshaji tu.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
kuuma maneno haisaidii, ukweli ni kwamba Tanzania yetu, MVUA ISIPONYESHA, SABABU YA KUSINGIZIA NI KINA CHA MAJI KIMEPUNGUA, MVUA IKINYESHA, LAZIMA WASEME GESI HAMNA AU MITAMBO INAHITILAFU, ili mradi tu kila wakati kuwe na mgao.
 
Wakuu zangu, msifikiri kwamba sisi Watanzania bado mazuzu kiasi kwamba habari hii ikawa na sababu za msingi wakati ni vichekesho vitupu. Songosongo kusema kweli hawawezi kufunga mitambo yao kwa ajili ya ukarabati wakati hawana stock ya kutosha kwa kipindi ambacho wanataka kufanya ukarabati huo.

Napowasoma hapa janvini inaonyesha kaa vile Songo wanapovuna gas basi huenda moja kwa moja kutumika wakati sivyo. Kama kweli kulikuwa na mpango wa kufanya ukarabati hawa songo walitakiwa kuzalisha gas ya kutosha na kuwa na stock ya kutosha ili kukidhi hizo siku wanazotaka kufunga, hivyo kutoathiri ugawaji wa gas au laa nachoweza kufikiria hapa ni kwamba Songos kama wakulima wa kwetu hawana maghala ya kutosha kuhifadhia gas ama ni shirika dogo ambalo uzalishaji wake ni mdogo sana kuliko mahitaji hivyo wanauza kila wanachovuna kila siku..
 
Wakuu zangu, msifikiri kwamba sisi Watanzania bado mazuzu kiasi kwamba habari hii ikawa na sababu za msingi wakati ni vichekesho vitupu. Songosongo kusema kweli hawawezi kufunga mitambo yao kwa ajili ya ukarabati wakati hawana stock ya kutosha kwa kipindi ambacho wanataka kufanya ukarabati huo.

Napowasoma hapa janvini inaonyesha kaa vile Songo wanapovuna gas basi huenda moja kwa moja kutumika wakati sivyo. Kama kweli kulikuwa na mpango wa kufanya ukarabati hawa songo walitakiwa kuzalisha gas ya kutosha na kuwa na stock ya kutosha ili kukidhi hizo siku wanazotaka kufunga, hivyo kutoathiri ugawaji wa gas au laa nachoweza kufikiria hapa ni kwamba Songos kama wakulima wa kwetu hawana maghala ya kutosha kuhifadhia gas ama ni shirika dogo ambalo uzalishaji wake ni mdogo sana kuliko mahitaji hivyo wanauza kila wanachovuna kila siku..

Mkuu,
Mfumo wao wa uzalishaji hauna storage tanks,inazalishwa na kutumika.Ni tofauti na gesi tunazotumia kupikia.
 
Mimi ni CCM damu damu ila sasa tunapoenda inasikitisha, is it possible less thn 15 % ya watz ndo wanatumia umeme alafu serikali inashindwa kuwahudumia effectively bila mgao?

Jamani i think kuna umuhimu kwa hii sekta kuruhusiwa private companies kusupply umeme i thnk hapo TANESCO watajirekebisha kama ttcl
 
Kikwete chukua maamuzi mzito hapa, kuna watu wanakuhujumu kwa interest zao za ubinafsi na wanadhani kufanya hivyo ni kufanikisha malengo yao ya kisiasa!
Siamini kama kweli kwamba taarifa ya kuadimika kwa gesi iwe ya ghafla hivyo, ikiwa vipimo vinaonyesha kiwango gani cha gesi ipo songosongo tangu kabla ya uwekezaji! Pia hao wawekezaji wanafaham ni kw vipi nchi inategemea umeme huo kwa kiwango gan:

kikwete bora uanze upya, achana na hawa kina mhando, wanatumiwa vibaya na Wasiokuwa wazalendo na huhura kwa sisi masikini.
 
Kwa wale wanaojua how the freemasons operate, hakuna jipya hapa.This is a deliberately created crisis.And mind you this will not be the last. They create one crisis after another ili tushindwe kupanga mambo yetu,tukose matumaini na to loose confidence in ourselves and evenly tuwe easy to manipulate and rule.


Significant occurrences in politics and
finance are speculated to be orchestrated by an unduly influential cabal operating
through many front organizations. Numerous
historical and current events are seen as steps in an on-going plot to achieve world domination
through secret political gatherings and decision-making
processes



Mkuu,
Sina uhakika na hilo la freemason lakini nimekuwa nikifuatilia kwa karibu kuhusu hiki kikundi. Je ni kweli matatizo ambayo yanasumbua nchi kama rushwa, ufisadi uliokithiri unasababishwa na freemason?
Wao kwa madai yao ndio watawala wa dunia ndio wanaotusababishia yote haya?
 
Guys please, upungufu huu wa umeme ni kutokana na habari MTM aliyoibandika hapo, tatizo la 15% kutokuwa na umeme ni kwaajili ya more than 70% wapo vijijini na hivyo kupelekewa umeme kunatokana na Rural Electrification Agency, maana sasa hivi TANESCO haina ruzuku kutoka serikali so it won't be economically viable to electrify villages for billions whilst returns are zero if they are expected kujiendesha kibiashara

Mvua zinazoendelea kunyesha zinanyesha na kujaza kidatu na kihansi na hale tu ambayo combine ni kama megawat 400 na kitu, Mtera ina only 80 ila ni muhimu kuipond maana ina reservoir

Kuanza mgao kwaajili ya Songosongo rebasin project ni ili kupanua na kuongeza uzalishaji wa gesi nchini, kutegemea umeme wa maji kwa nchi za Africa ambapo ni mpaka hali ya hewa iwe nzuri si busara

Kuna aliyeongelea zabuni nadhani unaelewa sheria ya manunuzi ya umma tangu kutangaza zabuni mpaka kuaward kwa mshindi...
 
  • Thanks
Reactions: EMT
DRC-inga hep kuna upanuzi mkubwa sana wa kuzalisha umeme hadi kufikia 10 000MW ,ETHIOPIA pia, UGANDA pia.sisi tunawaza mitambo ya diesel ya 50MW.Kwa nini hatuitumii rusumo river,au rufiji basin kupata umeme walau ifikie 50%?ya watz wapate umeme?
 
Back
Top Bottom