Kingcobra
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 1,000
- 309
Watanzania tungekuwa wazalendo wa kweli tunaoitakia mema nchi yetu, tusingeiruhusu ccm kwa mara nyingine tena iendelee kushika usukani wa uongozi wa nchi hii. Wakati wa uchaguzi wa mwaka jana tungetulia hata kwa nusu saa tu na kutafakari kwa kina namna ccm ilivyoshindwa kututatulia shida zetu ndani ya miaka 33 ya uongozi wake, sidhani kama ccm ingerejea madarakani. Sasa tunaona jinsi tunavyohangaika na mgao wa umeme katikati ya rasilimali nyingi za kuzalishia umeme ambazo kwa nchi zingine ni vigumu hata kuziwazia! Kwangu mimi, mgao wa umeme unaoendelea ni kipimo tosha cha uhovyo wa sera za ccm. Wanastahili waondolewe madarakani kwa njia yoyote ile.