Wananchi tumefurahi kwamba mgao wa umeme umesitishwa hasa kwa mikoa ambayo ilikuwa kwa njia moja au nyingine ilikuwa imeathirika na mgao huo.Lakini matamshi yaliyotolewa na TANESCO mbona hayaeleweki.Hivi TANESCO wanataka tuamini kwamba sababu za kusitisha mgao ni utengenezwaji wa mashine moja tu kati ya tatu na kuongezeka kwa uzalishaji Kidatu,Mtera na Pangani? Kwa mtizamo wa karibu,hii ina maana kwamba usitishwaji wa mgao umesababishwa hasa na kuongezeka kwa uzalishaji Kidatu,Mtera na Pangani,kwa vile mashine moja isingeweza kuongeza uzalishaji kiasi hicho.Mimi si elewi ni miujiza gani imetumika kuongeza umeme Kidatu,Mtera na Pangani,hasa tukizingatia kwamba maji yanaendelea kupungua kwa vile tumeshaanza kipindi cha ukame.Nionavyo mimi ni kwamba kuna ujanja wa sungura hapa.Tusisahau kwamba tunaelekea kwenye uchaguzi,na mambo mengi yatafanywa ili ionekane kwamba serikali ina wajali watu wake.Tuwe macho wadau,vinginevyo tutaingizwa mkenge.Inawezekana hata tatizo halikuwepo,'it could be an ochestrated scenario.'