James Kasonda
Member
- Apr 2, 2012
- 84
- 49
Aliyebuni jina la wadanganyika anapaswa kupewa tuzo. Manake watanzania hata tukiambiwa tutazambaziwa mabomba yanayotoa pesa vijiji vyote tutakubali tu. Hii habari ya umeme imekuwa kero, tena kero kuliko kero. Tunadanganywa kila kunapokucha na tunabweteka tu. Jamani hivi wanaoshabikia chama tawala kilichotutawala kwa shida zote hizi wana macho kweli? Eti umeme mpaka vijijini! Eti maisha bora! Eti elimu bora! Wenzetu wanakula bata sisi tunalishwa harufu, hata makombo hatuyaoni. Tumia kura yako vizuri uchaguzi ujao na usikubali kuwa mdanganyika!!