Mgao wa pesa kwenye vilabu vinavyoshiriki ligi ya mabingwa barani ulaya

Achraf Hakimi

JF-Expert Member
Mar 3, 2010
875
1,779

Timu zitakazoshiriki kwenye michuano ya ligi ya mabingwa kwenye hatua ya makundi zina uhakika wa mgao wa Euro Milioni 7.2 kwa kila timu mgao ambao unatokana na mapato yanayopatikana toka kwenye vyanzo mbalimbali vya udhamini.
Mgawanyo huu unaonyesha kuwa timu itakayotwaa ubingwa itajipatia Euro Milioni 31.5, Hii ni kwa mujibu wa mfumo wa ugawanywaji wa mapato ya ligi ya mabingwa kwa msimu wa 2011/12.
Kila klabu kati ya vilabu 32 vinavyoshiriki itapata bonus ya ushiriki ambayo ni Euro milioni 3.9, na zaidi ya hapo kila timu itapata mgao wa kila mechi ambao ni Euro 550,000 kwa kila mechi ambayo timu inacheza , sambamba na hizo kuna mgao mwingine wa Euro 800,000 kwa kila mchezo ambao timu inashinda , Euro 400,000 kwa kila mechi ambayo timu inatoa sare kwenye hatua ya makundi.
Timu zitakazofuzu kuingia hatua ya 16 bora zitapata Euro Milioni 3 kila moja na zinazoingia robo fainali zitapata Euro milioni 3.3 na hatua ya nusu fainali itazipatia timu zitakazoingia Euro milioni 4.2 huku washindi wa fainali wakipata Euro Milioni 9 na washindi wa pili watapata Euro milioni 5.6 .
Katika makadirio hayo , jumla ya Euro milioni 55 zitaelekezwa kwenye mechi za mtoano ambapo kila timu inayoshiriki itajipatia Euro milioni 2.1 . Pamoja na hayo , kama ilivyokuwa kwenye michuano ya misimu ya 2006-09 , Euro milioni 10 zitawekwa kando kwa ajili ya timu zitakazotolewa kwenye hatua ya mtoano wa kufuzu na timu zitakazotolewa na kucheza ligi ya Europa .
Jumla ya asilimia 75% ya mapato yote yanayotokana na haki za matangazo na mikataba ya kibiashara inayofikia kitita cha Euro Milioni 530 itaenda kwa vilabu huku kiasi kinachobaki ambacho ni asilimia 25% zitabaki kwa ajili ya soka la ulaya ambako UEFA itazitumia kugharamia uendeshwaji wa michuano hii ya ligi ya mabingwa huku fedha nyingine zikilipwa kwa vyama wanachama wa UEFA, vilabu na ligi mbalimbali.
Jumla ya asilimia 82% ya mapato yote yanayopatikana toka kwenye mkondo huo huo wa milioni 530 zitaenda kwa vilabu , huku 18 ikitumika kwenye uendeshwaji wa UEFA kwa ujumla .
Kiasi cha Euro milioni 341 ambazo zimebakia toka kwenye mkondo wa soko la televisheni zitagawanywa kwa kuendana na thamani ya kila soko la televisheni kama inavyowakilishwa na vilabu vinavyoshiriki kwenye ligi ya mabingwa kwenye hatua ya makundi la ulaya ambako UEFA itazitumia kugharamia uendeshwaji wa michuano hii ya ligi ya mabingwa huku fedha nyingine zikilipwa kwa vyama wanachama wa UEFA , vilabu na ligi mbalimbali.
Jumla ya asilimia 82% ya mapato yote yanayopatikana toka kwenye mkondo huo huo wa milioni 530 zitaenda kwa vilabu , huku 18 ikitumika kwenye uendeshwaji wa UEFA kwa ujumla .
Kiasi cha Euro milioni 341 ambazo zimebakia toka kwenye mkondo wa soko la televisheni zitagawanywa kwa kuendana na thamani ya kila soko la televisheni kama inavyowakilishwa na vilabu vinavyoshiriki kwenye ligi ya mabingwa kwenye hatua ya makundi kwenda mbele na pia zitagawanywa kwa timu kadri zinavyoshiriki toka kwa vyama husika vya nchi vya soka.
 
[h=2]Wachezaji wanaolipwa zaidi Serie A.[/h]



Hii ndiyo orodha ya wachezaji wanaolipwa mishahara mikubwa kwenye Serie A.
1 Ibrahimovic AC Milan € 9,000,000
2 Sneijder Internazionale
€ 6,000,000
3 Buffon Juventus
€ 6,000,000
4 Totti Rome
€ 5,200,000
5 De Rossi Rome
€ 4,600,000
6 Flamini AC Milan
€ 4,500,000
7 Julius Caesar Inter
€ 4,500,000
8 Milito Inter
€ 4,500,000
9 Amauri Juventus
€ 4,000,000
10 Cambiasso Inter
€ 4,000,000
11 Maicon Inter
€ 4,000,000
12 Gattuso AC Milan
€ 4,000,000
13 Mexes AC Milan
€ 4,000,000
14 Duck AC Milan
€ 4,000,000
15 Robinho AC Milan
€ 4,000,000
16 Thiago Silva AC Milan
€ 4,000,000
17 Chivu Internazionale
€ 3,500,000
18 Forlan Internazionale
€ 3,500,000
19 Pike Internazionale
€ 3,500,000
20 Pirlo Juventus
€ 3,500,000
21 Chiellini Juventus
€ 3,500,000
22 Van Bommel AC Milan
€ 3,500,000
23 Zambrotta AC Milan
€ 3,500,000
 
Back
Top Bottom