Mganga wa zahanati aliyedaiwa kubaka mwanafunzi jela miaka 30

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
MGANGA wa zahanati aliyembaka mwanafunzi wa sekondari na kumpa ujauzito, amehukumiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Tabora kutumikia kifungo cha miaka 30 jela. Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Jovin Kato alitoa adhabu hiyo kwa mganga huyo, Elipidius Kweyumba ( 31), baada ya kuridhika na ushahidi wa upande wa mashtaka.

Hakimu Kato alisema mahakama imeridhika pasipo shaka kwamba mshtakiwa ndiye aliyembaka na kumpa ujauzito mtoto chini ya miaka 18 ambaye pia ni mwanafunzi na alifanya naye mapenzi mara nne kwa siku tofauti.

Akichambua ushahidi wa mashahidi nane wa upande wa mashtaka, hakimu Kato alisema mshtakiwa baada ya kugundua amempa ujauzito mwanafunzi huyo, kwa kutumia utaalamu wake alimpa dawa ambazo zilimsababishia madhara. Awali upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Tumaini Pius ulidai mshtakiwa alitenda kosa hilo Machi, mwaka huu wakati wa kipindi shule zimefungwa kupisha janga la ugonjwa wa corona.

Wakili Pius aliiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshtakiwa kwa vile alitenda kosa hilo kwa makusudi ili asiweze kurudia na iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hizo.

Akitoa adhabu hiyo, hakimu Kato aliulaumu upande wa mashtaka kwa kutokuwa makini kwani wangeweza kumwongezea shtaka la pili mshtakiwa la kusababisha mwanafunzi akose masomo.

Akitoa utetezi wake ili apunguziwe adhabu, mshtakiwa alidai kuwa ana familia inayomtegemea wakiwemo mke, watoto na mama mzazi na kwamba mashtaka hayo ni ya kusingiziwa kwani alikuwa hajawahi kumuona binti huyo.

Mtanzania
 
Hakunaga kwenda jela kipuuzi kama huku.. wenzako wanaenda jela kwa kesi za ufisadi... wewe unaenda jela kisa papuchi ya mtoto asiyejua kuoga

Hapo inaonekana Jamaa alikuwa anakula huyo mtoto kwa maridhiano kabisa, ila ikatokea mimba alafu alivyotaka kuitoa ndo ikaleta shida hadi kujulikana.

kesi kama hizo mtaani ziko nyingi sana sema kuna ambae zitamuangukia kama hivyo alafu sisi tunaojiona watiifu tunalaumu ila kumbe tuko nayo huku.

Kifupi Watoto washule sio kabisa,nikujiweka nao mbali japo wanavishawishi sana .Alafu ndo hivyo sheria zinawabeba sana kiupendeleo .
 
Hapo inaonekana Jamaa alikuwa anakula huyo mtoto kwa maridhiano kabisa, ila ikatokea mimba alafu alivyotaka kuitoa ndo ikaleta shida hadi kujulikana.

kesi kama hizo mtaani ziko nyingi sana sema kuna ambae zitamuangukia kama hivyo alafu sisi tunaojiona watiifu tunalaumu ila kumbe tuko nayo huku.

Kifupi Watoto washule sio kabisa,nikujiweka nao mbali japo wanavishawishi sana .Alafu ndo hivyo sheria zinawabeba sana kiupendeleo .

Watoto wa Shule ni wadogo sana na are not stable, sasa wetumia madawa yao kutoa mimba, Mtoto Labda damu zimevuja nyingi then akashtukiwa!

Sasa Jamaa ana miaka 30 ana mke na watoto anafungwa miaka 30 jamani, akitoka Mtoto wake Labda na 34! Hatari kabisa hii! Kwa kosa la kijinga kabisa!

Tujirekebishe maana wakati anatafanya hayo hakuwaza yangemharibikia, ila ndo hivyo Kwa hiyo hizi tabia jaman wenye nazo ziacheni maana si nzuri!
 
Ubahili wa kuhonga unawatesa wanaume... daktari unashindwa kumega hata nesi ama mademu kibao wanaokuja kutibiwa kwako...kukwepa gharama unaenda gonga kitoto sabab hakipigi mizinga mikubwa
Inasikitisha Sana, kumuanza mtoto mdogo ngono nikumharibu kisaikolojia imagine jinsi ngono zinavotesa watu wazima sembuse mtoto, kwanza watoto hata huwa hawasikii Raha kuwaumiza tu, nadhani wanaume wa hivi hata ikiwandugu yangu aende tu jela, Kuna watu wazima wengi hawataki kuwafata wanakula Vitoto.
 
Inasikitisha Sana, kumuanza mtoto mdogo ngono nikumharibu kisaikolojia imagine jinsi ngono zinavotesa watu wazima sembuse mtoto, kwanza watoto hata huwa hawasikii Raha kuwaumiza tu, nadhani wanaume wa hivi hata ikiwandugu yangu aende tu jela, Kuna watu wazima wengi hawataki kuwafata wanakula Vitoto.
Watu wazima huwezi mpata bikra mkuu, afu mileage zimesoma pk mwisho
 
Back
Top Bottom