Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,268
- 33,040
JESHI la Polisi mkoani Arusha limefanikiwa kumkamata mganga wa kienyeji anayewasaidia majambazi toka jijini Dar es Salaam na Arusha kufanikiwa katika ujambazi huo
Mbali na kukamatwa na mganga huyo pia majambazi hao wapatao watano wamekamatwa katika msako huo uliofanywa na jeshila polisi kwa kushirikiana na kikosi cha pikipiki.
Watuhumiwa hao walinaswa wakiwa na bastola yenye risasi tisa, rungu, panga na tunguri, na dawa mabalimbali za kienyeji wakiwa kwenye harakati za kuvamia kwa mfanyabiashara mmoja maarufu wa Manispaa ya Arusha.
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Leonard Paul, alisema majambazi hao walinaswa wakiwa katika baa ya Zumbukuku wakwia na mganga wao huyo, wakiendelea na vinywaji huku wakijiandaa kuvamia kwa mfanyabiashara huyo kwa lengo la kupora mali
Alisema majambazi hao, pia walikutwa na gari aina ya Toyota Corolla T 153 ANY iliyotarajiwa kutumika katika uporaji huo na pikipiki aina ya Honda XL 250 T 375 ATY ambayo huitumia kwa uchunguzi kabla ya kufanya ujambazi wao.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Halidi Omari (35) mkazi wa Kibonde maji jijini Dar es Salaam ambaye ndiye mganga wao wanayetembea nae, Frank Sikawa (40) Temeke, Fredy Mkenya (30) mkazi wa Sombetini Arusha, Gift Mushi (28) mkazi wa Sakina na Silasi Msechu (29) wa makao mapya mjini hapa.
Hivyo ilidaiwa baada ya mahojiano hayo walibainisha kuwa walikuwa wanasaidiwa na nmganga huyo kufanikisha katika ujam,bazi wao waliouanza kwa muda mrefu.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=3580298&&Cat=1
Mbali na kukamatwa na mganga huyo pia majambazi hao wapatao watano wamekamatwa katika msako huo uliofanywa na jeshila polisi kwa kushirikiana na kikosi cha pikipiki.
Watuhumiwa hao walinaswa wakiwa na bastola yenye risasi tisa, rungu, panga na tunguri, na dawa mabalimbali za kienyeji wakiwa kwenye harakati za kuvamia kwa mfanyabiashara mmoja maarufu wa Manispaa ya Arusha.
Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Leonard Paul, alisema majambazi hao walinaswa wakiwa katika baa ya Zumbukuku wakwia na mganga wao huyo, wakiendelea na vinywaji huku wakijiandaa kuvamia kwa mfanyabiashara huyo kwa lengo la kupora mali
Alisema majambazi hao, pia walikutwa na gari aina ya Toyota Corolla T 153 ANY iliyotarajiwa kutumika katika uporaji huo na pikipiki aina ya Honda XL 250 T 375 ATY ambayo huitumia kwa uchunguzi kabla ya kufanya ujambazi wao.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Halidi Omari (35) mkazi wa Kibonde maji jijini Dar es Salaam ambaye ndiye mganga wao wanayetembea nae, Frank Sikawa (40) Temeke, Fredy Mkenya (30) mkazi wa Sombetini Arusha, Gift Mushi (28) mkazi wa Sakina na Silasi Msechu (29) wa makao mapya mjini hapa.
Hivyo ilidaiwa baada ya mahojiano hayo walibainisha kuwa walikuwa wanasaidiwa na nmganga huyo kufanikisha katika ujam,bazi wao waliouanza kwa muda mrefu.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=3580298&&Cat=1