Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,422
- 911,172
Mganga wa jadi kortini akidaiwa kutapeli Sh70 mil | Send to a friend |
Friday, 05 August 2011 08:47 |
Hadija Jumanne MGANGA wa jadi, Ismail Idd (42), amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala kujibu shtaka la kutapeli na kujipatia Sh70 milioni kwa njia ya udanganyifu. Idd, ambaye ni mkazi wa Yombo Buza, alipandishwa katika mahakama hiyo jana kujibu shtaka hilo baada ya kumlaghai mlalamikaji, Oscar Kushi, kuwa ampatie fedha hizo ili azitengeneze na zitaongezeka maradufu, huku akijua ni uongo. Mwendesha mashtaka wakili wa serikali, Sakina Sinda, alidai mahakamani hapo kuwa, mshtakiwa alitenda kosa hilo Novemba mwaka jana mtaa wa Zanaki, Dar es Salaam. Ilidaiwa kuwa mshtakiwa, siku ya tukio saa 5:00 asubuhi eneo hilo, mshtakiwa alijipatia Sh70 milioni, mali ya Oscar Kushi. Sinda aliendelea kudai kuwa, mshtakiwa alijipatia fedha hizo kutoka kwa mlalamikaji baada ya kumlaghai kuwa, ana uwezo wa kutengeneza fedha za majini. Alidai kuwa huku akijua kuwa ni uongo, mshtakiwa aliendelea kumlaghai mlalamikaji kuwa, angemtengenezea fedha za majini zikawa zinakuja nyumba kwake kila anapokuwa na shida. Mshtakiwa alikana shtaka na Hakimu Karimu Mushi, aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 18, mwaka huu itakapotajwa tena. Mshtakiwa alirudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana ya kuwa na wadhamini wawili wa kuaminika watakao saini nusu ya mali iliyoibwa. Katka kesi nyingine, Mkazi wa Kinondoni, Alex Katabazi (25), amefikishwa katika mahakama hiyo kujibu shtaka la wizi wa pikipiki. Mwendesha mashtaka, Wakili wa Serikali, Anuciatha Leopard, alidai kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Julai 29, mwaka huu eneo la Mnazi Mmoja, mtaa Indra Ghandi. Leopard alidai siku ya tukio saa 11:00 jioni, mshtakiwa aliiba pikipiki moja aina ya Bajaj yenye thamani ya Sh2.2 milioni, mali ya Samson Shikoya. Mshtakiwa alikana shtaka na Hakimu Janeth Kaluyenda aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 17, mwaka huu itakapotajwa tena. |