Nahitaji msaada mkubwa sana ili niweze kushinda hili.
Nilikuwa nafany kazi ambayo alinitafutia mama yangu. Nimefanya kwa muda, baadaye nilihitaji kujiendeleza. Nilivyomwambia kuwa naacha nataka nikasome aligoma sana.
Baadae ilibidi niforce mwenyewe maana ada niliomba kwa mzazi wa kiume. Nimefika shuleni nilianza vizuri kwa shangwe zote lakini baadaye hali ikabadilika ya kutotaka kusoma. Kuna muda nilikuwa nashika daftari na kuacha au nafunua page tu naacha.
Nikaona hali sio ya kawaida nikaamua kwenda kuombewa ikaonekana nina mapepo. Nikaombewa lakini roho ikawa bado inahangaika. Nikasoma hadi nikamaliza mwaka, sasa nahitaji kwenda kuendelea na mwaka mwingine nimeamua kwenda kwa mganga nimekuta ni kwenye familia kuna watu wamenifanyia mchezo kwa kunitupia jini.
Nimefanyiwa dawa za kulitoa lakini nimeishiwa sana nguvu ya kusoma hata mwili wangu uko tofauti. Kazi nilishaacha na ninategemea elimu inisaidie. Kichwa changu kina mawazo mengi sana kati ya kuacha chuo au nikaendelee?
Naombeni ushauri kwani nimechanganikiwa na huko kwa mganga nimemwona aliyefanya maana kuna sehemu unaangalia.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nilikuwa nafany kazi ambayo alinitafutia mama yangu. Nimefanya kwa muda, baadaye nilihitaji kujiendeleza. Nilivyomwambia kuwa naacha nataka nikasome aligoma sana.
Baadae ilibidi niforce mwenyewe maana ada niliomba kwa mzazi wa kiume. Nimefika shuleni nilianza vizuri kwa shangwe zote lakini baadaye hali ikabadilika ya kutotaka kusoma. Kuna muda nilikuwa nashika daftari na kuacha au nafunua page tu naacha.
Nikaona hali sio ya kawaida nikaamua kwenda kuombewa ikaonekana nina mapepo. Nikaombewa lakini roho ikawa bado inahangaika. Nikasoma hadi nikamaliza mwaka, sasa nahitaji kwenda kuendelea na mwaka mwingine nimeamua kwenda kwa mganga nimekuta ni kwenye familia kuna watu wamenifanyia mchezo kwa kunitupia jini.
Nimefanyiwa dawa za kulitoa lakini nimeishiwa sana nguvu ya kusoma hata mwili wangu uko tofauti. Kazi nilishaacha na ninategemea elimu inisaidie. Kichwa changu kina mawazo mengi sana kati ya kuacha chuo au nikaendelee?
Naombeni ushauri kwani nimechanganikiwa na huko kwa mganga nimemwona aliyefanya maana kuna sehemu unaangalia.
Sent using Jamii Forums mobile app