Mganga kaniambia nimerogwa na ndugu yangu, nimechanganyikiwa

Passed

JF-Expert Member
Dec 15, 2017
561
156
Nahitaji msaada mkubwa sana ili niweze kushinda hili.

Nilikuwa nafany kazi ambayo alinitafutia mama yangu. Nimefanya kwa muda, baadaye nilihitaji kujiendeleza. Nilivyomwambia kuwa naacha nataka nikasome aligoma sana.

Baadae ilibidi niforce mwenyewe maana ada niliomba kwa mzazi wa kiume. Nimefika shuleni nilianza vizuri kwa shangwe zote lakini baadaye hali ikabadilika ya kutotaka kusoma. Kuna muda nilikuwa nashika daftari na kuacha au nafunua page tu naacha.

Nikaona hali sio ya kawaida nikaamua kwenda kuombewa ikaonekana nina mapepo. Nikaombewa lakini roho ikawa bado inahangaika. Nikasoma hadi nikamaliza mwaka, sasa nahitaji kwenda kuendelea na mwaka mwingine nimeamua kwenda kwa mganga nimekuta ni kwenye familia kuna watu wamenifanyia mchezo kwa kunitupia jini.

Nimefanyiwa dawa za kulitoa lakini nimeishiwa sana nguvu ya kusoma hata mwili wangu uko tofauti. Kazi nilishaacha na ninategemea elimu inisaidie. Kichwa changu kina mawazo mengi sana kati ya kuacha chuo au nikaendelee?

Naombeni ushauri kwani nimechanganikiwa na huko kwa mganga nimemwona aliyefanya maana kuna sehemu unaangalia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pregabalin hunywewa usiku tu!
Tena ni kidonge kimoja, sasa inaonekana hujafuata maelekezo ya pharmacist.
 
  • Thanks
Reactions: amu
Sasa baada ya kujua kuwa unarongwa utafanyaje...utamwambia ndugu yako au utakaanalo rohoni?...Pole Sana...lakini Waganga wapiga ramli chonganishi sio wazuri?

Je na wewe utamroga au utafanyaje...Kama huwezi kuendelea acha tu shule fanya Mambo mengine

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Achana na waganga, watakumalizia hela zako. Ukiwazoea utashangaa hata ukijikwaa kidogo tu, utakimbilia kwa waganga kutafuta mchawi aliyesababisha ujikwae.
Sali kwa imani yako utakua sawa
 
Wanawake huwa mnapenda sana waganga sijui kwanini?
Mganga siku zote huwa hakosi sababu hapo hakuna cha jini wala kurogwa..
Elimu yako haijakusaidia hata kidogo!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nahitaji msaada mkubwa sana ili niweze kushinda hili.

Nilikuwa nafany kazi ambayo alinitafutia mama yangu. Nimefanya kwa muda, baadaye nilihitaji kujiendeleza. Nilivyomwambia kuwa naacha nataka nikasome aligoma sana.

Baadae ilibidi niforce mwenyewe maana ada niliomba kwa mzazi wa kiume. Nimefika shuleni nilianza vizuri kwa shangwe zote lakini baadaye hali ikabadilika ya kutotaka kusoma. Kuna muda nilikuwa nashika daftari na kuacha au nafunua page tu naacha.

Nikaona hali sio ya kawaida nikaamua kwenda kuombewa ikaonekana nina mapepo. Nikaombewa lakini roho ikawa bado inahangaika. Nikasoma hadi nikamaliza mwaka, sasa nahitaji kwenda kuendelea na mwaka mwingine nimeamua kwenda kwa mganga nimekuta ni kwenye familia kuna watu wamenifanyia mchezo kwa kunitupia jini.

Nimefanyiwa dawa za kulitoa lakini nimeishiwa sana nguvu ya kusoma hata mwili wangu uko tofauti. Kazi nilishaacha na ninategemea elimu inisaidie. Kichwa changu kina mawazo mengi sana kati ya kuacha chuo au nikaendelee?

Naombeni ushauri kwani nimechanganikiwa na huko kwa mganga nimemwona aliyefanya maana kuna sehemu unaangalia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe unastahili kuchezewa akili na waganga.
Tena urogwe mpaka ukome.
Nb: kumuini mganga na haya mambo ni imani yako. Mganga kakuchezea akili.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom