Francis12
JF-Expert Member
- Sep 30, 2016
- 7,533
- 22,276
Mganga aliyedai ana nguvu za kuzuia risasi apigwa risasi, afariki.
Chinaka Adoezuwe 26 ambae ni mganga wa Kienyeji amefariki baada ya mteja wake kujaribu iwapo ana nguvu za kuzuia risasi kuingia mwilini mwake na kumuagiza mteja wake kumpiga risasi alipokuwa akivaa nguvu hizo za kuzuia risasi katika shingo yake.
Kijana huyo alikuwa amemtembelea mganga huyo ili kupata nguvu za kuzuia risasi ambazo mganga huyo alimpatia, kulingana na mwanakijiji mmoja.
Ili kuthibitisha kwamba nguvu hizo zinafanya kazi, alisimama na kumpatia mteja wake Bunduki. Na hapo ndipo janga likatokea. :
Mwezi Januari, muuzaji wa dawa za kienyeji alikamatwa baada ya mtu mmoja aliyedaiwa kunywa maji ya kuzuia risasi kuuawa.
Muuzaji huyo anayeishi kaskazini magharibi mwa Nigeria aliripotiwa kumhakikishia mtu huyo kwamba hatofariki atakapopigwa risasi.
Polisi Nigeria wamethibitisha kumshikilia kijana huyo.
Chanzo .BBC Swahili.
Chinaka Adoezuwe 26 ambae ni mganga wa Kienyeji amefariki baada ya mteja wake kujaribu iwapo ana nguvu za kuzuia risasi kuingia mwilini mwake na kumuagiza mteja wake kumpiga risasi alipokuwa akivaa nguvu hizo za kuzuia risasi katika shingo yake.
Kijana huyo alikuwa amemtembelea mganga huyo ili kupata nguvu za kuzuia risasi ambazo mganga huyo alimpatia, kulingana na mwanakijiji mmoja.
Ili kuthibitisha kwamba nguvu hizo zinafanya kazi, alisimama na kumpatia mteja wake Bunduki. Na hapo ndipo janga likatokea. :
Mwezi Januari, muuzaji wa dawa za kienyeji alikamatwa baada ya mtu mmoja aliyedaiwa kunywa maji ya kuzuia risasi kuuawa.
Muuzaji huyo anayeishi kaskazini magharibi mwa Nigeria aliripotiwa kumhakikishia mtu huyo kwamba hatofariki atakapopigwa risasi.
Polisi Nigeria wamethibitisha kumshikilia kijana huyo.
Chanzo .BBC Swahili.