WomanOfSubstance
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 5,459
- 952
Watanzania.. hatutaacha kushangaa kila kukicha. Leo 7/8/08,kwenye taarifa ya habari, tumesikia taarifa ya kutoroka kwa mfungwa aliyekuwa anatumikia kifungo cha miaka 30 katika gereza la Karanga, kwa kosa la ujambazi akiwa analimishwa kwenye shamba la muwekezaji!!!Hii imekuja baada ya Kamishna Mkuu wa Magereza kupiga marufuku " utumikishwaji" huo.
Hebu someni habari hiyo hapo chini ......wonders! wonders!
Marufuku vigogo kuwatumia wafungwa
2007-11-27 15:47:21
Na Patrick Chambo, PST Moshi
Kamishina Mkuu wa Magereza Nchini, Bw. Augustino Nanyaro, amewapiga marufuku baadhi ya wakuu wa magereza nchini tabia ya kuwakodisha wafungwa kwa wawekezaji wa mashamba makubwa kwa ajili ya kuwalimia huku wafungwa hao wakiwalipa sigara, bangi na sabuni.
Kamishna Nanyaro aliyasema hayo mwishoni mwa wiki katika Gereza Kuu la Wagonjwa Tanzania la Karanga, Manispaa ya Moshi baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wafungwa na mahabusu zaidi ya 2,000 dhidi ya uongozi wa Gereza hilo.
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. Joel Bukuku, alithibitisha jana kutolewa kwa agizo hilo katika kikao chake na wafungwa na mahabusu alipokuwa akipokea malalamiko yao.
Imedaiwa kuwa, wafungwa hao walimueleza Kamishna kuwa, licha ya gereza hilo kutambulika kuwa ni la Wagonjwa Tanzania na sio la kilimo, wamekuwa wakilimishwa kwa wawekezaji, wakuu wa magereza, wilaya, mkoa hadi taifa zaidi ya ekari 300.?
Mmoja wa maofisa wa magereza, alisema mashamba ya wakubwa na wafanyabishara ndiyo yanayochochea biashara za kulawitiana magerezani.
Wakizungumza jana na PST baadhi ya wafungwa na mahabusu katika Mahakama Kuu Kanda ya Kilimanjaro na hospitali ya KCMC, walisema wamefurahishwa na kauli ya Kamishna Mkuu huyo.
Wameyataja maeneo yenye mashamba hayo kuwa ni Mbatakero, KIA, Longoi Mashine Tools na Kibosho kwa mwekezaji mmoja, Njiapanda ya Himo na maeneo TPC walikokuwa wakimlimia kiongozi mmoja wa serikali wilayani Moshi.
`Tukitoka gerezani, tunatoka kama RPC Genge, RPO Genge, CCP Genge au RC Genge, lakini tunakwenda kulima kwa wakubwa au wazungu na wananchi, na tukifika shambani, tunapewa sigara, bangi na sabuni, huku mnapewa soda na nyama mnalima ekari zaidi ya 100,? alisema mmoja wa mahabusu na kuongeza ?na hapo ndipo tunapohoji, mbona gerezani tumekunywa uji usio na sukari, ugali na mboga havina mafuta, je kweli ni shamba la Gereza.?
Wafungwa hao walimuomba Kamishana wa Magereza kuwalinda wasipewe adhabu ya kunyimwa kifungo cha nje na Parole kwa kuwa maofisa magereza wanawaandama na kuwasakama kuwa kwanini walitoboa siri nakuwa katika majalada yao watawaandikia wana tabia mbaya gerezani wasitoke kama njia ya kuwakomboa.
Bw. Nanyaro alisema amesikitishwa na taarifa za wafungwa kuna? baadhi ya wakuu wa magereza hapa nchini wanaowakodisha wafungwa na kwenda kulima katika mashamba ya matajiri na viongozi huku wakijua wazi vitendo hivyo ni kinyume cha taratibu za magereza.
Baadhi ya maofisa magereza waliozungumza na PST walisema, Kamishna Nanyaro ameahidi kuchukua hatua kali dhidi ya wakuu wa magereza na viongozi wa gereza hilo kama watabainika kuwa walikuwa wakiwakodisha wafungwa kwa wazungu wa mashamba ya maua na wananchi ikiwemo mashamba yao.
Hebu someni habari hiyo hapo chini ......wonders! wonders!
Marufuku vigogo kuwatumia wafungwa
2007-11-27 15:47:21
Na Patrick Chambo, PST Moshi
Kamishina Mkuu wa Magereza Nchini, Bw. Augustino Nanyaro, amewapiga marufuku baadhi ya wakuu wa magereza nchini tabia ya kuwakodisha wafungwa kwa wawekezaji wa mashamba makubwa kwa ajili ya kuwalimia huku wafungwa hao wakiwalipa sigara, bangi na sabuni.
Kamishna Nanyaro aliyasema hayo mwishoni mwa wiki katika Gereza Kuu la Wagonjwa Tanzania la Karanga, Manispaa ya Moshi baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wafungwa na mahabusu zaidi ya 2,000 dhidi ya uongozi wa Gereza hilo.
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. Joel Bukuku, alithibitisha jana kutolewa kwa agizo hilo katika kikao chake na wafungwa na mahabusu alipokuwa akipokea malalamiko yao.
Imedaiwa kuwa, wafungwa hao walimueleza Kamishna kuwa, licha ya gereza hilo kutambulika kuwa ni la Wagonjwa Tanzania na sio la kilimo, wamekuwa wakilimishwa kwa wawekezaji, wakuu wa magereza, wilaya, mkoa hadi taifa zaidi ya ekari 300.?
Mmoja wa maofisa wa magereza, alisema mashamba ya wakubwa na wafanyabishara ndiyo yanayochochea biashara za kulawitiana magerezani.
Wakizungumza jana na PST baadhi ya wafungwa na mahabusu katika Mahakama Kuu Kanda ya Kilimanjaro na hospitali ya KCMC, walisema wamefurahishwa na kauli ya Kamishna Mkuu huyo.
Wameyataja maeneo yenye mashamba hayo kuwa ni Mbatakero, KIA, Longoi Mashine Tools na Kibosho kwa mwekezaji mmoja, Njiapanda ya Himo na maeneo TPC walikokuwa wakimlimia kiongozi mmoja wa serikali wilayani Moshi.
`Tukitoka gerezani, tunatoka kama RPC Genge, RPO Genge, CCP Genge au RC Genge, lakini tunakwenda kulima kwa wakubwa au wazungu na wananchi, na tukifika shambani, tunapewa sigara, bangi na sabuni, huku mnapewa soda na nyama mnalima ekari zaidi ya 100,? alisema mmoja wa mahabusu na kuongeza ?na hapo ndipo tunapohoji, mbona gerezani tumekunywa uji usio na sukari, ugali na mboga havina mafuta, je kweli ni shamba la Gereza.?
Wafungwa hao walimuomba Kamishana wa Magereza kuwalinda wasipewe adhabu ya kunyimwa kifungo cha nje na Parole kwa kuwa maofisa magereza wanawaandama na kuwasakama kuwa kwanini walitoboa siri nakuwa katika majalada yao watawaandikia wana tabia mbaya gerezani wasitoke kama njia ya kuwakomboa.
Bw. Nanyaro alisema amesikitishwa na taarifa za wafungwa kuna? baadhi ya wakuu wa magereza hapa nchini wanaowakodisha wafungwa na kwenda kulima katika mashamba ya matajiri na viongozi huku wakijua wazi vitendo hivyo ni kinyume cha taratibu za magereza.
Baadhi ya maofisa magereza waliozungumza na PST walisema, Kamishna Nanyaro ameahidi kuchukua hatua kali dhidi ya wakuu wa magereza na viongozi wa gereza hilo kama watabainika kuwa walikuwa wakiwakodisha wafungwa kwa wazungu wa mashamba ya maua na wananchi ikiwemo mashamba yao.