Mfumuko wa Bei ni tatizo la kidunia 2021 na kuendelea 2022. Haliepukiki

bnhai

JF-Expert Member
Jul 12, 2009
2,778
2,298
Malalamiko ya mfumoko wa bei yamekuwa makubwa.

Kuanzia bei ya chakula, vipuri, mafuta, vifaa vya ujenzi nk.

Hii ni hali halisi sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania. Takwimu zinazotolewa na TBS zinaonesha kuwapo na ongezeko la bei za vitu mbalimbali. Hali hii ipo pia nchi nyingine kama Marekani ambapo mwezi Oktoba 2021 walirekodi mfumuko wa bei mkubwa sana ambao haujawahi kutokea kwa miongo kadhaa. Nchini Uingereza pia na nchi nyingine za Kiafrika.

Sababu kubwa ni ipi;
1. Katika kipindi cha Korona uzalishaji ulipungua kwa kiasi kikubwa kwa sababu ya lockdown zilizokuwepo. Kwa hivyo baada ya muda athari yake ndio inaanza kujitokeza ambapo mahitaji yamekuwa makubwa kulinganisha na bidhaa zilizopo.

2. Kwa upande wa mafuta, kumekuwa na control kubwa sana ya kuzalisha mafuta yanayoenda kuuzwa kupitia OPEC na wazalishaji wengine. Matokeo yake, yanatengeneza uhitaji ambapo bei inapanda. Mfano hai ni pale Marekeni ilipoamua kuachia akiba yake ya mafuta ili kuweza kupambana na hizi nchi zinazozalisha mafuta kidogo. Pamoja na chagua hilo, hawakufanikiwa. Itakumbukwa kwamba huko nyuma mafuta yamewahi kuuzwa kwa NEGATIVE PRICE. Hii ilitokana na uzalishaji mkubwa.

3. Mikopo iliyotolewa kupitia mapambano dhidi ya UVIKO-19 pamoja na ile mingine, imeongeza mzunguko wa fedha. Maana fedha imekuwa nyingi na hatimaye madhara ndio haya.
Pamoja na sababu hizi zipo nyingine nyingi tu zinazoongeza bei ya bidhaa.

Hivi karibuni tumesikia Serikali ikitaka uchunguzi wa bidhaa kuadimika au hata kupanda bei. Ukweli mchungu ni kwamba, malighafi za bidhaa husika zimepanda bei, hivyo wazalishaji hawaoni faida tajwa.

Zipo njia kadhaa za kupambana na huku kupanda bei;
1. Kuruhusu ushindani kutoka kwa wazalishaji wengine hata nje ya nchi kama uzalishaji wetu utakuwa ni wa gharama kubwa. Lakini madhara ya hili, ni kufifia kwa viwanda vyetu na kuua uchumi wa viwanda. Hivyo ni vyema kuona kama wazalishaji watapewa motisha fulani ili angalau uzalishaji wao uwe wenye tija kwa wananchi na kupunguza mfumuko wa bei.
2. Kutazama sana sera zetu za kifedha kama tunaingiza sana fedha kwenye mzunguko.
3. Kuongeza uzalishaji na kupunguza utegemezi wa malighafi.

Pamoja na hivyo, tutegemee kuongezeka kwa mfumuko wa bei kwa miezi kadhaa mpaka pale uzalishaji duniani utakapoimarika.
 
Sisi tuna viongozi wasio na maono na wanaojali matumbo yao zaidi, hapa ndipo tatizo kubwa.
 
Umetoa hoja nzuri ila solution mbovu.hatuwezi kukaa kusubiri tu mpk uzalishaji wa dunia uimalike bila ya kutafuta suluhu ya muda mfupi.

Serikali lazima itawale bei za vitu ,watu wanaongeza bei kiholela
 
Umetoa hoja nzuri ila solution mbovu.hatuwezi kukaa kusubiri tu mpk uzalishaji wa dunia uimalike bila ya kutafuta suluhu ya muda mfupi.

Serikali lazima itawale bei za vitu ,watu wanaongeza bei kiholela
Bahati mbaya Serikali haina uwezo wa kupanga bei ya kila kitu. Kiufupi, hatuzalishi. Namna pekee ya kupunguza bei, kwa muda mfupi, ni kupunguza kodi. Ambayo itaathiri utekelezaji wa shughuli za kawaida na maendeleo. Kwa muda mrefu, ni kujenga viwanda.
 
Asabte usalama wa taifa kwa ujinga huo unaotuletea..Vipi umerudi lini kutoka masomini russia?
 
Naona hata huku bei za bidhaa zimepanda sana ilianza na Petrol na diesel mwaka jana na kwa mara ya kwanza ikafika £1.50 ila imeshuka kidogo

Chakula kimepanda pia na bidhaa karibia zote
Mwezi wa Nne ndio balaa zaidi linakuja maana mpaka National insurance na PAYE tax zinapanda ila mshahara palepale

Kwa hiyo hamko peke yenu bali ni janga la dunia haswa
 
IMG_20220213_013304_593.jpg
 
Umetoa hoja nzuri ila solution mbovu.hatuwezi kukaa kusubiri tu mpk uzalishaji wa dunia uimalike bila ya kutafuta suluhu ya muda mfupi.

Serikali lazima itawale bei za vitu ,watu wanaongeza bei kiholela

Tupo katika ulimwengu wa kibepari sio kijamaa
 
Sasa hivi tunazungumzia vita vya Ukraine. Hivi vimeenda kufanya hali kuwa mbaya zaidi. Kama nchi kubwa hazitakaa mezani, tutegemee mfumuko wa bei mkubwa zaidi na njaa kutokea baadhi ya maeneo na umasikini kutamalaki.
Mwaka uliopita hali ya mvua haikuwa nzuri maeneo mengi nchini, hivyo uhitaji wa chakula utakuwa mkubwa na bei zitakuwa za juu.
Hali ya covid 19 na hivi vita, hali itakuwa mbaya zaidi kwenye eneo la mnyonyoro wa ugavi, hasa uzalishaji na usafirishaji.
 
"Necessity is the mother of invention" Uhitaji (umuhimu) ni mama wa uvumbuzi.

Kupanda (mfumuko wa bei) kwa bei za bidhaa inatubidi wadau wa ujenzi tubuni mbinu mpya za kupunguza gharama za ujenzi bila kuathiri ubora (quality and standards). Hapa darasa la ujenzi la waja wema, tumebuni aina ya ujenzi wa ngazi za kipekee, zenye kukidi viwango na kupitiliza viwango na zenye ubora wa hali ya juu kwa gharama nafuu. Bofya link ujionee: Darasa la ujenzi la Madrassatul Abraar latunukiwa Tuzo ya ubunifu wa ujenzi kutoka Shirika la Uingereza.
 
To know where the current inflation comes from, one must firstly understand the behaviour of profit making firm in relation to prices and outputs as firms are the first agent of inflation, the second being the money supply and third one being an exchange rate regime for imported products.

The current inflation is not caused by the excess liquidity as many economists and economic professors might be thinking!
It has largely been caused by the ability of many firms producing similar products to utilize RESERVE CAPACITY.
Once a firm has been able to utilize a reserve capacity, it has no incentive to charge the same price while it can still produce the same output with while charging higher prices.
Most firms with margins of 40% were able to absorb a costs shocks caused by increased prices of inputs. But they are not willing to absorb even a 5% increase in input factor but to transfer this to final consumer because there is no incentive to absorb the cost while it can be transfered to final consumer in an event a firm is producing at full capacity!
To tame inflation, firms should not be 'allowed' to produce goods and services at a full capacity.
Govt accross the world have to identify 20-50 products items that makes the 50-55% by weights of its basket of goods and services that is used to measure CPI and ensure that it produces at least 25% of the market share and sell those goods slightly below the market price to limit exccessive price increase.
That means govts need to get back into business to take over firms ability to utilize a reserve capacity.
They need to retake control of markets by producing 20-25% by market share of goods and services that are having heavy weights on CPI measurements.
Such goods are sugar, steel, rental houses etc...
The govts in Euro zone, Japan, Canada, China, India, Africa, Australia, Newsland South America and USA should not end their QE programs but rather they should re-allocate their 'QE money' in producing 20-25% of goods and services that account 50% of CPI hence to create jobs, spur growth and to tame inflation!
 
Back
Top Bottom