ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,017
- 7,220
Unaposafiri kwa ngalawa wakati wote usalama wa ngalawa hiyo ndio usalama wako. Hivyohivyo kwa wanasiasa, usalama wa chama ndio usalama wa mwanasiasa. Hivyo basi mwanasiasa siku zote ni lazima atakahihikisha anakitetea chama chake ili kiendelee kuwa kwenye nafasi nzuri na kikubalike ili na yeye anendelee kukubalika.Ndio maana kauli za " chama hakina tatizo, tatizo ni mtu mmojommoja" zimekuwa zikisikika sana.
Swali ninalojiuliza ni hili: je kuna ugumu gani kuongoza nchi bila chama chochote? Kila mwanasiasa akawa independent na tukaepukana na kansa ya kutetea maovu kwa maslahi ya chama. Obviously hata katika mfumo wa aina hiyo kutakuwa na wanasiasa watakaoungana in someway kuteteana, lakini adha yake haitakuwa kama ya kutetea chama kilichojisambaza nchi nzima na kinachotishia kufuta uanachama wale wote wanaohatarisha maslahi yake.
Tufute vyama vyote na tuunde Tanzania inayoongozwa na watanzania wasiofungamana na chama chochote.
Swali ninalojiuliza ni hili: je kuna ugumu gani kuongoza nchi bila chama chochote? Kila mwanasiasa akawa independent na tukaepukana na kansa ya kutetea maovu kwa maslahi ya chama. Obviously hata katika mfumo wa aina hiyo kutakuwa na wanasiasa watakaoungana in someway kuteteana, lakini adha yake haitakuwa kama ya kutetea chama kilichojisambaza nchi nzima na kinachotishia kufuta uanachama wale wote wanaohatarisha maslahi yake.
Tufute vyama vyote na tuunde Tanzania inayoongozwa na watanzania wasiofungamana na chama chochote.