MpiganajiNambaMoja
Member
- Sep 20, 2007
- 69
- 2
Pamoja na mabadiliko ya mawiziri ambayo tunayatarajia, pia mfumo wa utendaji kazi serekalini unahitaji mabadiliko makubwa.
Mpaka sasa mfumo wa utendaji kazi serikalini, kwa kiasi kikubwa umebakia ni ule uliorithiwa kutoka katika serikali ya kikoloni mwaka 1961. Mfumo huu umejaa usiri mkubwa usio wa lazima huku kila document ikipigwa chapa ya neno "CONFIDENTIAL" bila sababu za msingi. Pamoja na wimbo wa utawala bora amboa serikali imekuwa ikiuimba kila siku, mpaka kuanzisha wizara inayoshughulika utawala bora, hali imekuwa tofauti na dhana hiyo ambayo ina himiza UWAZI.
Pamoja na wizara kuwa na dira (Vision), mikakati (Strategic plan), sera (Policies) n.k lakini document hizo ambazo hugharimu fedha nyingi wakati wa uandaaji wake ikiwa ni pamoja na semina nyingi bagamoyo, mwisho wa siku huwekwa katika makabati na kuliwa na mende.
Kazi nyingi za wizara zimekuwa ni za zima moto, bila kufuata mipango zilizojiwekea, zikiambata na re-allocation za mafungu, kutoka kwenye kazi zilizopangiwa kwenda kwenye kazi ya zima moto. Mfano mzuri ni ziara ya mawaziri miezi michache iliyopita ambayo iligharimu zaidi ya Shs 100m, kazi ambayo haikuwepo kwenye mipango ya kazi ya wizara. Hali hii inasababisha kuto kusonga mbele ki maendeleo, kwani maafisa wengi huwa katika pilika pilika za kufanya kazi za zima moto na hivyo kutojipanga.
Muundo wa serekali umekuwa ni ule ule tangu miaka ya 70 pamoja na mabadiliko ya kitekinolojia, kiuchumi na kijamii ambayo yametokea katika miaka ya hivi karibuni, hivyo kuto kwenda na wakati. Muundo huu hauna tija kwani hata vyeo vingi vya serikali haviendani na majukumu mtu anayofanya, Vyeo kama Mchumi daraja I, Afisa ardhi daraja II, Afisa kilimo III n.k ambapo hukuta kama ni idara ya kilimo basi watu wote watakaojiriwa watakuwa ma afisa kilimo, halafu ndo hupangiwa kazi zingine za kufanya mfano kuchambua sera, kukusanya na kutunza takwimu, kupanga budget bila kuwa na taaluma stahili.
Pamoja na kwamba serikali ina watumishi wengi waliosoma vizuri, lakini mfumo wa sasa hauwaruhusu wataalam hao katika kutumia ujuzi wao kwa ufanisi. Mawaziri hujirundikia madaraka na kufanya maamuzi ambayo wakati mwingine huigharimu serikali hata kama wataalamu wanashauri vinginevyo.
Mimi naona hili ni tatizo kubwa, sijui wenzangu mnaonaje?
Mpaka sasa mfumo wa utendaji kazi serikalini, kwa kiasi kikubwa umebakia ni ule uliorithiwa kutoka katika serikali ya kikoloni mwaka 1961. Mfumo huu umejaa usiri mkubwa usio wa lazima huku kila document ikipigwa chapa ya neno "CONFIDENTIAL" bila sababu za msingi. Pamoja na wimbo wa utawala bora amboa serikali imekuwa ikiuimba kila siku, mpaka kuanzisha wizara inayoshughulika utawala bora, hali imekuwa tofauti na dhana hiyo ambayo ina himiza UWAZI.
Pamoja na wizara kuwa na dira (Vision), mikakati (Strategic plan), sera (Policies) n.k lakini document hizo ambazo hugharimu fedha nyingi wakati wa uandaaji wake ikiwa ni pamoja na semina nyingi bagamoyo, mwisho wa siku huwekwa katika makabati na kuliwa na mende.
Kazi nyingi za wizara zimekuwa ni za zima moto, bila kufuata mipango zilizojiwekea, zikiambata na re-allocation za mafungu, kutoka kwenye kazi zilizopangiwa kwenda kwenye kazi ya zima moto. Mfano mzuri ni ziara ya mawaziri miezi michache iliyopita ambayo iligharimu zaidi ya Shs 100m, kazi ambayo haikuwepo kwenye mipango ya kazi ya wizara. Hali hii inasababisha kuto kusonga mbele ki maendeleo, kwani maafisa wengi huwa katika pilika pilika za kufanya kazi za zima moto na hivyo kutojipanga.
Muundo wa serekali umekuwa ni ule ule tangu miaka ya 70 pamoja na mabadiliko ya kitekinolojia, kiuchumi na kijamii ambayo yametokea katika miaka ya hivi karibuni, hivyo kuto kwenda na wakati. Muundo huu hauna tija kwani hata vyeo vingi vya serikali haviendani na majukumu mtu anayofanya, Vyeo kama Mchumi daraja I, Afisa ardhi daraja II, Afisa kilimo III n.k ambapo hukuta kama ni idara ya kilimo basi watu wote watakaojiriwa watakuwa ma afisa kilimo, halafu ndo hupangiwa kazi zingine za kufanya mfano kuchambua sera, kukusanya na kutunza takwimu, kupanga budget bila kuwa na taaluma stahili.
Pamoja na kwamba serikali ina watumishi wengi waliosoma vizuri, lakini mfumo wa sasa hauwaruhusu wataalam hao katika kutumia ujuzi wao kwa ufanisi. Mawaziri hujirundikia madaraka na kufanya maamuzi ambayo wakati mwingine huigharimu serikali hata kama wataalamu wanashauri vinginevyo.
Mimi naona hili ni tatizo kubwa, sijui wenzangu mnaonaje?